Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 51,303
- 40,190
Jasusi, yaani mimi nacheka tu...wakati mwingine natamani hata kukaa kimya. Nimeuliza Abdulwahid Sykes alikuwa nani ndani ya TAA ilipoanzishwa mwaka 1948 baada ya Zanzibar kujitoa AA? Abdulwahid Sykes alikuwa nani ndani ya AA/TAA wakati Mwalimu tayari ni kiongozi wa AA Tabora mwaka 1945? Nimeuliza Abdulwahid Sykes alikuwa nani ndani ya TAA mwaka 1953 alipogombea uongozi wa juu wa TAA kwa kupambana na Mwalimu Nyerere?
Kwa hili swali la mwisho, waongo watadai Abdulwahid ndiye alikuwa Raisi! Hapana, Abdulwahid Sykes hakuwahi kuchaguliwa kuwa Raisi wa TAA toka iundwe mwaka 1948 hadi TANU inaasisiwa mwaka 1954...yeye alikuwa ni katibu tu, period. Ndiyo maana mimi nasema TAA ilizorota sana kwa kukosa uongozi baada ya uhamisho wa Raisi wake Dr. Vedasto Kyaruzi hadi inampata kiongozi mpya, Mwalimu Nyerere mwaka 1953.
Naona unajiuliza maswali kisha unajijibu mwenyewe, jibu lako hebu soma maneno ya Nyerere hapo juu.
Hivi kuna mtu muongo na mnafiki kama wewe si wewe ndiyo umetuletea habari humu jamvini kuwa mikutano ya TANU ilikuwa inafanyika PUGU nyumbani kwa Nyerere.
Hebu msome tena Nyerere hapo juu kwenye maandishi ya blue anaelezea jinsi alivyokuwa anatoka PUGU kwa miguu kuja mjini (Kariakoo) kufanya mikutano ya TANU, mpaka Wazee wetu wa kiswahili wanywa kahawa na wenye akili za madarassa wakamununulia baiskeli.
Wewe endelea kucheka lakini wanajamvi wanakusoma ulivyokuwa muongo na mtu wa hasad.