Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Elections 2010 Uchaguzi Igunga 2011: Uchukuaji fomu na kampeni kuelekea uchaguzi mdogo

Status
Not open for further replies.
Naanza kwa kuomba radhi kama nitafanya some technical mistakes katika posting yangu kwa vile ndio naanza kujiunga na forum hii, japo nimekuwa msomaji wake kwa muda. Nimejiunga na kuandika haya kwa uchungu ninaoupata na kisha sina pa kuyapeleka niliyoyapata hapa Igunga kisha nikabaki salama.

Mgombea wa CHADEMA kwa nafasi ya ubunge hapa Igunga Mwl Kashindye alikuwa mtumishi wa serikali akianzia ngazi ya chini kabisa ya Mwalimu wa UPE vijijini, alijiendeleza kielimu hadi kuhitimu chuo kikuu na kufikia kuwa Mkaguzi wa Elimu, vijiji vyote vya Igunga na watu wake na matatizo Yao anayajua vizuri sana, shida za waalimu anazijua vilivyo.

CCM ilikuwa imeshaandaa waalimu kuwa wasimamizi wa vituo, ili kuhakikisha kuwa CCM inashinda kwa Hali yoyote ile iwayo, lakini sasa kwa kuwa mgombea wa CDM ni Mwalimu mwenzao, wakati mgombea wa CCM, Dr Kafumu ni Commissioner wa madini katika wizara ya nishati na madini, wizara inayoongoza kwa utata hapa nchini, na yeye mwenyewe akiwa ndie mtaalam wa kutoa mikataba ya madini nchini, imeonekana uwezekano wa yeye Dr Kafumu kushinda kihalali itakuwa ni vigumu, inabidi "Mbinu Mbadala" zitumike.

Awali CCM ilitaka kuwabadilisha waalimu hao wa Igunga wasikae vituoni ili waletwe wengine kutoka Singida, lakini ikaonekana hawa wa hapa wanaweza kufanya hasira na wakampigia mwenzao kampeni ya kufa mtu.

Wakiachwa waendelee uchakachuaji vituoni utakuwa mgumu. Kamati ya siasa ya wilaya ya Igunga, ikishirikisha viongozi wa kimkoa na Taifa, akiwemo Mhazini Mkuu Taifa Ndg Mwigulu, iliketi na kuamua kwa kauli moja kumuita Mkurugenzi (DED) Ndg Magayane kuwa awasiliane na wahusika wa Wizara ya elimu ili profile nzima ya Mwl Kashindye ipatikane ili ichunguzwe itafutiwe kasoro, na kama hazipo basi lazima ziwe fabricated ili zitumike kumuengua.

Izingatiwe kuwa DED Magayane ana tuhuma nzito ya ufisadi katika ujenzi wa barabara fupi ya lami iendayo kwenye Halmashauri ya wilaya, ilikuwa afukuzwe kazi kabla ya uchaguzi huu, lakini amerejeshwa kazini kwa masharti kuwa lazima CCM ishinde, jimbo likipotea na yeye apotee.

Vipengele vya kumuengua vimeshapatikana inasubiriwa siku ifike DED Magayane afanye vitu vyake, ni siri kubwa, lakini kwa kuwa miongoni mwao kuna wanaochukia dhuluma, basi vimeshavujishwa na tutavipeleka kunako husika ili kuvidiffuse.

Aidha, Mkuu wa polisi wilaya ya Igunga ambaye alikataa kuzuia operation Sangara ya CHADEMA ilipoanza wilayani Igunga, licha ya kupelekewa barua kutoka CCM ya kumtaka afanye hivyo, keshatimuliwa na ameletwa OCD mpya spesheli kuikabili CHADEMA.

Hata aliekuwa Manager wa NMB Igunga keshahamishwa kisa eti ni Mchagga na anashabikia CHADEMA kwa hiyo imehofiwa kuwa atafanya kampeni kwa vile ana influence kubwa kwa wateja wake ambao ni wengi sana hapa Igunga.

Ni kweli kuwa Mwigulu anamwaga fedha kifashisti kwa kila taasisi na makundi ya jamii, waziwazi, lakini mitego ikitegwa na TAKUKURU wakiarifiwa waje wamshike live, TAKUKURU haohao wanamjulisha kwa simu kuwa wanakuja, anawaambia wasubiri kwanza amalize kugawa, akishamaliza na kuondoka, ndio anawapigia waende wakavamie hewa.

