Elections 2010 Uchakachuaji HAUPO! - NYARAKA HIZI HAPA NI FAKE

Elections 2010 Uchakachuaji HAUPO! - NYARAKA HIZI HAPA NI FAKE

Status
Not open for further replies.
Na mengi yaliyo katika barua hiyo wameshayatekeleza mbona hawa CCM wamejiandaa kuingiza nchi kwenye Vita kweli wako radhi tuchinjane ili kupindisha haki ya mwananchi ya kupiga kura,Najuta sana kumfahamu Wilson Kabwe nilifanya nae kazi huko Mbeya na Mwanza,Jamaa mchawi sana ,kwani hawezi kukataa maamuzi ya hao manyanq'au uzuri hii barua ni scanned tunaomba viongozi wa Chadema au CUF wangeitisha press conference haraka iwezekanavyo au hata Mzee Baregu aombe nafasi kwenye radio au TV asemee haya wanachi wajue,litawachwea hawaibi kura mwaka huu,majina hewa kwenye mtandao yameonekana ,vituo hewa vimeonekana wanazidi kuumbuka kabisa

Kama nilivyosema jana, tuzidi kumwomba MUNGU mipango yote mibovu ya CCM izidi kuumbuliwa. Watu wako wanaomba usiku na mchana na MUNGU anajibu maombi ya watu wake wanaomlilia kwa haki. Ni wakati muafaka sasa CCM wakaacha haki itendeke. Wawaache wananchi wachague vuongozi wanaowataka.
 
Mambo ya Kabwe haya hapa:

Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza azomewa mbele ya Raisi 07/06/2010
0 Comment(s)

Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Mwanza, Wilson Kabwe, amezomewa na wananchi mbele ya Raisi Kikwete.

Kabwe alikumbwa na mkasa huo baada ya Rais kumwita jukwaani na kumtaka atoe maelezo ya kina kuhusu kuwekewa alama za X kwenye baadhi ya nyumba za wananchi wa kata ya Mkolani jijini Mwanza.

Rais Kikwete ambaye yuko ziarani mkoani Mwanza, alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkolani ambapo pia alipata nafasi ya kuzungumza na wananchi huku akiwataka waeleze kero zao.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mkolani A, Mathias Kihamba, alipewa nafasi na Raisi Kikwete kueleza matatizo yanayowakabili ambapo mwenyekiti huo alisema kuwa wanaishi kwa wasiwasi katika nyumba zao kwa kuwa zimewekwa alama ya X pasina sababu za msingi. Kinyume na matarajio ya wengi, mkurugenzi huyo alishindwa kueleza sababu ya kuwekwa alama hizo za X zaidi ya kusema kuwa inawezekana kwa sababu watu wamejenga kiholela au ndani ya hifadhi ya barabara.

Rais Kikwete kusikia zomeazomea ikizidi kushika kasi, aliamua kumuokoa Mkurugenzi huyo kwa kumtaka kulifanyia kazi haraka jambo hilo ili kupunguza malamiko ya wananchi.

Raisi yupo mkoani Mwanza kwa ziara ya siku mbili ambapo alikagua ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Usagara hadi Geita na kusema hakuna barabara itakayosimama kujengwa kwa sababu ya kukosa fedha. Leo Jumapili ametembelea makumbusho ya kabila la Wasukuma na baadaye kufungua sherehe za Bulabo.

credit: Albert G Sengo/gsengo


from: Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza azomewa mbele ya Raisi -
 
With due respect. Invisible nakuaminia na nimekuwa napenda post zako. Kwa hili nasita kuamini. Kwanza kwa wale wenye kumbukumbu tarehe 16.10.2010 Kikwete alikuwa Mkoa wa Pwani ziara aliyoanza tarehe 15.10.10. Tarehe 17.10.10 alikuwa Mkoa wa Dar. Yaani hata hao walioandika barua ya magizo je hawakujua ratiba hiyo? Barua inaonesha mwandishi hajui kanuni za kuandika barua. Kwanza haina Kumbukumbu. Barua kama hizi lazima zipigwe muhuri wa "SIRI" au "Confidentail". Kichwa cha barua yenyewe kinatia mashaka. Na mwandishi anaonekana kukosa weledi wa kuandika barua za Kiserikali. Kwa mimi naona barua hiyo si barua ya kweli. Ebu rejea source ya barua hiyo na ujiridhishe kama ni credible.

