Uchaguzi Marekani

Uchaguzi Marekani

Mag3
Baada ya uchaguzi wa Indiana na W.Viriginia hali nyingine inajitokeza kwa Demo. Sanders aliwahilalamika kuhusu SD na kwamba wanapaswa kuunga mkono mgombea na sehemu alizoshinda

Wakati Sanders ameshinda Caucus 7 mfululizo ambazo kimatiki si ngome ya Democrat , kauli mbiu ilikuwa 'ushindi wa majimbo 7' na aungwe mkono na SD

Baada ya uchaguzi wa NY, Clinton alishinda majimbo 5 makubwa ikiwemo Pen, Conn, Maryland, Delaware. Kwa maneno mengi alishinda majimbo 6 kati ya 7.

Hakukuwa na kauli za 'ushindi' huo mfululizo licha ya ukubwa na umuhimu wake

Sanders amebadili kauli, anatumia kura za maoni kujenga hoja.

Anasema kura za maoni zinaonyesha akimshinda Trump kwa Point 20 huku Clinton akimshinda kwa ukaribu sana

Habari za wiki hii, vyombo vingi vya habari vimeondoka katika hoja ya SD na hesabu zinazomkabili Sanders,vinazungumzia kura za maoni kati ya Dem Vs Trump

Hili linafanyika makusudi kwa maana mbili.
Kwanza, 'kuwatisha' SD kuwa Clinton ni risk kwasababu Trump anamkaribia.

Sanders anataka kushawishi SD,huko nyuma alipinga influence yao katika primaries

Pili, kuendelea kuwashawishi wapiga kura kuwa Clinton hachag
uliki

Kitu ambacho ni intriguing ni namna vyombo vya habari vinavyoungana na Sanders katika kura za maoni dhidi ya Trump. Hili limechukua sehemu kubwa ya maongezi.

Tafiti zinazofanyika sasa hivi nyingi ni kuhusu Clinton/Sanders Vs Trump

Kwanini tafiti hizo zinatoka mfululizo kila siku, na kwa mpangilio fulani.
Inakuwaje watafiti walianza siku moja na kumaliza katika muda sawia?

Je, kuna mahusiano yoyote ya Sanders na wamiliki vya vyombo vya habari ambavyo kwa Marekani umiliki wake umehusishwa sana na makundi fulani ya jamii?

Je, kuna uhusiano wa watafiti na vyombo vya habari?

Tunauliza hivyo, kwasababu mwendo wa vyombo vya habari katika mazingira yaliyopo vingemuonyesha Sanders ugumu na pengine kuweka shinikizo ajitoe.

Vingeonyesha madhara yanayoendelea upande wa Democrat

Kinyume chake kumekuwa na kumtia moyo kwa kujenga hoja ambazo kila siku zinabadilika. Nini kinaendelea nyuma ya pazia na katika Democrat kwa ujumla?

Tusemezane
HALI ILIVYO NDANI YA DEMOCRAT

VYOMBO VYA HABARI NA USAIDIZI KWA SANDERS

MWELEKEO WA 'CONVENTION' UNAZIDI KUPATA KASI

Katika bandiko tulilonukuu tulieleza vyombo vya habari na ushiriki katika mchakato wa Democrat. Tulihoji 'mahusiano' ya vyombo hivyo na Seneta Bernie Sanders

Kwanza, kila ilipotokea Sanders kashinda mfululizo hiyo ndiyo ilikuwa habari.
Kwa mfano, kabla ya uchaguzi wa NY, Sanders alishinda majimbo 7 yakiwa na caucus zaidi. Habari katika vyombo ilikuwa ushindi mfululizo

Clinton alishinda NY, Penn, Conn, Delaware, Maryland mfululizo. Haikuwa habari

Hesabu zikaonyesha ugumu kwa Sanders, kauli ikabadilika uchaguzi lazima uende Philadelphia. Hoja ikawa kuwa wajumbe wa SD wasihesabiwe hadi kura katika mkutano mkuu. Hoja hiyo ilijibiwa kuwa ni utaratibu wa Dem kama ulivyotumika kwa Clinton 2008

Sanders akaja na hoja kuwa kwa kuangalia kura za maoni, yeye anamshinda Trump kwa mbali ukilinganisha na Bi Clinton. Kauli kairudia mara nyingi.

Tulihoji kwanini kuwe na ulinganifu kati ya Sanders na Trump na si Sanders na Clinton?

Vyombo vya habari vikaiuchukua habari hiyo na kuifanya habari ya kila siku.

Tulihoji kuhusu taasisi mbali mbali kuendesha kura ya maoni kati ya Sanders na Clinton Vs Trump. Democrat hawajamaliza mchakato na hali ilivyo Clinton anaongoza.

Iweje kuwe na kura ya maoni kumhusisha Sanders na Trump ili hali nafasi yake ni finyu?

Taasisi zikatoa kura za maoni za kitaifa zikionyesha kukaribiana kwa Clinton na Trump kila siku. Ndani ya wiki moja ambayo Trump alikuwa mapunzikoni katika hali ya kujiuliza , kura hizo zinaonyesha akiwa sawa na Clinton 'dead heat' na zingine akimshinda Clinton

Hili linafanyika kisayansi na kwa umakini wa hali ya juu sana.
Kwamba, Sanders ana nafasi kuliko Clinton na hivyo kujenga mazingira yafuatayo

1. Kuwakatisha tamaa wafuasi wa Clinton dakika za mwisho ili Sanders ashinde majimbo yaliyobaki kwa kiasi kikubwa na kujenga hoja ya kwenda convention

2. Kujenga mazingira ya kuwatisha Super Delegates (SD) kuwa Clinton hamwezi Sanders na hivyo wabadili mweleko na kumuunga mkono Sanders

Katika kushadidia hilo vyombo vya habari vinaonyesha kura za maoni vikisisitiza kipengele cha 'disliked candidates' katika historia ya Marekani kuwa Trump na Clinton.

Kwa maneno mengine tayari vinamjenga Sanders kuwa ni 'liked'

Katika wakati huu, Trump anaunganisha Republican licha ya upinzani mkubwa alio nao. Ni mapema mno kubaini republican wame rally behind him.

Clinton ana vita mbili, kwanza, na Sanders na pili Trump.

Hivyo kwa Democrat ni ngumu kupata idadi ya wapiga kura jambo linaloonyesha kura za maoni zinafanywa kwa makusudi na si kwa kuzingatia hali ilivyo.

Hakuna anayeeleza kuhusu mashambulizi ya Sanders na Trump dhidi ya Clinton na kwamba hilo si tu linabadilisha kura za maoni, bali linamumiza sana Clinton

Kwa mtazamo huo, uwezekano wa uchaguzi kwenda convention unaongezeka, si kutokana na namba bali usaidizi mkubwa wa vyombo vya habari kwa Sanders.

Kuna uhusiano gani kati ya Sanders na vyombo vya habari na kwanini na nani walioko nyuma ya mango huo?

