Uchapakazi wa Mohammed Mchengerwa TAMISEMI wawakosha Watanzania

Suala la walimu kudhibiti nidhamu kwa wanafunzi ningependa kukujibu kuwa wajibu wa kuwalea watoto ni jukumu la wote na linaanza kwanza na wewe mzazi.sasa wewe toto limekushinda,limezibuka hakina adabu wala heshima wala staha kwa watu na ubaliangalia tu kama sanamu pasipo kuchukua hatua zozote zile ndio unataka yeye mwalimu alidhibiti kwa njia zipi wakati wewe mzazi unayelala nalo nyumba moja na kula nalo ugali limekushinda? Unataka mwalimu akalipige kwa rungu kuzibua kichwa ? Malezi bora yanaanzia kwako mzazi na siyo kumtupia lawama mwalimu.

Suala la makusanyo katika halmashauri nalo Mheshimiwa waziri ameendelea kusisitiza ukusanyaji pamoja na kudhibiti mianya yote ya uvujaji wa mapato lakini pia kukemea na kuchukua hatua kwa wale wanatafuna pesa za halmashauri kama mchwa pasipo huruma wala uoga.

Suala la ubora wa majengo nalo limekuwa likisimamiwa vizuri na wataalamu katika halmashauri na ndio maana husikii kuwa kuna jengo limedondoka kwa kujengwa chini ya viwango.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…