Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Mkuu asante kwa hili darasa!mungu ukupe afya njema uendelee kutoa elimu hii
 
Ahsante sana kwa historia hii.

Lakini hebu pitia kumbukumbu zako.
Umemtaja Sheikh Issa bin Amir.

Nadhani umekusudia Sheikh Hassan bin Amir.

Hebu niweke sawa yule ni Maranta au Maranda?

Zidi kutupa darsa.
 

mkuu, kweli mzee Mshume halafu asiende kwenye maziko yake kama Sheikh Mohamed anavyodai?...hapa pahitaji utafiti.
 
Ahsante sana kwa historia hii.

Lakini hebu pitia kumbukumbu zako.
Umemtaja Sheikh Issa bin Amir.

Nadhani umekusudia Sheikh Hassan bin Amir.

Hebu niweke sawa yule ni Maranta au Maranda?

Zidi kutupa darsa.

Taarifa nilizo nazo ni kuwa aliitwa Shehe Issa bin Amir, na alikuwa ni mzee sana sawa na Kasisi Maranta kipindi wanakutana na kushauriana, huenda alikuwa baba wa Shehe bin Amir. Tuvute subira tafiti zijazo zaweza kuja kung'amua hili.


Ni MARANTA, uandishi tu ulinitereza.
 
Mkuu Mohamed Said,
Neno ngano umelileta nikajua ni wingi wa msamiati yako kama ule wa mnakasha uliotuletea hapa jamvini.
Sikujua laweza kutumbukia nyongo na kuleta muhali. Waungwana wanasema ada ya mja kunena kwa muungwana ni kitendo.

Sweke 34 kasema hujayatendea haki maoni yangu kwa kukimbia kupitia mlango wa ''ngano''
Platoozoom kasema yaweza kuwa ni maoni yangu kama unavyoniambia kila siku kuwa si lazima kuamini usemacho

Pamoja na yote hayo, nakusihi tuachane na ngano ili akina Warioba.E na wengine waliokuja kupata faida
waipate inshallah kwa mnakasha.

Kwa heshima ya wanajamvi naondoa neno lako ngano katika maoni yangu, basi nawe uwe radhia maridhyatan na utende haki kwa kujibu haya :


Kwa minajili ya mnkasha nisingependelea uchague maswali. Ningependelea uyajibu kama yalivyo.

Ahsante
 

Naaaam mkuu, bila shaka Mzee Said atajibu kwakuwa naamini ametawaliwa na busara za kiafrika.
 
Nasubiri mchango wa kanisa katika kupigania uhuru wa Tanganyika kama ulivyoahidi juzi.
Ukikamilisha tafadhali tushushie humu jamvini.
Hakuna mtu wala taasisi iliyopigania uhuru wa Tanganyika. Tulidai kistaarabu uhuru wetu kupitia UN na Waingereza walikuwa waelewa kwamba wao hawakuwa wakoloni wetu, wakatukabidhi nchi yetu, wakaondoka.
 
Hakuna mtu wala taasisi iliyopigania uhuru wa Tanganyika. Tulidai kistaarabu uhuru wetu kupitia UN na Waingereza walikuwa waelewa kwamba wao hawakuwa wakoloni wetu, wakatukabidhi nchi yetu, wakaondoka.

Sio kweli mkuu, watu walipigania uhuru wa nchi hii,

Hata Mkwawa, Kinjekitile, Mangi Sina nk walipigania uhuru

Soma makala ndogo niliyoieleza hapo juu
 

Itabidi nami niulize walionipita umri.

Sina kumbukumbu ya Sheikh Issa bin Amir sheikh ambaye alikuwa
na ushawishi kwa Waislam kiasi atafutwe na Father Maranta kuzungumzia
mambo makubwa ya nchi.

Lakini jambo ambalo nina hakika ni kuwa sheikh huyo hawezi kuwa baba
yake Sheikh Hassan bin Amir hata kwa mbali.

Nakushauri ujaribu "Sheikh Idrissa bin Saad" maana katika wakati huo usemao
yeye ndiye alikuwa sheikh maarufu kupita wote Dar es Salaam.

Sheikh Idrissa bin Saad alikuwa akikaa Mtaa wa Narung'ombe na Bonde nyumba
yake ikitazamana na msikiti wake.

Zipo taarifa kuwa kulikuwa na padri akimtembelea Sheikh Idrissa pale nyumbani
kwake na wakifanya mazungumzo ambayo hayakuwa ya faragha.

Hebu pita na huko.

Wajukuu wa Sheikh Idrissa bin Saad wapo na wanaishi nyumba hiyo hiyo
ya babu yao.

