zomba
Asante sana kwa kunifanya nicheke saana asubuhi hii. Siku imeanza vizuri.
Tatizo ni moja tu:
Kuna waislam ninawaheshimu hapa jamvini na hata mitaani kwetu, na haitakuwa busara kuijibu hiyo post yako wakati najua nitawaudhi na wengine. Na kwasababu mambo yenyewe hayahusiani na historia au uchochezi wa Moh, basi naomba kukubali kushindwa katika hoja hizi.
Turudi kwenye historia.
Ritz,Hata hiyo hatua ya Mwalimu kuitwa Mwenye Heri haijafikiwa. Ni kazi ngumu sana kuifikia hatua hiyo kuliko hata kutangazwa Mtakatifu.Unaweza kunitajia marais wangapi duniani ambao ni Wakatoliki ambao wamekidhi vigezo ivyo na kutangazwa wenye heri kisha watakatifu.
Wanaukumbi nafurahi kiasi naoa mjadala unaelekea ukingoni hoja mbali mbali zimejibiwa kiustaharabu na kwa ufundi wa hali ya juu sana.Nimefurahi kuona jambo moja likijitokeza wazi pasipo na shaka yoyote kwamba sumu iliyokuwa ikimwagwa kwa muda mrefu hatimaye imepata majibu stahiki.Ni wajibu wetu sote kuhakikisha masuala ya mazito kama haya yanapojitokeza yasiachwe yakisambaa kwa muda mrefu yakaharibu jamii yetu.
Nawashukuru wote waliojitolea muda wao mwingi na kushughulisha akili kwa faida ya VIZAZI VYA SASA NA VIJAVYO hapa pia napenda angalizo na Wickama lizingatiwe sana hii mitandao ina nafasi kubwa na pana kuliko hata vitabu ambavyo kwa sehemu kubwa havisomwi na vijana wengi ukilinganisha na mitandao.
Vipi kuhusu ukubwa wa taasisi kristo(Uwingi wa wakristo na mataasisi,miradi mbalimbali wanayoiendesha kuisaidia jamii-vitu ambavyo hupelekea kuomba misamaha ya kodi mfano vituo vya watoto yatima,makanisa,vyuo,mashule nk) ukilinganisha na ukubwa wa taasisi islamu(uwingi wao na upana wa wigo wa mambo wanayo yafanya)? Vipi kuna upendeleo wowote kwa taasisi za kiislamu zinazotoa huduma kwa jamii au misikiti kukataliwa misamaha ya kodi wakiomba serikalini? Ahsante!
Issue hapa inatokana na Dhana ya Serikali kutokuwa na Dini au Serikali ya Kisekula Dhana hiyo ni maarufu Tanzania. Mara nyingi katika masuala yahusuyo dini, viongozi wa serikali husikika wakisema «serikali haina dini, ila wananchi wake wana dini zao ». Hoja ya usekula wa serikali ni ya kihistoria. Ilijengwa kiasi cha miaka miambili iliyopita ikitaka serikali ijiepushe na shughuli za kidini hususan katika masuala ya elimu, mafundisho ya maadili na na ibada.Japokuwa Tanzania imekuwa ikidai kwamba serikali yake ni ya kisekula, hali halisi haioneshi hivyo. Pamoja na madai hayo, serikali ya Tanzania imewahi kuingia katika msuguano na Waislamu na baadhi ya wasiokuwa waislamu pale Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilipotaka kuanzisha somo la dini au maadili ya nchi. Kadhia hii ni maarufu kwa jina la "dini mseto". serikali ya kisekula haiwezi ikaja na mipango ya kusomesha dini kwa jina lolote lile liwe la maadili au vyovyote vile.
Mifano mingine inayotia wasiwasi usekula wa serikali ya Tanzania ni hii ifuatayo:
1. Wimbo wa Taifa – unaomba mungu aibariki nchi
2. Dua ya Bungeni – ina muomba mungu
3. Kuapishwa kwa wanaochukua nafasi za uongozi.
Japo wanaoapa huapa kwa dini zao, aneapishasi kiongozi wa dini husika bali wa serikali au wabunge.
Utaratibu huo hauendani na madai kuwa nchi au serikali ya Tanzania haina dini, bali wananchi wake ndiyo wenye dini. Swali ni je, tunapomtaja Mungu katika wimbo wa taifa au katika dua ya bungeni, na kadhalika, tunamkusudia mungu yupi? Mungu wa Waislamu? Wa Wakristo? Wa dini za asili? Je, kuna mungu wa kitaifa? Mungu huyo wa kitaifa ni yupi na ni wa dini gani?Je, katika hali hiyo, ni kweli serikali haina dini? Katika mazingira ya Waislamu kuandamwa na kukandamizwa na mila ya Mfumokristo, mfumo ambao unajidhihirisha zaidi katika vitendo vya kibaguzi vinavyofanyiwa Waislamu na sehemu kubwa ya watendaji serikalini na katika taasisi mbalimbali, kwa nini mwananchi Muislamu asiamini kuwa serikali hii si ya kisekula bali ni ya kidini; na dini yenyewe ni Mfumokristo.
According to TRA / HAZINA....
Mbinu zinazotumiwa na Mfumokristo katika Kujihakikishia Fursa TanzaniaUongozi wa Shule za Sekondari na Vyuo vya Ualimu nao umemilikiwa vilivyo. Nafasi za Maafisa elimu Wilaya na Mikoa na wakaguzi wakuu wa elimu wa Kanda kwa zaidi ya asilimia 85 zinaendelea kuwa miliki ya hawa Wakristo.
Mfumokristo ni hali ambayo Wakristo wa Tanzania wamehodhi madaraka ya ngazi zote muhimu katika serikali na katika vyombo vya maamuzi, na kuzitumia nafasi hizo kuwaendeleza Wakristo na Ukristo na kuwabagua Waislamu na dini yao.
1. Kuendeleza mfumo wa kibaguzi katika elimu kama ulivyoachwa na wakoloni. Wakoloni wa kijerumani ndio walioanzisha mfumo wa kuwabagua Waislamu katika elimu baada ya kushinikizwa na makanisa. Ushahidi wa mashinikizo hayo unaweza kupatikana katika rejea zifuatazo: Cameroon and Dodd 1970:56, Kurtz1972:19, Smith 1963:16. Hatimaye kutokana na mashinikizo hayo serikali ilikubali kufaya yafuatayo:-
i. Kuwafukuza kazi Waislamu waliokuwa serikalini na kuwaingiza Wakristo (Tazama Cameroon and Dodd1970: 25, 56, pia Roland 1970:205)
ii. Kuzipa shule za wamisheni msaada wa kifedha kutoka kodi za wananchi huku wakizibagua zile za Waislamu (Tazama Roland: 1970: 205,na Cameroon and Dodd 1970:50)
iii. Kuweka mpango mkakati wa kuwabagua na kuwahujumu Waislamu na Uislamu wao. Tazama Roland 1970:205, Kurtz 1972:29. Cameroon and Dodd 1970:114.
iv. Kujenga hoja kwamba Waislamu kwa asili yao si watu wa kuendelea na kuwa ni wavivu. Tazama E.B Castle 1966:37 ambaye anasema, " Islam hinders progressive attitude to change in society and a community that accepts Islam is less likely to advance in social welfare and education", yaani Uislamu ni kikwazo cha fikra za maendeleo na mabadiliko katika jamii, na kwamba jamii ikiukubali Uislamu haiwezi kamwe kupiga hatua za katika ustawi wa na elimu. Pia Abel Ishumi 1980:208 anasema, "From the beginning Muslims were opposed to western type formal education", Kwamba Waislamu walipinga elimu. Pia Abel Ishumi 1981:43, "Muslims believe highly in fatalism" Kwamba Waislamu wanabweteka na kuamini kwao kuwa mambo yameshakadiriwa.