Na hili linaeleza nini kuhusu hatma ya Bi Clinton kuanzia June 7 kuelekea Philadephia?

Tutajadili
 
TRUMP NA WAANDAMANAJI
CLINTON NA EMAILS
SANDERS 'HOJA YAKE YAPATA MIGUU'

REPUBLICAN
Donald Trump amekumbana na waandamaji katika majimbo ya New Mexico na Claifornia
Hii ni katika jitihada za kuwavuta jamii ya Walatino.

Kwa bahati mbaya kauli zake kuhusu Walatino zinakumbana na makundi ya waandamanaji wa Kilatino

Awali iliripotiwa kuwa makundi hayo ni ya vijana wa 'Sanders' pengine kumjenga kwamba analeta hamasa na ana uwezo wa kukabiliana na Trump.

Hili lina sura mbili, kwanza, linaweza kumjenga Sanders lakini pia linamweka katika wakati mgumu kwa kuzingatia vurugu za Nevada wiki iliyokwisha dhidi ya Bi Clinton

Trump alifanya kosa jingine akiwa New Mexico kwa kumshambulia gavana wa jimbo ambaye ni Mlatino na Republican. Gavana huyo ni maarufu kwa Walatino, kitendo cha kumshambulia kinawaondoa Walatino Zaidi kutoka katika kumuunga mkono

Kwa upande wa GOP hali hii inawatia wasi wasi kwani uwezekano wa kupoteza majimbo ya asili 'Red states' yenye walatino unaongeza katika uchaguzi mkuu.

Hofu Zaidi ni kuhusiana na makundi mengine ya jamii kama weusi, wanawake, wahamiaji kutoka Mideast n.k. na hivyo kumwacha na kundi la weupe.

Licha ya wingi wao, tatizo, kupoteza majimbo ya Walatino ni kupoteza 'electoral college'

Weupe wanaweza kuwa wengi na kupiga kura kwa wingi. Je, ikitokea wingi huo ni wa eneo Fulani nini hatma ya GOP kwa majimbo yenye makundi 'hasimu' na Trump?

CLINTON
Mkaguzi wa state dept, wizara ya Bi Clinton ametoa taarifa yake kuhusiana na suala la matumizi ya email binafsi kwa shughuli za umma.

Ameonyesha ukiukwaji wa taratibu aliotumia Bi Clinton

Wachambuzi wa masuala ya sheria wanasema, hakuna kosa la kisheria (legal problem) au jinai 'criminal' . Kilichotokea ni ukiukwaji wa procedure za ndani

Uchunguzi huu ni tofauti na unaoendelea wa FBI.

Katika hili kuna sura mbili, linaweza kuwa na nguvu za kisheria tatizo la kisiasa

Tuangalie hali hizo bandiko linalofuata

Suala hili limegubika habari za vyombo vya Marekani kwa siku ya leo.
 
CLINTON NA emails

Uchunguzi wa ndani unaweza kutokuwa na nguvu za kumtia matatani kisheria.
Hata hivyo, uchunguzi wa FBI unaendelea na unaweza kuja na matokeo tofauti

Likiingia suala la kisheria, Bi Clinton atakuwa katika wakati mgumu kisheria na kisiasa

Kisiasa, leo tu limeharibu taswira ya kampeni. Mazungumzo ni juu ya emails badala ya ujumbe. Anachokifanya ni demage control kuelekea June 7.

Hili si zuri kwasababu linazidi kumjengea taswira mbaya licha ya kuwa silaha

TRUMP: Keshaidaka hoja hii ambayo kwa muda mrefu imetafutiwa namna na GOP. Anaitumia kumshambulia Bi Clinton wakati huu anapohitaji sana ushindi wa mwisho

SANDERS: Kwa wasomaji wa mabandiko ya nyuma, tulizungumzia kwanini Sanders yupo katika ushindani. Kwamba, ana matumaini na jambo hili. Kauli ya mkewe 'uchunguzi wa emails umefikia wapi' inaeleza mazungumzo na mwandani wake

Sanders hajaongelea sana suala hili isipokuwa wapiga debe wake katika runinga

Anachokifanya ni kujitenga asionekane anasaidiana na Trump kumshambulia Clinton. Nyuma ya Pazia, Sanders anatumia sana hoja hii na anaomba ishike kasi

MTAUMAINI:
Matumaini ya Sanders ni kuitumia hoja kwa namna mbili. Kwanza, kuelekea June 7 kwenye majimbo yenye wajumbe Zaidi ya 700 hoja itamdhoofisha Bi Clinton na yeye kuziba pengo la tofauti kati yake na Clinton

Pili, anataka kuitumia hoja kuonyesha kuwa Clinton ni risk uchaguzi mkuu.
Kwamba ana political burden mbele ya safari. Kumbuka amesema anachotaka ni kwenda mkutano mkuu. Njia ya kuelekea Philadephia inaonekane kufunguka

NJIA INAFUNGUKA:
Anachokifanya Sanders ni hicho hapo juu, kwanza kuziba pengo la wajumbe ili ashawishi mwendo wa mkutano mkuu Philadephia

Hoja kubwa ni kuwatisha Super Delegates (SD). Hadi leo Clinton anahitaji wajumbe 81 kufikia magic number ya 2383. Sanders anahitaji wajumbe takribani 500

Hesabu hiyo ina namna ndani yake. Kwamba ukiondoa SD Clinton hatafikisha 2383
Hivyo Sanders anawatisha SD ili wabadili uelekeo.

Hadi sasa Clinton ana SD 500 na Sanders 42. Ikitokea SD 100 tu wakahamia kwa Sanders, Bi Clinton atakuwa na pungufu ya 2383 na kulazimika kwenda mkutano mkuu

kuna namna nyingine. June 5 kuna kura Puerto Rico kwenye wajumbe 64 na anakotarajiwa kushinda Bi Clinton. June 7 kuna wajumbe Zaidi ya 700 katika kura

Kwa utaratibu wa uwiano kwa vyovyote vile Bi Clinton atapata si chini ya wajumbe 200 katika assumption kuwa Sanders atashinda katika kiwango cha asilimia 65 hadi 70.

Hao 200 watafidia SD wanaoweza kutishika na hali ya Bi Clinton, hivyo bado atakuwa salama kwa kuzingatia kuna uchaguzi unaokuja.

Tatizo linalomkabili Bi Clinton bado linatoa nafasi kuwa mgombea.

Nafasi inazidi kuwa kubwa kwa kuzingatia kuwa wiki iliokwisha Sanders alikuwa na mtifuano na 'the establishment' na viongozi wa DNC kama Bi Wiessman Schult

Hili linampa ugumu kushawishi SD kuhamia kwake. Ni kosa ambalo laiti angelijua, asingelifanya. Halikumsaidia katika kuvuta SD kwa kuwashambulia.

Pamoja na yote, suala la emails ni tatizo jingine analokumbana nalo Bi Clinton kisiasa
Madhara yake si uchaguzi mkuu, bali wakati huu akiwa na wapinzani wawili, Trump na Sanders.

