Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Nguruvi,
Hebu soma upya hii post.

Unafanya haraka na matokeoa yake ndiyo hayo maneno ambayo mie sijaandika:
Angalia bold:

Umeandika maneno mengi sana.
Ni vigumu kukujibu nukta kwa nukta.

Umezungumzia maandamano kuwa sishiriki maandamano.

Hunijui...
Na wala sina haja ya kukueleza.

Umezungumza mimi kupanda ndege kwenda nchi za nje na kuwaacha ndugu zangu.

Hili nitakujibu.

Maandamano ya kwanza tumetokea Mtoro 1993.
Mabucha ya nguruwe.

Siku chache kabla nilikuwa nimetoka safari...Dar- Paris - Le Havre - Paris - London - Cardiff - London -
Dar - Zanzibar.

Zanzibar ndiyo sakata la OIC nilikwenda kuchapa majibu kwa Kanisa na Serikali katika Khayria Press na
mimi ndiye nilikuwa nilorudi na majibu hayo ambayo tuliyagawa kwa Wabunge wakati huo Bunge linakaa
Karimjee Hall.

(Nina paper nzima kuhusu OIC Insha Allah kama wanaukumbi watapenda nitaiweka jamvini.)

Nimefika Dar nimearifiwa mkutano wa dharura wa kuwawekea dhamana masheikh wetu waliokamatwa kwa
kuvunjwa kwa mabucha ya nguruwe.

Sina haja ya kukeleza nini kilitokea siku ile katika msikiti wa Mtoro ambao mimi nikiswali pale toka utoto wangu.

Sheikh Waziri Ramadhani ex - police officer ndiye aliyewasomea Waislam Qur'an na alichagua aya mnasaba na
hali iliyokuwapo siku ile.

Ilisomwa dua kubwa na tuliondoka kwa maandamano kuelekea Central Police.

Mbele yetu ndugu yetu tukimwita kwa jina la Darwesh alikuwa amebeba bendera ya kitambaa cheusi imeandikwa:
Lailaha Ilallah Muhammad Rasulullah.

Allah siku ile alijibu dua yetu pale pale.
Tumeondoka msikitini jua kali.

Tunafika Uhuru na Titi Street mawingu yanatanda na mvua ikaanza kunyesha.
Tulipambana na polisi Clock Tower na mabomu ya machozi yalirindima.

Ile mvua na upepo ukawa unapeperusha mabomu yale mbali na Waislam.
Nilikuwapo pale.

Mwenzangu alikamatwa na ndiyo ikawa sababu ya yeye kufungwa na kupoteza kazi bank.

Mimi baada ya mapambano yale nilirudi nyumbani kubadili nguo na kujitayarisha zaidi nikaja Mtoro.

Mnazi Mmoja nikakutana na rafiki yangu akanisihi nisende msikitini Mtoro kwa kuwa FFU wamezingira msikiti.

Nilimjibu kuwa nachelea kukimbia vita Allah ananiona.
Sikuweza kufika msikitini kwa kuwa Mtaa wa Mahiwa, Livingstone, Narung'ombe yote ilikuwa imefungwa...

Huwa sipendi kusema haya lakini nimeona nikueleze unijue.

Uoga si katika sifa zangu na ndiyo maana unaona nimeingia hapa na jina langu kamili bila kificho.

Wakuogopewa ni Allah SW pekee na Yeye kaweka ahadi kuwa atakaemuogopa atamfanya asiogope
chochote duniani.

Nami natamani niwe katika wale wasiomwogopa yeyote katika binadamu.
Nadhani tumefahamiana.

Mengine ulosema ni yale yale majibu ni yale yale tunazungusha humo kwa humo.

Nguruvi,
Cheza na watu saizi yako.
 
Mzee Mohamed,

Heshima kubwa unayopewa humu na kwingineko inatokana, pamoja na mambo mengine, usomi na weledi wako, uwezo wako mkubwa wa kufikiri na kupambanua mambo. Sasa kama mambo yenyewe ndio haya, dah, sitii neno.

Unajua fika kwamba AA, TAA, TANU na CCM ni asasi na taasisi tofauti kabisa hata kama vilirithishana baadhi ya watu na mambo kadhaa.


