Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Kama wameshinda mbona Ponda kapewa hukumu ya kifungo cha mwaka mmoja nje?
 
Mohamed Said
Mungu akubariki sana,haya madudu ya kina Adam Nasibu sisi tungeyajulia wapi??

The Big Show,

Amin ndugu yangu.
Moja ya sifa za Allah ni kuwa hadhulumu.

Nilipewa makaratasi ya Sheikh Bilal Rehani Waikela kabla sijakutana na yeye.
Wakati huo nilikuwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Waikela alikuwa katibu wa EAMWS Jimbo la Magharibi na ''mgogoro'' wa EAMWS
ulipoanza yeye alikuwa mmoja wa Kamati ya Upatanishi baina ya genge la Adam
Nasibu na Waislam.

Kwa ajili hii basi nyaraka zote na mgogoro ule na mikutano yote yeye alihudhuria.
Lakini kubwa zaidi Waikela alikuwa mmoja wa waasisi wa TANU Tabora na mmoja ya
watu waliokuwa karibu sana na Nyerere wakati wa kupigania uhuru.

Nyaraka za Waikela zilikuwa na mengi sana.
Nyaraka hizi ndizo zilizonisaidia kuandika sehemu ya mwisho ya kitabu changu sehemu
niliyoipa jina: ''Njama Dhidi ya Uislam.''

The Big Show,
Allah amlipe Sheikh Waikela kwa kuwa na ujasiri wa kuzitunza hizi nyaraka hadi zikatufikia
sisi baada ya miaka 20 kwa wakati ule.

Wenzake waliokuwa katika kamati ile walitishwa na serikali na wakatia moto nyaraka zao.
Waikela anasema yeye hakutishika alitafuta mahali salama akaficha zile nyaraka zake.

Nilipomuuliza ilikuwaje akaamua kufanya hivyo jibu lake lilikuwa ni kuwa yeye alijua Allah
kwa utukufu wake hawezi kuachia dhulma ikatamalaki iko siku atamleta mtu kuyaandika
yote yaliyotokea.
 
Hujui zaidi ya Waislam 50 waliokamatwa mahakama imewakuta hawana hatia kama siyo kushinda ni nini hebu tusaidie kaka.
Ritz,Mahakimu na Majaji wa NCHI hii ni WATANZANIA, WAZALENDO. Wanapoweza kuepusha vurugu, machafuko, ugomvi kwa kutumia hekima, busara na sheria zilizopo watafanya hivo kila mara. Hawa wafuasi wa Sheikh Ponda wanafahamika ni WATANZANIA wa aina gani. Wewe na Mzee Mohamed hamkwenda kule Chang'ombe. Kwa nini?
 
Mzee Mohamed,Haya madhila na taabu zote hizi ndiyo yaliyosababisha Mwalimu kutaifisha shule zote za madhehebu ya DINI ingawa wewe unaiona hatua hii kuwa haikuwa ya maana. Chuki yako kwa Mwalimu haiwezi kukuelekeza vinginevyo. Lipo tatizo kwenye mila, desturi na tamaduni za Kiislam ambazo kwa bahati zilikuja kubaliana na mila, desturi na tamaduni za baadhi ya Makabila nchi hii (Soma Mwananchi ya leo uk. wa 7 uone ya Mbarali ambako Waislam sio wengi).Katika mahubiri yako ya sasa waambie Mwalimu hayupo tena duniani kuwazuia Waislam kwenda shule na kwamba tunaye Rais Muislam safi tangu mwaka 2005.
 


Wild Card,
kwani huzioni shule zetu zinavyojengwa?

Huoni hijab asubuhi mabinti wakenda shule?
Tunajenga shule nyingi tatizo letu ni NECTA.
 

Wild Card,
Ponda hana wafuasi ana nduguze Waislam.

Hayo ya kwenda Markaz nakuachia mwenyewe.
Nilidhani unataka mjadala wa adabu na heshima.

Ikiwa umeshindwa staha na tuagane kwa amani.
 
Kama wameshinda mbona Ponda kapewa hukumu ya kifungo cha mwaka mmoja nje?

Jasusi,
Umekereka kwa kuona salama imepatikana?

Hujui hasama ambayo ingejengeka kwa Sheikh Ponda
kufungwa kwa kuupigania Uislam?

Sasa hivi viongozi wetu wanahimizi uelewano katika
jamii.
 
Mkuu THE BIG SHOW ikiwa hakuna sheria inayozuia waIslamu kujianzishia jumuiya zao,na wewe binafsi umekiri mmeshaanzisha jumuiya nyingi amabazo unadai zina ushawishi mkubwa katika jamii ya kiIslamu kuliko BAKWATA.

