Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


We mzee una matatizo kweli yaani mimi nimeleta hansard wewe umeenda kujinukuu kuna ulinganisho hapo?? Halafu eti nimepoa, au sijui nimekukimbia hahahaha!!!! Nadhani hiyo hansard imekuchoma sana and I betcha ni mara yako ya kwanza kuiona halafu unatamba eti umeandika historia ya Tanganyika what a joke? Karibu JF.

Tatizo mzee wetu unafanya mjadala kwa ushindani na kinachokusumbua ni ile "trophy collecting mentallity" katika kila mjadala. Hiyo ningekushauri uwaachie vijana wako, haipendezi kwa umri na staha yako. Hansard hiyo ni fact kitu amabacho katika hadithi zako huweki. Yaani hata vipande vya magazeti vya wakati huo umeshindwa kuleta.

Unachotakiwa kufahamu sisi wengine tuko busy, you have to work, play some games, pick kids from school, sleep etc. Sasa wewe ndugu yetu uliyeamua kukesha humu you know how you get ur bread.
 

Wee mzee acha uongo, unakumbuka niliwahi kukuambia nini kuhusu hii ngano yako? Wewe kukutana na Haroub Othman, kumpa kitabu chako hakuna anayepinga lakini hili la uandishi wa bayografia ya Nyerere kuwa ni kutokana na kitabu chako ni uongo unaotakiwa kuuacha sasa maana tumeshakueleza lakini bado unakoleza tu as if that will turn into some truth.

Na hii ya kusema jambo hili lilieta ubishani sana hapa JF ai kweli, ulitoa tuhuma nikakujibu kwa evidence ukaishia kulalama na kusema "ooh! ni kitabu changu" Lakini kwa sababu ya ile "tropy collecting mentallity" unaendelea kushupalia uongo huu ili ionekane ulishinda hhahahahah ahahahaha. Muogope Mungu we Mzee. Haya nakukumbusha tena.


Wakati mwingine uone aibu Mzee Saidi.
 
Mzee ms,

Kwa story za namna hii mnaweza mkakesha, hakuna anae kuweza.
Sasa tatizo linakuja ukigongwa swali weeeee!!!???....
Unaluka kimanga..... Utasikia mala oooo hiyo ni historia ya wazee wangu, mala na nyie andikeni.
Jalibu uwe unajibu kila swali midhali upo hapa.
Tofauti na hivyo basi tujue tu kuwa una ajenda yako ya sili.
 

Na kwa taarifa yako Tanganyika in 1950 ilikuwa Trust Territory under UN charter na siyo Mandate Territory, soma Hansard iliyotundikwa open mindedly usiisome kwa jicho na angle yako ya siku zote.
 

Nyambala nisamehe kama nimekuudhi.
Mimi nishaeleza mara kadhaa kuwa sijinukuu.

Hayo niwekayo ni mfano wa kurasa kutoka kitabu
changu nakiweka watu wapate kusoma.

Kubwa huwa kwa mfano kwako sikudhamirii wewe.

Nawakusudia hawa wengine ambao historia hii hata
siku moja hawajaisikia.

Huna lolote kwa yale nilobandika jinsi mambo yalivyokuwa
TAA HQ 1950 na hali ya Mandate Territory?

Mimi si mtu wa kuchomwa kirahisi.
Waislam tunavumilia mengi nchi hii.

Na ni kweli hiyo Hansard sikupatapo kuiona lakini kutokuiona
hakukunizuia mimi kuandika historia ya wazee wangu.

Nakushukuru sana kwa kunionyesha nyaraka hii.
 
Duuh!
Nyambala, all I can say is ulikuwa wapi?

Mkuu huyu Mzee Said kuna wakati huwa naona hakuna haja ya kujibizana naye lakini kwa kwa trend ya hadithi zake ni dhahiri kabisa kuwa amenuia kuikoroga jamii ya watanzania come what may! Sasa halitakuwa jambo jema tukawa tunatizama tu, when time is available basi kuna umuhimu wa kuchangia to put the records straight.
 

Tatizo unaendelea kujinukuu hahahaha ahahahaha!!!!!!!
 

Nyambala,

Hayo yote hapo juu ulosema mie nimeyajua kabla yako.

Hayo niloeleza ni kweli kabisa lakini kama we unadhani
mimi ni mwongo na kwa hakika umeniita hivyo sina uwezo
wa kukuzuia.