Naamini unajua umuhimu wa tarehe katika HISTORIA. Naamini unajua umuhimu wa wahusika katika tukio lolote lile la kihistoria.


Haiwezekani ukalazimisha kuwapa nafasi kubwa wasiostahili wazee wako hawa katika historia ya TANU, TANGANYIKA na TANZANIA.
 
Generalization aliyosema Mwanakijiji. Maandamano ya kwanza kwenda wapi? Usisahau hapo chini umeweka mabucha ya nguruwe! ukimaanisha maandamano ya kwenda kuvunja mabucha ya nguruwe.

Mimi nasema hapana hayo kama yalikuwepo ni ya pili ya kwanza ni yale ya kwenda kuvunja mabucha yakitokea Kichangani Magomeni, kupitia Morogoro rd, usalama, mwembechai hadi eneo la tukio.

Ninyi mnasema hakukuwa na kitu hicho, tena Mohamed katika kitabu chako umeeeleza jinsi ''youths.... swiftly moved like trained commando''. Nasema si kweli walipita bara barani kuelekea kwenye mabucha.

Hawakugusa jengo lingine isipokuwa kule walikokusudia wao.Ni ukweli mnaufaham lakini basi tu !
Hili lifike mwisho maana tutarudi katika kitabu na kufukua jinsi lilivyokuzwa na kuwekewa nakshi na kupotoshwa.
 

Nguruvi3,

Mimi sijasimuliwa na mtu hizo ni fikra zako bahati nzuri Magomeni Mapipa ni kwetu mtaa wa Tosheka ni nyumbani kwa ndugu zangu kwa hiyo kuhusu tukio la Mwembechai hakuna mpuuzi yeyote ambaye atanifahamisha.

Nguruvi3 kuhusu Mwembechai kaa kimya wafahamishe wengine kuna watu mpaka sasa hivi hawatakiwi kufika kabisa Msikiti wa Mwembechai wakifika tu wanakamatwa na watu wa uslama.

Narudia tena Maandamamo ya Waislam kuhusu mabucha ya nguruwe yaliitishwa kupitia Misikiti yote kesho yake yakielekea Posta siyo kuvunja mabucha.

Kwa kukufahamisha zaidi vibaka waliokuwa maeneo ya usalam walivyoona watu wanaelekea mwembechai nao wakajichanganya na kuanza kupora watu vitu na kwenye magari.
 
Mohamed Said,

Chinuo Achebe amefariki leo huko Marekani! Kila nafsi itaonja mauti! nakumbuka kitabu chake cha Things fall apart cha mwaka 1958! kama unajua wasifu wake na kama alihusika na uandishi vita vya Biafra? vita ambavyo Tanzania ilijihusisha moja kwa moja na kuegemea upande mmoja!
 

Kadogoo,
Chinua Achebe huyo ni mwamba katika miamba ya fasihi Afrika.

Afrika imeondokewa.
 

Nguruvi,
Hivi unaona shida gani kusoma kwa utulivu?

Hiyo nukuu siyo kutoka katika kitabu.
 

Nguruvi,
Unaweza kuamini unachopenda na kutaka.

Sisi ndiyo wenye shughuli na tumekupa taarifa ya mambo
yalivyokuwa.

Hatuwezi kukulazimisha kitu.
 

WC,

Unataka tubishane kwa kitu ambacho waliasisi wazee wangu
na mie kuijua historia yake?

Hivi wewe utaijua AA kuliko mimi mjukuu wa waasisi hawa?
Hivi wewe utaujua undani wa TANU kunishinda?

Huo ni muhali.
 
WildCard, hata usisumbue akili yako...huyu mchochezi Mohamed Said ni mtu wa ajabu sana na hatari lakini taratibu wengine tunaanza kuigundua janja yake na hila zake...kamwe si bure.

