Uchache wa abiria na mizigo wafanya SGR nchini Kenya kuendeshwa kwa hasara. Je, Tanzania tutakwepa hali hii?

Uchache wa abiria na mizigo wafanya SGR nchini Kenya kuendeshwa kwa hasara. Je, Tanzania tutakwepa hali hii?

Jibu zuri, kwa kuongozea, Treni za Tanzani zitakuwa na uwezo wa kuhifadhi umeme kwa muda wa dakika 45 hivyo basi hata kama kukitokea hitilafu kwenye njia ya umeme bado kazi itaendelea hadi pale mambo yatskspo kaa sawa.

Pia SGR ya Tanzania imejengewa msongo wake maalum uliounganishwa na chanzo cha umeme wa Kinyerezi na chanzo cha umeme wa Kidatu na baadaye chanzo cha umeme wa Stieglers. Kwa hio suala zima la umeme wako vizuri sana.
Kama hali itakuwa hivi kabisa. Basi tunaweza fanya vizuri, moja ya hofu yangu pia ilikuwa umeme huo je utatosheleza kufanya operations? Kwasababu kuna kipindi fulani south Africa ilawapa kidogo changamoto. Ikabidi watu waende tena General Electric kuchukua GEU30 ambayo ni ma Diesel locomotives. All in all tunaombea mema hizi juhudi.
 
, tukiangalia nchi kama USA makampuni makubwa ya usafirishaji kwa njia ya reli Kama SOUTHERN PACIFIC, BNSF, NOLFORK n.k wanatumia diesel electric locomotives na electrification imefanyika katika reli za mijini kwa ajili ya abiria. Rejea Sout h Africa, Australia n.k kwanini bado wanatumia diesel Electric locomotives zaidi kuliko Electric locomotives??
Unaijua nguvu ya ushawishi ya mashirika ya mafuta Marekani? Hawa ndiyo waliouwa treni za mijini (zaidi ya miaka 100 iliyopita). Miji mingi sana ya Marekani (miaka ya 1890 -1910) ilikuwa na mitandao ya treni za umeme, jamaa wakazing'oa ili watu wanunue model T.
 
White elephant projects!Ni ujinga wa viwango vya lami.Hizi nchi zinakurupuka,just imagine hizi nchi masikini zinaanzisha miradi ambayo haiitajiki halafu miradi inayohitajika sana kama vile maji,afya,elimu,barabara,makazi nafuu,etc inatupiliwa mbali!Haya hutokea pale ambapo umasikini wa akili ni mkubwa kuliko umasikini wa kipato
 
Unaijua nguvu ya ushawishi ya mashirika ya mafuta Marekani? Hawa ndiyo waliouwa treni za mijini (zaidi ya miaka 100 iliyopita). Miji mingi sana ya Marekani (miaka ya 1890 -1910) ilikuwa na mitandao ya treni za umeme, jamaa wakazing'oa ili watu wanunue model T.
Sahihi. Je vipi kuhusu India, Brazil, Australia n.k maana hata wao electrification imefanyika katika maeneo baadhi.
 
Wewe ndiyo ziro brain kabisa sijui shule mnaenda kusomea ujinga yaani hujui cost-benefits za railway electrification ukilinganisha na Diesel locomotives. SGR ya Kenya inatumia diesel locomotives ambazo gharama zake za uendeshaji ni kubwa sana lakini SGR ya Tanzania itatumia train za umeme ambazo gharama zake za uendeshaji ni ndogo sana hivyo hakuna hasara yoyote itakayopatikana kwa Tanzania. Kwa kutumia umeme watakuwa wamepunguza gharama za uendeshaji kwa kiasi kikubwa sana.
Hiyo "sana" unavyoikazia sasa.Utafikiri ni kweli Tanzania itapona katika hili!
 
kenya tatizo si uchache wa abiria wala mizigo
Tatizo mradi ulijengwa kwa gharama kubwa mno,marejesho ni madogo kuliko gharama za uendeshaji
Treni ya tanzania ni ya umeme,itakimbia 220km per hour,treni ya kenya ni ya kerosene inatembea 90km per hour