wewe ni mpumbavu nani amekwambia hii barua ya kiselikari

kama hutaki ondoka hapa
 
Kumbe Pweza Mtu alikuwa sahihi, hii ni irregularity tosha ya kuahirisha uchaguzi mpaka hapo daftari la wapiga kura na wahusika wa uchafu na udhalimu huu washughulikiwe na vyombo vya dola. Uchungu unakuja pale vyombo vyenyewe vya dola ni mawakala wa mafisadi hawa
 
Wacha propaganda zako kabisa wewe mtu. mgombea anazungukwa na waandishi mpaka kwenye kitanda???? umeambiwa hii ishu ilifanyika usiku. uwe makini unapokuja na hoja za kijinga hapa
Tunajua yanayojiri na kinachotendeka kizani tunakijua.
Mgombea gani aliyewahi kuongozana na mwandishi kwa waganga wa kienyeji??? sasa kuhusu hii barua haina tofauti na uchawi dhidi ya taifa.
MBONA hamna huruma na watanzania ninyi watu?????

Wanachadema mna hasira kweli!!!!!!!!!! Sasa hapo una maana gani kutumia Phrase "hoja za kijinga". Nafikiri utabigwa butwaa sana tarehe 31. Kapige kura then subiri uone kama wewe tu ndiyo hauna hoja za kijinga!
 
Naomba leo JK akanushe hii taarifa wakati anazungumza na vyombo vya habari, kwa wale wenye signature za Kabwe tunaomba watuwekee hapa ili tuweze kulinganisha kama ni kweli au ni uchakachuaji. otherwise uchaguzi inabidi uairishwe.

Nyaraka hiyo ilikuwa ikitoa maelekezo ya Mpango huu ufanyike soma hapa chini na linganisha sasa:

Ili JK aweze kushinda kwa 80% kikao hicho kiliandaa njia hii!

CCM tayari wameshajihakikishia ushindi kwa vile tayari wameshakamilisha kazi yao. Katika uchaguzi wamekuwa wakitimiza ratiba tu lakini matokeo ya uchaguzi yanatambulika na mpango kamili wa kukamilisha matokeo hayo ni huu.

A). Upangaji wa vituo
NEC imekuwa ikiendesha zoezi la upangaji wa vituo chini ya uangalizi maalum wa watalaam wa IT (kama ambavyo imekwsiha kuelezwa na baadhi ya wadau hapa JF, ambao ni wa 16 na MBWA MKALI katika Post zilizopita).

i).Utaratibu wa awali ulikuwa ni kuandaa vituo halali ambavyo viliandaliwa na kukamilika.
ii). Utaratibu wa pili ulikuwa ni kuandaa vituo hewa ambavyo viliandaliwa baada ya vituo vya kwanza kukamilika (Hii ni kwa lengo la kutambua vituo awali na kutofautisha vile vya kuchahachulia).

Vituo Hewa:
Jambo hili limekuwa likiwatatiza wengi sana na wengine kushindwa kuamini iwapo jambo hili linawezekana. Ukweli linawezekana na hapa natoa mmoja ya kituo hewa.
· Hapa kwa mujibu wa tume vituo vimepangiliwa kwa majina/namba.
· Kituo ambacho nawatolea mfano hai ni Na. 00020941. Ama kwa jina kinaitwa Kituo cha Shule ya Msingi Kapangaja. Kipo katika Kata ya Bugongwa wilaya ya Ilemela na jimbo la Ilemela.
-Eneo hili la shule ya msingi limegawanywa na kuzaa jumla ya vituo 5.
-Tatizo lipo katika vituo viwili ambavyo ni kituo namba 4 na namba 5.
· Kituo Na. 4: Orodha ya majina ya wapiga kura imebandikwa ikiwa na kurasa 21. Kurasa hii inajumla ya wapiga kura 490. Kwa mujibu wa rekodi za Computer kituo hiki (kwa maana ya orodha yake) kilichapishwa Septemba 16, 2010.
-Ukiangalia kwa makini utakuna majina yake ambayo yamebainishwa kuwa ndiyo ya wapiga kura katika kituo hicho yanajirudia katika kituo namba 5.
-Tofauti iliyopo ni kuwa katika orodha hiyo ya namba 5 majina huku yamepunguzwa toka 490 na kuwa 402 hivyo kuwa na kurasa za majina 17 toffauti na 21 za kituo namba 4.
-Lakini orodha ya majina ya wapiga kura hiyo inaonyesha kuwa imechapishwa katika Computer Oktoba 16, 2010. (Maana yake ni kuwa hiki kimezalishwa baada ya kuwa vituo vyote vine vimekamilika hiyo Septemba 16, 2010). Hivyo ni kipya.