Tusemezane
 
Kwa upande wa Republicans, Donald Trump amefikisha idadi ya wajumbe wanaotakiwa na hivyo moja kwa moja kuwa mgombea mteule wa kiti cha Urais Marekani. Kinachosubiriwa sasa ni baraka tu za Convention Cleveland.

Na kwa upande wa Democrats mambo ni magumu kidogo na ingawa wajumbe maalumu (superdelegates) wanazidi kuchagua upande, Sanders bado amekomaa na Clinton.

Hadi sasa idadi ya wajumbe kwa kila mgombea ni kama ifuatavyo;

Wajumbe wa kuchaguliwa

  1. Hillary Clinton....1769
  2. Bernie Sanders...1499
Wajumbe maalum
  1. Hillary Clinton....541
  2. Bernie Sanders...43
Jumla ya wajumbe
  1. Hillary Clinton....2310 (pungufu kwa 73)
  2. Bernie Sanders...1542 (pungufu kwa 841)
Kwa hesabu hizi haijulikani Bernie Sanders bado anatafuta nini katika mbio hizi! Hata hivyo Clinton taratibu anakaribia ile idadi ya wajumbe wanaotakiwa na yawezekana akafikkisisha idadi hiyo kabla ya Convention Philladelphia.
 
KUELEKEA JUNE 7-DEMOCRAT

MWELEKEO WA HABARI WABADILIKA

Kuelekea June 7 kumekuwa na mwendelezo wa uchaguzi katika sura tofauti

Kama tulivyosema, vyombo vya habari vimebadili mwelekeo na kuingia awamu nyingine

Awamu ya kwanza ilikuwa kubadili kura za maoni kati ya Clinton na Sander kuwa Clinton na Trump,vikionyesha Clinton akiongoza kila siku Trump anapunguza pengo baina yao

Awamu ya pili ilikuwa kuonyesha kura za maoni kati ya Clinton na Trump na Sanders na Trump. Hapa vilionyesha kuwa Sanders anafanya vema dhidi ya Trump kuliko Clinton

Awamu ya nne, ni kura za maoni zikionyesha wamefungana 'neck t neck' kati ya Clinton na Trump na sasa Sanders anaongoza dhidi ya Trump kitaifa.

Baada ya hilo kufanikiwa, vyombo vya habari vimeanza kuonyesha kuwa ndani ya democrat kuna hofu kubwa kwa Clinton kushindwa.

Watoa Makala wanaonyesha 'nadharia' za kwanini Clinton atashindwa na Trump.

Hayo ni kuwatia hofu super delegates kama alivyosema Sanders.

Sanders ambaye amekuwa kimya kuhusu suala la emails, taratibu anaibuka na kueleza SD 'to take a hard look' kwamba ni tatizo mbele ya safari kwa Bi Clinton

Siku za nyuma alikataa kuongelea kutoonekana akisaidiana na Trump kummaliza Clinton.

Mazungumzo ya Sanders alipoulizwa kuhusu Umakamu wa Rais, alisisitiza bado ana matumaini ya kushinda, hata hivyo alisema, kwa mtu atakayekuwa VP wa Clinton lazima awe na sfia alizozitaja kama zake. Hili linaonyesha nini kinapeleka aendelee na kampeni

Kura za maoni majimbo ya California na New Jersy hazionekani kuwa na ukaribu kwake

Sanders ameanzisha 'timbwili' jingine akitaka watu waruhusiwe kujiandikisha California.

Amefikisha madai yake mahakama kuu ya jimbo. Hii ni baada ya muda wa kujiandikisha kwisha huku akiwa na matumaini na 'independents' ambao hawakujiandikisha

Hili linatokea baada ya kubaini kuwa matokeo ya California hayawezi kumpa nafasi aliyotaraji. Kwamba hata akishinda kwa tofauti ya point 10 bado uwiano hautampa wajumbe Zaidi ya 100 ili kupunguza pengo, wakati New Jersey akiwa nyuma kwa point 10

Mtafaruku na viongozi wa DNC

inaendelea
 
MTAFARUKU NA VIONGOZI WA DNC

Sanders amekuwa na mtafaruku na viongozi wa DNC wawili akipinga uwepo wao katika maandalizi ya convention. Ni ugomvi ambao kimtazamo ni wa kutengeneza bila mantiki

Wakati hilo likendelea, aliyekuwa kiongozi wa DNC na Mgombea Urais mwaka 2004, Seneta wa Vermont Bw Howard Dean, amemtaka Sanders asitoe matumaini ya uongo kwa wafuasi wake. Dean anasema uchaguzi unaongozwa na sheria za DNC

Dean alikuwa akijibu hoja ya Sanders juu ya kufungua madai ya kuongeza muda wa registrations kwa wafuasi wake, kesi aliyofungua California

Dean anasema sheria haziwezi kubadilishwa tena inapotokea matokeo yapo wazi akimaanisha sheria za uchaguzi wa DNC zpo wazi, na kwamba, Sanders alizitambua.

Kitendo cha kutakkuongeza muda wa registration ni kubadili sheria katika ya 'mchezo' tena akijua tayari ameshapoteza matumaini

Hili linaeleza jinsi gani viongozi wa DNC wanavyokerwa na kampeni za Sanders.

Katika mchanganuo wa kura za maoni zinazotolewa,Sanders akiondoka kura zinampa nafasi Clinton dhidi ya Trump ingawa halielezwi na vyombo vya habari kwa uwazi

Democrat wanaamini anachofanya Sanders ni kuleta ktafaruku ndani ya chama.
Ni habari njema kwa Clinton inapotokea viongozi kutokubaliana na Sanders.

Kwa kutazama wajumbe wa SD, hadi wakati huu waliomuunga mkono Sanders ameongeza mmoja na kufikia 42. Ikumbukwe wapo SD Zaidi ya 200 ambao hawajachukua upande, na waliopo wanaweza kubadili mwelekeo wakati wowote

Kwa wajumbe 800 waliobaki, ni wazi Sanders hawezi kushinda hata kama atashinda kwa asilimia 70. Ikitokea SD hawahesabiwa, hakuna jinsi bali kwenda convention.

Lakini, kutohesabiwa kwao itakuwa ni kinyume na sheria za DNC, ambazo mwaka 2008 zilitumika kumuengua Bi Clinton dhidi ya Obama

Kwa upande mwingine Trump anaunganisha Republican ingawa kauli zake zisizotabiri zinazidi kuwatibua baadhi.

Jana chama kingine cha Liberitarian kimechagua wagombe wake Bw G.Johnson akibeba bendera. Hili limezidi kuwatia hofu republican hasa wasioridhika na Trump, lakini pia linaathari kwa Clinton ikiwa takuwa mgombea wa Dem.

Tutajadili hili sehemu inayofuata

Tusemezane
 
Sanders ambaye amekuwa kimya kuhusu suala la emails, taratibu anaibuka na kueleza SD 'to take a hard look' kwamba ni tatizo mbele ya safari kwa Bi Clinton.