Naomba unitajie hizo jumuiya zenye ushawishi kuliko BAKWATA zimefanya maendeleo yapi mpaka sasa,mfano ujenzi wa mahospital,vyuo vikuu na nk.


 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ritz

Sielewi ni kwa jinsi gani serekali inaweza kuwalazimisha waIslamu wote Tanzania wawe chini ya BAKWATA.Jambo moja lililowazi pasipo shaka ni kuwa jumuiya nyingi za kiIslamu kukosa mtandao ulioenea Tanzania nzima.Ukijaribu kuangalia kwa undani utakuta taasisi nyingi zimejazana hapo Dar ukitoka nje ya Dar hazipo sasa utakapoitaka serekali ifanye mawasiliano na jumuiya yenye mtandao unaoanzia Kariako na kuishia Kibaha inakuwa taabu kubwa.

Shida nyingine ya BAKWATA ni Sheikh Mkuu kuchaguliwa na waIslamu 20 baraza la maulama (wewe umesema kikundi ambao wamechaguliwa na serekali mimi nimeweka tafsiri yangu ni waIslamu nadhani unasema kikundi kwasababu haukubaliani nao).Hivi Sheikh Ponda na Ilunga wamechaguliwa na kikundi cha watu wangapi ?,tangu nianze kumsikia Ponda miaka mingi imepita sijasikia taasisi yake ikifanya uchaguzi,utaona ni afadhali BAKWATA wanaomchagua kiongozi wao kuliko Ponda &... wasiotaka utaratibu wa uchaguzi kabisa.

Taabu nyingine ni uteuzi wa Masheikh wa mikoa kuteuliwa na Sheikh Mkuu na umetoa mfano wa Sheikh wa Dar hana Ilm yoyote ya kuwa kiongozi wa waislam.Nadhani huo ni utaratibu waliojiwekea BAKWATA wa kuwateua masheikh wa mikoa,kwani jumuiya zenu zimenyimwa kuchagua viongozi wa mikoa ?.Umesema BAKWATA haina uhalali wa kuwaamulia waislam wote shida ni pale wanapojiwekea taratibu zao linawakera !.Iweje BAKWATA usiyoikubali ikifanya jambo likukere,kwanini usijushughulishe zaidi na taasisi uanyoikubali.



 
Last edited by a moderator:

Nguruvi3,

nafikiri itakubidi ufanye utafiti kidogo katika mambo ya kiuchumi hususan ya uthibiti wa wa fedha lakini pia kujua sharia za nchi yako kuhusu utaratibu wa kuthibiti fedhwa haramu.

Kifupi wenye mamlaka ya kuthibiti fedhwa kutoka nje ni kazi ya Serikali kupitia wizara yake ya Fedha katika Benki Kuu. Kwani wana kitengo maalum kufuatilia hayo wakishirikiana na vyombo vingine vya usalama.

labda nikuulize je kwa wakristo wanathibitiwa na nani? nakushauri pitia bajeti yenu ya mwaka wowote uone jedwali la msamaha wa kodi kwa taasisi za kidini utaona na kuthibitisha hicho unachosema kuwa si kweli kwa upande wa wakristo huko Tanzania.

Vipi lakin umeshaondoka Bonde?
Tiugusie

 


Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza.

Labda nikuulize swali kidogo kutoka huko Tanzania hususan Bara. Je unajuwa Swala za idi zote ni lazima ziratibiwe na BAKWATA na vile vile viongozi wote waandamizi wa Serikali LAZIMA waswali kwenye misikiti ya BAKWATA? Fanya utafiti kwa hilo utagundua . Mimi nilikutana nalo nilipokuwa Mwanza.

Jiulize Je kwa wakristo ipo hivyo pia? Kwanini Serikali isiyokuwa na DINI ilazimishe viongozi wake waislam waswali katika misikiti ya BAKWATA. je kuna dili gani kati ya Bakwata na Serikali ya JMTz.

Pole sana
 

Muheshimiwa Nguruvu3,

Nashukuru na nakusoma kwa makini. Nitakua mchoyo na mwivi wa fadhila kama pia simtashukuru Al Akhiy Barubaru kwa jitihada zake kukujibu kwa minajil ya uwezo wake.

Ahsantani ndugu zangu nafarijika kwa haya maelekezo yenu.

Shukran kusikia pakacha langu nalo lakurubia kuwa tayari.

Vipi,naona Shariff Ritz alikuuliza kile kisuali kiduchu hujampatia jibule,unani!?ahaha!!

Tuendelee na mnakasha.

Shukran.
 
Ponda amehukumiwa kufungwa, sasa ushindi wa "waislam" uko wapi?
 
