Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

KUMBE TAA,hapo mwanzo ilikuwa kijiwe cha wazee wa kariakoo,kama ilivyokuwa SAIGON,asanteni sana kwa darasa
Ndio historia ya TAA maana kabla ya mapinduzi ya Abdul Wahid kumpindua baba yake na kuongoza, chama cha TAA kilikuwa kijiwe tu cha wazee wa Kariakoo tena niseme gerezani.. Hivyo enzi hizo wakristu wengi walikuwa wakiishi kuanzia Ilala kota Msimbazi na kuelekea Magomeni na hawakuwa sehemu ya kijiwe hicho.

Hivyo waliposhika kina Abdul uongozi ndio wakaanza kuchukua wanachama kutoka sehemu mbali mbali nchini pasipo kujali dini wala makabila na kukifanya chama hicho cha kisiasa. Walimhitaji Nyerere sana tu kutokana na elimu, kipaji na uwezo wake ktk kuwaunganisha Watanzania wote, jambo ambalo baadhi ya wanachama kina Takadir hawakupenda kuona TAA inachukua hata watu kutoka bara. Sasa tujiulize kama hawa watu kina Takadir hawakutaka watu kutoka bara, hicho chama cha TAA kingekuwa kinapigania Uhuru wa kina nani?
 

Mkandara,

Kijiwe cha kahawa unaweza kukipindua kweli na ukayaita mapinduzi.
 
Ritz nondo hizo,nimesema na ninarudia Mohamed Said humu JF alipa underestimate-watu wameshusha zana-mpaka wote tumejua historia na where we stand in regards to watu kama MS
 
Last edited by a moderator:
Mkandara,

Kijiwe cha kahawa unaweza kukipindua kweli na ukayaita mapinduzi.
Sikusema kilikuwa kijiwe cha Kahawa isipokuwa chama hicho hakikuwa na lengo la kuutafuta Uhuru isipokuwa haki zao kama wafanyakazi maana walikuwa vijana wakati huo wakifanya kazi bandari na wengine makarani tu.
 
you never learn,mwachie Mohamed Said hajibu haya mambo-huoni kwamba kakaa kimya anaogopa kunasa kwenye corner

Kwa akili yako mimi naweza kumzuia Mohamed Said kutojibu. Mohamed Said habari ingine wote mtatosha yumo humu mwezi sasa ukiona yupo kimya hujue anakusanya "Component"
 
Last edited by a moderator:

1) pitia hii kuhusu hoja yako ya Waluo hapo juu: Decolonization & Independence in Kenya: 1940-93 By Bethwell Allan Ogot, William Robert Ochieng'.

2) Mimi sikusomeshwa bure na Nyerere, hizo fedha alikuja nazo kutoka Mwisenge?

Mengine ni fikiria zako na una haki ya kufikiri upendavyo.
 
Sikusema kilikuwa kijiwe cha Kahawa isipokuwa chama hicho hakikuwa na lengo la kuutafuta Uhuru isipokuwa haki zao kama wafanyakazi maana walikuwa vijana wakati huo wakifanya kazi bandari na wengine makarani tu.

Mkandara mbona ueleweki mwanzo umesema TAA ilikuwa kijiwe tu tena gerezani hapo hapo unasema Abdulwahid na Mwapachu walipindua mie ndiyo nakuuliza unajua maana ya mapinduzi hivi ukienda kufunga kijiwe pale Msimbazi utayaita hayo ni mapinduzi unapindua nini ili iweje.
 
Mkuu wangu, Hao kina Ogot na Ochieng wameandika kwa jinsi walivyosimuliwa na ku base upande mmoja kama Mohammed Said kama vile kuna ukweli wasijitazame wao, lakini wakati huo huo UHURU haukuletwa na Mjaluo isipokuwa Mkikuyu alonyimwa elimu na ndiye alimwaga damu yake.