Lakini kuna wengi wanaoniamini.

Ningekueleza mradi kama huo wa Oxford University Press
ambao ningehusika lakini nachelea ghadhabu zako.

Inaelekea akili yako inakataa kuwa hayo nilosema hakika sifa
inarejea kwangu.

Haroub Othman sikumpa kitabu changu na sikuwa na haja ya
kufanya hivyo.

Ukweli ni kuwa nimeandika mengi na wengi wananifahamu
kutokana na maandishi yangu.

Sina uwezo na hata wewe huna uwezo wa kuzuia hilo.
 

Unayafahamu haya hapa chini????







 
Tatizo unaendelea kujinukuu hahahaha ahahahaha!!!!!!!

Nyambala,

Sijinukuu.

Naweka hapa yale niloandika ili wasomaji wasome nilichoandika
miaka mingi ilopita.

Ikiwa inakukera ni bahati mbaya lakini wengi wananufaika na ndiyo
unaona uzi huu Insha Allah utagonga 100,000.

Hawa wanakuja kunisoma mimi.
Haya ninayoshusha hapa hawakupatapo kuyasikia hata siku moja.
 
Mbinu za kukwepa hoja tumezoea. Tutakuwepo hapa kuuonyesha ulimwegu jinsi gani unavyoghilibiwa.

Leo ulimwengu kuanzia Cambrige na huko USA wanaamini Nyerere alianza kutamka neno siasa baada ya kukutana na Sykes kwa mara ya kwanza alipofika Dar mwaka 1950. No thank you sir! big liar.

Leo ulimwengu unajua Jamiatul Islamiya iliuawa na Nyerere bila tamko! no thank you sir

Kwamba kilitakiwa kijengwe chuo kikuu kuchukua wanafunzi wa shule ya msingi Maneromango! uzushi mwema kabisa huu

Kwamba K.Sykes alianzisha chama peke yake na kuwa katibu mkuu! was this an NGO? No thank you sheikh

n.k.

Tutaonyesha contradictions zako bila haya aibu wala kificho.
This is the moment!
Relentlessly we will never give you the platform to spread malicious idea in order to divide the country on the basis of Manyema,Zulu, Nubis Moslesms, Christians etc.
 
Hapana. Kumetokea tatizo tangu Mwalimu alipofariki. RTD au sasa TBC ni chombo pekee ambacho kimeweka kanda za hotuba zote za Mwalimu na siyo kila Tom and Athumani anaweza kwenda pale na kuomba na kupewa kiholela. Nilichosikia ni kwamba wanasubiri mpaka pale Nyerere Foundation itakapokuwa na makao yake ziorodheshwe na ziwekwe pale ili kila mtu anayekwenda pale aweze kuzisikiliza kama walivyofanya wale waliojenga Memorial ya Martin Luther King jr hapa US.
It has nothing to do with mfumo. Nakumbuka 1985 Mwalimu alipokuwa anakaribia kustaafu nilikwenda pale na kuomba nakala kadhaa za hotuba zake kwa sababu nilikuwa natayarisha kipindi juu yake. Nilipewa. Lakini kwa sasa itakuwa vigumu kwa mtu kama Yericko kwenda pale na kupewa tu kwa sababu hizo nilizoziainisha hapo juu. Na kwa sababu aliyenisaidia kupata baadhi ya hizo hotuba 1985 bado yuko pale na nina hakika atanisaidia wakati huu kuipata hiyo hotuba ya kuaga kwake. Na ndio maana nimesema tuwe na subira na tuombe uzima. Hazitolewi kiholela kama njugu.
 
Unajua kwa muda mrefu mzee SAid alikuwa amepata mimbari huru mbele ya kundi la vijana wasiojua kuhoji wala udadisi wa fikra. Aliwakuta vijana (labda na wazee) ambao kuona Uislamu "Unatetewa" na maadui wa "Uislamu" wakibainiswa wazi basi walijikuta hawana jinsi isipokuwa kumuunga mkono. Histohisia ya Mohammed Said isingekamilika na wala isingekuwa na nguvu kama asingeweza kutumia 'common denominator' ya dini.

Ni kwa sababu hiyo utaona kuwa histohisia hiyo kaiandika akitumia dini kama kigezo cha 'nani alisahauliwa' na nani alipewa sifa. Nimeanza kupitia nyaraka mbalimbali za TANU na tayari nimeshakuta majina ya Abdul Sykes akitajwa na wazee wengine ambao Mzee Said alidai wamesahauliwa.