Mkuu Barubaru

Shida yako kubwa ni kwasababu viongozi waandamizi wa serekali wanaswali kwenye misikiti ya BAKWATA ha ha ha ha.


 

Halafu ukishatajiwa hizo jumuiya ndio iweje! haya kuna Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi Tanzania(BARAZA KUU) sio Bakwata iliyoanzishwa na Waislamu wenyewe tena wa nchi nzima mwaka 1991! baraza hili limefanya kazi nyingi na za faida kwa Waislamu mfano: kutoa mikopo isiyo na riba kwa wajasirimali, kutetea na kuwaelimisha Waislamu haki zao, kujenga na kuulinda umoja wa Kiislamu, kutoa elimu ya uraia kwa Waislamu kinyume na bakwata ambayo hujenga fitina na kuwachonganisha Waislamu!, jumuiya zingine siwezi kuzitaja hapa kwani tunajua umetumwa na maadui wa Waislamu ili uchukue habari zetu kwa kusudio la kutudhuru! lakini tambua Jumuiya hizi kwa kushirikiana na Waislamu wameweza kujenga shule nyingi za Kiislamu mfano: Shule zinazosimamiwa na African Muslim Agency, Jabal Hira High Schoo Morogoro, Kirinjiko Islamic high School Same, Mudio High School Machame, Thaqafa School Mwanza, Ansaar Sunna Islami primary, secondary and high School Tanga, na shule nyingi Jijini Dar na mikoa mingine!

Kumbuka Jumuiya hizi nyingi zimeanzishwa kipindi cha ruksa! haya wewe mwanachama na mtetezi wa Bakwata nitajie shule zenu na nini mmewafanyia Waislamu tangu Nyerere alipowaanzishia Bakwata lenu mwaka 1968?
 

Sheikh Mohammed Said,

Asalaam Alaykum Al Akhiy.

Wallahi nitakuwa nimeifanyia dhuluma nafsi yangu kama sitakushukuru kwa bayana yako hii adimu hapa jamvini. Insha Allah Mola takulipa kwa yoote,na kuzidi kuikurubisha darja yako,akuweke uwe miongoni mwa waja wake alowaenzi pasi mipaka.

Nimependa jinsi ulivyonyambulisha hizo ingredients japo kiduchu,lakini itajaribu kutoa picha kwa ndugu zetu wengine watuchekao na kutufanzia kebehi,japo wajue sisi Waislamu tumeanzia wapi kusakamwa na kuandamwa.

Hayo masuala ya Madrassa ni topic kubwa na ni ndefu mno,najua hapo umechelezea tu kiduchu. Ndo maana mimi huona fahari iso kifani pale niitwapo mtu wa akili za Madrassa!

Kwa wale ndugu ndugu zetu watakao kujua, japo kiduchu embu chungulieni japo kiduchu hii paper.
Paper presented by Dr. Anne K. Bang Univ. of Bergen Norway;Reasserting connections,commonalities and cosmopolitan: The Western Indian Ocean since 1800's. This paper was delivered at Yale University Nov. the 3rd.-5th. 2000. Kuna mengi humo kuhusu nchi yetu Tanganyika/Zanzibar na historia ya ilm ya Waislam na Madrassa imenyambuliwa kwa kina.


Kuna Bwana mmoja akiitwa Sheikh Pera Bin Ridhwan Gombe. Huyu bwana asili yake ni pale Mnyanjani Tanga. Alikua ni mmojawapo wa Waalimu wa mwanzo kutoka Madrassa na kukubaliwa kufundisha Government Schools.
Baadae aliajiriwa kwa contract na UDSM-Institute of Kiswahili Research kama Researcher. Mambo na kazi nzito zilizokua zimekwama na alizofanza pale Taasisi,na ambazo zilikwama kwa miaka mingi,Wallahi hakuna mfano wake. Matokeo yake alipomaliza hizo shughuli,alitupwa bila ya hishma yoyote. Tena kwa kebehi yakuwa Mzee samahani hatuwezi kukupa permanent contract kwa sababu huna Degree inayotambulika na Serikali hapa nchini!?

Wakati hao ma-Professor takriban woote,walitumia kazi zake na manuscripts alizoshughulika nazo mpaka kupata hizo PhD!? Kwa mtazamo ule basi hata wale ma-Professor nao pia hadhi zao za kitaaluma ingelazim zipitiwe upya maana ndani yake pana utata mwingi!?

Kuna huyu nae Sheikh Khamis Bin Akida Bin Said,ambae nafikiri hata Mwanakijiji anamfahamu na pia ni maaruf kwa waTanzania wengi. Nae pia ni kichwa cha Madrassa. Alikua ni multi-Linguist. Alifanya mambo mengi mno na ya ustadi mwingi pale UDSM-Institute of Kiswahili Research. Alikua ni Malenga bingwa na sifa zake mpaka kesho zimo vyuo vingi sana duniani na kwa Wanataaluma wengi mashuhuri.Yeye alikua ni nguli wa Etymology na Lexicography.

