Maandiko ya Ben niliyaona kule kwenye mjadala juu ya Kambona,
Juu ya Kambona na Mwalimu Nyerere watu wengi wamepandikiza hoja na mijadala isiyo sahihi,
Hakuna aliyewahi kumsikia Nyerere au Kambona enzi za uhai wao kuwa wao wanamgogoro,
Ukweli unasimama kuwa Kambona alikuwa na mgogoro na serikali ya Tanzania, hilo lilikuja baada ya kuasi tu na sio Mwalimu Nyerere!
Wenzake Bibi Titi Mohamed siku wapofikishwa Mahakamani yeye aliikimbia nchi na kwenda uhamishoni nchini Uingereza alikoishi hadi 1993 aliporudi tena katika ardhi ya Tanzania hiyo ni baada ya mfumo wa vyama vya siasa huria!
Sahihisho:
Kambona alirudi home 1992 tena kiubavu ubavu pamoja na Lyatonga Mrema kutishia kumkamata atapokanyaga ardhi ya TZ! na baadae alihutubia ktk uwanja wa Jangwani na mimi nilikuwepo siku hiyo Kambona akaanza kuwataja wapigania uhuru wa Tanganyika na kuwaombea dua na mwisho kuwaomba Nyerere, Amir Jamal na Kawawa kurudisha fedha za wananchi walizoweka Benki za Uswisi!
Nyerere baadae alijibu tuhuma hizo na kuchekesha watu pale alipomtetea Kawawa na kusema kama ni yeye hana neno kuhusu fedha hizo ila Rashidi kwa anavomjua hawezi kuwa na fedha hizo Ulaya!