Ahsante kwa darsa.
 

Kwa kuongezea kaburi la Sheikh Idrissa bin Saad lipo hapo hapo msikitini kwake mtaa wa Narung'ombe.
 
Sio kweli mkuu, watu walipigania uhuru wa nchi hii,

Hata Mkwawa, Kinjekitile, Mangi Sina nk walipigania uhuru

Soma makala ndogo niliyoieleza hapo juu
Wote hawa hawakupigania uhuru wa TANGANYIKA. Walipigania uhuru wa himaya zao. Tanganyika haikuwepo wakati huo. Tanganyika imekuwepo baada ya vita kuu ya kwanza. Iandikeni historia ya Tanganyika kama ilivyo.
 
unaleta taarifa ambazo hujazifanyia utafiti.Labda utafiti wako unaufanyia hapa JF.haya maelezo yako yanaangukia neno lako kwamba ni ngano.Unachojaribu kuandika kipeleke kwa Mohamed Said akusahihishe kama anavyofanya hapa
 
Last edited by a moderator:
mkuu, kweli mzee Mshume halafu asiende kwenye maziko yake kama Sheikh Mohamed anavyodai?...hapa pahitaji utafiti.

Yapo maneno yakizungumzwa na wazee wa Dar es Salaam kuhusu kushiriki kwa Nyerere katika maziko ya wanaharakati Waislam.

Wanasema kuwa baada ya maneno yaliyosemwa baada ya maziko ya Abdu Sykes Nyerere aliona itakuwa bora ajitenge nao kwa mbali sana.

Unafahamu ikiwa Nyerere atahudhuria maziko ya mtu yoyote watu watataka kujua ule uhusiano kati yao.

Mathalan alipohudhuria maziko ya Abdu Sykes na akatembea kwa miguu nyuma ya jeneza la Abdu kutoka Mtaa wa Lindi hadi Msikiti wa Kitumbini kisha kutoka hapo hadi Makaburi ya Kisutu wasiojua uhusiano wa Abdu na Nyerere hata ndani ya TANU na serikali wakati ule walipigwa na mshangao mkubwa.

Jambo la kustaajabisha magazeti ya TANU chini ya Benjamin Mkaoa hayakupa uzito msiba ule ila walichoandika ni kuwa Nyerere kahudhuria mazishi ya Abdu Sykes.

Hawakueleza chochote katika mchango wake wa kumpokes Nyerere Dar es Salaam wala wa kufadhili TAA hadi TANU wala mchango wake katika kuasisi chama.

Rafiki zake Abdu kama Ahmed Rashad Ali na hata baba yangu wakawa wanasema inaelekea Nyerere hapendi kunasibishwa na historia yake mwenyewe.

Iweje Abdu asiandikiwe taazia sawa na makamu na heshima yake?
Hata binti yake Abdu alikasirishwa na jinsi historia ya baba yake ilivyopuuzwa na hawa wote walielekeza shutuma zao kwa Nyerere.

Sasa hata alipokufa Sheikh Hassan bin Amir Nyerere hakuhudhuria maziko yake, Sheikh Mohamed Ramia, Idd Tulio, Jumbe Tambaza, Dossa Aziz nk.

Swali likaja kuwa ule udugu watu hawa waliomfanyia Nyerere umekwenda wapi?
Mbona picha iliyojitokeza ni kama watu hawa hawakupata hata kujuana?

Ndiyo tena yakafuatia na haya mengine ya hao wote kufutwa katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
Leo gari alotoa Dossa kumpa Nyerere kwa ajili ya shughuli za TANU New Street hakuna ajuae inaulizwa gari ya Chief Thomas
Marealle ambayo iko Butiama.
 
unaleta taarifa ambazo hujazifanyia utafiti.Labda utafiti wako unaufanyia hapa JF.haya maelezo yako yanaangukia neno lako kwamba ni ngano.Unachojaribu kuandika kipeleke kwa Mohamed Said akusahihishe kama anavyofanya hapa

Pole sana mkuu, soma mantiki ya nilichokieleza,

Muulize Mohamed Said anaelewa maana ya tunachojadili hapa!
 
Last edited by a moderator:
Wote hawa hawakupigania uhuru wa TANGANYIKA. Walipigania uhuru wa himaya zao. Tanganyika haikuwepo wakati huo. Tanganyika imekuwepo baada ya vita kuu ya kwanza. Iandikeni historia ya Tanganyika kama ilivyo.

Mkuu naomba utupe 'darsa' kwa faida ya wengi,kunaweza ibuka mkanasha mwingine hapa ninavyoona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…