Uchaguzi 2020 Uchaguzi huu Waandishi hatujatimiza wajibu ipasavyo

Uchaguzi 2020 Uchaguzi huu Waandishi hatujatimiza wajibu ipasavyo

MtuHabari

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2020
Posts
321
Reaction score
1,019
Kuna tofauti kubwa sana iliyojitokeza jinsi tulivyo ripoti taarifa za uchaguzi za 2015 na hali ya sasa tunavyo endelea kuripoti.

Kwanza tumetawaliwa na woga usiokuwa na sababu, na woga huu ukiangalia ni kutokana na vyombo vyetu vya usimamizi kama MCT, TAMWA, JUKWAA LA WAHARIRI hata ile taasisi ya mtu binafsi ijiitayo UTPC kama mwamvuli wa vilabu vya upigaji hela za SIDA vijiitavyo Press Clubs kutojitoa na kuweka miongozo ya waandishi wako salama kiasi gani kutokana na wao kutumika.

Tunahitaji Uhuru zaidi wa habari siku za usoni, lakini ni muhimu hivi vyama kuundwa upya kukidhi mahitaji ya Uhuru huo wa habari na heshima ya taaluma nzima.

Kwanza karibu vyote viko hapa Dar vikiwa vimejikita kabisa kasoro kile kilichoko Mwanza kama mwamvuli wa Clubs ambacho kiuhalisia kinamilikiwa na mtu binafsi mjanja mjanja mmoja aliyetengeneza network ya ulaji na anaweka viongozi YES BWANA huko mikoani.
(Anyway hilo tutalijadili baadae ni hoja ndefu hasa kuelekea uchaguzi wa UTPC).

Je, wana habari hali hii ya kushindwa kutoa huduma yetu wakati muhimu kama huu wa uchaguzi twaionaje?
 
Wazee Wa Bahasha Za Kaki, Wana Njaa Mno Hawa
Kaki nayo ndio moja ya vitu vinatufanya tushindwe kufanya kazi kwa weledi. Lakini kubwa ni kukosa misimamo kwa vyombo vyetu vya uwakilishi.
Majuzi tumeona jinsi Balile alivyo nunulika hadi kuanza kutoa matamko ambayo kila mwenye akili aligundua kuwa katumika na CCM kuikandamiza Chadema kuhusu suala la kufukuzwa TBC1 kwenye mkutano wao
 
Waandishi wamekuwa wachumia Tumbo kama pascal Mayalla.

Tanzania tuna Waandishi makanjanja..
 
Sasa hivi waandishi wengi mmekuwa walamba viatu vya Magufuli na wasaidizi wake. Mnaandika utopolo badala ya kutimiza majukumu yenu kulingana na weledi wenu ili kubembeleza uteuzi. Hamnq maana kabisa.
 
Kuna tofauti kubwa sana iliyojitokeza jinsi tulivyo ripoti taarifa za uchaguzi za 2015 na hali ya sasa tunavyo endelea kuripoti...

Jee wana habari hali hii ya kushindwa kutoa huduma yetu wakati muhimu kama huu wa uchaguzi twaionaje?
Kama kuna 'Jambo' huwa si tu 'linaniumiza' bali pia 'linanikera' Kulisikia ni pale 'Watanzania' wanapodhani Tanzania ya sasa ina 'Journalists' mahiri.
 
Sasa hivi waandishi wengi mmekuwa walamba viatu vya Magufuli na wasaidizi wake. Mnaandika utopolo badala ya kutimiza majukumu yenu kulingana na weledi wenu ili kubembeleza uteuzi. Hamnq maana kabisa.
Ndipo Magufuli alipoifikisha Tanzania. Ni hatari tupu. Sio waandishi wa habari tu waliopoteza uhuru wao, bali pia makundi kama wanaakademia/taaluma wa vyuo vikuu ambao academic freedom ni haki yao, nayo imeporwa.

Ukisikia hoja za wahadhiri na maprofesa wa chuo kikuu kama cha DSM (ambacho kiliwahi kushika namba kama chemchem ya fikira mpya miaka ya 70 na 80) unatamani uingie shimoni.

Nao wapo wanaimba hapa kazi tu kama chekechea!! Huwa tunasema nchi kupatwa na majanga, hili nalo ni janga ambalo athari zake zitahitaji kizazi kizima kuweza kufutika.
 
We are survivors, tutasonga mbele regardless. Chema chajiuza kibaya chajitembeza. Kaeni na vyombo vyenu uchwara, kaeni na mamlaka zenu, kaeni na woga wenu, kaeni na unafiki wenu. No press coverage for Mh. Tundu Antiphas Lissu is coverage enough!

Hatuhitaji mabango, hatuhitaji redio zenu na TV zenu, hatuhitaji kubebwa na kupakatwa...we will walk with and stand on our own feet, shame on you walamba viatu vya watawala, your days are numbered...eti waandishi, waandishi wenyewe uchwara hawa akina njaa!
 
Ndipo Magufuli alipoifikisha Tanzania. Ni hatari tupu. Sio waandishi wa habari tu waliopoteza uhuru wao, bali pia makundi kama wanaakademia/taaluma wa vyuo vikuu ambao academic freedom ni haki yao, nayo imeporwa. Ukisikia hoja za wahadhiri na maprofesa wa chuo kikuu kama cha DSM (ambacho kiliwahi kushika namba kama chemchem ya fikira mpya miaka ya 70 na 80) unatamani uingie shimoni. Nao wapo wanaimba hapa kazi tu kama chekechea!! Huwa tunasema nchi kupatwa na majanga, hili nalo ni janga ambalo athari zake zitahitaji kizazi kizima kuweza kufutika.
Asante kwa chakula kizuri cha fikra.
 
We are survivors, tutasonga mbele regardless. Chema chajiuza kibaya chajitembeza. Kaeni na vyombo vyenu uchwara, kaeni na mamlaka zenu, kaeni na woga wenu, kaeni na unafiki wenu. No press coverage for Mh. Tundu Antiphas Lissu is coverage enough!

Hatuhitaji mabango, hatuhitaji redio zenu na TV zenu, hatuhitaji kubebwa na kupakatwa...we will walk with and stand on our own feet, shame on you walamba viatu vya watawala, your days are numbered...eti waandishi, waandishi wenyewe uchwara hawa akina njaa!
Mkuu Mag3 nimekusoma vizuri. Tasinia ya habari kwa kweli tuna matatizo makubwa sana. Shida ni kuwa taaluma hii imevamiwa na makanjanja wengi na ndio maana wajanja ndani ya taasisi za habari wanapinga sana ile Sheria ya Habari 2016 hasa kipengele cha kutambua wanahabari wawe na kiwango gani cha elimu.
Wakijaa wenye elimu ya Diploma na degree walaji ndani ya MCT, TAMWA, UTPC wanaotafuna fedha za wa Sweden, Denmark nk watazilaje? Wao wanawakusanya mfano vikundi vikundi Mara press clubs nk kisha kuwapatia ukoko wale wenyewe wakipiga mpunga wa kutosha kwa masharti ya kutoandika mambo yasiyo iumiza serikali na chama tawala.
Lakini umuhimu wa waandishi hauishii kwenye habari za uchaguzi pekee, hivyo tasnia hii ni muhimu tuijenge vyema ili hata Lissu naye akipata madaraka na kwenda kinyume aongozwe njia sahihi ya kufuata
 
Back
Top Bottom