Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mchambuzi,

Ni kweli Bibi Titi Mohamed hakuwa kati ya wanachama 20 wa mwanzo wa TANU.
 
Last edited by a moderator:

MKuu Ritz, n
imekufatilia tangu mwanzo wa huu mnakasha na mara nyingi unakuwa ndani ya mstari na mara chache unaingia kwenye marumbano yasiyo na hoja, lakini naomba nikiri kuwa una vitu vingi ama niseme una info nyingi lakini unazitoa kwa kubanabana au kwa kutega watu, ningekuomba uiweke hapa List sahihi ya waasisi wote wa TANU bila kujali itikadi zao za Imani wala Kikabila, naliomba hilo kwa faida ya wote tunaofatilia manakasha huu

IKUMBUKWE PIA WAFATILIAJI WOTE WA MNAKASHA HUU WANAKUBALI KUWA KUNA MAPUNGUFU KWENYE HISTORIA YETU, KUNA KUSAHAULIWA KWA MATUKIO AMA WAASISI WA TAIFA LETU
kinachopingwa humu ni kile kitendo kuwagawa waasisi wa Uhuru wetu kwa minajili ya Kidini (Islam), Kikabila (Zulu and Manyema) na Kikanda (Gerezani-Mzizima)
 
Nimekuuliza mwanzo kabisa nitajie wanachama 20 wa mwanzo ndiyo ukaniwekea haya majina.
hivyo ndivyo historia niliyosoma inanieleza, kama una ufahamu zaidi, hapa ndio sehemu yake ya kutuelimisha wengine;

Haya majini nilikuandikia nimekuuliza hakuna hata mmoja alikuwa mwanachama wa mwanzo wa TANU.
kwanini hautoi ufafanuzi na kujadili hoja zako kwa kina kama nia yako ni kutuelimisha?

,

Ni kweli Bibi Titi Mohamed hakuwa mwanachama wa mwanzo wa TANU?

Hapa tunajifunza mengi kuhusu historia yetu.

Kwa mujibu wa historia niliyosoma, suala la Bibi Titi na involvement yake katika TANU lilikuja kuingia utata na nadhani unaelewa historia juu ya hili; Lakini nia yako hapa ni nini hasa - to question the history - kwamba kwanini yalitokea yaliyotokea kwa Bibi Titi Mohamed? Au una question kwanini Bibi Titi Mohamed hayupo katika orodha ya waasisi wa TANU?
 
Ni kweli, na binafsi sielewi kwanini ilitokea hivyo; Lakini kwa wale wenye upeo mdogo kama zomba, wanaweza kudai kwamba haya yalikuwa ni makosa ya Nyerere wakati TAA ilikuwa ni chombo ambacho Nyerere hakuwa na mahusiano nacho kabla ya 1954;

Unapingana na Nyerere? amma kweli huelewi:

Unajuwa Nyerere alikuwa Makerere mwaka gani na haya chini ni maneno ya nani?


Bado hutaifut hiyo kauli yako ya mwaka 1954? nakuongeza na hii:


Hiyo wala usihangaike kuitafuta, ipo post # 1 ya nyuzi hii hii na ilibandikwa na mwenzako, hapo inakuwa amma Yericko Nyerere kazuwa au wewe umezuwa au Julius Nyerere kazuwa. Utajaza.


Halafu wewe huyo huyo ndiye uliingia kwa papara na makeke na kuniambia mimi historia ya nchi yangu siijui? wewe uijuayo nakuuliza, kiko wapi? hapachakachuliki hapa.
 

Ndugu yangu Kituko,

Hapa tunajifunza mengi sana mie najua machache kutokana na kuambiwa na Wazee wangu na kujisomea tu. Kuna watu humu wana vitu vingi sana tatizo mitazamo tuendelee kusoma humu ndugu yangu tutajua mengi.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu yangu Kituko,

Hapa tunajifunza mengi sana mie najua machache kutokana na kuambiwa na Wazee wangu na kujisomea tu. Kuna watu humu wana vitu vingi sana tatizo mitazamo tuendelee kusoma humu ndugu yangu tutajua mengi.

Mkuu hatugombani, weka hiyo list watu wanajaribu kupata historia sahihi ya Nchi hii, kila kitu kinachowekwa kinajadiliwa na kile ambacho hakina shaka huwa kinapita na wale wenye kukusanya information sahihi wanfanya hivyo kwa faida ya nchi hii, hakika mijadala kama hii ikifanywa kwa njia ya kutafuta ukweli itatufikisha kwenye ukweli bila kuwa na uegemezi wa kiimani wala kikanda
 
Hivi nia yako ni kujaribu kubaini iwapo ninafahamu au hauna ufahamu na unataka kuelimika katika hili;

Kaka nia yangu ni kujifunza wala sina nia ingine ili jukwaa letu sote hakuna ubaya kufahamishana historia.
 

Achana na ANC hapa tunaongelea mambo ya nyumbani, usiwe kama mwenzako alipoona maji yanamzidi kimo akaanza Somalia, mara Nigeria.

Kwa hiyo, hao waasisi wa TANU Burma ambao wewe unasema ni muendelezo wa ujuaji, unawajuwa na kwenye historia yako ya kivukoni wamo? Na ulilijuwa hilo kabla hujamsoma Mohamed Said?
 
Kaka nia yangu ni kujifunza wala sina nia ingine ili jukwaa letu sote hakuna ubaya kufahamishana historia.

Kikubwa hapa bwana ritz ni kwamba Nyerere ndiye alikuwa kiongozi wa msafara kama Kikwete anavyokuwa katika misafara ya leo, whether kaenda na Membe, Muhongo, Sita, we care less;

Nachojua zaidi ni mwalimu aliongea nini line by line kwenye address yake to the UNO in November 1956 na pamoja na impact ya aliyoongea mwaka 1956 katika Tanganyika kama koloni, na Tanzania ya leo kama taifa huru kisiasa;

Vile vile nachojua ni kwamba safari ile ilifanikishwa na michango ya watanzania mbalimbali wahindi, weusi (kina rupia), wakristo, waislamu, wasiokuwa na dini zinazojulikana rasmi, ili mradi tu Mwalimu aende kufanikisha lengo husika;

Pia najua kwamba Chief Marealle alitumiwa na wakoloni kupotosha juhudi na malengo ya Mwalimu UNO;

Mwisho, nafahamu kwamba Elly Anangisye alikuwa ni Katibu Mkuu wa TANU Youth League wakati ule na alikuwepo kwenye ule msafara;

Mjadala wetu utakuwa na manufaa zaidi (kama taifa) iwapotutajikija zaidi katika issues, sio watu, misafara n.k; Tafadhali usiniulize katika safari ile wajumbe walilipwa posho kiasi gani kwani kwa mwendo wako, hili linaweza kuwa swali linalofuatia;
 
Mchambuzi,

Ni kweli Bibi Titi Mohamed hakuwa kati ya wanachama 20 wa mwanzo wa TANU.
WANAOONEKANA KWENYE WEBSITE YA CCM NI 17,SASA WA 18-20 SIJUI NINANI.
Waasisi wa TANU ambao walihudhuria na kushiriki katika Mkutano wa kuzaliwa kwa TANU walikuwa 17:

  1. Mwalimu J.K. Nyerere – Rais wa TAA/TANU
  2. Geremano Pacha – Jimbo la Magharibi
  3. Joseph Kimalando – Jimbo la Kaskazini
  4. Japhet Kirilo – Jimbo la Kaskazini
  5. C.O. Milinga – Jimbo la Mashariki
  6. Abubakari llanga – Jimbo la Ziwa
  7. L.B. Makaranga – Jimbo la Ziwa
  8. Saadani A. Kandoro – Jimbo la Ziwa
  9. Suleman M. Kitwara – Jimbo la Ziwa
  10. Kisung'uta Gabara – Jimbo la Ziwa
  11. Tewa Said Tewa – Jimbo la Mashariki
  12. Dossa A. Aziz – Jimbo la Mashariki
  13. Abdu Sykes – Jimbo la Mashariki
  14. Patrick Kunambi – Jimbo la Mashariki
  15. Joseph K. Bantu – Jimbo la Mashariki
  16. Ally Sykes – Jimbo la Mashariki
  17. John Rupia – Jimbo la Mashariki

 

Hoja ya msingi hapa ni kwamba mjadala kuhusu TANU iliasisiwa wapi hauna maana kwani hata hiyo Tanganyika yenyewe iliwekwa mipaka na watu ambao hawakuwa watanganyika;
 

Nakubaliana na wewe 100% kwenye nyekundu, kwenye buluu umechakachuwa, nnakuuuliza tena, umesahau au hujui kuwa TANU iliasisiwa Burma?
 
Hoja ya msingi hapa ni kwamba mjadala kuhusu TANU iliasisiwa wapi hauna maana kwani hata hiyo Tanganyika yenyewe iliwekwa mipaka na watu ambao hawakuwa watanganyika;

Haina maana? hivi chama kilichodai Uhuru na waasisi wake waliofikiria kuiunda unasema haina maana? lakini kuyaleta ya ANC ndio unaona yana maana?

Unamjuwa Sheikh Takadiri, nilikubandikia post ya Mohamed Said inayomuelezea naona umeamuua kuuchuna.

Na bado hujajibu swali, Jee, hao waasisi unawajuwa?

Bado pia rejea post yangu 3034 unayoipita kama hujaiona.
 
Kwa kujua au kutokujua, kwa makusudi au kwa bahati mbaya kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana kuhusu hasa ni akina nani waliodai Uhuru wa Taifa letu Tanganyika.

Upotoshaji hauishii hapo tu bali hata dhana halisi ya Maadhimisho yenyewe,Leo usikia wanasema nisherehe za Uhuru wa Tanzania Bara,

Hakuna nchi au taifa duniani linaloitwa- Tanzania Bara, halijapata kutokea na halitotokea katika uso wa dunia hii taifa au nchi iitwayo Tanzania Bara.

Muunganano wa Tanganyika na Zanziber ni mfano wa kuigwa duniani, hakuna muungano wenye hadhi kinadharia na kivitendo dunia kama huu, Kila aliye muamini wa amani duniani na aupiganie kuulinda na kuuhuisha uwe na mafaa kwa wa Tanzania

Lakini muungano unaomeza taifa lingine na kubaka fikra za Watanganyika huku ukipuliza kwa dhihaka Wazanzibar haufai, yatupasa tuuhuishe mapema kabla mbongo za wahafidhina hazijamka na kushuhudia hasira ya Mtanganyika chini ya uvuli wa fikra za ccm mfilisi.

Sihubiri KUUVUNJA muungano huu murua bali, nahubiri uwepo wa Tanganyika na Zanzibar zenye kuwajibika kwa watu wao na uwepo Tanzania yenye kujikita Kimuungano.

Suala hili ni kama halina mantiki ya mageuzi ya mstakabali wa Mtanganyika, lakini aliye Mtanganyika anatambua mafaa ya matokeo ya hili.

Zanzibar ni nchi, yenye mamlaka kamili ya ndani, ina KATIBA, ina rais, ina jeshi, ina mahakama, ina bunge, ina makamu wa rais na zaidi ina makamu wa pili wa rais.

Je Tanganyika ipo wapi????? ilikufa ili iweje???

Vita baridi ilishaisha tunaitaka nchi yetu ikiwa na mipaka ileile.

CCM wamekuwa na kapropaganda kakidikteta kwa mtu yeyote azungumzia Muungano, huitwa mchochezi na zaidi MUHAINI.- Ni faida gani ccm mnzopata kwenye aina ya muungano huu?

Mimi nashauri mfumo wa serikali TATU ndiyo suluhu ya manung’uniko ya wakaazi wa pande zote za muungano huu.


Na katika hili, historia ya wapigania uhuru wa nchi yetu iwekwe sawa, Inaamini kuwa wazee 17 kutoka pande zote za nchi yetu walishiriki kikamilifu kudai uhuru wetu kinyume na historia inavyopindishwa au kuaminishwa kwamba ni watu wa Kariakoo pekee walifanya hivyo.

Orodha ya waliodai uhuru wa Taifa hili ni kama ifuatavyo:


Julius Kambarage Nyerere, Ali Sykes, Lameck Makaranga, Gosbert Milinga, Gelmandus Pacha, Joseph Kimalando, Japhet Kirilo, Abubakar Ilanga, Saadan Kandoro, Suleiman Kitwara, Kisunguta Kabara, Chewa Said Chewa, Dosa Aziz, Patrick Kunambi, Joseph Kasela Mbantu, John Rupia, Abdulah Sykes

Kama kuna yeyote niliyemsahau naomba masahihisho wanamnakasha wenzangu!
 
Haina maana? hivi chama kilichodai Uhuru na waasisi wake waliofikiria kuiunda unasema haina maana? Unamjuwa Sheikh Takadiri, nilkubandikia post ya Mohamed Said inayomuelezea naona umeamuua kuuchuna.

hapa unatakiwa kutuelimisha juu ya umuhimu wa hoja kwamba TANU iliasisiwa Burma ambalo lilikuwa ni koloni lingine, na sio Tanganyika ambayo nayo ilikuwa ni koloni lingine kwa mujibu wa mipaka ya Berlin Conference (1885);
 
Nakubaliana na wewe 100% kwenye nyekundu, kwenye buluu umechakachuwa, nnakuuuliza tena, umesahau au hujui kuwa TANU iliasisiwa Burma?

Nitachakachuaje historia ambayo inaeleza kwamba hao kumi na saba ni founders wa TANU?

Narudia tena kwamba unatakiwa kutuelimisha juu ya umuhimu wa hoja kwamba TANU iliasisiwa Burma ambalo lilikuwa ni koloni lingine, na sio Tanganyika ambayo nayo ilikuwa ni koloni lingine kwa mujibu wa mipaka ya Berlin Conference (1885)
 

Barubaru,

Mtu kama Mzee Jumbe Tambaza mwenye historia Dar es Slaa kwa wasiomjua eneo la Muhimbili Hosptal lilikuwa mali yake. Leo hii hayumo hata kati ya wale wanachama 20 wa mwanzo wa TANU.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…