Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Tunamuona Mzee Mwanakijiji, yuko chini, chali, si yeye tu jamani, hata sisi hii ngumi iliyompeleka chini hatukuona ilipotokea.

1........2.........3..........4..........5.........6...........7.........8.........9.........."Knocked out, totally flat out". Hili sumbwi lilikuwa fupi lakini ni zito sana, tunaona anagaragara chini pale, miguu kila mmoja umeelekea unakojuwa wenyewe, refa anakwenda kumtoa kile kiziba meno asije akakosa pumzi, tunamuona promota wa pambano hili Yericko Nyerere ameinamisha kichwa chini akiwa na huzuni.

Mohamed Said kama kawaida amenyanyua mikono yote miwili juu akiashiria ushindi hata kabla refa hajatangaza. Hata jasho halimtoki, hii jamani ni ile ngumi inayoitwa "phantom" Mzee Mwanakijiji hakuiona ilipotokea, ngoja tusubiri akiamka, tumuombee aamke salama maana anatapatapa pale chini...

Baada ya dakika kumi za kulala chini bila fahamu tunaona Mzee Mwanakijiji kaamka pale kwa kusaidiwa na Ritz huku bado miguu haikanyagi chini vizuri, sumbwi limemlewesha, tunamsikia anaongea aahh anasema Khalifa Hamis, jamani kachanganyikiwa bado, anasema hovyo. Tunaomba watu wa kona yake wakina Mag3 na Nguruvi3 na promota wa pambano hili na mshabiki mkuu Yericko Nyerere wamsaidie mwenzao, kajeruhiwa vibaya sana.

Pigo lililonyooka, pigo takatifu.
 
Mambo ya kike haya nayo tuiite HISTORIA! Mzee Mohamed, hukupaswa kuyaandika haya.
 

Zomba,

Ahsante sana.
Sina zaidi.

Allah akujaze kheri.
 

Ha haa ha! Anasema zamani alikuwa anakipuuza kitabu cha Mohamed Said saizi ameamaua kukichambua ili wasomi wakifahamu sijui anazungumzia wasomi wa wapi.

Cha kuchekesha anataka kuchambua kitabu wakati historia ya TAA na TANU hana.

Kila anapogusa anakutana na nondo.
 

Basi kama unaamini haya masimulizi na unasema una umri huu wote na huwezi kuuliza maswali sahihi basi kuna tatizo kubwa zaidi.
 
Mambo ya kike haya nayo tuiite HISTORIA! Mzee Mohamed, hukupaswa kuyaandika haya.

WC,

Mambo ya "kike" hao ni mama na bibi zangu.
Ahsante sana.

Nimechota mengi kutoka kwao.

Kama si hawa akina mama zangu wewe
ungekisikia wapi kisa hiki cha sumu?

Wapi ungesikia kuhusu kabati la fedha la
Abdu Sykes lililokuwa wazi kwa TANU?

Mambo ya "kike."
Ahsante sana.
 
Mambo ya kike haya nayo tuiite HISTORIA! Mzee Mohamed, hukupaswa kuyaandika haya.

Umekosa hoja. Andika yako unayoona yanapaswa kuandikwa, kamtazame mwenzako Mzee Mwanakijiji bado yupo ICU, kala sumbwi takatifu.
 
Last edited by a moderator:
Basi kama unaamini haya masimulizi na unasema una umri huu wote na huwezi kuuliza maswali sahihi basi kuna tatizo kubwa zaidi.


Tunaona Mzee Mwanakijiji kaamka, anaanza kumshambulia mtu aliyemsaidia kumnyanyua, inaonesha bado ngumi imemlewesha na amesahau alikuwa na nani ulingoni, bado fahamu hazijamrudia Msaidieni jamani, kachanganyikiwa. Ohoo sasa anasema Mwanza, ilikuwa ni Bagamoyo kwa Sheikh Ramia, kasahau jamani.
 
Last edited by a moderator:
M,


Hakuna anaeweza kupinga uwezo wa Nyerere wakati
wa kudai uhuru.

Lakini uzi huu hatubishani kwa hilo.