B). Upigaji Kura.
Kwa vile zoezi la upangaji kura limekamilika, kazi imebaki katika kupiga. Ukweli tukubali kura kwa sasa haziibiwi kwa kupiga, ingawa njia hii pia imeandaliwa kama njia ya dharula, lakini ni kwamba kura zitapigwa hivi.
· Kwa vile orodha ya majina iliyoonekana katika kituo namba 4, ndiyo yaliyojirudia kituo namba 5, basi watu hao (ambao ni wana CCM damu ama Polisi au JWT kama watakavyokuwa wameandaliwa) watajihimu kupiga kura na kukamilisha taratibu zote kituo namba 4.
· Kwa vile kila unapopiga kura kidole huwekwa wino maalum kama alama ya kumtambua aliyekwisha piga, basi wakitoka hapo watakwenda kufuta wino huo na kasha kubadili nguo zao na muda wa kurudi kituoni tena kwa ajili ya kupiga kura nyingine. Kura hii itakuwa kura ya pili kwa mtu mmoja kwa idadi ya watu 402 kituo namba 5 kati ya watu 490 wa idadi ya kituo namba 4.
· Watu hao watakuwa wakitumia shahada zao zile zile na kwa kuwa majina yao yamo katika daftari la kudumu la wapiga kura, na wino katika vidole vyao umefutwa kitaalam, basi watapiga kura bila ya wakala kulipwa hela kumshinikiza akubali au kumzuia kwa vile anachoangalia yeye ni shahada na kama imo katika daftari vitu ambavyo ni kweli vipo.
· Kwa vile wakali aliyewaona wakipiga kura katika kituo namba 4 hatotoka kuingia katika kituo namba 5, basi mamluki hao hawatabainika na hivyo watakuwa wamepiga bao la kisigino.
C). Kujumuisha matokeo.
Uchaguzi ukiisha kazi ya kujumuisha matokeo itakuwa imekwisha kwani wakifanikiwa hapo hawatakuwa na haja ya kuongeza kura nyingine juu yake kwani jambo hili litaleta utata na kuwafanya wabainike kama ambavyo ilitokea Kenya kwa kula kuzidi kutokana na ujumuishaji wake.
Hivyo Kikwete atashinda kwa 80% na CCM wataingia mtaani kushangilia wakati Chadema wakilia na kusaga meno na hapo uchaguzi utakuwa umeisha.

NJIA NYINGINE ZA WIZI ZINAZOTANGAZWA:
Kwa hakika mpaka sasa njia zote hizo zinatangazwa sitaki kuzipuuza kwa vile zote zinaweza kutumika lakini nyingi ambazo zimejulikana sasa zimetangazwa kwa makusudi kwa ajili ya kuwazubaisha wakazanie kuangalia huko huku wakitoa akili zao katika katika njii hii ambayo ilikomboa Jimbo la Busanda na Biharamulo.
 
Tena nimesahau... Kwakuwa barua hii ni FAKE, na kwakuwa mnatakiwa kuipuuza basi wakuu wangu tuanze ku-deal na issues za kuangalia rais mtarajiwa (yeyote awaye) ataapishwaje na sherehe ni wapi.

Watu wazushi sana.

Pia mjue kama kungekuwa na uchakachuaji basi ungefanyika kwa MITANDAO TU kwakuwa wanaofanya uchakachuaji ni WATAALAMU sana na hawawezi kwenda kienyeji kiasi hiki.

TAFADHALI: Msiiamini hii barua wakuu
 
Inawezekana hizi barua ni feki.

CHADEMA muwe makini,,mkiingia kichwa kichwa kuitisha press bila kujiridhisha ni kweli,itakula kwenu.
 
Sure, hii barua msihangaike nayo wakuu... Ni usanii tu. Mimi nilitaka mfahamu kuwa kuna kitu kama hicho na mjue ni FAKE tuuuuu!

Kazi ipo


kuna watu humu wanadhani huwa unakurupuka, mimi baada ya kuiona hii barua hapa nimepiga simu kwa mdogo wangu pale la-kairo hotel na amethibitisha

invisible usihangaike na majuha wa jf wapo wengi
 
Inawezekana hizi barua ni feki.

