Leo 2013, ndio unaliona hili, vipi kwa yule aliyesimamia kwa nguvu zake zote kuhakikisha anauvunja mshikamano wa Waislam wa Afrika ya Mashariki (East African Muslim Welfare Society) na kuwawekea chombo chenye katiba inayofanana na ya TANU?Suala la BAKWATA mimi naungana na wanaotaka mageuzi juu ya chombo hiki,
Nilazima kutazama kama kinamanufaa kwa waislamu ama kinamanufaa kwa serikali na chama tawala,
Misingi inayoleta viongozi wa chombo hii ni lazima itazamwe upya!
Manung'uniko kwa waislamu juu ya chombo hiki ni lazima yasikilizwe ama sivyo huku ni kuhatarisha ustawi wa uislamu Tanzania!
Mag;
God bless sio lugha inayotumiwa na Waislamu! tamko hilo la kichochezi dhidi ya Sheikh Ponda ni la kwako na washirika wako!
Leo 2013, ndio unaliona hili
RITZ;
Hawa wenzetu kwa kujikomba kwa Wakoloni na mabeberu hawajambo! Livingistone akifufuka leo nakumwambia Mzee Mwanakijiji kuwa ni yeye ndie aliyegundua Mlima Kilimanjaro bila shaka atamwamini! yaani Wazee wangu walioishi chini ya huo mlima karne na karne leo Mzungu anakuja dai ati ni yeye kaugundua! hawa hata Vasco da Gama akiwaambia alikuja Afrika mashariki kutafuta njia ya kwenda India kutafuta viungo vya chai na pilau wataamini!
Kadogoo,
Hawa jamaa zetu wanafurahisha sana Mwakajiji anaamini yaliandikwa na Listowel Judith wakati huyo Listowel Judith wakati anaandika kitabu chake cha "The Making of Tanganyika" alikua anaadithiwa na Ally Skyes.
Leo hii Mohamed Said akiwapa watu habari za kina Ally Sykes na Abdulwahid Sykes watu hawataki.
Mtu yupo radhi akanunue nyanya Shoprite kuliko kununua sokoni kariakoo.
Anajisikia fahari kanunua nyanya kwa mzungu.
Yericko;
Labda wakati umefika tena tumuombe Shekh MOHAMED Said na Ritz wakuandalie tena kinywaji na vitafunio murua ktk barza kwani kwa maoni yako haya naona unaanza kujirudi! lakini kwa sharti la kuendeleza mnakasha kielimu sio kukurupuka na kutubandikia vitabu hewa na makala yasiyo na kichwa wala miguu kuhusu ugaidi!
Kama Mzee wetu atakubali basi mimi niko tayari kulipa gharama!
Mi nipo hapa kupata ilm na naufutilia sana uu mnakasha.naomba kaka Yericko unielezee kidogo jinsi gani marekani inaweza husika kwenye Arusha-bomb issue.Ahsante
Niwie radhi kama nimekukwaza maalim,
Nikweli tunakwenda kwa mpango,
Tumeueleza udhaifu katika maandishi yako juu ya uhuru wa Tanganyika,
Kimsingi tulitakiwa kutua Zanzibar lakini kulingana na aina ya michango ya wa dau na tukio la kigaidi kule Arusha, tumejikuta tumeingia kwenye mjadala uliostahili kuwa wa hitimisho katika uzi huu, yaani vita dhidi ya ugaidi!
Naendelea kumpa darsa kijana wako Ritz bila uchoyo, nampa kile ninachokijua kwa undani tena nilichoanza kukiandika mimi tangu mwaka 1998 mpaka hii leo uandishi haujakamilika kamili!
Lakini kijana wako ananipa kop & Pesti kutoka kwa wanaharakati wa ughaibuni!
Huu ndio usomi ngoja tuendelee bila shaka tunapeana darasa lenye mafaa kwa wanajf wote!
Kuhusika kwa maana ya uchunguzi au kuhusika kwa maana ya Marekani ndio iliyofanya tukio?
Kama kwa maana ya kusaidia uchunguzi, mimi nitakujibu hivi:
Kutokana na ubora wa teknolojia yake na uwezo mkubwa wa ujasusi wa kigaidi,
Sisi kama taifa tunaweza kuwaomba waje wasaidie uchunguzi huo!
Vilevile zingatia kuwa sheria ya kupambana na ugaidi duniani tuliyoridhia 2003 inaipa mamlaka marekani yakufanya shughuli za kijasusi katika taifa lolote lile panapotokea tukio la kigaidi ama kuhisiwa kuwepo kwa ugaidi!