Ndugu zangu wanaJF, ni mengi mno yatakayoikwamisha CHADEMA hapa Igunga, hata sijui niwasilishe lipi na niache lipi, maskini CHADEMA, pamoja na kupendwa na wengi sijui itashinda vipi dhidi ya dhulma hizi, au labda tupige sana kelele za mwiziii kwa pamoja mpaka ardhi itikisike!

Naishi kijiji cha Imalanguzu, Kata ya Mwamashimba, Tarafa ya Igurubi, Wilaya ya Igunga. Niulizeni swali lolote kuhusiana na hali ilivyo nitajibu nitakayoweza bila ya woga.

Naomba Kuwasilisha!
 
Mh¡Shughuli imeanza,haya ngoja tuskize na wana jamvi wengine mi nitarudi Badae muda wa daku huu
 
Karibu sana jukwaa hili la JF ni lako hivyo jisikie uko nyumbani, mawazo huru zaidi LAKINI bila umbeya wowote.

MgungaMiba hebu tuhbarishe zaidi ynayojiri Igunga na vitongoji / vijiji vyake vyote kuhusiana na AZMA YA WATANZANIA KUUNG'OA UFISADI WA ROSTAM AZIZ na magugu yake yote.
 
Umetumwa kupima upepo, huu umbea peleka huko huko kwenye magamba, msiogope kivuli chenu kazi pevu inakuja.
 
Mimi niko Igunga hakuna kitu kama hicho nitashangaa tukiendelea kujadili tetesi.
CCM walitegemea atachaguliwa Tumbo vile vile walitegemea kumtumia Mahona lakini kadri siku zinavyokwenda Kashindye anakuwa tishio kwao ndio maana wanakuja na mbinu kama hizi zisizo na kichwa wala miguu.
 
Kwani mbona Mwanza walimuenguwa Wanje kwa hila lakini alirudi!

Nyie chukueni fedha ni zenu walizoiba lakini kura hakuna kuwapa, maana kama wanawe kutenga milioni 800 za rushwa lakini hawawezi kununu mitambo ya umeme hamuoni hao ni vijaa na hawafai kuongoza tena?
 
Hizo tetesi cdhani kama ni za kweli. Information nyeti ulizonazo ni nyingi kiasi kwamba unanitisha, Time will tell
 
Siku zote wanasema mtu smart anajifunza kutokana na makosa aliyofanya siku za nyuma lakini mtu smart zaidi anajifunza kutokana na makosa ya wengine!

Mwigulu na Nape hapa ndipo walipo onyesha kuwa siyo smart hata kidogo; let us give time a time tutaona mwisho maana lazima mwisho utafika.

Mwigulu kama alitaka kufanya hiyo kazi ya kuweka hazina ya Mafia Group alipaswa kujuwa waliomtangulia walipatwa na dhahama gani ili ajifunze, akianza na Maheremu Salome Mbati, Rostum A na Makala ndugu yake. Haya ya kizembe hivyo ili mradi umepata cheo yanafanyika Africa tu! na hasa Tanzania, na ndio ya Nape halishindwa hata kujiuliza kuwa iweje mimi leo nipewe kazi ya kushika mabango yenye matusi ya kumtukana mtu ambaye alikuwa rafikiye bwana mkubwa wa damu ambaye hawaku kukutana barabara na kuanzia hapo angejuwa la kujifunza kabla hajaanza kufoka kifua mbele bila kujuwa kesho itamka vipi.

Sitaki kusema ya kesho, lazima lazima kila kesho uja na vibweka vyake, tusubiri.
 
Hizo tetesi cdhani kama ni za kweli. Information nyeti ulizonazo ni nyingi kiasi kwamba unanitisha, Time will tell
Umeona eh too much informations, mara DED kajenga nusu barabara mara OCD kabadilishwa mara manager wa NBC ni mchaga mara walimu wabadilishe waje wa Singida dah!!! hata kudanganya sio hivo umeji defend mno hadi umetufanya tuwe na wasiwasi na habari yako, kwa kutufanya tukuamini eti unatutajia hadi kijiji anachotoka kidding ....sisi si wa hivyo kajipange upya..
 
Kwako mgumbamwiba,

Asante sana kwa insider information je umeshafanya namna ya kuwasiliana na mawakili wa CHADEMA ili kuangalia namna ya kuweza kupambana
na hujuma kwa maana CCM wanaweza kufanya hivyo kama ulivyosema, kwa maana wakipata ushindi wa technical kwao itakuwa nafuu kubwa kwani watakuwa ni kama hawana mshindani ?

