Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nitajitahidi kutafuta kwenye hifadhi za kumbukumbu,

Mshume Kiyate inafahamika wazi kuwa alikuwa rafiki wa karibu na mzee, nitajitahidi kupata picha zao pia.

Kwa kuwa umekubali kuwa Mshume Kiyate alikuwa ''rafiki wa karibu'' wa baba yako nakuwekea hapa kisa cha Mshume Kiyate na Julius Nyerere.

Nakuwekea hapa kwa kuwa naamini baada ya kusoma utachukua juhudi kuwaeleza wakubwa wampe heshima yake rafiki wa baba yako na wabadilishe kibao cha Mtaa wa Tandamti kisomeke ''Mshume Kiyate.''

Kifuatacho ndicho kisa chenyewe ambacho Nyerere alikipa jina ''the TANU spirit:''

Mwalimu Nyerere siku moja akizungumza na Dossa Aziz, Lucy Lameck, na Ahmed Rashad Ali katika kukieleza kile alichokiita ''the TANU spirit'' yaani ghera ya wana TANU alisema kuwa siku moja wakati wa kudai uhuru alikuwa anatoka nyumbani kwake Magomeni akija Kariakoo kwa miguu akielekea sokoni kutafuta mahitaji yake, lakini mfukoni alikuwa hana hata senti moja.

Njiani akakutana na Mzee Mshume Kiyate. Alipomuuliza anakwenda wapi, alimfahamisha kuwa anakwenda sokoni lakini hana fedha za kununua chochote. Mzee Mshume aliingiza mkono katika koti lake akatoa shilingi mia mbili akampa. (Ukitaka kujua thamani ya fedha ikutoshe tu kuwa wakati ule inasemekana nyumba ya vyumba sita kujenga Kariakoo ilikuwa inagharimu shilingi mia tano).

Kutokana na hali hii Mshume Kiyate aliona itakuwa ni kumtwisha Nyerere mzigo ikiwa atakuwa anashughulika na kuwatafutia wanae chakula na wakati huo huo anafanya kazi za TANU. Mzee Mshume akajitolea kuihudumia nyumba ya Nyerere kwa chakula.

Alifanya hivyo hadi uhuru ulipopatikana. Baada ya uhuru Nyerere alimwomba Mzee Mshume aache kufanya hivyo lakini alikataa na akamtafadhalisha Nyerere aendelee kula chakula chake na kile ambacho kinatolewa na serikali kwake yeye kama mkuu wa nchi alimuomba Nyerere awape wageni wake.

Mzee Mshume alifanya mengi katika kudai uhuru na baada yake. Baada ya maasi ya wanajeshi wa KAR tarehe 20 Januari, 1964, kuzimwa na Jeshi la Kiingereza, TANU ilifanya mkutano mkubwa sana Jangwani.

Mzee Mshume kwa niaba ya wazee wa TANU alipanda jukwaani na kumvisha Nyerere kilemba kama ishara ya kumuunga mkono. Picha ya mzee Mshume akimvisha Nyerere kilemba ilichapishwa katika magazeti mengi.

Halikadhalika picha nyingine mashuhuri ya Mzee Mshume na Nyerere ni ile iliyopigwa Novemba 1962 wakati wa Uchaguzi Mkuu. Picha hiyo inamuonesha Mzee Mshume akiwa amevaa koti, kanzu na kofia amemshika Nyerere mkono akimsindikiza kupiga kura.

Magazeti ya Chama na Serikali - Uhuru na Daily News yamekuwa yakiitumia picha hii kila baada ya miaka mitano katika uchaguzi wa rais kama njia ya kuwahamasisha watu kupiga kura na kumchagua Nyerere.

Kwa bahati mbaya si chama wala magazeti hayo yamekuwa na ujasiri wa kuandika maneno chini ya hiyo picha kueleza lini picha hiyo ilipigwa na huyo aliyekuwa kwenye picha na Nyerere ni nani.

Mwaka 1995 watu wa Dar es Salaam walipoamua kuubadilisha jina mtaa aliokuwa akiishi Mshume Kiyate, Mtaa wa Tandamti na kuuita ''Mtaa wa Mshume Kiyate'' kwa kuthamini mchango wake katika kupinga ukoloni, wanasiasa wageni, wasiojua mchango wa Mzee Mshume na baadhi ya magazeti yanayomilikiwa na Wakristo walitia dhana kuwa kilichowasukuma watu wa Dar es Salaam kufanya hivyo ni udini.

Kitu cha kusikitisha ni kuwa wakati magazeti yanapinga hatua hiyo si chama wala Nyerere rafiki yake aliyetetea jina la Mzee Mshume kwa kusema kuwa alikuwa anastahili heshima hiyo.

Kama wahusika wanavyotishwa na kueleza Abdulwahid Sykes alikuwa na mchango gani katika historia ya Tanganyika, vivyo hivyo wahusika wanaogopa kumueleza Mzee Mshume alikuwa nani.

Abdulwahid akiwa Market Master soko la Kariakoo na Mzee Mshume akiwa mmoja wa wauza samaki pale sokoni, pamoja walifanya mengi kuhamasisha harakati na kupata michango kutoka kwa wauza biashara wa pale kuijenga TANU.

Hadi kitabu hiki kinachapishwa kwa mara ya kwanza katika lugha ya Kiingereza mwaka 1998 kibao cha kuutambulisha mtaa ule kwa jina la Mshume Kiyate hakijawekwa. Kisa hiki kwa mara ya kwanza kabisa kilihadithiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ditopile Mzuzuri Mkiwaona kada wa Chama Cha Mapinduzi.

Ditopile alikieleza kisa hiki kama alivyokieleza Nyerere kwa nia ya kuonyesha "moyo wa TANU." Kwa bahati mbaya waandishi wa magazeti wakapotosha kisa kizima.

Badala ya kutoa umuhimu kwa moyo wa ukarimu wa Mzee Mshume na kumuueleza kama mzalendo aliyejitolea katika kupigania uhuru, magazeti yakageuza maneno ya Ditopile kuwa masimango kwa Nyerere, yaani alikuwa akilishwa chakula bure.

Kwa ajili hii nafasi ambayo ingeliweza kutumiwa ili kueleza umuhimu wa Mzee Mshume ikapotezwa.

Kisa kingine cha kueleza "moyo wa TANU" ambacho Mwalimu Nyerere amepata kukieleza ni kile alichomueleza marehemu Profsesa Malima. Nyerere alikuwa anazungumza na Profesa Malima nyumbani kwake na katika mazungumzo Nyerere akamsikitikia Profesa Malima kuwa kuna watu wanamshutumu yeye kuwa hawapendi Waislam.

Nyerere alinyanyuka alipokuwa amekaa na kwenda chumbani kwake akatoka na moja ya picha za wakati wa kudai uhuru, akamuonyesha Malima. Nyerere akasema ''Profesa unaona picha hii, Waislam watupu, Mkristo ni mimi peke yangu, vipi mimi leo niwachukie watu walionifikisha hapa?''


Naamini hutakichukulia hiki kisa cha mapenzi, hisani, utu, huruma na wema baina ya baba yako na Mzee Mshume Kiyate kama ''ngano'' nyingine ya Mohamed Said. Bahati mbaya sana Mshume Kiyate amekufa na kuzikwa Nyerere hana taarifa na hakupata kusikika hata siku moja kumtaja, hata pale magazeti yalipokuwa yakipinga majina ya baadhi mitaa ya Dar es Salaam kupewa majina ya mashujaa wa uhuru, wazalendo wa Dar es Salaam, Nyerere hakusema lolote kuwaadhimisha wazalendo hawa kwa yale waliyofanya wakati wa kudai uhuru.

*Ahmad Rashad Ali ni yule niliyemtaja katika moja ya post zangu kuwa mwaka 1950 alikuwapo Nairobi Abdulwahid Sykes alipofanya mazungumzo na Kenyatta.
 