CHADEMA muwe makini,,mkiingia kichwa kichwa kuitisha press bila kujiridhisha ni kweli,itakula kwenu.


Read btn the lines hivi unamwelewa invible wewe?
 
CCM wajanja kweli kweli, wamewaingiza CHADEMA kichwa kichwa kwenye barua ambayo ukisoma kidogo tu unagundua wazi ni HOAX.

Mwambieni Dr. Slaa aiongelee majukwaani.

Ni yale yale ya Tunduma na lorry la karatasi za kura.

Ila Watanzania kuweni macho. Mauaji ya Rwanda na hata Kosovo yalianza kwa uvumi ambao baadaye ilikuja julikana kwamba haukuwa na ukweli. Wakati huo ilikuwa too late na watu walishaanza kuchinjana.

Jiandaeni kupiga kura kwa amani na kupunguza pressure na stress za kwenye JF.
 
Sure, hii barua msihangaike nayo wakuu... Ni usanii tu. Mimi nilitaka mfahamu kuwa kuna kitu kama hicho na mjue ni FAKE tuuuuu!

Kazi ipo

Mkuu Invisible. Kuwa makini na jinsi unavyopost hizi thread. The stakes are too high at this moment. Kwa jinsi ulivyo weka title ya thread na mtu kukumbana na barua hii ya utata - kwa mtu mwenye hisia za harakaharaka anaweza sababisha vurugu. Please be careful with the position you have. Suala la hisia za kisiasa sio mchezo. Ungebandika barua hizi, ila ungetumia lugha tofauti kuwapa onyo watu.
 
Ndugu zanguni, kama haya yanafanyika mchana kweupe namna hii, je watakaosababisha damu kumwagika ni kina nani?-Ni wao wenyewe. Ikumbukwe Dr Slaa alishatahadharisha mapema kuwa kuna barua zimeandikwa kwa wakurugenzi wa halmashauri kuwataka wahakikishe CCM inashinda. Najua wakuu inafahamika kuwa wakurugenzi wa halmashauri ndio returning officers wa NEC wakati wa uchaguzi. Sasa kama imeshindikana kuleta mabadiliko kwa sanduku la kura tutumie mbinu gani nyingine wakuu? I am dissappointed!



Hakuna Marefu Yasiyokuwa na Ncha
 
Sure, hii barua msihangaike nayo wakuu... Ni usanii tu. Mimi nilitaka mfahamu kuwa kuna kitu kama hicho na mjue ni FAKE tuuuuu!

Kazi ipo

Siyo Fake - so much has already been said - and as kiswahili saying goes "Lisemwalo Lipo"

Kikwete alisema "..tusiposhinda, tutajishindisha..": tatizo wa-tanzania huwa hatufuatilii hotuba za Mkuu wa kaya - zina so man loose comments ambazo ukiunganisha unapata taswira nzima ya ni nini kiko nyuma ya hizo hotuba.

This time around - at least itakuwa ngumu kidogo kuendesha zoezi la wizi wa kura - hii inaitwa CATCH 22!:A S angry:
 
If So the Case na ndio Maana niliwaambia JWTZ walitoa hiyo kauli yao ya kuwaambia mkubali matokeo na pili kama hamtokubali they'll take over tha country period hakuna jinsi.

Kufanyika hivi ni kuwepo mapungufu makubwa sana kutoka kwa seriklai ya wanamtandao JK na wenzake sasa mwaniamini niliwaambieni kuwa walijipanga kuingia IKULU na hawakujua wanatakiwa enda kufanya nini IKULU.

Na ndio Maana harufu ya damu kumwagika ilikuwa yanukia wenzenu walienda kwa JWTZ kupata Methodology za kuwamaliza upinzani na wananchi wapenda mageuzi kutoka kwa JWTZ.

Ridhwani Unajipalia mkaaaa shemeji yangu 2015 hutapata pa kutokea nakwambia. hawa wazeee ndio wanaondoka ati kaaa mbali na siasa za hao watu khaaaaa.