Hivyo, ukiitazama historia ya Kenya utakuta ni wanyonge walopigana kuikomboa nchi hiyo, wakati Waluo walokuwa wakiwa support wazungu leo wanapiga makelele. Huyo Ogot na Ocheing ni sawa na Mtikila akiandika kitabu kuhusu Uhuru wetu anaweza kuandika mengi ya ukweli dhidi ya Nyerere ambayo wewe msomaji ndiye unatakiwa kuyapima maandishi hayo kufahamu yana malengo gani
 
Umesoma bure,na leo matunda tunayaona unapiga keyboard,elimu imekujuza mengi,mpaka life expectancy yako imepanda,anything else ungekuwa history-inabidi ushukuru sana huu mfumo-nchi kama kenya ungekuwa mnywa ghahawa 24/7
 
Maana ya Mapinduzi ni kuondoa uongozi uliopo madarakani pasipo hiyari yao na ndivyo walivyofanya Abdul na Mwapachu, labda muulize Mohammed Said akufafanulie zaidi. Chama chochote kinakuwa na uongozi hata kiwe cha Mpira au bao maadam kinaitwa chama hua kina viongozi na wanachama wake.

Kwa hiyo Abdul Wahid alipochukua Uongozi wa TAA sii kwa hiari ya baba yake Kreist ama viongozi wengineo isipokuwa Abdul Wahid na Mwapachu walikaa na kuona haja na sababu ya kijiwe hicho kichukue mwelekeo mpya wakachukua uongozi wao na mwelekeo mpya..
 

Hao wazee wake ni wazee wa Kiarabu na baadhi ya Waafrika walioiga utamaduni wa Kiarabu. Lakini hazungumzii hao wazee wa kiarabu walivyochukua ndugu zetu utumwa. Yeye shida na adui ni Mkiristo na Ukristo hapa Tanzania. Niliandika siku za majuzi kuwa kwanini lawama anapewa Nyerere na Ukristo pasipo kujadili japo kwa kiasi tamaduni za watu wa Pwani amabao kwa kiasi pia zimewafanya wawe tofauti na jamii za bara?? Watu wa Pwani wao kwao wanaona ni fahari kujinasibisha na Uarabu ndio mana hakuna mahali wanalalamika ujio wa Waarabu katika eneo letu. Lakini ukizungumzia atahri za wakoloni ukataja Wazungu pekee bila kuwataja Waarabu bado utakua hujaeleza athari hizo vema.

Wayahudi walibaguliwa sana Ujerumani na Ulaya yote, waliteswa, kuuwawa kubaguliwa sana, lakini vyote hivyo havijawazuia Wayahudi kuendelea. Sasa je Nyerere alifanya hata kwa sehemu ubaguzi au unyama kama wa Hitler kwa Waislamu wa Tanzania??
Siku zote binadamu ni wazuri sana kutafuta sababu zaidi ya ufumbuzi wa tatizo.

Labda namimi nianze kuandika na kudai juu ya wazee wa kabila langu amabao hawajatajwa katika historia ya nchi hii.
 
Katika hili mkuu wangu unataka kupotosha Ukweli maana waliotuchukua utumwani ni WAZUNGU, hao waarabu walikuwa madalali tu kama waswahili wengine kia Tip tip kutokana na kwamba wao walikuwa na access ya kuingia bara wakakusanya watumwa na kuwaleta Pwani kuwauza kwa wazungu, tena soko likiwa ktk makanisa yenye under ground tunnel. hakuna merikebu wala hata moja la watumwa lilotoka Zanzibar au Tanganyika kwenda Oman kuuza watumwa...
Enzi hizo Utumwa ndio ulikuwa dhahabu na hivyo mwarabu asingekusanya watumwa kama soko lisingekuwepo Marekani na Ulaya..
 