Ushauri kwa chadema ni kuakikisha kuwa ujazaji fomu hadi udhamini unafanyika kwa makini sana chini ya usimamizi wa wanasheria wao. wadhamini wao lazima wawe ni watu wenye kueleweka na kufahamika ndani ya chama maana ccm inaweza kupandikiza watu ndani ya CHADEMA na watu hao kujitoa dakika za mwisho.

Makosa yote yaliyofanywa na kusababisha wagombea mbalimbali kuondolewa wanasheria wa CHADEMA wahakikishe hayapewi mwanya this time.
 
Dawa ni kusema hapana, kama watataka kujizika hao magamba, walete tuhuma za kipuuzi ili wamuengue huyo mgombea wa CDM.
 
Peoplez....... Power!!!
Wanataka kujzka wenyewe kama walivyojzka kwa Wenje. Nguvu ya Umma inaizd upupu wa magamba.
 
Mimi nawashangaa baadhi ya watu hapa JF, bila shaka ni mapandikizi ya magamba. Ni afadhali ukaamini kuwa Mungu yupo na asikuwepo kuliko ukaamini kuwa hayupo na ukakutana naye siku ya kiyama.

Ushauri wangu kwa CHADEMA, msipuuzie jambo lolote kwa hili, ila muwe na tahadhari, ili likitokea la kutokea, tuwe na solution tayari na siyo kukumbuka blanketi asubuhi.
 
Mimi nawashangaa baadhi ya watu hapa JF, bila shaka ni mapandikizi ya magamba. Ni afadhali ukaamini kuwa Mungu yupo na asikuwepo kuliko ukaamini kuwa hayupo na ukakutana naye siku ya kiyama. Ushauri wangu kwa CHADEMA, msipuuzie jambo lolote kwa hili, ila muwe na tahadhari, ili likitokea la kutokea, tuwe na solution tayari na siyo kukumbuka blanketi asubuhi.

Nakushukuru kwa kuunga mkono, nami kwa moyo huo huo naungana na wewe kuwa CHADEMA iwe makini sana na hila za CCM. Wakati mwingine si CCM bali wakatumiwa CUF kama jimbo fulani ktk uchaguzi mdogo kama huu, CUF ilimwekea pingamizi mgombea wa CHADEMA na jimbo hilo likaenda CCM. Kama sikosei ni kati ya Mwanza, Shinyanga, Tabora nakumbuka tu kuwa aliyeshinda ni mbunge m/ke. Kwa hiyo tahadhari ni kitu kizuri zaidi, kama CHADEMA mpaka sasa bado hamjajifunza hila za wenzenu mtajaza wenyewe.

Mtoa mada ametoa taarifa za kiintelejensia hata kama si sikweli zitatusaidia kuwa makini zaidi. Tukumbuke kuwa kuku mwoga ana vifaranga vingi. Take CARE. Hatutaki tukose jimbo hili kwa uzembe hata kidogo kwa hiyo kila mtu atimize wajibu wake.

Ndugu Mwita kazi unayo hapo Igunga angalia Mwl mwenzako asije akashiindwa kwa uzembe. Simamia kiukamilifu zoezi hili mpaka kieleweke.
 
CHADEMA ikishinda Igunga nahamia Zanzibar.
 
Je, tuseme kuwa tunataka kujifunza mbinu za kiwizi za CCM sasa? Kama ndivyo basi tayari 3-0. CCM ni wezi hilo kila mtu analifahamu, kama CHADEMA hamlijui hilo basi msiwapotezee muda Watz. Tukumbuke kuwa pamoja na mbinu hizo pia kuna wasimamizi wa uchaguzi pamoja na tume yenyewe. Ni uhuni mtupu.

Wakati wa mapambano ndio huu kila askari awe macho.
 
CHADEMA ikishinda Igunga nahamia Zanzibar.[/QUOTE

Tunashukuru kwa kuwa wewe ni Rabana na umesema kuwa CHADEMA haitoshinda na uamini hivyo. Ikishinda na ubaki hivyo hivyo kuwa haikushinda ila mawazo ya watu tu. Wala hakuna sababu ya kuhamia Zanzibar utabaki hapo hapo ulipo umekalia masaburi yako.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom