Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base)

Uchina itaiomba Tanzania (kama bado haijafanya hivyo) iwapatie kituo cha kijeshi (military base)

Vizuri umeuliza unataka kujua. Maana wengi hapa wanaposhindwa kujua wanatukana! Huu ndiyo upumbavu wa watu wetu.

Kwa ufupi, UAE ni nchi very pragmatic kama utafuata siasa zake. Hivi nisemavyo wanazungumza na Iran! Nataka Tanzania iwe hivyo na kujali maslahi yake tu. Hakuna mjomba kwenye siasa!

Juu ya habari hiyo ya base ya Wachina hebu google: 'UAE secret Chinese base' ujisomee mwenyewe.
Nimesoma hiyo naval facility iliyokuwa inajengwa kwa siri na China imezuiwa baada ya Marekani kugundua faulo ile. US hawezi kubali UAE kutumika na China, ila sikutarajia kama hapo kabla UAE ingeweza kufikia hatua hiyo
 
Marekani wakati wa utawala wa Bush hadi utawala wa Obama walikuwa wanataka kuweka makao makuu ya kamandi ya Afrika hapa Tanzania kwa sababu kadhaa; sasa hivi makao makuu ya kamandi ya Afrika nadhani bado yako Ujerumani. Sababu kubwa ya marais Bush na Obama kuja Tanzania na kusaka kiwanja cha kujenga makao makuu hayo, lakini maombi yao yalikataliwa, nadhani kwa msukumo fulani kutoka AU. Nakumbuka kipindi hicho watu wakisema nchi inatambulika sna hadi maraisi wa marekani wanashindana kuja Tanzania, lakini ukweli walikuwa wanakuja kutafuta maslahi yao.
Ukitaka kula, nawe ukubali kuliwa (Hii ni falsafa kubwa sana kwa anayejua dunia. Hakuna namna nyingine. Maisha yote ya binadamu yanazunguka kwenye falsafa hiyo!). Wajerumani walifanya hivyo, Wajapani, Wakorea....hata Wachina wenyewe, waliliwa kwanza!
 
Marekani iwaambie Tanzania kama ikifungamana na China, Marekani itaitambua rasmi Zanzibar kama nchi na itaisaidia kutambulika UN. Na vile vile Marekani iisadie Zanzibar kwa kuwapa silaha za kujilinda kama CCM wakitaka kuleta chokochoko Zanzibar. Kihistoria Zanzibar ilikuwa ni sehemu ya Oman na Oman wana uhusiano mzuri na Marekani. Zanzibar watumie mwanya huu kuchomoka na kupata maendeleo.
 
Back
Top Bottom