Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,096
- 4,948
Chama cha siasa katika siasa za vyama vingi ujipima kukubalika kwake kwa kuruhusu wananchi kupiga kura
Kwa hali ilivyo sana nchni ni wazi hakuna tena utaratibu wa kupata viongozi kupitia uchaguzi bali viongozi wa kisiasa wanateuliwa na tume ya uchaguzi au wasimamizi wa uchaguzi
Ni vigumu kusema huu ni msimamo wa chama cha mapinduzi au la, kwani hata wanachama wa chama hicho nao wanaandamana kukatwa majina kwenye chaguzi za ndani.
Wana CCM kwa siku za hivi karibuni wameogopa kabisa hata kuvaa nguo za chama wala kupeperusha bendera za chama maeneo mbalimbali. Wana CCM wamekuwa wanyonge kuchangia mada kwenye majukwaa mbalimbali kwa sababu kila wakisimama wanaonekana watu wasio na akili na maarifa bali wanategemea kusaidia kila jambo.
Kwa kifupi Tanzania wakati majirani zetu wakiimarisha mifumo ya uchaguzi na kujenga trust Duniani sisi tunabomoa mifumo ya uchaguzi na kuiga mbinu na mikakati ya mataifa yanayoongoza kwa mkono wa chuma.
Tumeona mfumo wa uchaguzi Kenya, S. Africa, Botswana, Ghana nk hakuna taarifa za wagombea wa kisiasa kukatwa majina. Mfumo wa ukataji majina upo kwenye nchi ambazo usiku na mchana kuna uvunjifu wa amani.
Najiuliza, kama wana CCM wanatamani na wao wawe huru kwenye nchi yao kufanya siasa lakini mfumo unakataa! Nani yupo nyuma ya uchafuzi huu.?
Kwa hali ilivyo sana nchni ni wazi hakuna tena utaratibu wa kupata viongozi kupitia uchaguzi bali viongozi wa kisiasa wanateuliwa na tume ya uchaguzi au wasimamizi wa uchaguzi
Ni vigumu kusema huu ni msimamo wa chama cha mapinduzi au la, kwani hata wanachama wa chama hicho nao wanaandamana kukatwa majina kwenye chaguzi za ndani.
Wana CCM kwa siku za hivi karibuni wameogopa kabisa hata kuvaa nguo za chama wala kupeperusha bendera za chama maeneo mbalimbali. Wana CCM wamekuwa wanyonge kuchangia mada kwenye majukwaa mbalimbali kwa sababu kila wakisimama wanaonekana watu wasio na akili na maarifa bali wanategemea kusaidia kila jambo.
Kwa kifupi Tanzania wakati majirani zetu wakiimarisha mifumo ya uchaguzi na kujenga trust Duniani sisi tunabomoa mifumo ya uchaguzi na kuiga mbinu na mikakati ya mataifa yanayoongoza kwa mkono wa chuma.
Tumeona mfumo wa uchaguzi Kenya, S. Africa, Botswana, Ghana nk hakuna taarifa za wagombea wa kisiasa kukatwa majina. Mfumo wa ukataji majina upo kwenye nchi ambazo usiku na mchana kuna uvunjifu wa amani.
Najiuliza, kama wana CCM wanatamani na wao wawe huru kwenye nchi yao kufanya siasa lakini mfumo unakataa! Nani yupo nyuma ya uchafuzi huu.?