Siku za nyuma alikataa kuongelea kutoonekana akisaidiana na Trump kummaliza Clinton.
Mkuu Nguruvi3 habari zilizovuja zinadai kwamba ukimya wa Sanders kuhusu Emails za Clinton ulikuwa ni mpango maalum uliosukwa na wapambe wake ili kuficha kilichokuwa kinafanyika nyuma ya pazia. Wakati Sanders yuko kimya upelelezi wa kimya kimya ulikuwa ukifanyika kwa ushirikiano wa idara mbali mbali za kijasusi kuhusiana na hizo Emails.

Inadaiwa kwamba Sanders kaonekana kuridhishwa na ushahidi uliopatikana nyuma za hizo Emails na ndiyo maana kaamua kukomaa na Clinton. Kama mdahalo wake na Trump ungefanikiwa California angetumia nafasi hiyo kumshutumu Clinton kama mtu asiyeaminika na asiyefaa kuchaguliwa kuiongoza Marekani akijua ataungwa mkono na Trump.

Mkakati huo wa Sanders bado upo na sasa bado anataka mdahalo ufanyike jimboni California kati yake na Clinton kabla ya primary wiki ijayo ili hoja zake zisikilizwe na maamuzi anayoyaita sahihi yafanyike. Kama hili litashindikana Sanders bado ana nia ya kuushitaki uongozi wote wa Democrats na kuweka zuio hadi mabadiliko ya sheria anayoyataka yafanyike.

Kwa kweli Democrats wana mtihani mkubwa sana mbele yao na tamko lililotolewa na State Department inspector general dhidi ya Emails za Clinton limezidi kukoleza moto. Inavyoonekana Sanders pamoja na kukaa kimya, hii ripoti tayari watu wake walikuwa nayo mikononi na ilikuwa ni swala la muda tu akisubiri muda muafaka baada ya kuibuliwa na mtu mwingine.

Tatizo alilo nalo Sanders ni kwamba hawezi kumzuia Clinton kufikisha idadi ya wajumbe wanaotakiwa hata afanye nini hivyo njia pekee aliyo nayo ni hii tuhuma za Emails. Bahati yake ni kwamba watu wa Trump nao wanapanga kukomalia siyo tu hizo Emails za Clinton bali na kashfa zinazomhusu mume wake wakati akiwa madarakani.

Kwa maana nyingine ni kwamba Clinton mpaka sasa anao wapinzani (maadui) wawili, moja wa ndani na mwingine wa nje. Asichotilia maanani Sanders ni kwamba, kwa analofanya ama kwa makusudi au kwa kutojua, anamsaidia na kumpigia kampeni mgombea wa Republicans, Donald Trump...hiyo ndiyo homa waliyo nayo wana Democrats.
 
Mkuu Mag3 ka,a unakumbuka tulihoji sana kwanini Sanders anaendelea

Katika mambo tuliyojadili ni hili la emails baada ya uchaguzi wa NY, Penn, Conn, Delaware na Maryland.

Utakubuka chaguzi hizo Sanders alishindwa na Clinton, na katika mikutano yake mkewe alisema 'Hivi habari za emails na Benghaz mbona hazijadiliwi na serikali?

Tulimnukuu huko nyuma, na sasa ni wazi , mkewe alijua nini kinaendelea

Frustrations zinaongeza baada ya kuona kura za maoni California na New Jersey zinampa nafasi Clinton.

Si nafasi ya ushindi bali 50/50 na hivyo Sanders kupoteza matumaini kabisa

Kaomba mdahalo Claifornia, kwa bahati mbaya amesahau aligombana na viongozi wa DNC kuhusu mjadala wa Brooklyn.

Kule NY aliomba, mwisho akasema ukifanyika siku chache kabla ya uchaguzi unamuumiza. Kwa maana kuwa hana nafasi ya kusambaza 'sumu yake'

Sasa anaomba tena nafasi akijua alishawatibua DNC

Clinton amekataa kuwa na mdahalo tena. Naye anafahamu azma ya Sanders

Katika hali ya kushangaza, Sanders alitamani afanye mdahalo na Trump ili Trump azushe suala la email na Benghaz Sanders adakie. Trump amekataa

Kuna tatizo kubwa sana Democrat, na hasa namna ya kumu-handle Sanders na kundi lake. Naye ametambua hilo anawaendesha.

Wasipochukua hatua kwa kumuogopa, mtafaruku utakuwa mkubwa

Hoja ya Sanders ni kutafuta njia ya kwenda convention.

Kupitia wajumbe inashindika sasa anatafuta jingine.

Tusemezane
 
Nguruvi3 said:
Kuna tatizo kubwa sana Democrat, na hasa namna ya kumu-handle Sanders na kundi lake. Naye ametambua hilo anawaendesha.

Wasipochukua hatua kwa kumuogopa, mtafaruku utakuwa mkubwa
Tayari aliyewahi kuwa gavana wa Vermont anakotoka Sanders na mwenyekiti mstaafu wa DNC na mgombea Urais 2004, Howard Dean, amejitokeza na bila kumung'unya maneno kasema DNC haitabadilisha sheria zake kama anavyotaka Sanders. Amedai kuwa Sanders toka awali alizijua hizo sheria na kuzikubali na hivyo madai yake ya sasa hayana msingi na kuishauri na kuitaka DNC isiyakubali. Bila shaka wako na wengine watajitokeza kumpa support na katika hali hiyo yawezekana Sanders na watu wake wakatekeleza tishio lao la petition kuweka zuio kwa convention Philladelphia!
 
Hadi leo tarehe 31/5/2016 idadi ya wajumbe kwa kila mgombea kupitia tiketi ya Democrats ni kama ifuatavyo;

Wajumbe wa kuchaguliwa

  1. Hillary Clinton....1769
  2. Bernie Sanders...1501
Wajumbe maalum
  1. Hillary Clinton....543
  2. Bernie Sanders...44
Jumla ya wajumbe
  1. Hillary Clinton....2312 (pungufu kwa 71)
  2. Bernie Sanders...1545 (pungufu kwa 838)
 
Mkuu Mag3 naziangalia hizo namba na kubaki na swali moja, mategemeo ya Sanders yana kitu gani nyuma yake? Tumeona anasubiri emails ili ashawishi wajumbe SD wabadili mwelekeo. Hata hivyo hesabu bado zinakataa

Kuna wajumbe 800 waliobaki wa kuchaguliwa. Kwa maana ya mjadala tutengeneze nadharia kuwa Sanders akishinda kwa asilimia kubwa sana atapata wajumbe 500 na Clinton 300

Clinton ana 2312 wakijumlisha na ''300 wa nadharia'' atakuwa na 2612
Sanders atakuwa na 2045 'wakijumlishwa na hao 500 wa nadharia''

Tufikiri kuwa SD wapatao 200 watabadili mwelekeo na kumuunga mkono Sanders
Sanders atakuwa na wajumbe 2245 na Clinton atapunguza hadi 2412

Katika hali hii nini Sanders anachotumaini? Tunasema hivi kwasababu ongezeko la SD katika miezi miwili ni chini ya 5. Kwanini hadi sasa hawajabadili mwelekeo?