Kuna wakti alifanza ziara ya Vienna,Bonn,Uk na Tehran. Alipofika Tehran alipewa fursa ya kukutana kiduchu na Maulana Ayatollah Khomein. Aliweza kuzungumza fluent ki-Persia bila hata ya mkalimani. Ayatollah akamuuliza;hapa Iran ulikaa lini na ulisomea University ipi!? Sheikh Khamis Akida akamjibu,la Maulana...hii ndiyo mara yangu ya mwanzo kukanyaga ardhi hii tukufu alokupeni Allah,namimi hii lugha yenu nilisomeshwa kitambo kwenye Madrassa ya kule kwetu Mwarongo Tanga!

Kwa kifupi,huyu Bwana nae pia Sheikh Khamis Akida alipotakiwa "kustaafu";Prof. TSY Sengo wakti huo akiwa Director pale UDSM-Institute of Kiswahili Research, alipendekeza yakuwa anastahili na apewe PhD ya heshima kwa mchango wake wa kitaaluma pale UDSM. Basi huo msukosuko na upinzani alopata huyo Professor TSY Sengo mwenyewe ilikua almanusur nae pia apoteze hata ule wadhifa wake wa u-Director. Aliambiwa na kushutumiwa ati analeta udini!? Na vikaletwa ati vipengele vya kitaaluma yakuwa Sheikh Khamis Akida,alitakiwa awe na first degree ili atunukiwe hiyo PhD ya heshima!? Wakati takriban nusu ya wanafunzi wake huyu Sheikh Khamis Akida wakti huo ndo walokua ma-Professor pale Taasisi!? Sasa hii contradiction ya kitaaluma,si pia itawakumba mpaka hao ma-Professor wengine kwa kusomeshwa na mtu wa Madrassa,na kutumia manuscripts,research papers zake kwa uchunguzi na masomo yao, halafu huyo huyo si ndie mtu alosahihisha hiyo mitihani yao!?

Huyu Sheikh Khamis Akida,alikua ni mtaratibu mno na mstaarabu mno hakutaka malumbano, na watu wengi walikua wakimuhishimu na kumstahi kwa hali yajuu. Alichofanza ni kumwambia tu Prof. TSY Sengo aachane ni hiyo issue,na yeye malipo yake yapo kwa Allah. Embu fikiria,mtu anajaribu kudai haki za Wazee wetu tena kwa kufuata taratibu na sharia anaitwa mdini na kufanyiwa misukosuko iso kifani!?

Huyu Sheikh Khamis Bin Akida Bin Said,wakti "anastaafu" pale UDSM,alikua ni Senior Research Fellow.

Nilifarijika mno,nilipokwenda pale University ya Warsaw-Poland na kutembelea Faculty of Foreign Languages...nilionyeshwa baadhi ya kazi za huyu Sheikh Khamis Akida na picha kiduchu alizopiga na rafikiye Marehemu Prof. Ohly wakati alipotembela Poland.
Ni aibu kubwa Wazee wetu kuenziwa na watubaki nasisi kuwanyapaa.

Kuna kisa cha Nyerere na Sheikh Khamis Akida miaka ya sitini,waligombana kiduchu. Malenga Khamis Akida alitunga shairi refu na lakina cha kihistoria,kupinga Pare kwanini imo mkononi mwa Mkoa wa Kilimanjaro!? Shairi alilita; "Tokea lini Pare kuwa Kilmanjaro"!?

Basi Nyerere,alimwita Ikulu. Akamwambia yakuwa;Baba nakuheshimu saana. Lakini nakuomba kwa sasa, siasa niachie mimi nawewe nakuachia masuala ya kitaaluma na sitakuingilia asilan!ahaha!!

Shukran na tuendelee na mnakasha Insha Allah.
 


Ama kwa hakika dhulma haiwez kupotea,
Nakusoma sana Ndugu Yangu Moh Said,khabari zako nzito kweli kweli...
 
MGASHI;
Hivi kuvimba shavu ni dalili ya kupona?

Kadogoo,

Huwa nasikiliza sana radio iman, na watangazji huwaaminisha wasikilizaji kuwa Mrema amelaaniwa kwa kuwapiga mabom enzi zile alikuwa waziri wa mambo ya ndani.
Kumbe mtu mwenyewe alikuwa mgonjwa wa sukari na alikuwa kapigika mbaya. Ila toka amepata uhakika wa mlo wa maana anatoka shavu kaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…