Lakini we, Yericko mbona mbishi kias hicho? Siunaambiwa kiasi marazote kua hicho kitabu cha kivukoni unacho kitetea hakina mpango hakija timia, kime ficha ukweli na ndio maana hivi sasa hakisomwi na wengi
 
Mohammed Said umemtaja Ditopile ambaye ni marehemu kama chanzo cha kisa chako hicho. Na mara zote unakwepa kujibu maswali ya msingi. Kwa mfano:

a. Kisa cha Ditopile nani mwingine anakifahamu? Na sijui ni mtu gani anaweza kufikiria katika akili timamu ati Nyerere alikuwa anatembea kwa mguu kwenda sokoni lakini mfukoni alikuwa hana kitu na kwa bahati nzuri akakutana na rafiki yake ambaye alimpatia fedha? Kweli unataka kusema Nyerere alikuwa anaenda sokono akitegemea kuokota fedha njiani? au kisa chenyewe kimetiwa chumvi? Bahati mbaya tulikuuliza mwaka jana uliwahi kumuuliza mama Lucy Lameck juu ya kisa hicho naye akasemaje? hukujibu wakati ule!

b. Kisa cha Kighoma Malima umeandika na kuacha swali. Je jibu la Malima lilikuwa nini baada ya Nyerere kuuliza ''Profesa unaona picha hii, Waislam watupu, Mkristo ni mimi peke yangu, vipi mimi leo niwachukie watu walionifikisha hapa?''
 
tuambiwe wewe ukweli ni upi unapomkanusha mwenzio.Kazi yenu kupinga kila kinachoelezwa lakini hamleti kilichosahihi.Tatizo nyerere alitaka historia ya kupigania uhuru imtambue yeye pekee.Ni mnafiki na mtovu wa shukrani wazee wetu wamempokea akiwa na kaptula,baadae anajaribu kuwafuta ktk historia ya nchi
 
Ndugu yangu. hakika skuli ni kitu muhimu sana na hasa unapozungumza na watafiti. Awali ya yote JE UNAJUA UTAFITI NI NINI? NI KITU GANI UNACHOWEZA KUKIJUA WEWE MWENYEWE WAKT KINATOKEA WEWE ULIKUWA HIJAZALIWA. Narudia tena kusema Skuli ni muhimu sana hususan unapo fanya mnakasha na watafiti. NA KWA KUKUSAIDIA ZAIDI SIKU ZOTE UTAFITI UNAPINGWA KWA UTAFITI NA SI KELELE NA KEJELI. KAMA UMESOMA VIZURI HUKO MWANZO WA MNAKASHA HUU TULIONA KUNA kitabu cha historia ya tanu KILICHOANDIKWA CHUO CHA kivukoni NA aHALI YANGU Mohammed Said AKAFANYA UTAFITI WAKE NA KUJA NA HISTORIA YA HIYO HIYO TANU ILIYOSAHAULIKA. Huo ndio tunaita usomi wenye kuelimika. Pole sana
 

Mzee Mohamed Said, kwamara nyinine napingana na wewe na kuiona ngano yako ni yakufikirika tu tena yakijiweni mchikichini (ditopile)

Ninafahamu vema urafiki wa Mzee Mshume na Mzee Nyerere tena kwa undani zaidi,

Urafiki wao ulikuja wakati Mwalimu akiwa ni kiongozi wa TANU mwaka 1957, tayari alikuwa na magari mawili, moja lile alilonunuliwa na Marealle na lingine alipewa na mzungu mmoja nimemsahau kidogo, huyu mzungu alikuwa nisehemu ya wafadhili wa TANU,

Kwakifupi ni kuwa Mwalimu alijenge urafiki na Mzee Mshume kwasababu ya mambo mawili tu.

1) Alikuwa mcheza bao hodari pale mtaa wa Tandamti hivyo Mwalimu alijifunza mchezo huo kwake.

2) Alikuwa na ushawishi mkubwa kwa wachuuzi wa pale sokoni kariakoo hivyo alikuwa mhamasishaji wa watu wa kariakoo sokoni kuiunga mkono TANU. Hilo lilikuwa tiketi ya Mwalimu kumpenda na kuwa karbu na rafikiye huyu.

Na zaidi mwalimu alikuwa ndie mfadhiri wa wazee wacheza bao katika kijiwe cha Mzee Mshume kwa kuwanunulia KAHAWA kila ifikapo machweo.

