Uchaguzi Mwenyekiti CHADEMA ni aibu na Demokrasia kwa wakati mmoja

Uchaguzi Mwenyekiti CHADEMA ni aibu na Demokrasia kwa wakati mmoja

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20250122_103017_Google.jpg


Hii ni fundisho kwa viongozi wote kwamba Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu,na sauti ya umma si yenye kudharauliwa hata kidogo,ni wakati umefika sasa kwa viongozi wengine kujifunza haya yalitokea Chadema

Jana nilikuwa nafuatilia matangazo ya Television ya uchaguzi wa Chadema,nilivutiwa na mchambuzi wa maswala ya siasa bwana Buberwa,alisema hivi nanukuu " Ukiona kiongozi umekaa miongo mitatu madarakani mpaka vizazi vipya vimekukuta na wewe upo tu basi ni wakati wa kukaa pembeni"

Na wataalamu hao wa mambo ya siasa walisema hata Mwalimu na baba wa taifa Julias Nyerere watu walimchoka pamoja na kuanza kumuita mchonga meno na mambo kama hayo,hii inaonyesha kwamba inafika kipindi kama kiongozi inabidi ujitathimini na kufanya maamuzi sahihi

Mheshimiwa Mbowe bahati mbaya sana hakuliona hilo na kibaya zaidi alidharau sauti ya umma na mwisho wa siku tumeyaona yaliyo tokea,amejifunza in a hard way,badala ya kustaafu kwa heshima baada ya kukijenga chama kwa mda mrefu matokeo yake amestaafu kama loser

Tunaelekea katika Uchaguzi mwaka huu na hapana shaka mama yetu kipenzi Samia Suluhu Hassan atapeperusha bendera ya Tanzania tena kama raisi wetu,kuna maneno maneno mengi yanasemwa kwamba huenda mama yetu kipenzi akagombea tena mwaka 2030

Basi ni busara sana kwa washauri wake walione hili mapema ili mama yetu amalize ngwe yake kwa heshima na kumkabidhi mtu mwingine kijiti ili asipate kuchafua heshima aliyojiwekea,naamini chama chetu cha ccm kina azina kubwa ya wanasiasa wenye busara na maono makubwa

Nimalizie kwa kusema kwamba kwa upande wa Chadema imetuonyesha demokrasia kwa upande mwingine wa shilingi kwa uchaguzi kufanyika kwa haki,na wajumbe kwa nyakati tofauti walijipambanua wazi wazi kwamba wanamuunga mkono mgombea fulani,hakika wameonyesha uthubutu na ukomavu wa kisiasa,kongole kwao

Mungu ibariki Afrika na Mungu ibariki Tanzania

Ni hayo tu!
 
Kilaa lenye mwanzo halikosi mwisho ,na mwisho Huwa mnzuri au mmbaya kulingana umefikaje mwisho wako ...
Mapunziki mema kwake mbowe juhudi zake zakujenga chama hazitasahaulikaa kamwee...
 
Wewe kumbe nawe veggies 😹
Haya utueleze kwann mnapitishana bila kupingwa?
My dear,nitumie maneno ya mkongwe na katibu mstaafu wa ccm Mzee Makamba alisema "hizi kanuni na katiba tulizitunga sisi na tunaweza kuzibadilisha" mwisho wa kunukuu

Ni hayo tu Lamomy
 
Kilaa lenye mwanzo halikosi mwisho ,na mwisho Huwa mnzuri au mmbaya kulingana umefikaje mwisho wako ...
Mapunziki mema kwake mbowe juhudi zake zakujenga chama hazitasahaulikaa kamwee...
Katiba ya nchi inamzuia mama kugombea uchaguzi wa 2030. So relax. 2030 tutakuwa na maingizo mapya✍️
 
Huyu naye chawa aliyechangamka ila hataki kujionyesha 😹😹
Eti mama atakuwa rais tena, kura tushapiga kwani??
Uchawa una level zake my dear,nipo level ya juu kabisa,huku chini vijana wetu wanatuwakilisha
 
My dear,nitumie maneno ya mkongwe na katibu mstaafu wa ccm Mzee Makamba alisema "hizi kanuni na katiba tulizitunga sisi na tunaweza kuzibadilisha" mwisho wa kunukuu

Ni hayo tu Lamomy
Alitunga yeye na nani?? Mbona kashindwa kutumia sheria hiyo hiyo kumfanya mwanae achukue fomu? 😹😹
 