Zaidi, katika wiki mbili amekuwa anashambulia establishments ambao ndio wanaotengeneza SD sehemu kubwa na DNC!

Nadhani kuna analojua kuhusu emails na FBI na anasubiria hilo ikijulikani kuwa suala la emails linachagizwa naye na Republican kwa pamoja

Tusemezane
 
Mkuu Mag3 naziangalia hizo namba na kubaki na swali moja, mategemeo ya Sanders yana kitu gani nyuma yake? Tumeona anasubiri emails ili ashawishi wajumbe SD wabadili mwelekeo. Hata hivyo hesabu bado zinakataa

Kuna wajumbe 800 waliobaki wa kuchaguliwa. Kwa maana ya mjadala tutengeneze nadharia kuwa Sanders akishinda kwa asilimia kubwa sana atapata wajumbe 500 na Clinton 300

Clinton ana 2312 wakijumlisha na ''300 wa nadharia'' atakuwa na 2612
Sanders atakuwa na 2045 'wakijumlishwa na hao 500 wa nadharia''

Tufikiri kuwa SD wapatao 200 watabadili mwelekeo na kumuunga mkono Sanders
Sanders atakuwa na wajumbe 2245 na Clinton atapunguza hadi 2412

Katika hali hii nini Sanders anachotumaini? Tunasema hivi kwasababu ongezeko la SD katika miezi miwili ni chini ya 5. Kwanini hadi sasa hawajabadili mwelekeo?

Zaidi, katika wiki mbili amekuwa anashambulia establishments ambao ndio wanaotengeneza SD sehemu kubwa na DNC!

Nadhani kuna analojua kuhusu emails na FBI na anasubiria hilo ikijulikani kuwa suala la emails linachagizwa naye na Republican kwa pamoja

Tusemezane
Kama tulivyoona mwaka 2008, Clinton alijitoa akiwa na wajumbe 1640 idadi ambayo Sanders hajaifikia mpaka sasa. Wakati huo Obama alikuwa na wajumbe 1764 tofauti kati yao ikiwa ni wajumbe 104 tu. Lakini leo Clinton kafikisha wajumbe 2312 huku Sanders akiwa na wajumbe 1545 tofauti kati yao ikiwa ni wajumbe 767 lakini Sanders bado haoneshi kabisa nia ya kujitoa! Swali ni kitu gani anachokitafuta?

Hebu tuangalie hali halisi ilivyokuwa miezi miwili iliyopita na ilivyo leo kwa wajumbe maalum ambao Sanders anategemea kuwashawishi kubadilisha kura zao, je ukweli ni upi?

Mwezi wa April mwanzoni Clinton alikuwa na wajumbe maalum 469. Wakati huo Sanders alikuwa na wajumbe maalum 31 tu.

Toka wakati huo Clinton kaweza kuongeza idadi ya wajumbe maalum 74 na hivyo kufikisha 543 huku Sanders akiongeza wajumbe maalum 13 tu na kufikisha 44!

Je tunajifunza nini hapa? Ukweli ni kwamba pamoja na kudai anao uwezo wa kuwashawishi baadhi ya wajumbe maalum kubadilisha kura zao, matokeo mpaka sasa ni tofauti kabisa.

Kuna uwezekano mkubwa wa Clinton kufikisha idadi inayotakiwa hata kabla ya primary ya California na hasa baada ya caucus jimbo la New Jersey wiki hii! Lakini Bernie bado hakubali, hataki wajumbe maalum wahesabiwe na anataka ikibidi sheria za caucus na primaries zibadilishwe kwanza.

Kwa sasa pia amewataka wajumbe wawili Barney Frank na Dannel Malloy katika kamati za sheria na uongozi ndani ya DNC waondolewe lakini uongozi tayari umemkatalia. Barney Frank kwa upande wake kasema hajiuzulu na amemtaka Bernie Sanders awe mstaarabu, akubali kushindwa. Je ni kitu gani kitafuata?
 
WIKI HII
Tarehe 5 kuna uchaguzi Puerto Rico kwenye wajumbe 64

Tarehe 7 ni majimbo takribani 5, California na New Jersey yakiwa na wajumbe takribani 600.

Kura za maoni zinaonyesha , California Clinton anaongoza kwa point kati ya 5-6. Hili linaeleza jambo moja kuhusu Sanders

Kwamba, ikitokea akashinda, ushindi utakuwa katika asilimia 51-55 ambazo haziwezi kupunguza tofauti ya pengo lililopo. Ndivyo ilivyo New Jersey

Hili limelazimu kampeni ya Sanders kuja na hoja nyingine, kwamba katika utafiti Sanders anaongoza kwa vijana wa chini ya umri wa 30 katika asilimia 60 kwa 30

Hawa under 30 ni independents ambao hakuna anayejua kwa uhakika wanaunga mkono hoja za Sanders au wanatumika kisiasa kumdhoofisha Clinton

Tafiti hizo hazielezi kuwa katika kile kinachoitwa 'political base' ya democrat, Clinton anungwa mkono kwa asilimia kubwa

Hoja inayosumbua hapa ni kuwa ikiwa 'independents' wanamuunga mkono Sanders, iweje hadi sasa ana upungufu wa kura milioni 3 dhidi ya Clinton?

Lakini pia independents kama wanavyojulikana wana uhuru (siyo committed).
Je, kipi bora kwenda na loyal voters au kwenda na independents?

Drmocrat lazima wakubali kuwa Sanders si kuwa anawasumbua bali anawadoofisha katika kampeni.

Huu ulikuwa wakati wa maandalizi dhidi ya Trump, kinyume chake kinatokea.

Kwa upande wa Trump, msimamo wake huwa ni thabiti, tatizo lake bado hajaweza kucheza na siasa kwa werevu.

Kauli zake tata zinazidi kumkwaza katika kuungwa mkono na Republican.

Na mitifuano na wenzake haimsaidii hasa ikiwa haina ulazima
 
KUELEKEA JUNE 7
UCHAGUZI WA DEMOCRAT

Tarehe 7 kutukuwa na uchaguzi wa Democrat katika majimbo ya California, New Jersey, New Mexico, Montana, South and North Dakota

Kabla ya hapo, June 4 kutakuwa na uchaguzi Virginia Island.
Hakuna kura za maoni zilizofanyika, hata hivyo kutokana na mgawanyo wa watu, Virginia ina weusi waliompa ushindi Obama 2008.

Kwa mwelekeo huo, Clinton anayefanya vema kwa watu wa rangi anategemewa kushinda. Kuna wajumbe 7 pengine ndiyo maana uzito wake hauonekani.

Kwa mgawanyo wa uwiano wa Dem tofauti ya wajumbe kati yao inaweza kuwa 4:3 au 5:2

Tarehe 5 June , ni Puerto Rico. Kuna wajumbe 60 katika sanduku la kura.
Hakuna kura za maoni zilizopatikana.

