UCHAWI GEREZANI/KIZUIZINI/KIFUNGONI

kibombonya

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2018
Posts
326
Reaction score
564
Habari zenu wadau wa JF, siku zote nimekua najiuliza Sana hili suala la imani za ushirikina/ uchawi. Kiukweli nabaki njia panda pale ninaposikia wachawi wanauwezo wa kuingia ndani ya nyumba wakafanya wanachotaka na wakatoka bila kuonekana, hata wakitaka kusafiri wanasepa tu kiulaini kabisa. Ebu tujiulize kwanini/ iweje wanashindwa kufanya uchawi kwenye magereza wanapofungwa wanashindwa kutoka na kurudi makwao? Mwenye ufahamu na hili tudadavulie!! Naomba kuwasilisha......[emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi kutoroka kwani huwezi kutumia zana zako ukiwa huru , vitu vingine ni siri na gerezani hakuna usiri . Mf. Kiungo cha binadamu utakionyesha ??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu aya mambo yapo mpaka uko....
Around 2007 kipindi cha operation ya kufagia majambazi kuna Jambazi mmija mkubwa alikamatwa Tanga akatupwa Mahabusu Maweni.......

Kama wiki hivi siku jamaa akaamka na furaha zake akawaaga wadau mpaka na askari akawaambia leo Mama yake anakuja kumchukua, unaambiwa usiku ilipiga mvua moja ya hatari nasauti za paka kwa wingi, asubui jamaa akuwe na kuna nondo ya juu kwenye dirisha ilikutwa imepinda kidogo, jiulize amepitaje na ukizingatia gereza lilikua limezungukwa na katani......

Akawaachia msala askari zamu ya ulinz.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…