Alitunga yeye na nani?? Mbona kashindwa kutumia sheria hiyo hiyo kumfanya mwanae achukue fomu? 😹😹
Alishindwa kwasababu ccm tuna utaratibu wetu wa kupeana miaka kumi,kwahiyo hatukutaka mambo yawe mengi
 
Siona haja ya kulaumu au kusema Mbowe hakusoma alama za nyakati. Uwepo wake kama mgombea umefanya CDM izungumzwe sana na watu wote bila kujali chama wala dini. Na uchaguzi huu pia umeonyesha ku a demokrasia ndani ya CDM
 
Siona haja ya kulaumu au kusema Mbowe hakusoma alama za nyakati. Uwepo wake kama mgombea umefanya CDM izungumzwe sana na watu wote bila kujali chama wala dini. Na uchaguzi huu pia umeonyesha ku a demokrasia ndani ya CDM
Kuzungumzwa ni jambo lingine na kuwa loser ni jambo lingine,lakini mwisho wa siku historia haitaandikwa kuwa watu walikizungumzia sana chadema,ila itaandikwa kwa wino wa dhahabu kwamba aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema kwa miaka 20 ya uongozi wake alishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025

Ukubali ukatae habar ndio hiyo,ila binafsi kwa roho safi kabisa nawapongeza wanachadema kwa demokrasia mlio tuonyesha hasa kwa wajumbe kuwa na udhubutu wa kutoa maoni yao hadharani,hakika nimeipenda hii
 
Kuna tatizo historia ikiandikwa hivyo? Si ndio demokrasia yenyewe wanayojivunia Wanachadema?
Kuna tatizo kubwa sana,hapa Freeman Mbowe ameonekana na ndio ukweli alikuwa bado ana ng'ang'ania madaraka,hayo sio maoni yangu tu bali ni mitazamo maono ya watu wengi ,wakimewemo watu wake wa karibu

Siku zote na kwa nafasi ya FAM ambaye amekuwa mwanachama wa Chadema kwa mda mrefuna mwenyekiti kwa takribani miaka 20,kuacha nafasi yake kwenye ballot box ni aibu sana tena sana,hapo inamaana Alikitaka chama lakini chama hakikumtaka,ukiangalia katika big picha utaona hili ila ukiangalia kwa mtazamo wa mapenzi kwa FAM hutaweza kuliona hili

Unapata heshima na hadhi pale unapoacha madaraka kwa utashi wako na si kwakuondolewa katika box la kupigia kura

Ndio maana hata viongozi ambao huwa wanajiudhuru wenyewe baada ya kuboronga historia huwa heshimisha na kuwapa second chance,mfano Marehemu raisi mstaafu All Hassan Mwinyi Allah amrehemu,alijiuzuru alipokuwa waziri wa mambo ya ndani baada ya mauaji kutokea,lakini hustoria ili muheshimisha kwa kuwa Raisi wa Jamhuri ya Tanzania
 
Kuna tatizo kubwa sana,hapa Freeman Mbowe ameonekana na ndio ukweli alikuwa bado ana ng'ang'ania madaraka,hayo sio maoni yangu tu bali ni mitazamo maono ya watu wengi ,wakimewemo watu wake wa karibu

Siku zote na kwa nafasi ya FAM ambaye amekuwa mwanachama wa Chadema kwa mda mrefuna mwenyekiti kwa takribani miaka 20,kuacha nafasi yake kwenye ballot box ni aibu sana tena sana,hapo inamaana Alikitaka chama lakini chama hakikumtaka,ukiangalia katika big picha utaona hili ila ukiangalia kwa mtazamo wa mapenzi kwa FAM hutaweza kuliona hili

Unapata heshima na hadhi pale unapoacha madaraka kwa utashi wako na si kwakuondolewa katika box la kupigia kura

Ndio maana hata viongozi ambao huwa wanajiudhuru wenyewe baada ya kuboronga historia huwa heshimisha na kuwapa second chance,mfano Marehemu raisi mstaafu All Hassan Mwinyi Allah amrehemu,alijiuzuru alipokuwa waziri wa mambo ya ndani baada ya mauaji kutokea,lakini hustoria ili muheshimisha kwa kuwa Raisi wa Jamhuri ya Tanzania
FAM alikua anang'ang'ania lakini ameruhusu demokrasia ichukue mkondo wake. Uchaguzi huru na wa haki, kashindwa na kakubali matokeo, kakaa pembeni. Hutaki apongezwe kwa hilo?!
 
Back
Top Bottom