Vivyo hivyo sheria hiyo inasema mtu yeyote atakaekamatwa kwa tukio la kigaidi linaloilenga Amerika atashitakiwa katika mahakama ya Amerika!
Sisi hatuna hata vifaa vyakutambua aina ya mabomu ni vigumu kubaini hata wahusika!
Bwana Mohamed Said
Mbona unaweka dhihaka tena?
Yawezekana hili suala la ugaidi limekukera sana, ili mimi nimelisotea mpaka kufika hatua ya leo kutoa kile ninachokifahamu!
Juu ya Zanzibar kwanza naomba nifahamu msimamo wako,
Je na wewe unaamini mapinduzi yale yalikuwa ni dhidi ya uislamu ama dhidi ya Sultan?
Yericko,
Waamerika weshafanya hapa huo upelelezi unaousifia kuwa una nyezo ambazo Tanzania hawana.
Soma hapa chini nilichowaeleza Waamerika katika mkutano Chuo Kikuu Cha Ibadan:
''After 9/11 the United States passed the Patriot Act of 2001.The Prevention of Terrorism Act of 2002
Kuhusika kwa maana ya uchunguzi au kuhusika kwa maana ya Marekani ndio iliyofanya tukio?
Kama kwa maana ya kusaidia uchunguzi, mimi nitakujibu hivi:
Kutokana na ubora wa teknolojia yake na uwezo mkubwa wa ujasusi wa kigaidi,
Sisi kama taifa tunaweza kuwaomba waje wasaidie uchunguzi huo!
Vilevile zingatia kuwa sheria ya kupambana na ugaidi duniani tuliyoridhia 2003 inaipa mamlaka marekani yakufanya shughuli za kijasusi katika taifa lolote lile panapotokea tukio la kigaidi ama kuhisiwa kuwepo kwa ugaidi!
Vivyo hivyo sheria hiyo inasema mtu yeyote atakaekamatwa kwa tukio la kigaidi linaloilenga Amerika atashitakiwa katika mahakama ya Amerika!
Sisi hatuna hata vifaa vyakutambua aina ya mabomu ni vigumu kubaini hata wahusika!
Yericko,
Niwekee maneno ya dhihaka niloweka hapa.
Yericko,
Huna ''intellect'' ya kumpa darasa yoyote yule katika jamvi hili.
Wala huna hata udole wa kufanya talii katika kitabu chochote.
Unachoweza kufanya wewe ni sasa kuanza kupinda mgongo usomeshwe.
Sie wenzako katika udogo wetu tulikaa chini tukapiga magoti tukasomeshwa.
Vinginevyo utabaki kama tunavyokuona hapa...
[/FONT] [/I]
Unazidi kujidhalilisha na upunguani wako nchi nyingi tu duniani zimeikataa iyo sheria ya kipuuzi ya ugaidi ya Marekani.
Nenda Kenya tu hapo kwa majirani zetu walikataa huyo upuuzi.
Acha uongo wewe eti Marekani anaweza kufanya shughuli za kijasusi nchi yeyote sijui hii umeipata wapi wewe kauzu.
Waende basi wakafanye shughuli zao za Ujasusi, China, Urusi, Uturuki Iran au Korea Kaskazini au Somalia, Cuba, Venezuela.
Haya hapa,
Hii ni dhihaka
Unaweza ukahisi kwamba watu wanakuona wa maana kwa mabandiko yako hapa kwasababu ya sifa wanazokupa ila UNAJIDHALILISHA sana ndugu yangu hao wanaokupa sifa hawaandiki hayo matusi japo na wenyewe wanaweza kuwa na chuki sawa na zako...
Kauli zako zinaonyesha ni mtu uliyekulia kwenye malezi gani japo inaonyesha uliingia Darasani kidogo
Jaribu kuwa na heshima kwenye Majadiliano
Lugha zako hazifanani na mtu anayepigania DINI yake na HISTORIA yake
Ndugu usikurupuke,
Haya ninayoyaongea yanazihusu nchi zilizoridhia sheria hizo ikiwemo Tanzania,
Wabunge wa chama chako ccm waliridhia sheria hiyo mwaka 2003
Na kwakukusaidia zaidi ni kuwa kile kilichotajwa na Mohamed Said kuwa Balozi wa USA
"alilihutubia Bunge la Jamhuri"
badala ya kusema alizungumza na WABUNGE wa bunge la jamhuri,
Hicho ndicho kilikuwa kikao chakuwatongoza wabunge wakifika bungeni wairidhie hiyo sheria ambayo inaukikwaji mkubwa wa haki za binadamu ndani yake!
Ni bunge la Pius Msekwa chini ya wabunge 99% wa ccm ndio waliobariki uhalifu huo!
Haya hapa,
Hii ni dhihaka