Uchambuzi wa mwanzo wa katiba inayopendekezwa: Tusikubali maslahi binafsi yashinde maslahi ya taifa

Uchambuzi wa mwanzo wa katiba inayopendekezwa: Tusikubali maslahi binafsi yashinde maslahi ya taifa

Kama Humfrey na wengine wanaona kuwa rasimu ya 3 haijakidhi matakwa ya wengi, kuna nafasi moja kubwa imebaki, nayo ni kuwashawishi wananchi na kuikataa hii katiba kwenye kura ya maoni, vinginevyo kulalamika mitandaoni na kwenye TV ambazo zinawaafikia watu wachache sana tena, wengi wao sio wapiga kura haisaidii. Ni ushauri tu.
 
Mimi nashangaa mnaangaika eti tutaipigia kura, nini? Tupigie vijizuu vya ccm, ivyo watapigia wao, cku ya kura tunaweka vituo vyetu tunaenda kupigia rasmu ya mzee warioba. Maana ipo complete haiitaji discussion
 
Humu ndani kuna watu mawazo yao kama wamekunywa maji ya chooni coz ccm wamelewa madaraka na wao wanawaendekeza
 
Kwa katiba hii ccm bye bye .atakama katiba inawekwa kabatini .adhabu lazima tuwapeni 2015 .kuhakikisha hamshindi kuja kuipitisha 2016 ..
 
Nchi hii inaviongozi ambao wamejigeuza vichaa hata aibu hawana? Chenge katiba wapi na wapi kafanya madudu chi hii bado kunamijitu inasifia tu bila kujua matatizo yanayoweza tokea sasa wanaonesha wazi kwamba watakufa na utawala sasa tunapiga chini wote maccm afu tuone kama hamtahitaji hiyo rasimu ya pili ndo katiba in short maana walikaa wasomi nakuchambua maoni ya wananchi leo uwapelekee akina komba hawajui chochote wanajua maslah tu
 
Nimeisoma Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa, nimeisoma yote, ni bahati mbaya inapigiwa upatu kwamba imebeba mambo ya wananchi, mambo ya wakulima, wafugaji, wavuvi, vijana na kadharika. Jamani hayo ni hadaa, msingi wa muundo umebadilishwa, Tanganyika imevalishwa koti jipya la Muungano, ambalo tusipokuwa makini itaendelea kuishi nalo muda mrefu zaidi. Kigezo cha kukataa serikali 3 hakina hoja zenye mashiko, wanasema Hati ya Makubaliano ilisema serikali 2 hivyo hatuwezi badili, huu ni uongo, mbona Hati ilisema mambo ya Muungano ni 11, mbona wao wameweka 14, uhalali wa kubadili mambo ya Muungano kama Hati haibadiliki wanaupata wapi.? Hii ni double standard. hati haikujieleza kwamba kwa baadhi ya maeneo mwiko kubadili na ruksa kwa mengine, Amka ee Mtanzania.


Unasema katika Sura ya Pili unaanzisha Tume ya Mipango ya Taifa ilhali ukijua Zanzibar wana Tume ya Mipango pia, nashangaa sana. Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa inasema Kutakuwa na Dira, Ohoo, kutakuwa tena, nilidhani inapaswa itamkwe, na kwa asili ya "Programmatic Constitutions" Dira inakuwa ni ujumla wa Lengo Kuu la Katiba Pamoja na Malengo Mahususi kama ilivyokuwa kwenye Rasimu..


Wamefuta kumwajibisha Mbunge, wamefuta ukomo, wamefuta mbunge asiwe waziri, wamefanya ugombea binafsi kuwa mgumu zaidi, wamevuruga Tume ya Uhusiano na Uratibu, wao wamesema Tume hii ni kwa Mambo ya Muungano, hili ni kosa kubwa la kisanifu (design), Mambo ya Muungano yanasimamiwa, yasiyo ya Muuungano yanaratibiwa. Wameweka Baraza la Vijana, vijana wenzangu hii ni hadaa, walio wengi ni wanawake mbona lao hawakuliweka, ninazingatia haki hapa, wanataka kuwahamasisha kwa mambo ambayo katika utalaamu na uandishi wa Katiba hayapo, yamewekwa ili msahau yale waliyofuta.


Wamerudisha wakuu wa Mikoa, wananchi mlisema sana juu ya uwepo wa wakuu wa mikoa na wilaya.. kwa namna walivyo rudi sitashangaa wakiendelea kuwa makada wa vyama vya siasa. Haya maoni ya kuwaweka wakuu wa mikoa katika namna hii wameyatoa wapi.? Maoni hayo mimi sikuyaona Tume ya Katiba kipindi chote nilichokuwepo.