  • Kwa makusudi kabisa hamtambui kiongozi mkuu mwanzilishi na Raisi wa kwanza wa AA mwaka 1929, Mwalimu Cecil Matola wala msaidizi wake Makamu wake Ramadhani Ali! Cha ajabu anamtambua katibu wake Kleist Sykes na kumpa heshima zote za uasisi eti toka akiwa Burma!
  • Kwa makusudi kabisa hamtambui kiongozi mkuu muasisi na Raisi wa kwanza wa TAA wa kuchaguliwa mwaka 1950 Dr. Vedasto Kyaruzi wala Makamu wake! Cha jabu anamtambua katibu wake Abdulwahid Sykes mtoto wa Kleist Sykes na kumpa sifa zote za kuongoza mabadiliko ndani ya TAA!
  • Kwa makusudi kabisa hamtambui kiongozi mkuu muasisi na Raisi wa kwanza wa TANU mwaka 1954 Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wala Makamu wake John Rupia na badala yake sifa zote zinaelekezwa kwa katibu Abdulwahid Sykes, kipenzi cha wengi aliyekuwa na mvuto wa pekee!
Sasa hapa swali linakuja, kwa nini ameamua kupindisha mambo hivyo? Huyu Mohamed Said, mtoto wa Kimanyema, mbona anawatetea sana hawa Wazulu ambao hata kwenye Uislaam hasemi waliingia lini na kwa sababu zipi? Ana uchungu gani? Uhusiano kati ya koo hizi mbili unatokana na nini?

Kwa nini anafanya sana jitihada za kuwaengua viongozi wa juu waanzilishi wa AA, TAA na TANU na badala yake anawapa sifa wasaidizi wao? Toka lini Katibu anakuwa na nafasi ya juu kuliko Raisi/Mkurugenzi? Kwa mfano;

  • Amewahi kudai kuwa pamoja na msomi Mwalimu Cecil Matola kuwa Raisi muasisi wa AA hakuwa chochote bali ni katibu wake Kleist Sykes aliyepanga na kuiendesha AA.
  • Amewahi hata kudai kuwa mwaka 1950 ni katibu wa TAA Abdulwahid Sykes ndiye alimteua bosi na Raisi wake Dr Vedasto Kyaruzi kwenye kamati iliyoandaa mikakati na malengo ya TAA.
  • Amewahi kudai kuwa pamoja na Mwalimu Nyerere kuchaguliwa kuwa Raisi muasisi wa TANU mwaka 1954 ni katibu wake Abdulwahid Sykes ndiye aliyesimamia mipango yote ikiwa ni pamoja na kumuandalia hotuba aliyoisoma UN.
  • Amewahi kudai kuwa pamoja na Makamu wa TANU mwaka 1954 kuwa mfanya biashara mkuu mwenye uwezo mkubwa kifedha, John Rupia lakini ni Abdulwahid Sykes na ndugu zake ndio waliokuwa wakitoa fedha zao kuiendesha TANU.
  • Amewahi kudai kuwa pamoja na Mwalimu Nyerere kulipwa mshahara mkubwa wakati huo, hakuweza kujitosheleza hata kwa nauli achilia mbali kununua mboga hadi mchuuzi wa Kariakoo Mshume Kiyate alipomfadhili.
  • Amewahi kudai kuwa pamoja na msomi Mwalimu Nyerere kuanza siasa toka akiwa chuoni Makerere kwenye miaka ya 1940s ilibidi apigwe msasa, kupewa shule na kufundishwa ustaarabu na wazee wa Gerezani kuhusu siasa!
Huyo ndiye Mohamed Said anayepiga lecture ughaibuni kuhusu harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na wazee wake walivyosahauliwa na kunyanyaswa baada ya uhuru na Mwalimu Julius Nyerere! Kwa nini, huyu Abdulwahid Sykes anayemuongelea sana na kupiga kelele, watoto wake wako kimya! Je kulikoni?

Mohamed Said ni mjanja sana, katoka mbali toka wakati wa WARSHA na MSAUD akiwa na Pro. Njozi na Dr. Dau. Bahati mbaya nyumba waliyoijenga ya theluji wanashuhudia kwa macho yao ikianza kuporomoka kwani jua linaanza kujitokeza! It is just a matter of time, njama na hila zake zote zitaanikwa.
 
Jamaa ameamua kubisha mpaka dakika ya mwisho.
Ritz,Ndicho akijuacho.
Ha ha ha! Mohamed, tulia wala usiwe na jazba au ghadhabu. Maneno hayo ni uchungu unaokumbana nao.Kaa chini pata funda tatu za maji ujikusanye tena

Nimethibitisha upotoshaji wako 100 times. Recently nimekuonyesha takwimu zako (aibu sana) ambazo mtu mwenye degree aliyezungukwa na wasomi asingethubutu kuziweka hadharani. Umeshindwa kusimama kwa wingi wa jasho.

