Uchaguzi huu wa Serikali Mauzauza yanafanyika hadharani hamna uwoga tena

Uchaguzi huu wa Serikali Mauzauza yanafanyika hadharani hamna uwoga tena

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Huu uchaguzi wa serikali za mitaa ni wa mauzauza sana jamani. Siku kadhaa zilizopita nilikuwa saluni akapita mjumbe wa mtaa wa Matawi, maeneo ya Skanska, akatusalimia pale na kuanza kuongelea mambo ya uchaguzi na kusema akidai kwamba chama kinawalinda watu wake na hakiwezi kukubali mtu wa nje.

Katika mchakato wa kuchukua fomu za wagombea, ni dhahiri kuwa watu wa nje ni wagombea wa chama pinzani, CHADEMA, na vyama vingine watawanyimwa fursa hiyo.

Awali, katika mtaa huohuo niliwahi kusikia malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba wajumbe wanapita kutoa fedha kwa ajili ya kujiandikisha, huku wakidai hela zinatolewa kwa wanaojuana na wengine hawapewi.

Sasa najiuliza, ni kwa nini kuna wananchi wachache wanapewa fedha ili waende kujiandikisha, Uchaguzi huu utakuwa wa haki kweli au ndo tutapikwa kama kawaida?
 
Huu uchaguzi wa serikali za mitaa ni wa mauzauza sana jamani. Siku kadhaa zilizopita nilikuwa saluni akapita mjumbe wa mtaa wa Matawi, maeneo ya Skanska, akatusalimia pale na kuanza kuongelea mambo ya uchaguzi na kusema akidai kwamba chama kinawalinda watu wake na hakiwezi kukubali mtu wa nje.

Katika mchakato wa kuchukua fomu za wagombea, ni dhahiri kuwa watu wa nje ni wagombea wa chama pinzani, CHADEMA, na vyama vingine watawanyimwa fursa hiyo.

Awali, katika mtaa huohuo niliwahi kusikia malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba wajumbe wanapita kutoa fedha kwa ajili ya kujiandikisha, huku wakidai hela zinatolewa kwa wanaojuana na wengine hawapewi.

Sasa najiuliza, ni kwa nini kuna wananchi wachache wanapewa fedha ili waende kujiandikisha, Uchaguzi huu utakuwa wa haki kweli au ndo tutapikwa kama kawaida?
siasa ni kazi kama kazi zingine za kuingiza kipato kwahiyo huu ni wakati wa mavuno
 
Back
Top Bottom