Kerosene?![emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sio lazima Tanzania SGR ipate hasara kama Kenya, sababu ziko nyingi.
1. Imeshasemwa SGR ya Tanzania itatumia umeme ya Kenya Diesel. Hii kwa Tanzania itaokoa gharama nyingi za matengenezo, vipuri, uendeshaji, muda wa safari, nk.
2. Mkopo-SGR ya Kenya imejengwa kwa mkopo mkubwa wakati ya Tanzania imejengwa kwa asilimia kubwa kwa fedha za ndani. Hii inafanya Kenya waweke bei kubwa na nauli kubwa ya usafiri na usafirishaji ili waweze kufikia lengo la kulipa deni. Nauli na bei juu inawafanya wasafiri na wasafirishaji wasitumie SGR watumie barabara.SGR inakosa mzigo. Tanzania haitalazimika kuweka bei juu kwa sababu haitakuwa na deni kubwa la kulipa. Gharama zikiwa nafuu wasafiri na wasafirishaji watapunguza matumizi ya barabara watahamia SGR.
3. Idadi ya nchi zinazotegemea bandari ya tanzania ni kubwa kuliko Kenya. Tanzania inazungukwa na nchi nane ambazo zinategemea bandari ya Tanzania. Kenya nchi za karibu ziko kama tatu ambazo zina mbadala wa bandari. Hizi nchi zinaangalia unafuu na ubora wa huduma. Sasa vile bandari za Tanzania zinaboreshwa na SGR ya umeme asilimia kubwa ya mizigo ya nchi hizi itapita Tanzania. Hata Uganda mshirika wa karibu na jirani na Kenya, mizigo yake itagawanywa Tanzania na kenya.
4. Uongozi-Tanzania kwa sasa kuna uongozi imara ambao hauna maswala ya nenda uje kesho. Rushwa inapigwa vita sana. Hii itasaidia kuondoa urasimu na ukiritimba kwenye utoaji huduma. Hapa Mizigo ikitoka bandari ni kwenye SGR mpaka nchi husika. SGR itakapokamilika hata Congo itapata mizigo yake bila kupitia nchi nyingine.
5. Ukuaji wa sekta ya viwanda vya ndani-viwanda vya ndani vinakua kwa kasi na kuongezeka Tanzaniana. Hii itaongeza mzigo wa kulisha SGR , Kenya ambayo uchumi wake unasimamia uwekezaji. Inachoangamoto ya wawekezaji kufunga uzalishaji na kuhamia maeneo mengine. Hapa mzigo unaweza kupungua.
6. Malighafi- Tanzania ina mashamba makubwa ya kuzalisha malighafi za kuja kutumika viwandani. Na reli ya mkoloni ilijengwa hasa si kutoa mizigo bandalini kwenda mikoani bali ilikuwa inalenga kutoa malighafi mashambani kwenda bandarini. Mazao karibunyote makuu Tanzania uzalishaji umeongezeka. Hivyo tutashuhudia SGR Ikienda na kurudi na mzigo hii italeta faida. Wakati Kenya uzalishaji wa malighafi na mazao uko chini hivyo SGR inaweza beba mzigo one way kutoka mombasa na mabehewa yakarudi mombasa tupu.
7. Mifugo- Kuna wakati niliishi shinyanga pale, mbali na mafuta na pamba kuchukua mabehewa mengi lakini pia niliona wasukuma walivyokuwa wakigombania mabehewa kusafirisha ng'ombe kuja Dar ea salaam. Sasa Tanzania ina machinjio mbili za kimataifa. Mifugo itachukua sehemu kubwa ya mzigo kuja pwani.
8. Idadi ya watu-Tanzania ina idadi kubwa ya watu , na wanapapenda kwao. Maendeleo hayako Dar na dodoma tu. SGR itarahisisha usafiri na tiketi zitakuwa zinakuwa full booked. Wakati wakenya wanapambana kubaki nairobi. Volume kubwa ya safari iko december tu wakienda kuona maji mombasa. Tanzania december watu wako station wanatafuta usafiri wa kwenda mikoani kwao na wilayani kwao wakale sikukuu . Kwa hiyo mgawanyo wa safari utarahisisha SGR ya Tanzania kutemgeneza mapato.

Wakenya niendeleee.....

Wewe ukizama shimoni, sisi tunaokuja nyuma shimo tunaliona lazima tulikwepe. Na hapo ndipo anayeanza huwa anaachwa njiani!
Hiyo namba mbili kuwa SGR ya Tanzania imejengwa zaidi kwa fedha za ndani kuliko mkopo ni la kisiasa zaidi kwa sababu hakuna ushahidi wa kuthibitisha haya madai.Iondoe katika comment yako
 
Mkuu sababu kubwa ni hizi.
Electrification ni Teknolojia ya kisasa. Na hizo nchi waliwekeza kwenye reli zamani. Sasa kubadili mfumo kwenda kwenye umeme inakuwa changamoto sana. Ndio maana unaona wanatia Diesel. Hata hapa Tanzania hatukuibadilisha MGR iwe SGR na badala yake tukaja na SGR mpya kwa sababu kuweka mpya na kuboresha ya zamani gharama hazipishani sana. Hizo treni za mijini kwenye hizo nchi nyingi ni mpya zilizoletwa kutokana na kukua kwa miji na teknolojia ya electification of the line tayari ilikuwepo.
Sababu nyingine ni upatikanaji wa umeme wa kutosha kuendesha SGR. Baadhi ya nchi hazijafanya SGR ya umeme kutokana na kutokuwa na umeme wa uhakika kuendesha SGR.
Sababu nyingine ya kutumia treni zenye umeme na diesel kwa pamoja ninkwa sababu ya baadhi ya maeneo ya njia hayajawekewa umeme hasa maeneo ya kuingia kwenye baadhi ya station hivyo train inaweza kuingia hayo maeneo na kutoka kwa kutumia diesel.
Pia pale changamoto ya umeme kukatika au mifumo ya umeme kuharibika basi safari iweze kuendelea kwa kutumia diesel.
Mkuu umepangua hii hoja kisomi sana![emoji119][emoji119][emoji119]
 