Demography inaonyesha Walatino/Wahispania ni wengi. Clinton anatarajiwa kushinda kwa mtazamo kuwa alishinda Florida na NY kwenye watu wenye asili hiyo kwa margin nzuri.

Hivyo Puerto Rico na Virginia zinatoa takriban wajumbe 67. Hii ni kati ya 4 na 5 Juzi

Tarehe 7
Calfornia ina wajumbe 475
New Jersey ina wajumbe 126

Majimbo haya mawaili ndiyo yenye zawadi nono ya siku yakiwa na wajumbe jumla 601

New Mexico 34
Montana 27
North Dakota 18
South Dakota 20

Jumla 109 katika majimbo hayo 4 hapo juu

Hili linaeleza kwa nini wagombea hawakuhangaika kwenda maeneo hayo kwa kampeni kali.
Hata hivyo, ipo hali inayojitokeza katika mazingira ya shaka.

Clinton amefanya kampeni New Jersey na California. Sanders ametumia muda mwingi sana California. Kwanini?

Ukitazama ramani, maeneo ya Wayomin, Idaho, Utah, Minnesota yamepakana na majimbo ya Montana, South and North Dakota. Hivyo, Sanders ana uelekeo wa kushinda majimbo hayo

Ushindi wake kwa asilimia 70 hauwezi kupunguza pengo la wajumbe kwa kiasi cha maana

New Mexico inatumia uchaguzi ambao ni 'closed' Clinton ameshinda chaguzi hizo.
Pamoja na ukweli huo, NM inapakana na Utah na Colarado Sander anaweza kushinda pia.

Kwa mtazamo mwingine, New Jersey peke yake ina wajumbwe wengi (126)kuliko Montana, New Mexico, North and South Dakota. kwa pamoja.

Kwa kutumia hesabu ina maana kuwa Clinton akishinda New Jersey kwa 60% kama inavyotarajiwa, na Sanders akashinda New Mexico, Montana na Dakota kwa 60% , aliyeshinda New Jersey atapata wajumbe wengi.

Symbolically Sanders atashinda majimbo mengi, practically Clinton atapata wahmbe wengi
Ndiyo maana kampeni imezama sana California.

Zipo sababu kubwa mbili tutafafanua
 
TRIBUTE
MOHAMED ALI

Wanajamvi kabla ya kuendelea na mijadala, tuhcukue nafasi hii kuheshimu na kuthamini mchango wa Bondia maarufu duniani Cassius Marcellus Clay au Mohamed Ali.

Mohamed Ali ni bondia na mwanaharakati wa kisiasa.

Alizaliwa mwaka 1942 Louisville, Kentucky na atazikwa huko Ijumaa ijayo

Rekodi ya Mohamed Ali ina utata akiwa ni mtu aliyeleta hamasa kubwa duniani katika mchezo wa ndondi, lakini pia utata katika mambo mengi.

Alikataa kujiunga na jeshi la Marekani kwenda vitani na kuzuiliwa kucheza kwa miaka 3.5

Mohamed alikuwa mwanaharakati siasa za ubaguzi jambo lililopunguza umaarufu wake katika vyombo vya habari vya Marekani,pia kumuongezea umaarufu kwa wanaharakati.

Mohamed aliishi zama za akina Martin Luther King,J.Jackson na wanaharakati wa kiislam kama Farhan na Elija Muhamad aliyempa jina la Mohamed Ali

Mohamed alifika Afrika kama kule Kenya katika 'harakati ' zake za kisiasa akiwa bondia

Hata hivyo, ujio wake mkubwa ni ule wa pambano linalosemwa kuwa la karne ya 20, The rumble in the Jungle, kule Kinshasa dhidi ya bingwa G.Foreman

Pambano hilo liliteka dunia likiwa na ufadhili wa Don King akiwa mchanga na Mobutu alisaidia sana kulileta. Ni moja ya mapambano makubwa yaliyowahi kufanyika nje ya Marekani na linabaki katika historia ya dunia.

Pambano hilo lilifanyika oktoba 30, 1974 mjini Kinshasa huku Mohamed Ali akishangiliwa kwa maneno 'Ali Bumaye' kwa maana Ali Mtwangwe.

Pambano lilikuwa lifanyike Sept 25 likaahirishwa kutoka na Foreman kuumia mazoezini.

Kabla ya Oktoba 25, matamasha ya muziki yaliendelea mjini Kinshasa kwa siku kadhaa, yakifanywa na akina , James Brown(RIP) maarufu kwa wimbo wa Sex machine, Mariam Makeba (RIP), B.B King (RIP), Manu Dibango, the crusaders n.k.

Ali alishinda pambano hilo kwa KO.

Mohamed Ali ametunukiwa heshima kubwa za nchi ya Marekani na viongozi wakuu
Kifo chake kimegusa jamii ya wana ndondi, Sanaa n.k.

Mohamed alikuwa bondia aliyeleta msisimko sana katika ndondi.

Alikuwa hodari wa kuzungumza akipanga maneno kama mashairi.

Ndiye hasa aliyewavutia waliofuata baada yake na kuufanya mchezo wa ndondi kuwa na heshima kubwa sana duniani

Kwa wale walioshi zama hizo kama mkuu Mag3 , hili litamgusa sana. Sikumbuki msisimko mkubwa wa ndondi kuliko zama za Ali.

Leo dunia inaombeleza, hata majukwaa ya wanasiasa wa Marekani yamemzungumzia

Habari zake zimefunika shughuli nyingi za uchaguzi ambako Virginia Island Clinton ameibuka mshindi , huku majimbo yaliyobaki yakiendelea kuleta sintofahamu

Tutajadili yanayoendelea bandiko lijalo, hili lilikuwa la kuthamini mchango wa Mohamed Ali, 'the greatest of all time'

RIP Mohamed Ali
 
Mkuu Mag3 ka,a unakumbuka tulihoji sana kwanini Sanders anaendelea

Katika mambo tuliyojadili ni hili la emails baada ya uchaguzi wa NY, Penn, Conn, Delaware na Maryland.

Utakubuka chaguzi hizo Sanders alishindwa na Clinton, na katika mikutano yake mkewe alisema 'Hivi habari za emails na Benghaz mbona hazijadiliwi na serikali?

Tulimnukuu huko nyuma, na sasa ni wazi , mkewe alijua nini kinaendelea

Frustrations zinaongeza baada ya kuona kura za maoni California na New Jersey zinampa nafasi Clinton.

Si nafasi ya ushindi bali 50/50 na hivyo Sanders kupoteza matumaini kabisa

Kaomba mdahalo Claifornia, kwa bahati mbaya amesahau aligombana na viongozi wa DNC kuhusu mjadala wa Brooklyn.