Hizo hadithi za akina Ditopile almaarufu wazee wa gahawa sio sahihi na umepotosha
mkuu na ninaamini wewe ni mkubwa kwa Ditopile, hivyo mengi unayajua kuliko yeye, siamini kama ulikubaliana ngano yake iwe stahiki kwako.

Hata baada ya uhuru, urafiki wao uliendelea kuimarika, lakini hilo sio hoja kuwa kwanini Mwalimu hakumuenzi rafikie huyu kwa kutetea mtaa uitwe jina la Mzee Mshume.

Kumbuka mwalimu alikuwa na marafiki wengi wakubwa na wadogo, nje na ndani ya nchi, hivyo sio kila rafiki angemuenzi.

Labda nikuulize, kuna rafiki wa Mwalimu Nyerere ambae Mzee Nyerere alimpenda zaidi ya Msweeden aliyekuwa mfadhiri mkuu wa nchi hii?

Katika vitu vilivyomliza Nyerere katika uhai wake alikuwa ni Msweeden, nchi ikaingia kwenye maombolezo utadhani msiba upo hapa nchini kumbe msiba upo Scandinavia huko.
 

Najua lazima mtapata tabu kuamini haya nisemayo kwa kuwa
mmenyanyukia mmekuta TANU iliyokuwa inajiweza sana.

Mmeikuta TANU ina hazina ya serikali haina shida.
Lakini ukweli ni kuwa hata Mama Maria alifunguliwa biashara ya
kiduka mkoba Mtaa wa Mchikichi akiuza mafuta ya taa.

Unasema nimuulize Lucy Lameck kuhusu mambo niliyoeleza.
Mbona huo ni muhali?

Hivi kweli mimi habari za Nyerere na TANU nikamuulize Lucy
Lameck?

Haya mambo yote yanatendeka wazee wangu wanayaona na
wako na Nyerere leo niwatilie shaka hawa kauli yao nikamwamini
Lucy Lameck?

Ngoja nikufahamishe hapo sokoni Kariakoo walikuwapo wazee wangu
wengi tu.

Aliwapo Sharif Mwamadi pale Karikoo huyu mimi ni babu yangu. Yeye
alikuwa na biashara ya kuku. Akimjua vyema Nyerere akimuona akija pale
ofisini kwa Abdu Sykes.

Alikuwapo Shariff Mbaya Mtu. Alikuwapo Shariff Attas. Alikuwapo Mzee Abdallah
muhudumu katika ofisi ya Abdu.

Huyu Mzee Abdallah ndiye alikuwa akichukua kuku walokuwa wakitolewa na wana
TANU pale sokoni akichinja na kupeleka nyumbani kwa Abdu kama kitoweo cha Nyerere.

Pale Mtaa wa Mchikichi kwenye duka la mafuta ya taa ilikuwapo nyumba ya Mwalimu
Bahia shoga wa mama yangu.

Hivi kweli niwaache hawa wote nikatafute habari za TANU kwa Lucy Lameck.
Mama Maria yu hai watafiti wanaweza kumuuliza kuhusu siku zile za mwanzo.

Naamini bila shaka watapata habari kamili za harakati zilivyokuwa miaka ile ya
1950.

Nasisitiza kama ilivyo kawaida yangu kuwa simlazimishi mtu kuamini niliyoandika.
Wasomaji wana akili watatafakari na kuamua wenyewe.
 
Hivi kwa nini kulalama kuhusu Nyerere wakati wa utawala wake tu Je miaka kumi ya MWINYI isingetosha kubadili mfumo , kwa nini NYERERE TU? JE KIKWETE, MKAPA.Nafikiri huyu SAID NI MDINI KUPINDUKIA nasikia kichwa kuuma kusoma. Wanahistoria waliobobea wanajua kuwa maisha ya mifumo ni kutokana utwala wa kizungu Nyerere alipambana kulingana na uwezo wake MWINYI alitakiwa kuweka misingi ya kuwakumbuka wapigania uhuru ambao walisaulika. Mkapa naye kwanini? Nyerere tu?
 
ndio nyerere ni mbaya sana,ndo ameleta malalamiko yote unayoyaona.Ameweka matabaka na misingi mibaya ya udini nchi hii Mohamed Said anaweka wazi unafiki na ubaya wa huyo mzee nyerere kuficha ukweli juu ya wazee waliopigania uhuru
 
Last edited by a moderator:

Unajua Yericko hii post yako ni nzuri sana tatizo unaandika umekasirika
kwa hiyo unajaza maneno ya kihuni.