Hapa kuna swali la Nyerere kuasisi TANU na mchango
wake na Kanisa katika kuupiga vita Uislam baada ya
uhuru kupatikana.

Mwisho ni nafasi ya Waislam katika kuutokomeza ukoloni.
 
M,


Hakuna anaeweza kupinga uwezo wa Nyerere wakati
wa kudai uhuru.

Lakini uzi huu hatubishani kwa hilo.

Hapa kuna swali la Nyerere kuasisi TANU na mchango

Nyerere hakuwa miongoni mwa waasisi wa TANU tena Rais wao?


wake na Kanisa katika kuupiga vita Uislam baada ya
uhuru kupatikana.

Mwisho ni nafasi ya Waislam katika kuutokomeza ukoloni.

Hadi leo hii hujaweka neno hata moja baya la Nyerere ama dhidi ya Uislamu au dhidi ya Waislamu. Huna hotuba, hona andiiko wala huna rekodi yeyote ambapo unaweza kusema "Nyerere alisema hivi kuhusu kuukandamiza Uislamu au kuwanyima Waislamu haki zao".
 
Akili yako na uwezo wako wa kufikiri ni zaidi ya simulizi hizi za akina mama. Tuwekee simulizi zote kama unaweza! Tuwekee Abdu alivyowazaa akina Meya wetu,..., Abdu alikuwa anastarehe wapi na nani,...
 
Basi kama unaamini haya masimulizi na unasema una umri huu wote na huwezi kuuliza maswali sahihi basi kuna tatizo kubwa zaidi.

Bahati nzuri mimi nakusoma siku nyingi kwa kukumbusha tu nimeanza kusoma toka pale Nyerere alipokuwa anampigia kampeni Mkapa pale Mwanza kwenye uwanja wa Nyamagana, mie nilikuwa nipo kwenye jengo la Posta pembeni ya uwanja. Nilisoma ulichoandika wakati huo bado upo CCM ujaenda Chadema.
 
Akili yako na uwezo wako wa kufikiri ni zaidi ya simulizi hizi za akina mama. Tuwekee simulizi zote kama unaweza! Tuwekee Abdu alivyowazaa akina Meya wetu,..., Abdu alikuwa anastarehe wapi na nani,...

WC,

Inawezekana umetoa kauli hii kwa kutojua.
Hayo maneno ni MATUSI MAKUBWA.

Abdu Sykes ni baba yetu na mama yake
Kleist ni mama yetu.

Tufanye mjadala wa historia ya TANU na
tuchunge murua na mipaka ya adabu.
 
Akili yako na uwezo wako wa kufikiri ni zaidi ya simulizi hizi za akina mama. Tuwekee simulizi zote kama unaweza! Tuwekee Abdu alivyowazaa akina Meya wetu,..., Abdu alikuwa anastarehe wapi na nani,...

Alikuwa anastarehe Arnatouglou na Nyerere.
 

MM,

Tatizo si hilo.
 
Uislam upi alooupiga vita Mwalimu? Huu wa akina Rashid Kawawa, Salim Ahmed Salim, Abdulrahman Moahamed Babu, Amani Abeid Karume, Harith Bakari Mwapachu, Jakaya Mrisho Kikwete, Mohamed Gharib Bilal, ..., au huu wa akina Mohamed Said, zomba, Ritz, Ponda Issa,...

Uasisi wa TANU ni kule Burma, kwenye mafaili ya Abdu, Vichwani mwa akina Abdu au 1953- 7.7.1954?
 
Last edited by a moderator:

Mohamed Said

Unaweza kututhibitshia kuwa Mwalimu alipiga VITA uislamu baada ya Uhuru?

Acha kudanganya watu kweupe hivi, nimekwambia zaidi ya mara 20 hapa jukwaani kuwa baada ya uhuru Mwalimu alianza mageuzi makubwa ya kufuta UDINI katika NCHI, sio kufuta uislamu bali kuufuta udini!

Ndio sababu za kulivunja baraza la wazee wa TANU baada ya kubainika limeingiza UDINI ambao ni hatari kwa ustawi wa Taifa, kumbuka nilikuuliza swali hili hapo nyuma kwa lengo maalumu lakini ukapepea kama kawaida yako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…