Karibu sana rafiki, pole sana kwa adhabu ya jf,
Nakusihi zingatia sheria za jf mkuu wangu ili tusonge mbele salama na kuwasomesha wenzetu historia ya nchi yetu.
Shukrani sana ndugu.
BAKWATA ilianzishwa kuwanusuru na janga la bloodbath between yourselves.Mzee Masasi alijitahidi sana kwa cause ya waislam Tanzania
Mimi mzee nikikusupport wanasema nilamba viatu vyako lakini mzee kuhusu ili swala la BAKWATA yaani umeongea points sana NYERERE NDIE ALIYEANZISHA BAKWATA hilo swala wala halihitaji tochi ishaalah mzee MS mungu akujalie umri.
Na inazidi kupanda mbele ya Watanzania wanaoitakia nchi hii mema. Wiki chache zilizopita, wiki ya mwisho ya mwezi Februari hapa Marekani wanaadhimisha president's day. Wakati natembea kwa mazoezi nilishangaa jirani yangu mzungu kaweka picha kubwa ya George Washington mlangoni kwake, ingawa president's day ni ya marais wote waliotangulia mbele ya haki Marekani. Nikajiuliza, iweje huyu jamaa kaamua kuadhimisha George Washington peke yake? Jibu likaniijia haraka, "founding father." Ndiyo Nyerere huyo. Licha ya laana tulla zenu Nyerere ataendelea kuenziwa na majority ya Watanzania.BH,
Amin ndugu yangu.
Ndiyo maana hadhi ya Nyerere imeshuka mbele
ya macho ya Waislam.
Huu ni ukweli.
Unatisha unaogopesha lakini huu ndiyo ukweli
unaotukabili hivi sasa.
Twende Kazi,
Inawezekana kwa kuwa wewe ni Mkristo ukawa hujui madhila
yanayowasibu Waislam katika elimu, kazi na fursa nyinginezo.
Huhisi ubaguzi.
Inawezekana kabisa.
Kuna Waislam hivi sasa wako mahakamani na wako rumande
Segerea.
Ni vijana wadogo walikamatwa wakitoka msikitini Ijumaa mbili
zilizopita.
Wanashtakiwa kwa kosa la kuandamana.
Vijana wanamuuliza hakiumi nini maandamano.
Hakimu akaeleza.
Vijana wakazema hapo tulipokamatiwa sisi wala hapakuwa na
maandamano ila tuliona watu wakiwakamata waliovaa kanzu na
mimi nilikuwa nimevaa kanzu.
Kosa langu ni hilo.
Wajerumani Vita Vya Pili Vya Dunia wanawapiga na kuwatesa
Wayahudi kisha wanawauliza hivi mnajuakwa nini tunakupigeni?
Tunajisikia raha tukikupigeni.
Hili ndilo lilikuwa jibu la Manazi.
Hapa ndipo tulipoifikisha Tanzania.
Kuonekana na alama za Uislam unahatarisha maisha yako si njiani
hata shule, vyuoni na makazini.
Katika hali kama hii nani wa kuonewa huruma?
Huu mkataba umesoma?.Hauna sehemu unayosomeka pesa itatoka Ujerumani.Kama hujausoma USOME BASI.
Nilichokiona zaidi ni kutajwa kanisa na serikali.Ikitajwa serikali walipakodi ni sisi.Wajerumani na wakoloni wenzao hawana mali wanatumia ujinga wenu kujineemesha
Ritz,
Karibu.
Tumekutandikia busati jipya.
Tumeagiza kahawa safi toka
Ethiopia.
Zomba kaahidi kuja na halwa
ya lozi.
Uje na rafiki yangu Yericko.
Insha Allah.
Mohamed,'Jasusi,
Citation iko hapo na pg. no.