Baada ya mapinduzi hayo wakamtafuta kafir msomi Dr. Vedasto Kyaruzi wakamfunda, wakamfundisha kuvaa, wakamfundisha siasa...kisha wakamkabidhi madaraka awe Raisi wa kwanza wa TAA...je kwa nini baada ya Abdulwahid kumpindua baba yake, ikawa lazima atafutwe huyo wa kuja kuiongoza TAA?
Wakamtafuta kafir Nyerere, wakamfunda, wakamfundisha ustaarabu wa mjini, wakamfundisha siasa na alipoiva wakamkabidhi uongozi wa TAA na miezi kumi na tano baadaye baada ya wazee hao wa Gerezani kuunda TANU wakamkabidhi uongozi awe Raisi wa kwanza wa TANU.

Mkuu Mkandara, ni kwamba tunarudi kule kule...wazee wa Mohamed Said baada ya kuunda AA mwaka 1929 wakamtafuta msomi, wakuja Myao, CEcil Matola, wakamfunda, wakamfundisha ustaarabu kabla ya kumkabidhi madaraka awe Raisi wa kwanza wa TAA.

Hayo ndiyo maelezo ya Mohamed kuwa wazee wake ndio waliopigania uhuru, hao wengine walipewa tu madaraka...swali linalotusumbua wengine na gumu kulielewa ni kwa nini hawa wazee waliopigania uhuru si kama Watanganyika bali Waislaam, waliweza kukabidhi uongozi kwa makafir. Zuberi Mtemvu, Muislaam, akaamua kuanzisha chama (sijui kama yeye alikianzisha peke yake) lakini akakataliwa na Watanganyika kwa ujumla wao.

Kuona hivyo Waislaam ambao hawakutaka kuongozwa na makafir, wakaanzisha chama cha Waislaam AMNUT, lakini nao wakakataliwa na Waislaam wenzao. Kulingana na simulizi za Mohamed Said, tunashuhudia mara tatu wazee wake wanaanzisha vyombo na mara zote tatu wakakabidhi madaraka kwa makafir...kulikoni? Haya, hata baadaye kama wanayodai Kafir huyo huyo akaamua kuwaundia baraza lao BAKWATA lakini nalo wakalikataa!

Akaja Mwinyi, Muislaam mwenzao, akasema kila kitu ruhsa, akaamua kuvunjilia mbali misingi yote aliyojenga Kafir, akatuzalishia wachochezi na walalamishi...akina Ponda, akina Mohamed Said, akina zomba...duh!
 

Mkuu wangu mbona unayameza maneno yako mie nakuuliza wewe sina haja ya Mohamed Said wewe ndiyo umesema TAA ilikuwa kijiwe hapo ndiyo ugomvi wetu.

Mimi najua historia ya TAA kwa kusoma na kwa kuadithiwa najua kama Abdulwahad na Mwapachu walifanya mapinduzi kwenye chama na kumtoa ofisini Clement Mtamila.

Mwaka 1950 wakaitisha uchaguzi Arnatouglo na Dr Vedasto Kyarunzi alichaguliwa kuwa rais Abdulwahid Katibu wake.

Napingana na wewe kuwa TAA ilikuwa kijiwe. Unamjua rais wa kwanza wa TAA.
 
Yote uloandika ni ya kweli kabisa lakini sii Mwinyi alowaleta kina Mohammed said na Zomba isipokuwa Mwinyi ndiye alotuletea CCM tunayoikataa leo ya kina Lowassa, Rostam na wahuni wengine wengi wasiojali kabisa UHURU na UTU wetu bali KUTAWALA...Mwinyi ndiye alorudisha KUTAWALIWA na kina Mohammed Said wanayasikia machungu yake lakini hawataki kuona ukweli uliopo isipokuwa kurudi nyuma na kumtafuta mchawi..

Wewe hushangai Miafrika inalia na hali ngumu ya maisha na jinsi serikali ilivyowasahau lakini hawa hawa ndio wanaipigia kura CCM na kuvaa nmagwanda ya kijani na njano?..Mohammed Said, Zomba na hata Ritz ni member wa CCM wakereketwa, chama cha Nyerere ambacho kwa madai yao wenyewe ndicho kinawapa hali ngumu waislaam nchini toka Uhuru!!!..Hii kweli inaingia akilini?