Vyanzo vya mapato ni vile vile kwa serikali ya muungano (Katiba ya 1977) na wakadhani mwarobaini ni kurejesha Tume ya Pamoja ya Fedha ambayo haikuwahi kufanyiwa kazi (kuna sababu kubwa zaidi kuliko kuwa na Tume ya Pamoja ya Fedha), Bahati mbaya Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa imelikosa hili.


Rasimu ya Katiba inayopendekezwa inasema Makamu wa Rais Watatu, Makamu wa Kwanza (Muungano), Makamu wa Pili (Rais wa Zanzibar) na Makamu wa Tatu (Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano)... Jamani watanzania wenzangu, huu UTATU mbona tunapewa kwa mgongo wa chupa, TATU tunaziogopea nini.? Tume ya Pamoja ya Fedha iliwaambia anzisheni akaunti ya pamoja ya fedha, ikawa kigugumizi, leo kipi kitafanya tuweze?


Mnasema Mahakama Kuu ya Zanzibar na Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano zitakuwa na Mamlaka sawa (concurrent jurisdiction), hata kwa jina hapo si tunadanganyana.? Hakuna kitu kama Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano, kwasababu ninyi mnajua haina Mamlaka Zanzibar sasa kuiweka kwenye Muungano kunani.?


NINAENDELEA NA UCHAMBUZI, KAMA NILIVYOSEMA KAZI NDIO KWANZA IMEANZA.


Kwa taarifa zaidi ungana nami hapa Humphrey Polepole kisha LIKE na tutakuwa pamoja.


Waraka huu sijauhariri.

kwani we nani kwenye nchi hii uwaamulie watu?
 
Mlitaka kutengeneza katiba yenu na mzee warioba lakini sasa ndiyo basi hii ni katiba ya watanzania hatutaki katiba ya walevi kama wewe na warioba.

Hapa ndo magamba mliposhindwa, kujibu hoja kwa hoja.
 
kwani we nani kwenye nchi hii uwaamulie watu?

Wacha uPUMBAVU unadhani wote wanafikiri kwa kutumia UTUMBO km wewe,,,,!! JINGA KABISA mnajifanya mnahatimiliki nahii NCH subirini km hamjahama na mifuko ya RAMBO
 
Ukiuona huu Ufarao wa CCM unalazimisha haya kwa kutufunika sote katika magunia, basi ujue kuwa Mwenyezi Mungu analazimishwa kuwauwa wazaliwa wote wa kwanza wa Tanzania ili kufanikisha uhuru na demokrasia. Katiba mpya na bora iko njiani imevikwa magunia inaomboleza, lakini mwisho itafika.
Asante Ndugu Humphrey tuendeleze Mapambano. MUNGU ni Mwema.
 
Kinachoendelea Dodoma kiturudishe kwenye HOJA ya MTIKILA huenda 6 na GENGE lake uRAIA wao unawalakini mimi siamini km ni PESA tu cz km ni pesa wanazo nyingi lkn kinachofanyika pale ni uHALIFU,,!
 
Wacha uPUMBAVU unadhani wote wanafikiri kwa kutumia UTUMBO km wewe,,,,!! JINGA KABISA mnajifanya mnahatimiliki nahii NCH subirini km hamjahama na mifuko ya RAMBO

hata huyo unayemsikiliza hana hati mikiliki na nchi hivyo mawazo yake hayawezi kutuamulia hatma yetu
 
Natamani siku wakituletea hiyo 'toilet paper' ya Chenge, NTAICHANACHANA hadharani kama walivyofanya Zanzibar kipindi kile. Hapa ndipo ntakapofia wanajamvi. Najua Intarahamwe kuua ni kawaida yao, watanipiga mpaka uhai utanitoka. Lakini potelea mbali bora nife napigania Taifa kuliko kufa na kwa Ebora au Ukimwi!
 
Weka hoja basi. Hizo fujo sasa. Au unataka useme lolote tu ili hiyo buk saba ionekane ilivyotumika.

Nikuwekee hoja za nini wakati yupo unayemwona mungu wako wa mawazo-kura ya maoni itaamua
 
Nikuwekee hoja za nini wakati yupo unayemwona mungu wako wa mawazo-kura ya maoni itaamua

Unaitajataja sana kura ya maoni. Mshajipanga na huko nn? Au nayo umekariri kwenye maagizo ya leo. Mungu ni mmoja tu. Na atawaonyesha tu safari hii.
 
hata huyo unayemsikiliza hana hati mikiliki na nchi hivyo mawazo yake hayawezi kutuamulia hatma yetu

Kila mtu anahaki yakuckilizwa hata nyie mnaofikiri kwa kutumia UTUMBO tunawackiliza ndio maana tunajua yaliyojaza Mioyo yenu,,,,,!!
 
Back
Top Bottom