Lugha ya ujuvi inaondoa ladha yote ya yale usemayo.

Naomba nikusahihishe kidogo.
Ditopile ni mkubwa sana kwangu.

Mimi ni sawa na mdogo wake marehemu Abdallah.
Hilo la kwanza.

La pili Mshume Kiyate hakujuana na Nyerere 1957.
Alijuana na Mshume Kiyate 1953 alipoacha kazi na kuja
kukaa na Abdu mjini Dar es Salaam.

Pale sokoni Kariakoo Abdu alikuwa na wenzake wanaharakati
walokuwa wanapanga njama dhidi ya serikali hapa wakisubiri
kuibuka na TANU.

Kundi hili la soko la Kariakoo ndiyo watu wa mwanzo kufahamiana
na Nyerere na kukata kadi za TANU.

Mjomba wangu Bwana Hamisi ni mmoja wa wafanyabiashara hao na
yu hai hadi leo.

Hizo gari usemazo kama zilikuja hapo itakuwa miaka ya mbele sana kwa
maana gari aliyotumia Nyerere ilikuwa ile alotoa Dossa kisha TANU
wakanunua Landrover iliyokuwa ikiendeshwa na Said Tanu.
 
Ukumbi ungenufaika pakubwa sana kama ungechangia katika hayo niloweka kwenye post.
Naamini sote tungenufaika.
Leo hii kama rais wa nchi hii angekuwa Mkatoliki ungesema anadidimiza maendeleo ya mikoa ya kusini kwa kujenga bomba la gesi kuja Dar kwa sababu mikoa hiyo ina waislam wengi.
Nitachangiaje wakati hoja hazijibiwi. Angalia post ya #569 . Ni ukumbusho tu wa mlolongo wa vitu vingi ambavyo huwezi kuvitetea...
 
Yeriko, una admit kuwa kitabu kilichoandikwa na chuo cha kivukoni kimeacha historia kubwa sana.

Mzee Mohamed Said anakuja na kujaza mashimo, wewe unakataa. Hebu tuambie, kitu gani hasa unakataa kilichoandikwa na mzee Mohamed Said? Na kwa misingi gani unakataa?

Hilo la kwanza, la pili, weka nafasi katika ubongo wako wa kupokea mambo ambayo huyajui. Unaweza kuwa umekulia katika mazingira flani huku ukiamini A lakini kama kuna ushahidi wa kubatilisha imani yako ya A na kuwa B ndio sahihi, weka nafasi wa kulipokea hilo, fanya upembuzi yakinifu.

Msomi yeyote huja na counter argument based on facts. Na wewe tupe facts ili mjadala uendelee uzuri. La kama huwezi, funga mjadala

La mwisho, mzee Mohamed Said katika majibu yake yote, hatumii lugha ya jazba na ya kejeli. Haiti argument zako "ngano". Na wewe tunategemea umpe heshima hiyo. Kama mmepishana kwa arguments, isiwe ndo sababu ya kutumia lugha mbovu kama "simulizi za vijiweni" n.k.

Nawasilisha
 
Nina assume na ushahidi alioutoa Mohamed Said na wenyewe unaita ni facts.
Leo hii mimi nikikuambia fulani alininong'oneza kitu fulani utayaita hayo maelezo facts?
 

Ahsante sana ndugu yangu.
Bwana Nyerere amekumbana na mtihani mkubwa sana.

Na wala usistaajabu.

Kila aliyesoma maisha ya Abdu Sykes alimaliza kitabu akiwa
na maswali mengi sana.

Wengine ni watu ambao walikuwa na Nyerere katika serikali lakini
wameingia TANU baada ya uhuru.

Kuna wenye ujasiri wamenitafuta wanione khasa kama kweli mimi
nipo na nisemayo ni kweli.

Prof. Haroub Othman yeye alikwenda hadi kwa Nyerere na kumuomba
aandike maisha yake ukweli ujulikane.