Sisi wengine hatukuondoka CCM kwa sababu tunakichukia chama kwa sababu ya Kikwete muislaam, bali tunajua chama kimepoteza mwelekeo hatutafuti mchawi wakati unayetula yuu nguoni mwetu..
 

Mkandara sijasema uongo.
Wazungu walichukua utumwa sana nchi za Magharibi mwa Afrika kwani ilikuwa rahisi kusafirisha kwenda Amerika na Ulaya, kumbuka kipindi hicho Suez Canal ilikuwa haijajengwa ili kuwezesha meli za Ulaya kuja Pwani yetu kirahisi. Hapakuwa na haja ya kuchukua watumwa Afrika Mashariki ilihali palikuwa na wengi tena wenye nguvu na miili mikubwa Afrika ya Magharibi. Kumbuka biashara ya Utumwa ya Atlantiki (Atlantic Slave Trade).

Waarabu hawakua madalali tu, madalali walikuwa baadhi ya machifu kama Mkwawa,Mirambo n.k hawa waliwauza watumwa kwa waarabu, waarabu wakawapeleka Zanzibara kisha wakapelekwa nchi za Kiarabu. Watumwa waliopelekwa nchi za Amerika na Ulaya wapo hadi leo hii vizazi vyao lakini waliopelekwa nchi za Kiarabu ni wachache sana na kuna sababu mbalimbali zimetolewa katika hili. 1) walihasiwa (castration) ili wasije wakazaa na mabinti wa hao mabwana (masters) zao. 2) Hawakuruhusiwa kuoa mabinti wa masters zao. Lakini walipelekwa wengi tu huko. Tip Tip ni muarabu pia.

Kanisa la Angalikan la hapo Mkunazini lilijengwa siku za baadae wakati Uingereza ikiwa imepitisha sheria ya kuzuiz Biashara hiyo ya utumwa, hivyo walijenga kanisa maksudi ili kuwasaidia kupambana na biashara ya Utumwa.

Mkandara soma historia vema, ukitaja wakoloni pasi na kuwataja waarabu utakuwa bado hujawataja vema hao wakoloni.
 
Mohamed Said, pole sana! Huyu ndiye mkandara ambae nilikuambia before...huyu ni muislaam safi asiyependa ufiadini wala
udini. Maana wakina Nguruvi3 na mzee mwanakijiji walipokujengea hoja makini na kukuita wewe ni mdini uliwabishia kwa kuwaona wao ni wagalatia. Sasa huyu Mkandara ni Muislaam mwenzako. Haya kukurukanae kwa hoja sisi tunawasomeni.
 
Mkuu wangu wewe unazungumzia mwaka 1954 ile yote transformation ya chama wakati miye nazungumzia Kleist kama muasisi na sii viongozi wake..nani alikuwa nani sii hoja hapa isipokuwa malengo ya chama ndio malumbano yetu..Jiliwaze kidogo na habari ambayo hakuiandika Mohammed Said bofya
 

Kwanza uliandika hivi:

...Ebu fikiria Kenya leo wajaluo waliokuwa wamemezwa na Wakikuyu wakianza nao kuandika kitabu juu ya harakati za Wajaluo kupigania Uhuru watafika kweli....

Para ya pili kwenye post hiyo hiyo ukayaona makosa yako ukaandika hivi:

Pengine nimekosea ktk hilo maana Wajaluo wameanza nao kujitambulisha kama wao...

Mimi kwa kukuonesha tu kuwa Wajaluo wameshaandika sana tu historia yao, nikakuwekea hii:

1) pitia hii kuhusu hoja yako ya Waluo hapo juu: Decolonization & Independence in Kenya: 1940-93 By Bethwell Allan Ogot, William Robert Ochieng'.

Ingawa ulikubali kuwa umekosea lakini ikabidi tu ubishane na ukaunganisha Waluo na Mohamed Said:


Unajuwa unashangaza sana! hueleweki.

Usitake tuazishe darsa la Mau Mau na Waluo hapa. Sijui kama unaelewa kuwa Mluo leo hii ndio Rais wa USA?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…