Kitu ambacho nimegundua ni kuwa wazee awa waliwekwa kwenye nafasi yao sahihi ya kihistoria - yaani washirika wa karibu wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere katika harakati za Uhuru. Wengine bila ya shaka walimtangulia katika siasa (kutokana na umri wao au kutoka na nafasi walizokuwepo) lakini wote wanabadilishwa maisha yao na siasa zao wanapokutana na Nyerere.

Ni Nyerere ambaye anafunua wazo kuwa Tanganyika ni zaidi ya Gerezani, Tanganyika ni zaidi ya Dar-es-Salaam na Tanganyika ni zaidi ya kundi la wazee wa Dar (Wakristu na Waislamu). Mzee Said kwa makusudi kabisa anajaribu kupuuzia jaribio la kuwagawa wapigania uhuru kwa misingi ya dini. Kundi la Wazee wa Kiislamu ambao walitaka upendeleo wa pekee na ambao waliamini wanastahhili zaidi walijaribu kuhujumu harakati za Uhuru.

Uongozi thhabiti wa Nyerere ulionesha tu kuwa hali mbaya ya maisha haikuwa kwa watu wa Gerezani peke yao na wala hhaikuwa ni kwa Waislamu tu. Kulikuwa na jamii nyingi katika Tanganyika ambazo utawala wa Mkoloni ulizisahau. Nyerere katika dhamira safi asingeweza kabisa kupendelea kundi la 'marafiki' zake kama Mohammed Said anavyotaka na akapuuzia mamilioni ya WAtanganyika waliotawanyika katika ardhih yetu maridhawa.

Dhambi kubwa kabisa ya Nyerere ukimsoma vizuri Mohammed Said ni kuwa hakuwapendelea Waislamu au kuwapa nafasi ya pekee dhidi ya Watanganyika wengine. Nyerere aliwachukulia Waislamu kama ndugu zake, rafiki zake na aliwaamini kwa maisha yake. Katika kufanya ivyo aliongozwa kabisa na dhana ya "binadamu wote ni sawa". Bahati mbaya kina Mohammed Said wanaeneza (na tunaona matokeo yake) nadharia kuwa 'binadamu wote ni sawa' lakini "Waislamu tu ndio ndugu zangu". Hivyo, Mohammed Said hawezi kujali dhulma dhidi ya Wakristu au jamii ya Kikristu au Wasio waamini lakini atapiga kelele akisikia ni Waislamu wanadhulumiwa.

Hii ndio tofauti kubwa kati ya Nyerere na Mohammed Said na watu wanaomuunga mkono. Nyerere aliamini kuwa undugu wa binadamu ni mkubwa zaidi kuliko dini, rangi, jamii, au mahali. Na kwa muda Watanzania tuliamini hivyo ivyo pia. Hadi watu kama Mohammed Said walipoibuka na kutuambia kuwa wao ndugu zao wa karibu na walio tayari kuwatetea ni Waislamu wenzao. Na somo ihli limepata waumini. Cha kusikitisha ni kuwa hata hao Waislamu siyo Wote ambao wanaamini ni ndugu zao. Wao Waislamu ni wale wenye kukubaliana nao kisiasa na kimtazamo siyo wanaokubaliana nao kiimani juu ya Mungu Mmoja na Mtume Mohammed.

Wale Waislamu wasiyokubali histohisia hii na ambao wanaamini katika undugu wetu na wako tayari kumpinga ndio wamegeuzwa maadui. Wanaturudisha kule ambapo baba zao walifanya mwaka 1958 na mapema mwanzoni mwa miaka ya sitini - Waislamu ni lazima wampinge Nyerere, wapingane na ndugu zao Wakristu na wajitenge na wengine.

This is to me is the tragegy of Mohammed Said's antics..
 

MM,

Hutoweza kujibu kitabu changu kwa maneno hayo yako hapo juu.
Wala sitapoteza nguvu zangu kufanya uchambuzi wa kauli yako.

Inatosha tu kukuambia kuwa kama umekutana na nyaraka za wazee
wangu huko ulikozikuta mbona basi Kivukoni College walipoandika
wazee wangu hawakutajwa katika kitabu chao ''Historia ya TANU 1954-
1977?''
 

Nguruvi3,
Insha Allah nami nasuburi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…