mzee wa kijiwe
JF-Expert Member
- Jun 25, 2012
- 947
- 685
ASahau habari ya Makambo ambaye ndiye mchezaji anayeongelewa kwa wingi sasa hapa Tanzania, Sahau habari ya Tambwe mchezaji tishio kwa wana Msimbazi wote, yupo mchezaji ambaye ndiye roho ya wana Jangwani kwa sasa, huyu ndiye aliyekuwa anakosekana kwenye timu yetu ya Taifa ili kuleta uwiano mzuri kati ya washambuliaji na viuongo wachambuliaji
Hapa sii mzungumzii mwingine Bali ni Ibrahim Ajib kiungo mshambuliaji mwenye kuweza kuudhibiti mpira mguuni na mpira ukamtii, mwenye uwezo wa kuinua kichwa na kuona mahali sahihi aliposimama mshambuliaji wa timu yake. Ajib wa sasa amezaliwa upya, huyu anayo pumzi na stamina, anakimbia pande zote za uwanja bila kuchoka lakini anayo sifa kuu moja ambayo ndiyo inayompambanua na aina ya viungo wengine waliopo hapa nchini kwa sasa.
Ajib anapiga pasi za nwisho maarufu kama assists ambazo ni chakula kwa washambuliaji wengi.
Kwa muda mwingi nchi yetu ilikosa vyakula vya namna hii, Samata Leo hii angekuwa amevunja rekodi zote za Taifa hili katika ufungaji kama angecheza na huyu Ajib wa Leo. Kazi yake ingelikuwa ni rahisi sana, kucheka na nyavu.
Mlimwona Makambo kwenye mechi ile ya Yanga na Costal Union? Kwa wale walioitizama ile mechi hawawezi kusahau kamwe kile ambacho Ajib alikifanya. Unajua ni kwanini Makambo aliomba kutoka uwanjani? Wengine watasema eti Makambo aliumia ,hakuna kitu kama hicho. Makambo aliomba poo kwa lugha yetu ya mtaani.Ajib alipeleka chakula kingi kuzidi uwezo wa mlaji, Ajib alipiga mipira yote kwa Makambo, na mipira asilimia tisini ilimfikia Makambo, ilimlazimu Makambo kukimbia kulia, kushoto na katikati, ukweli ni kwamba Ajib alimchosha sana Makambo.
Ubora wa Tambwe kwenye mechi kati ya Yanga na Singida United umetokana kwa sehemu kubwa na kazi murua ya Ajib.
Ni kiungo yupi mshambuliaji anayeweza kuuleta mipira juu ya kichwa cha mfungaji kama Ajib? Ajib anapiga pasi zile zinazo katiza uwanja, nimeziona pasi za Ajib zinafanana kabisa na pasi anazopiga Pogba pale OT na pia Alex Sancches.
Nasubiria kumwona Ajib wa tarehe 30/9 pale uwanja wa Taifa, nasubiria kumsikia kocha mkuu wa Taifa stars Amunike akichanga karata zake za jinsi ya kuelekea Afcon 2019, Ajib amebeba siri ya mafanikio ya Amunike, sitegemei kumshauri Amunike ili amwite Ajib kwenye kikosi chake, nilimwona Amunike pale uwanja wa Taifa akicheka kila Ajib alipogusa mpira, kichwani niliwaza Amunike hayupo pale uwanjani bali mawazo yake yote yalirudi nyuma miaka kumi iliyopita pale Nigeria ilipokuwa ikifanya mambo makubwa chini ya kiungo mshambuliaji asiye na mfano JJ Okocha.
Je Ajib nguvu za soda? Ni swala la muda tuu, hii ni mechi yake ya NNE akitoa assist mfululizo na yeye mwenyewe akifunga moja ya magoli ambayo yataingia kwenye kinyanganyiro cha goli bora la msimu.
Huu ni uchambuzi huru mitandaoni wa mwanamichezo
Peter John
0715829576
Hapa sii mzungumzii mwingine Bali ni Ibrahim Ajib kiungo mshambuliaji mwenye kuweza kuudhibiti mpira mguuni na mpira ukamtii, mwenye uwezo wa kuinua kichwa na kuona mahali sahihi aliposimama mshambuliaji wa timu yake. Ajib wa sasa amezaliwa upya, huyu anayo pumzi na stamina, anakimbia pande zote za uwanja bila kuchoka lakini anayo sifa kuu moja ambayo ndiyo inayompambanua na aina ya viungo wengine waliopo hapa nchini kwa sasa.
Ajib anapiga pasi za nwisho maarufu kama assists ambazo ni chakula kwa washambuliaji wengi.
Kwa muda mwingi nchi yetu ilikosa vyakula vya namna hii, Samata Leo hii angekuwa amevunja rekodi zote za Taifa hili katika ufungaji kama angecheza na huyu Ajib wa Leo. Kazi yake ingelikuwa ni rahisi sana, kucheka na nyavu.
Mlimwona Makambo kwenye mechi ile ya Yanga na Costal Union? Kwa wale walioitizama ile mechi hawawezi kusahau kamwe kile ambacho Ajib alikifanya. Unajua ni kwanini Makambo aliomba kutoka uwanjani? Wengine watasema eti Makambo aliumia ,hakuna kitu kama hicho. Makambo aliomba poo kwa lugha yetu ya mtaani.Ajib alipeleka chakula kingi kuzidi uwezo wa mlaji, Ajib alipiga mipira yote kwa Makambo, na mipira asilimia tisini ilimfikia Makambo, ilimlazimu Makambo kukimbia kulia, kushoto na katikati, ukweli ni kwamba Ajib alimchosha sana Makambo.
Ubora wa Tambwe kwenye mechi kati ya Yanga na Singida United umetokana kwa sehemu kubwa na kazi murua ya Ajib.
Ni kiungo yupi mshambuliaji anayeweza kuuleta mipira juu ya kichwa cha mfungaji kama Ajib? Ajib anapiga pasi zile zinazo katiza uwanja, nimeziona pasi za Ajib zinafanana kabisa na pasi anazopiga Pogba pale OT na pia Alex Sancches.
Nasubiria kumwona Ajib wa tarehe 30/9 pale uwanja wa Taifa, nasubiria kumsikia kocha mkuu wa Taifa stars Amunike akichanga karata zake za jinsi ya kuelekea Afcon 2019, Ajib amebeba siri ya mafanikio ya Amunike, sitegemei kumshauri Amunike ili amwite Ajib kwenye kikosi chake, nilimwona Amunike pale uwanja wa Taifa akicheka kila Ajib alipogusa mpira, kichwani niliwaza Amunike hayupo pale uwanjani bali mawazo yake yote yalirudi nyuma miaka kumi iliyopita pale Nigeria ilipokuwa ikifanya mambo makubwa chini ya kiungo mshambuliaji asiye na mfano JJ Okocha.
Je Ajib nguvu za soda? Ni swala la muda tuu, hii ni mechi yake ya NNE akitoa assist mfululizo na yeye mwenyewe akifunga moja ya magoli ambayo yataingia kwenye kinyanganyiro cha goli bora la msimu.
Huu ni uchambuzi huru mitandaoni wa mwanamichezo
Peter John
0715829576