Mohamed,'
Samahani kama nitakuwa nakusumbua. Umesema hiyo citation ya kanisa kuona uislamu kama adui iko page 37 katika toleo la 1992. Mimi nina toleo la 2001 na page 37 inazungumzia jinsi viongozi wa kanisa walivyounga mkono ujamaa: 1967- 1977. Hapa nitakutajia chapters (sura) zilizomo kwenye hicho kitabu ili uniambie ni sura gani kwa sababu huenda page zinatofautiana kati ya toleo la 1992 na 2001 ambalo ndilo ninalo. Sura ya 1 ni Utanguliz. Sura ya 2 Viongozi wa Kanisa Katoliki na Watawala wa TANU/CCM. Sura ya 3: Mafundishi Rasmi ya Maaskofu Juu ya Siasa na Uchumi 1953-1966. Sura ya 4: Viongozi wa kanisa walivyounga mkono ujamaa: 1967-1977. Sura ya 5: Viongozi wa kanisa walivyosita kuunga mkono ujamaa: 1967-1977. Sura ya 6: Viongozi wa kanisa na hali ngumu ya maisha 1977-1985. Sura ya 7: Muhtasari. Ningependa kujua ni sura gani hiyo quote inapatikana ili niisome na kuona mukhtadha wake. Asante sana.
Mohamed Said,
Shukrani sana maalim wetu na mie nimekuja na zawadi ya bokoboko la mbuzi na swamri kidogo, pamoja na vipopo, jerebi, pera maziwa pamoja na radu.
Ndugu yetu Yericko atafaidi sana ngoja nimwambie zomba, ampe kwanza ngisi wa kuchoma.
Mohamed Said umesema wakati wa kugombania uhuru,kabla nyerere ajahutubia kulikuwa na mtu anapandisha munkhar/kuhamasisha kabla nyerere ajaingia kufunga kazi.Tumekuomba utumie lugha ya ki academia hii lugha "hadhi ya nyerere imeshuka mbele ya waislam"kama vile unaongea kariakoo shimoni waachie vichwamaji akina Ritz wewe shusha nondo
Mzee Said, this is too low kwa Mwandishi na 'Mtafiti' kuamini kuwa watuhumiwa hao Wislamu wamekamatwa kwa kuonewa kwa kusikiliza wanavyojitetea mbele ya Hakimu. Ni dni baya mno, na inaonyesha dhahiri kuwa kwako linapokuja suala linalohusu Waislamu basi unalihusisha moja kwa moja na kuonewa kwa Waislamu, hili si jema katu na linaonyesha jinsi gani jinsi ulivyo 'biased' linapokuja suala la Uislamu.
Kama 'utafiti' uliopelekea Kitabu chako ni wa aina hiyo, kusikiliza upande mmoja na kuhitimisha kuwa ni ukweli basi unafanya kosa kubwa sana kiutafiti maana hata katika uandishi wa kawaida wa habari tu, unamdai Mwandishi kudi taarifa na upande wa pili.
Umenisikitisha sana kkabisuchukua utetezi wa vijana hao waliokamatwa Ijumaa kuwa ni kweli na amina, hili linakuondoa kabisa ktk ethics za uandishi na utafiti.
Mohamed Said,
Shukrani sana maalim wetu na mie nimekuja na zawadi ya bokoboko la mbuzi na swamri kidogo, pamoja na vipopo, jerebi, pera maziwa pamoja na radu.
Ndugu yetu Yericko atafaidi sana ngoja nimwambie zomba, ampe kwanza ngisi wa kuchoma.
Na inazidi kupanda mbele ya Watanzania wanaoitakia nchi hii mema. Wiki chache zilizopita, wiki ya mwisho ya mwezi Februari hapa Marekani wanaadhimisha president's day. Wakati natembea kwa mazoezi nilishangaa jirani yangu mzungu kaweka picha kubwa ya George Washington mlangoni kwake, ingawa president's day ni ya marais wote waliotangulia mbele ya haki Marekani. Nikajiuliza, iweje huyu jamaa kaamua kuadhimisha George Washington peke yake? Jibu likaniijia haraka, "founding father." Ndiyo Nyerere huyo. Licha ya laana tulla zenu Nyerere ataendelea kuenziwa na majority ya Watanzania.