Kule NY aliomba, mwisho akasema ukifanyika siku chache kabla ya uchaguzi unamuumiza. Kwa maana kuwa hana nafasi ya kusambaza 'sumu yake'

Sasa anaomba tena nafasi akijua alishawatibua DNC

Clinton amekataa kuwa na mdahalo tena. Naye anafahamu azma ya Sanders

Katika hali ya kushangaza, Sanders alitamani afanye mdahalo na Trump ili Trump azushe suala la email na Benghaz Sanders adakie. Trump amekataa

Kuna tatizo kubwa sana Democrat, na hasa namna ya kumu-handle Sanders na kundi lake. Naye ametambua hilo anawaendesha.

Wasipochukua hatua kwa kumuogopa, mtafaruku utakuwa mkubwa

Hoja ya Sanders ni kutafuta njia ya kwenda convention.

Kupitia wajumbe inashindika sasa anatafuta jingine.

Tusemezane
Mkuu Nguruvi3, Bernie Sanders hamna namna ya kuweza kuwa mgombea wa Democrats na natabiri, kwa namna mambo yanavyozidi kujitokeza, si muda mrefu itabidi asalimu amri.

Mpaka leo hii tarehe 5/6/2016 hii hapa chini ndiyo hesabu na kwa vyovyote vile Sanders kafikia mwisho wa safari na iliyobaki ni usanii tu...labda awe na jingine;

Wajumbe wa kuchaguliwa
  1. Hillary Clinton....1776
  2. Bernie Sanders...1501
Wajumbe maalum
  1. Hillary Clinton....547
  2. Bernie Sanders...46
Jumla ya wajumbe
  1. Hillary Clinton....2323 (pungufu kwa 60)
  2. Bernie Sanders...1547 (pungufu kwa 836)
Kuna uwezekano wa Clinton kufikia ile idadi ya wajumbe 2383 siku ya leo Jumapili na ikitokea hivyo Sanders atatakiwa asalimu amri hata kama hataki.
 
TRIBUTE
MOHAMED ALI

Kwa wale walioshi zama hizo kama mkuu Mag3 , hili litamgusa sana. Sikumbuki msisimko mkubwa wa ndondi kuliko zama za Ali.

Leo dunia inaombeleza, hata majukwaa ya wanasiasa wa Marekani yamemzungumzia

Tutajadili yanayoendelea bandiko lijalo, hili lilikuwa la kuthamini mchango wa Mohamed Ali, 'the greatest of all time'

RIP Mohamed Ali
Mkuu Nguruvi3, Tribute ya Mohamed Ali, Mungu ampumzishe pahala pema peponi, inahitaji uzi wa pekee. Tupo tuliofuatilia sana harakati zake katika ulimwengu wa ndondi toka mwanzoni wa miaka ya 1960s.

He was the fastest, the greatest, the best and the only one in the boxing world to ever capture the attention of sports lovers from all corners of the globe regardless of colour, gender or age...yeah, Mohamed Ali aka Casius Clay! RIP.
 
UCHAGUZI: DEMOCRAT
PUERTO RICO

MTIFUANO UNASHIKA KASI NDANI YA DEM

Baada ya Virginia Island na Puerto Rico,Clinton ameshinda

Virginia Island ilikuwa ni symbolic victory kwasababu wajumbe waliopo ni 7.
Kwa utaratibu wa Democrat wa uwiano mshindi atapata kati ya wajumbe 4 au 5.

Umuhimu wake ni pale ynapotajwa majimbo na idadi ya ushindi

Puerto Rico ina wajumbe 60, kiasi hicho kina maana mbili, symbolic na idadi ya wajumbe. Uwiano utatoa tofauti ya wajumbe. Wajumbe wa Puerto Rico ni nusu ya wajumbe wa New Jersey, na wengi kuliko wajumbe wa Montana, North and South Dakota combined (55)

Hesabu zinaonyesha, Clinton ameshinda Puerto Rico, akipoteza Montana, North and south Dakota, hatapunguza tofauti ya kura na Bernie Sanders.

Kwa maneno mengine, jumanne atakuwa anaangalia New Jersey na California.

Matumani ya kushinda NJ kwa mujibu wa kura za maoni ni makubwa
California Bernie na Clinton wapo neck in neck,probability ipo kwa pande zote

Hata hivyo, California ina umuhimu kwa pande zote

Clinton: Ushindi utazuia kauli za Sanders kuhusu ushindi katika jimbo kubwa.
Ushindi utasiadia Dem kuweka shinikizo zito kwa Sanders kujitoa

Sanders: Anachotaka California kilikuwa ushindi wa asilimia 67 ili ajenge hoja ya contested convention. Kwa hali ilivyo, ushindi kati yao utakuwa kati ya 51 hadi 55.

Sanders amebaini hilo na sasa anakuja na kauli nyingine

Sanders anasema,Trump na Clinton wana negative public image kubwa, na kwaba yeye anawashinda wote katika kura za maoni kitaifa

Kama mtakumbuka tulisema,''vyombo vya habari na taasisi'' vilianza kumjengea mazingira hayo Sanders ili kumpa kauli kwa kura za maoni kati ya Trump na Clinton/Sanders.

Vyombo hivyo vilionyesha Clinton akipoteza umaarufu kila siku na sasa vimefikia mahali pa kusema Trump atamshinda Clinton.

Hizo ni hesabu ili kumjenga Sanders. Kuna 'interest' kati ya taasisi zinazofanya tafiti, vyombo vya habari na Sanders. Interest gani hiyo? Tutafafanua Jumatano ijayo siri hiyo

Kura za maoni kitaifa haziwezi kueleza chochote tukijua Dem hawana mgombea

Mtifuano mpya waanze tena, Democrat waanza kuondoa uvivu kwa Sanders

Inaendelea...
 
SANDERS NA MASHAMBULIZI MAPYA

Jumapili akiwa katika TV ya CNN Sanders amemshambulia Clinton na Clinton foundation.
Anasema foundation imepokea pesa za nje,litaleta conflict of interest kwa Clinton WH

Madai haya yameanzishwa na Republican na Sanders anazidi kuyasimamia kidete

Hii ni baada ya kuendelea kumshambulia Clinton akiwa California kwa takribani wiki tatu
Kwa upande mwingine Trump naye akipiga kutokea kona nyingine

Sanders amevitaka vyombo vya habari kutomtangaza Clinton kama mtarajiwa
Amesisitiza uchaguzi utamalizika katika contested convention-Philadephia

Wengi wanatarajia baada ya matokeo ya New Jersey, habari itakuwa Clinton
Sanders amewahi kuvitahadharisha vyombo hivyo kwa makusudi kabisa.

Tuangalie nadharia ya Sanders halafu tufikirie nini atasema California masaa Jumanne

Njia za kwenda mkutano mkuu

1. Idadi ya wajumbe wa kuchaguliwa, Clinton 1776(kabla ya Puerto Rico) Sanders 1501.

2. Kura za wananchi(popular vote) Clinton ana 3 milioni Zaidi ya Sanders

3. Idadi ya majimbo waliyoshinda, Clinton anayo mengi Zaidi ya Sanders.

4. Maeneo waliyoshinda, Clinton ameshinda mashariki-magharibi, kaskazini na kusini.
Sanders ameshinda magharibi, mashariki. Kusini hakushinda. Hoja inakosa mashiko

5. Idadi ya Super delegates, Clinton ana 500 , Sanders 43.
Kinadharia, ili Clinton anahitaji SD takribani SD 500, Sanders atahitaji 700.