Nime prove kuhusu hoja za Africa Events na sasa Maandamano achilia mbali huko nyuma uliposepa hoja lukuki.
Nafahamu unaniona kama spoiler wa mission yako. Unajua nasoma between the lines na natumia akili.
Sitegemei neno zuri toka kwako. Mimi siyo gogo vivu! hewala bwana, tawire n.k! siyo lugha ninayoijua.

Ninakuhakikishia kuwa nipo hapa ukienda nje ya mstari nakupeleka katika kona, 100K wanabaki wakisema Ali Bumayeee, Ali Bumayeee! ni jab ukinyanyua kichwa upper cut. ha ha ha

By the way, Kadinali Pengo kesharudi kutoka Rome, nasikia ataitisha Alumni wote wa St Joseph Catholic school wahudhurie semina. Umesha reply kwa ajili ya seat! Nitapinga na kulaani mfumokristo kama hawatakuweka high table.

Miaka 15 ya upotoshaji sasa basi, ni makosa kukaa kimya kizazi kikiendelea kunajisiwa.
That will never happen on my watch.
 

Mag3,

Kwani ndugu yangu kipi kinachokuuma?
Si na wewe andika historia yenu kama unavyoiona?

Kivukoni wameandika mimi nimeandika na wewe andika.
Hakuna ugomvi wala kutoleana maneno ya kifedhuli.

Ila nijuacho mie ni kuwa TANU haikuanza 1954 na safari
ya UNO iliratibiwa na Baraza la Wazee wa TANIU chini
ya Mwenyekiti Sheikh Suleiman Takadir na mweka fedha
wa safari ya UNO alikuwa Idd Faiz Mafongo nk. nk.

Umezungumza kuhusu watoto wa Abdu Sykes.
Hawajakuwa kimya.

Daisy kaandika historia ya babu yake angalia Modern
Tanzanians Iliife (Ed) ''Kleist Sykes the Townsman.''

Ukipenda fika maktaba ya Chuo Kikuu angalia East
Africana angalia Daisy Sykes ''The Life of Kleist Sykes.''

Hii ni semina paper ya 1968.

Nimepata mengi kwa wanae na siku Abdulwahid na Ally
Sykes walipopewa medali ya kutambua michango yao
katika kupigania uhuru wa Tanganyika...

Tulisheherekea pamoja kwa vicheko...baadae katika
kujikumbusha tulivyokuwa wadogo na wazee wetu wa
hai wapo waliotoa machozi.

Siwezi kukujibu yote maana tunazunguka humo kwa
mumo.
 
Mohamed Said mbona hili swala linarudiwarudiwa-kanusha au kubali- wewe ni product wa catholic school????????


"By the way, Kadinali Pengo kesharudi kutoka Rome, nasikia ataitisha Alumni wote wa St Joseph Catholic school wahudhurie semina. Umesha reply kwa ajili ya seat! Nitapinga na kulaani mfumokristo kama hawatakuweka high table."
 
Last edited by a moderator:

kama ni kweli basi wewe huna fadwila-YOU are biting the hand,that taught you how to feed yourself
 

Nguruvi,
Hapa ndipo ulipofika?
Mbona kitabu ni mashuhuri?

Una uwezo wa kikiondoa kutoka
katika mzunguko kisisomwe wala
kuchapwa?
 
kama ni kweli basi wewe huna fadwila-YOU are biting the hand,that taught you how to feed yourself

Son...

Mbona Waislam ndiyo waliokuwa mstari wa mbele
katika kupigania uhuru lakini matunda mnafaidi nyie
peke yenu?

Nanyi wezi wa fadhila?
 
Son...

Mbona Waislam ndiyo waliokuwa mstari wa mbele
katika kupigania uhuru lakini matunda mnafaidi nyie
peke yenu?

Nanyi wezi wa fadhila?

Mohamed,
Hujajibu swali. Waislamu walitujengea shule za kutuelimisha? Umesoma shule ya misheni. Hizi harakati za kupigania uhuru tumeshiriki sote. Umefaidi matunda ya mfumokristo, lakini hilo mpaka sasa hutaki kukiri. Have some humility, my brother.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…