Kama kuna Mtu anaweza ifikisha kwa wasimamizi wa Umoja wa Ulaya/SADEC aipeleke faster au BBC ipostiwe Live
 
With due respect. Invisible nakuaminia na nimekuwa napenda post zako. Kwa hili nasita kuamini. Kwanza kwa wale wenye kumbukumbu tarehe 16.10.2010 Kikwete alikuwa Mkoa wa Pwani ziara aliyoanza tarehe 15.10.10. Tarehe 17.10.10 alikuwa Mkoa wa Dar. Yaani hata hao walioandika barua ya magizo je hawakujua ratiba hiyo? Barua inaonesha mwandishi hajui kanuni za kuandika barua. Kwanza haina Kumbukumbu. Barua kama hizi lazima zipigwe muhuri wa "SIRI" au "Confidentail". Kichwa cha barua yenyewe kinatia mashaka. Na mwandishi anaonekana kukosa weledi wa kuandika barua za Kiserikali. Kwa mimi naona barua hiyo si barua ya kweli. Ebu rejea source ya barua hiyo na ujiridhishe kama ni credible.


tarehe 16 majira ya tano usiku kikwete alifika La-kairo hotel mwanza, hotel hii ipo karibhu na uwanja wa ccm kirumba na walifanya kikao cha zaid ya masaa mawili na kuondoka hapo saa saba usiku

taarifa hizi nimepewa na ndogo wangu anafanya kazi hapo la -kairo hotel sasa hiv baada ya barua hii kuwekwa humu

Nani yuko sahihi hapa?
 
Nyaraka hiyo ilikuwa ikitoa maelekezo ya Mpango huu ufanyike soma hapa chini na linganisha sasa:

Ili JK aweze kushinda kwa 80% kikao hicho kiliandaa njia hii!

CCM tayari wameshajihakikishia ushindi kwa vile tayari wameshakamilisha kazi yao. Katika uchaguzi wamekuwa wakitimiza ratiba tu lakini matokeo ya uchaguzi yanatambulika na mpango kamili wa kukamilisha matokeo hayo ni huu.

A). Upangaji wa vituo
NEC imekuwa ikiendesha zoezi la upangaji wa vituo chini ya uangalizi maalum wa watalaam wa IT (kama ambavyo imekwsiha kuelezwa na baadhi ya wadau hapa JF, ambao ni wa 16 na MBWA MKALI katika Post zilizopita).

i).Utaratibu wa awali ulikuwa ni kuandaa vituo halali ambavyo viliandaliwa na kukamilika.
ii). Utaratibu wa pili ulikuwa ni kuandaa vituo hewa ambavyo viliandaliwa baada ya vituo vya kwanza kukamilika (Hii ni kwa lengo la kutambua vituo awali na kutofautisha vile vya kuchahachulia).

Vituo Hewa:
Jambo hili limekuwa likiwatatiza wengi sana na wengine kushindwa kuamini iwapo jambo hili linawezekana. Ukweli linawezekana na hapa natoa mmoja ya kituo hewa.
· Hapa kwa mujibu wa tume vituo vimepangiliwa kwa majina/namba.
· Kituo ambacho nawatolea mfano hai ni Na. 00020941. Ama kwa jina kinaitwa Kituo cha Shule ya Msingi Kapangaja. Kipo katika Kata ya Bugongwa wilaya ya Ilemela na jimbo la Ilemela.
-Eneo hili la shule ya msingi limegawanywa na kuzaa jumla ya vituo 5.
-Tatizo lipo katika vituo viwili ambavyo ni kituo namba 4 na namba 5.
· Kituo Na. 4: Orodha ya majina ya wapiga kura imebandikwa ikiwa na kurasa 21. Kurasa hii inajumla ya wapiga kura 490. Kwa mujibu wa rekodi za Computer kituo hiki (kwa maana ya orodha yake) kilichapishwa Septemba 16, 2010.
-Ukiangalia kwa makini utakuna majina yake ambayo yamebainishwa kuwa ndiyo ya wapiga kura katika kituo hicho yanajirudia katika kituo namba 5.
-Tofauti iliyopo ni kuwa katika orodha hiyo ya namba 5 majina huku yamepunguzwa toka 490 na kuwa 402 hivyo kuwa na kurasa za majina 17 toffauti na 21 za kituo namba 4.
-Lakini orodha ya majina ya wapiga kura hiyo inaonyesha kuwa imechapishwa katika Computer Oktoba 16, 2010. (Maana yake ni kuwa hiki kimezalishwa baada ya kuwa vituo vyote vine vimekamilika hiyo Septemba 16, 2010). Hivyo ni kipya.