2. Kuhujumu taasisi za Waislamu na kuweka viongozi mamluki.
Baada ya uhuru Serikali ya Tanzania imekuwa na muelekeo wa kuziandama taasisi zinazoonekana kuwa na mipango madhubuti ya kuwakomboa Waislamu kuondokana na ujinga na umaskini. Rejea Bergan 1981:26 na Sivalon 1992:3 kuhusu kuvunjwa kwa EAMWS na kuanzishwa kwa BAKWATA. Pia soma Anuur na. 13 la Agosti 1992 juu ya taarifa ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ya kuitaka Serikali kuifuta EAMWS. Pia tazama Njozi 2000:31. "Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania kuhusu kadhia ya kuvamiwa kwa Msikiti wa Mwembechai na hatimaye kuuliwa kwa Waislamu.
3. Kuhodhi mfumo wote wa elimu nchini.
Tangu kuondoka kwa Mkoloni Wakristo wamekuwa kama mabaki ya wakoloni na ukoloni. Ukiondoa shule za msingi na sekondari za Kata, huko katika shule za sekondari za Serikali, vyuo vya kati na vyuo vikuu wanafunzi na wafanyakazi ni Wakristo kwa zaidi ya asilimia 80. Siku hizi katika shule za Kata wanafunzi Waislamu wameanza kuonekana. Katika taasisi za elimu mfano T.I.E, TEA, NECTA, Bodi ya Mikopo, I.A.E na vyuo vyote nchini, uongozi umekuwa ni mali ya Wakristo.
Huko mwanzo walidai kwamba hamna Muislamu mwenye elimu ya kutosha kuongoza. Kwa siku za hivi karibuni madai yao kwa wale Waislamu wachache waliofanikiwa kupata elimu ni kuwa hawafai kwa vile wana, "udini".
Aidha katika Wizara ya Elimu (MOEVT) tangu Wizara hiyo kuundwa uongozi umekuwa mali ya Wakristo kwa zaidi ya asilimia 90. Nafasi kama ya Kamishina wa Elimu haijawahi hata kuwa na Kaimu Muislamu na wala haitarajiwi chini ya Mfumochristo. Nafasi zawakurugenzi nazo zimemilikiwa na Wakristo. Mfumokristo umejikita barabara.
Mfumokristo ni hali ambayo Wakristo wa Tanzania wamehodhi madaraka ya ngazi zote muhimu katika serikali na katika vyombo vya maamuzi, na kuzitumia nafasi hizo kuwaendeleza Wakristo na Ukristo na kuwabagua Waislamu na dini yao.
1. Kuendeleza mfumo wa kibaguzi katika elimu kama ulivyoachwa na wakoloni. Wakoloni wa kijerumani ndio walioanzisha mfumo wa kuwabagua Waislamu katika elimu baada ya kushinikizwa na makanisa. Ushahidi wa mashinikizo hayo unaweza kupatikana katika rejea zifuatazo: Cameroon and Dodd 1970:56, Kurtz1972:19, Smith 1963:16. Hatimaye kutokana na mashinikizo hayo serikali ilikubali kufaya yafuatayo:-
i. Kuwafukuza kazi Waislamu waliokuwa serikalini na kuwaingiza Wakristo (Tazama Cameroon and Dodd1970: 25, 56, pia Roland 1970:205)
ii. Kuzipa shule za wamisheni msaada wa kifedha kutoka kodi za wananchi huku wakizibagua zile za Waislamu (Tazama Roland: 1970: 205,na Cameroon and Dodd 1970:50)
iii. Kuweka mpango mkakati wa kuwabagua na kuwahujumu Waislamu na Uislamu wao. Tazama Roland 1970:205, Kurtz 1972:29. Cameroon and Dodd 1970:114
iv. Kujenga hoja kwamba Waislamu kwa asili yao si watu wa kuendelea na kuwa ni wavivu. Tazama E.B Castle 1966:37 ambaye anasema, " Islam hinders progressive attitude to change in society and a community that accepts Islam is less likely to advance in social welfare and education", Yaani Uislamu ni kikwazo cha fikra za maendeleo na mabadiliko katika jamii, na kwamba jamii ikiukubali Uislamu haiwezi kamwe kupiga hatua za katika ustawi wa na elimu. Pia Abel Ishumi 1980:208 anasema, "From the beginning Muslims were opposed to western type formal education", Kwamba Waislamu walipinga elimu. Pia Abel Ishumi 1981:43, "Muslims believe highly in fatalism" Kwamba Waislamu wanabweteka na kuamini kwao kuwa mambo yameshakadiriwa.