Khasa katika nafasi yake kama muasisi wa TANU na njama dhidi ya Uislam.
Prof. Haroub alimtahadharisha Nyerere kuwa asipofanya hivyo hadhi na heshima
yake itaathirika vibaya.

Hii ilikuwa mwaka 1998 wakati kitabu kilipotoka kwa Kiingereza huko Uingereza.

Leo hii lile alilotabiri Prof. Haroub ndilo hili tunashuhudia.
Leo tuko katika mjadala mkubwa.
 
Nina assume na ushahidi alioutoa Mohamed Said na wenyewe unaita ni facts.
Leo hii mimi nikikuambia fulani alininong'oneza kitu fulani utayaita hayo maelezo facts?

Vijana wa leo mna bahati mbaya sana.
Mmekuta shuke zisizokuwa na vitabu.

Mmekuta vyuo vikuu visivyokuwa na maktaba madhubuti.
Mmekuta miji haina maduka ya vitabu isipokuwa vishelf vya
kuuza text book za shule chache sana.

Nyie mmekuja kwenye enzi ya kuona DVDs siyo kushika kitabu
ukasoma.

Mimi nimekuwa katika enzi ya vitabu, vitabu, vitabu na nilikuwa mkutubi
wa darasa langu.

Mimi ndiyo natunza vitabu.

Kuna maswali nayasoma humu ndani najua huyu muulizaji si mjuzi wa kusoma
na usomi wenyewe.

Jaribu kutafuta kitabu chochote ''memoir'' kinachoeleza maisha ya mtu fulani.
Soma utapata picha ya uandishi wa historia.

Hebu soma ''Long Walk to Freedom'' cha Mandela.
Soma ''Biography of Malcolm X'' cha Alex Hailey.
Soma ''Roots of Freedom'' cha Bildad Kaggia.

Hivyo vitabu huenda vikawa msaada kwako.
Ukipenda tafuta kitabu chochote cha Research Methodology.

Utafaidika.
 


ukitaka kumficha zuzu,weka ujumbe kwenye kitabu.

Ndugu yangu sisi tunafaham umuhimu wa kusoma,ndio maana tunakuelewa sana,,
"laqad anz'ranaa ilayqum kitaban' fihi dhikri'qum afalaa taa'qiluun'??"
tunaambiwa pia ya kwamba,,"hakika tumeshushiwa kwetu sisi kitabu ambacho ndani yake kuna mawaidha kwetu je hatufikirii na kuwa na akili??

Kwa kulitambua hilo hatukuwa wavivu kushughulisha bongo zetu kuichimba chimba elimu yenye manufaa,japo dharau nyingi zipo ya kwamba ni wakimbia shule na wakimbia kusoma,.,ila ukweli sisi hatujausiwa ububusa,,

nakufatilia vyema sana ndugu yangu.
 

"innal batil kanna dha'huuka"

NI KWELI SIKU ZOTE KWENYE HAKI NA BATILI,BATILI HUWA NI YENYE KUJITENGA.

TUTASHUHUDIA MENGI SANA.
 

Mimi sipo humu kutetea kitu chochote katika kitabu changu.
Wala simo humu kwa ajili labda ya kulumbana na mtu ili nishinde.

Mimi niko humu kueleza kile ambacho wengi hawakijui.
Naamini wazi kabisa wewe hukuwa unajua chochote kuhusu mbinu
zilizotumika kuanzisha chama cha TANU.

Hukuwa unajua hizo mbinu wala wapikaji wa mipango hiyo.

Lakini humu umesoma na kupata kile ambacho hakikuwa hadhir
kwako.

Hii ni hata kama unasema mimi sisemi kweli.
Hilo kwangu si shida.

Kuna wasomaji wengi sana lakini wao ni wasomaji tu.
Hawachangii.

Hawa naamini kabisa wanasoma humu na wanafaidika na
historia hii.

Napokea email nyingi sana za pongezi na pole kwa matusi na kejeli.
 

Nashukuru kwa kuwasilisha!

Hoja na maswali yako yote nimevijibu katika mnakasha huu tena kwa ufasaha,

Rejea majibizano yangu ya hoja na Mohamed Said post kwa post mpaka hapa tulipo utaona ndugu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…