Uchimbaji madini na uharibifu wa mazingira kata ya Galigali-Mpwapwa

Uchimbaji madini na uharibifu wa mazingira kata ya Galigali-Mpwapwa

Rusumo one

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
3,458
Reaction score
4,283
Habari za usiku wakuu na wote humu. Nijikite kwenye mada juu.

Katika mihangaiko yangu nipo eneo la Kata ya Galigali Kijiji cha Matonya na pia Kuna mida nakuwa Kitongoji cha Idete hapa baridi kali Sana huku nikiendelea kusaka maharage kwaajili ya biashara. Nachosikitika ni kuona madini yakichimbwa Hadi kwenye vyanzo vya mito na kelele zilizopo ni kwamba hata EIA haijafanyika, wananchi waliletewa wachimbaji na kutambulishwa na afisa madini wakiwa na afisa mazingira Wilaya ya Mpwapwa.

Niseme tu hii haipo sawa uharibifu mkubwa unafanyika isitoshe hawa watu inasemekana hawana hata vibali vya uchimbaji ni uhuni tu. Hivi huku hakuna mbunge? Simbachawene anakula posho anasahau wananchi wake Ila ingekuwa mwakani kipindi Kama hichi angeshafika, WEO,VEO na vitongoji wamelala. Taarifa zilizopo ni kuwa hata vyombo vya uchunguzi TISS,PCCB na PT wana taarifa Ila wamekalia kimya.

Napaza sauti Serikali kupitia wizara ya Madini iingilie kati suala hili makamu waziri mkuu fika huku ujionee mambo na watu wa mazingira mkuje.Kila usiku land cruiser zinazama na kubeba madini pia malori yanabeba madini usiku kwa usiku wakati Vijiji haviingizi kitu. Karibuni Matonya,Idete,Kinusi,Mbuga,Ipera.Mng'ang'a,Kikuyu mjionee fahari ya wahehe.

Nawasilisha.

Kamweneee!!!
 
Ila kifupi hii kitu ni mchongo wa wakubwa inaonekana ni chaka lao maana hata mitambo inakuja na kupaki shule msingi Matonya kimtindo na kuchochora kuja Idete kibishi hapa naongea Kuna Prado imeingia naona inapakia then inachimba kurudi ilipotoka plate number imefunguliwa yaani wizi mtupu.
Ngoja niendelee kukusanya maharage maana barabara inaweza toweka malori yanaharibu barabara niwahi kurudi Tandale
 
IMG-20240611-WA0024.jpg
 
Hizi picha nilifanya utundu wangu wa IT niliopata pale UCC nikapata maeneo migodi hii ilipo utaona Kuna mlima unakatwa na mingine ipo mabondeni
 
Habari za usiku wakuu na wote humu. Nijikite kwenye mada juu.

Katika mihangaiko yangu nipo eneo la Kata ya Galigali Kijiji cha Matonya na pia Kuna mida nakuwa Kitongoji cha Idete hapa baridi kali Sana huku nikiendelea kusaka maharage kwaajili ya biashara. Nachosikitika ni kuona madini yakichimbwa Hadi kwenye vyanzo vya mito na kelele zilizopo ni kwamba hata EIA haijafanyika, wananchi waliletewa wachimbaji na kutambulishwa na afisa madini wakiwa na afisa mazingira Wilaya ya Mpwapwa.

Niseme tu hii haipo sawa uharibifu mkubwa unafanyika isitoshe hawa watu inasemekana hawana hata vibali vya uchimbaji ni uhuni tu. Hivi huku hakuna mbunge? Simbachawene anakula posho anasahau wananchi wake Ila ingekuwa mwakani kipindi Kama hichi angeshafika, WEO,VEO na vitongoji wamelala. Taarifa zilizopo ni kuwa hata vyombo vya uchunguzi TISS,PCCB na PT wana taarifa Ila wamekalia kimya.

Napaza sauti Serikali kupitia wizara ya Madini iingilie kati suala hili makamu waziri mkuu fika huku ujionee mambo na watu wa mazingira mkuje.Kila usiku land cruiser zinazama na kubeba madini pia malori yanabeba madini usiku kwa usiku wakati Vijiji haviingizi kitu. Karibuni Matonya,Idete,Kinusi,Mbuga,Ipera.Mng'ang'a,Kikuyu mjionee fahari ya wahehe.

Nawasilisha.

Kamweneee!!!
KAMWENE, mnyalukolo.

Tunaamini viongozi wote wa ngazi zote wanaona kinachofanyika, ni wakati sasa kuwaomba kufuatilia jambo hilo bila UOGA wowote kulinda Mazingira, haki za wanakijiji pamoja na kuingia makubaliano / mikataba ya madini kisheria, ili Pindi makubaliano yatakaposhindwa kufikiwa wawe na haki ya kudai kisheria.

Asanteni,wana JF wote ,kwa michango yenu mizuri na yenye tija kwa wananchi wa sehemu hiyo Tajwa.
 
Back
Top Bottom