Sahihi. Je vipi kuhusu India, Brazil, Australia n.k maana hata wao electrification imefanyika katika maeneo baadhi.
Hizi nchi ulizozitaja, tofauti na ulaya, zote ni kubwa kieneo na zilishaweka mitandao yao ya reli za kawaida. Gharama za kuweka nyaya ni kubwa (mf kwenye mahandaki n.k).
 
Bei ya kusomba mizigo ama watu kutumia SGR Ya Kenya ni Mara mbili ya malori na mabasi. Sababu zikiwa
1) Uwendeshaji wa reli kutumia wachina
2) Wizi wa ticketi za abiria
3) Riba ya kinyonyaji kwa mkopo wa reli
4) Kutumia treni za kizamani ambazo zinahitaji matengenezo kila wiki
5) Bei ya diesel hubadilika kila siku

Tanzania na tumai itakwepa ujinga huu..
Bora bei ya kusomba mizigo iwe 50% chini ya malori faida ni lazima
 
Bei ya kusomba mizigo ama watu kutumia SGR Ya Kenya ni Mara mbili ya malori na mabasi. Sababu zikiwa
1) Uwendeshaji wa reli kutumia wachina
2) Wizi wa ticketi za abiria
3) Riba ya kinyonyaji kwa mkopo wa reli
4) Kutumia treni za kizamani ambazo zinahitaji matengenezo kila wiki
5) Bei ya diesel hubadilika kila siku

Tanzania na tumai itakwepa ujinga huu..
Bora bei ya kusomba mizigo iwe 50% chini ya malori faida ni lazima
Watu ni wapuuzi kweli wanafanananisha mining country na pia nchi itakayo-host gas and crude pipelines to great lakes na ushuzi wa nchi inayotegemea cargo kwa jirani!
Rwanda, Burundi, Tanzania plan joint railway project
 
Bei ya kusomba mizigo ama watu kutumia SGR Ya Kenya ni Mara mbili ya malori na mabasi. Sababu zikiwa
1) Uwendeshaji wa reli kutumia wachina
2) Wizi wa ticketi za abiria
3) Riba ya kinyonyaji kwa mkopo wa reli
4) Kutumia treni za kizamani ambazo zinahitaji matengenezo kila wiki
5) Bei ya diesel hubadilika kila siku

Tanzania na tumai itakwepa ujinga huu..
Bora bei ya kusomba mizigo iwe 50% chini ya malori faida ni lazima
More of that Reli itatukima kubeba Makontena kupeleka Bandari mpya Bandari kavu Kwala-vigwaza Malori hayatakua yakifika Mjini tena [emoji848][emoji848]
 
Ukiikosa SGR unaweza kupigwa mawe au ukaitwa msaliti
 
Endelea kujidanganya hivyo
Kwa hiyo SGR Kenya wakipata hasara na SGR Tanzania itapata? unajua gharama za kuendesha electric locomotives ukilinganisha na diesel locomotives? Kenya wanatumia diesel locomotives ambazo gharama zake za uendeshaji kubwa sana wakati Tanzania treni zake zitatumia umeme ambazo gharama zake za uendeshaji ni ndogo sana.
 
Inajengwa kwa mikopo
Kama wakenya na uchumi wao mkubwa kuliko wetu wanapata hasara, sisi hatuwezi kunusurika kupata hasara pia, japo inaweza kuwa kidogo, sababu wanasema SGR ya Kenya imejengwa kwa mkopo kutoka China, hivyo kuna mapato ya SGR ya Kenya serikali ya China inayachukua moja kwa moja kwa kipindi fulani (sikumbuki ni miaka mingapi).

Hii SGR ya kwetu wanasema inajengwa kwa fedha zetu za ndani, hivyo inawezekana serikali itakuwa inakusanya mapato moja kwa moja baada ya mradi kukamilika, jambo la msingi ni gharama za uendeshaji, je, wataweza kuzifanya ziendane na hali ya kipato cha mtanzania wa kawaida ili wengi waweze kumudu gharama za huo usafiri? ukizingatia hali mbaya ya uchumi wa mtanzania wa kawaida ilivyo hivi sasa, wakiweza ni vizuri; vinginevyo, SGR inaweza kugeuka Bombardier wataoweza kumudu gharama ni wachache.
 
Back
Top Bottom