Hii maana yake ni kuwa SD wa Clinton wakihamia kwa Sander bado hataifikisha 238.
Waliobaki takribani 200 wakielekea kwa Sanders, ndipo anaweza kufikia namba

Je, kwa hali ilivyo, kuna uwezekano wowote wa Clinton kuwa na SD chini ya 300?

Kwa mtazamo huo, hakuna hesabu zinazompa Sanders nafasi hata kwa asilimia 10.

Je ni kwanini anataka kwenda convention?

Ushindi wa aina yoyote California kwa Sanders utampa kauli ya kwenda convention.

Si kwasababu atashinda, utamsaidia ku prolong process wakati anasubiri matokeo ya FBI
Anachotaka ni kutumia matokeo ya ''FBI''kuwashawishi SD wahamie upande wake.

Mategemeo kuwa atatangaza kuachia ngazi Jumanne hayapo.
The writings on the wall yanamwambia, lakini kuna anachovizia

Amewekeza nguvu nyingi sana California. Kwanza alitumaini angeshinda kwa asilimia Uwezekano huo unaonekana kuwa mgumu, sasa anahitaji 50.01% aseme ameshinda

Lengo ni kutafuta sababu za kusogeza mbele uchaguzi akisubiri matokeo ya FBI

Inaonekana Dem wamechoka, na leo mmoja wa viongozi wa zamani wa DNC Dona Brazili ameweka wazi, utaratibu hauwezi kupinduliwa dhidi ya matakwa ya wapiga kura

Pundits na surrogates wanaonekana kuvunja ukimya na kumwambia Sanders sasa ni wakati. Wanamlaumu kuungana na Republican kwa madai ya Clinton foundation

Clinton atafikisha 2383 Jumanne saa 2 usiku kabla ya matokeo ya California.

Matokeo ya California hayawezi kubadili azma ya Sanders kwa namna yoyote

Hatafunga kampeni na atakuja na madai mapya ku prolong uchaguzi hadi July

Hatari ya vurugu kule Philadephia ipo wazi kabisa

Tusemezane
 
SANDERS NA MASHAMBULIZI MAPYA

Jumapili akiwa katika TV ya CNN Sanders amemshambulia Clinton na Clinton foundation.
Anasema foundation imepokea pesa za nje,litaleta conflict of interest kwa Clinton WH

Madai haya yameanzishwa na Republican na Sanders anazidi kuyasimamia kidete

Hii ni baada ya kuendelea kumshambulia Clinton akiwa California kwa takribani wiki tatu
Kwa upande mwingine Trump naye akipiga kutokea kona nyingine

Sanders amevitaka vyombo vya habari kutomtangaza Clinton kama mtarajiwa
Amesisitiza uchaguzi utamalizika katika contested convention-Philadephia

Wengi wanatarajia baada ya matokeo ya New Jersey, habari itakuwa Clinton
Sanders amewahi kuvitahadharisha vyombo hivyo kwa makusudi kabisa.

Tuangalie nadharia ya Sanders halafu tufikirie nini atasema California masaa Jumanne

Njia za kwenda mkutano mkuu

1. Idadi ya wajumbe wa kuchaguliwa, Clinton 1776(kabla ya Puerto Rico) Sanders 1501.

2. Kura za wananchi(popular vote) Clinton ana 3 milioni Zaidi ya Sanders

3. Idadi ya majimbo waliyoshinda, Clinton anayo mengi Zaidi ya Sanders.

4. Maeneo waliyoshinda, Clinton ameshinda mashariki-magharibi, kaskazini na kusini.
Sanders ameshinda magharibi, mashariki. Kusini hakushinda. Hoja inakosa mashiko

5. Idadi ya Super delegates, Clinton ana 500 , Sanders 43.
Kinadharia, ili Clinton anahitaji SD takribani SD 500, Sanders atahitaji 700.

Hii maana yake ni kuwa SD wa Clinton wakihamia kwa Sander bado hataifikisha 238.
Waliobaki takribani 200 wakielekea kwa Sanders, ndipo anaweza kufikia namba

Je, kwa hali ilivyo, kuna uwezekano wowote wa Clinton kuwa na SD chini ya 300?

Kwa mtazamo huo, hakuna hesabu zinazompa Sanders nafasi hata kwa asilimia 10.

Je ni kwanini anataka kwenda convention?

Ushindi wa aina yoyote California kwa Sanders utampa kauli ya kwenda convention.

Si kwasababu atashinda, utamsaidia ku prolong process wakati anasubiri matokeo ya FBI
Anachotaka ni kutumia matokeo ya ''FBI''kuwashawishi SD wahamie upande wake.

Mategemeo kuwa atatangaza kuachia ngazi Jumanne hayapo.
The writings on the wall yanamwambia, lakini kuna anachovizia

Amewekeza nguvu nyingi sana California. Kwanza alitumaini angeshinda kwa asilimia Uwezekano huo unaonekana kuwa mgumu, sasa anahitaji 50.01% aseme ameshinda

Lengo ni kutafuta sababu za kusogeza mbele uchaguzi akisubiri matokeo ya FBI

Inaonekana Dem wamechoka, na leo mmoja wa viongozi wa zamani wa DNC Dona Brazili ameweka wazi, utaratibu hauwezi kupinduliwa dhidi ya matakwa ya wapiga kura

Pundits na surrogates wanaonekana kuvunja ukimya na kumwambia Sanders sasa ni wakati. Wanamlaumu kuungana na Republican kwa madai ya Clinton foundation

Clinton atafikisha 2383 Jumanne saa 2 usiku kabla ya matokeo ya California.

Matokeo ya California hayawezi kubadili azma ya Sanders kwa namna yoyote

Hatafunga kampeni na atakuja na madai mapya ku prolong uchaguzi hadi July

Hatari ya vurugu kule Philadephia ipo wazi kabisa

Tusemezane
Baada ya Puerto Rico usiku wa leo, hii ndiyo update ya wajumbe wa kila mgombea kwa Democrats;

Wajumbe wa kuchaguliwa
  1. Hillary Clinton....1809
  2. Bernie Sanders...1520
Wajumbe maalum
  1. Hillary Clinton....548
  2. Bernie Sanders...46
Jumla ya wajumbe - idadi inayotakiwa 2383
  1. Hillary Clinton....2357 (pungufu kwa 25)
  2. Bernie Sanders...1566 (pungufu kwa 817)
Na hapa California na New Jersey bado. Kwa kweli haijulikani Bernie Sanders anataka nini! Clinton sasa anahitaji wajumbe 25 tu afikie ile namba wakati Sanders anahitaji 817!
 
Back
Top Bottom