B). Upigaji Kura.
Kwa vile zoezi la upangaji kura limekamilika, kazi imebaki katika kupiga. Ukweli tukubali kura kwa sasa haziibiwi kwa kupiga, ingawa njia hii pia imeandaliwa kama njia ya dharula, lakini ni kwamba kura zitapigwa hivi.
· Kwa vile orodha ya majina iliyoonekana katika kituo namba 4, ndiyo yaliyojirudia kituo namba 5, basi watu hao (ambao ni wana CCM damu ama Polisi au JWT kama watakavyokuwa wameandaliwa) watajihimu kupiga kura na kukamilisha taratibu zote kituo namba 4.
· Kwa vile kila unapopiga kura kidole huwekwa wino maalum kama alama ya kumtambua aliyekwisha piga, basi wakitoka hapo watakwenda kufuta wino huo na kasha kubadili nguo zao na muda wa kurudi kituoni tena kwa ajili ya kupiga kura nyingine. Kura hii itakuwa kura ya pili kwa mtu mmoja kwa idadi ya watu 402 kituo namba 5 kati ya watu 490 wa idadi ya kituo namba 4.
· Watu hao watakuwa wakitumia shahada zao zile zile na kwa kuwa majina yao yamo katika daftari la kudumu la wapiga kura, na wino katika vidole vyao umefutwa kitaalam, basi watapiga kura bila ya wakala kulipwa hela kumshinikiza akubali au kumzuia kwa vile anachoangalia yeye ni shahada na kama imo katika daftari vitu ambavyo ni kweli vipo.
· Kwa vile wakali aliyewaona wakipiga kura katika kituo namba 4 hatotoka kuingia katika kituo namba 5, basi mamluki hao hawatabainika na hivyo watakuwa wamepiga bao la kisigino.
C). Kujumuisha matokeo.
Uchaguzi ukiisha kazi ya kujumuisha matokeo itakuwa imekwisha kwani wakifanikiwa hapo hawatakuwa na haja ya kuongeza kura nyingine juu yake kwani jambo hili litaleta utata na kuwafanya wabainike kama ambavyo ilitokea Kenya kwa kula kuzidi kutokana na ujumuishaji wake.
Hivyo Kikwete atashinda kwa 80% na CCM wataingia mtaani kushangilia wakati Chadema wakilia na kusaga meno na hapo uchaguzi utakuwa umeisha.

NJIA NYINGINE ZA WIZI ZINAZOTANGAZWA:
Kwa hakika mpaka sasa njia zote hizo zinatangazwa sitaki kuzipuuza kwa vile zote zinaweza kutumika lakini nyingi ambazo zimejulikana sasa zimetangazwa kwa makusudi kwa ajili ya kuwazubaisha wakazanie kuangalia huko huku wakitoa akili zao katika katika njii hii ambayo ilikomboa Jimbo la Busanda na Biharamulo.

Natofautiana na wewe, ungetaja Nyamagana labda kidoooogo NINGEJARIBU kukuamini. Unadhani Ilemela nako kuna upinzani? Hawana hata haja ya kufoji vituo. Kuna mengine ni makosa tu yanafanyika. tena ni makosa ya kawaida tu. Kila kitu mnahusisha na uchakachuaji tu.
 
With due respect. Invisible nakuaminia na nimekuwa napenda post zako. Kwa hili nasita kuamini. Kwanza kwa wale wenye kumbukumbu tarehe 16.10.2010 Kikwete alikuwa Mkoa wa Pwani ziara aliyoanza tarehe 15.10.10. Tarehe 17.10.10 alikuwa Mkoa wa Dar. Yaani hata hao walioandika barua ya magizo je hawakujua ratiba hiyo? Barua inaonesha mwandishi hajui kanuni za kuandika barua. Kwanza haina Kumbukumbu. Barua kama hizi lazima zipigwe muhuri wa "SIRI" au "Confidentail". Kichwa cha barua yenyewe kinatia mashaka. Na mwandishi anaonekana kukosa weledi wa kuandika barua za Kiserikali. Kwa mimi naona barua hiyo si barua ya kweli. Ebu rejea source ya barua hiyo na ujiridhishe kama ni credible.



wewe ni mpumbavu nani amekwambia hii barua ya kiselikari

kama hutaki ondoka hapa

Barua inayohusisha usanii kama huu haiwezi kuwa na muhuri wa 'confidential'

Pili, hivi hujui kama JK ni juha? Ni zuzu? Ni msahaulifu? Ni kilaza?

Hujui?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom