Uchafu kwenye Masoko ya Dar es salaam

Walnut Creek

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2009
Posts
5,830
Reaction score
6,315
Wanabodi,
Ningependa kujua ni nani anasimamia usafi na miundombinu ndani ya masoko yetu Dar es salaam. Mvua ikinyesha kidogo masoko yetu yanakuwa kama Goma, Congo ni mwendo wa tope na uchafu wa kiwango cha kuleta kipindupindu. Inabidi tuzimulike Mamlaka zinazohusika zifanye kazi yake. Naomba nianze na soko la Tandale.
 
Hivi ule usafi wa kila wiki uliisha?
Hata Modi wa India alijitahidi wananchi wakasema uchafu ni mazoea yao kwa hiyo ni kazi bure
 
BASHITE yuko busy anaingilia ndoa na mahusiano ya watu.....Zero brain with large Booty
 
BASHITE yuko busy anaingilia ndoa na mahusiano ya watu.....Zero brain with large Booty
Mdau bado napenda kuishi uraiani. Ni bora tope la Tandale kuliko debe la Segerea.
 
Sawa Mkuu. Lakini pale Tandale hadi macourier wanaliona lile tope ni kero.
Utafikiri tumerogwa
Wanaona sana tu huo uchafu
Lakini kero za hivi naona wangegoma kulipa ushuru mpaka watengenezewe
Sasa unalipaje sehemu isiyo salama kwa afya?

Wakishindwa hilo sasa itabidi wajichangishe wamwage zege tu hakuna lingine.
 
Utafikiri tumerogwa
Wanaona sana tu huo uchafu
Lakini kero za hivi naona wangegoma kulipa ushuru mpaka watengenezewe
Sasa unalipaje sehemu isiyo salama kwa afya?

Wakishindwa hilo sasa itabidi wajichangishe wamwage zege tu hakuna lingine.
Hilo neno,ushuru sijui unapotelea wapi. Pia hata sisi walaji tuna jukumu la kupiga kelele haiwezekani ndizi, nyanya, viazi, nyama etc zinawekwa chini karibu na matope halafu hatupigi kelele kama vile matumbo yetu yana kinga by default labda huu uchafu ni chanzo cha watu kuduma bila kujua.
 
Uchafu wa soko unatokana na aina ya bidhaa. Ukiona soko ni chafu basi ujue hata bidhaa zinazoletwa pale sokoni ni za kiwango cha chini yaani inferior goods.
Sasa jiulize gharama za kuondoa uchafu huo zinakuwa recovered vipi maana ni kubwa kuliko bidhaa.
 
Valid point lakini niambie soko la Tandale lina inferior goods?
 
Inferior goods ni substandard goods kwa uelewa wangu huwezi kusema mazao kwa ujumla ni inferior goods. Au kuna kitu sijaelewa?
Usikariri hivyo. Ni hivi maganda ya makabechi au ndizi ama mananasi kwa mfano thamani yake ni ndogo lakini bei ya kuzoa taka hizo ni kubwa. Hii inatokana na gharama za vibarua, gharama za uendeshaji magari ya taka na ushuru mbalimbali pamoja na fidia ya thamani za mikataba na halmashauri mbalimbali.
Kifupi kuzoa taka ni gharama kubwa sana kulinganisha na kinachopatikana kutokana na taka zenyewe.
 
Inferior goods ni substandard goods kwa uelewa wangu huwezi kusema mazao kwa ujumla ni inferior goods. Au kuna kitu sijaelewa?
Kuzoa taka kunahitaji subsidy kutoka serikalini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…