2. Kuhujumu taasisi za Waislamu na kuweka viongozi mamluki. Baada ya uhuru Serikali ya Tanzania imekuwa na muelekeo wa kuziandama taasisi zinazoonekana kuwa na mipango madhubuti ya kuwakomboa Waislamu kuondokana na ujinga na umaskini. Rejea Bergan 1981:26 na Sivalon 1992:3 kuhusu kuvunjwa kwa EAMWS na kuanzishwa kwa BAKWATA. Pia soma Anuur na. 13 la Agosti 1992 juu ya taarifa ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ya kuitaka Serikali kuifuta EAMWS. Pia tazama Njozi 2000:31. "Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania kuhusu kadhia ya kuvamiwa kwa Msikiti wa Mwembechai na hatimaye kuuliwa kwa Waislamu.
3. Kuhodhi mfumo wote wa elimu nchini. Tangu kuondoka kwa Mkoloni Wakristo wamekuwa kama mabaki ya wakoloni na ukoloni. Ukiondoa shule za msingi na sekondari za Kata, huko katika shule za sekondari za Serikali, vyuo vya kati na vyuo vikuu wanafunzi na wafanyakazi ni Wakristo kwa zaidi ya asilimia 80. Siku hizi katika shule za Kata wanafunzi Waislamu wameanza kuonekana. Katika taasisi za elimu mfano T.I.E, TEA, NECTA, Bodi ya Mikopo, I.A.E na vyuo vyote nchini, uongozi umekuwa ni mali ya Wakristo. Huko mwanzo walidai kwamba hamna Muislamu mwenye elimu ya kutosha kuongoza. Kwa siku za hivi karibuni madai yao kwa wale Waislamu wachache waliofanikiwa kupata elimu ni kuwa hawafai kwa vile wana, "udini". Aidha katika Wizara ya Elimu (MOEVT) tangu Wizara hiyo kuundwa uongozi umekuwa mali ya Wakristo kwa zaidi ya asilimia 90. Nafasi kama ya Kamishina wa Elimu haijawahi hata kuwa na Kaimu Muislamu na wala haitarajiwi chini ya Mfumochristo. Nafasi za wakurugenzi nazo zimemilikiwa na Wakristo. Mfumokristo umejikita barabara. Uongozi wa Shule za Sekondari na Vyuo vya Ualimu nao umemilikiwa vilivyo. Nafasi za Maafisa elimu Wilaya na Mikoa na wakaguzi wakuu wa elimu wa Kanda kwa zaidi ya asilimia 85 zinaendelea kuwa miliki ya hawa Wakristo.
4. Kukataa kutunga sera za kuondoa upendeleo wa Wakristo katika elimu na kuendeleza ulaghai dhidi ya wananchi wasiokuwa Wakristo. Mara baada ya uhuru ilielezwa na viongozi wetu akiwemo Mwl. Nyerere kuwa serikali itachukua hatua kuondoa mpango ulioasisiwa na Wakoloni wa kuwabagua Waislamu. (tazama A. Jumbe 1994:123, Court 1976 na Nyerere in Hansard Desemba 10, 1962). Badala yake hatua zilizochukuliwa hazikulenga kuondoa tatizo la ubaguzi wa kidini katika elimu nchini na kuwaondoa pia katika ajira na madaraka.Mfano wa hatua hizo ni pamoja na:
i. Kufuta ada shule za msingi na sekondari miaka ya 1960/70.
ii. Kuweka kikomo cha elimu ya msingi kuwa miaka 7 bila kusita.
iii. Kuondoa mitihani ya darasa la 4 na 5. iv. Kuanzishwa kwa mpango wa UPE.
v. Kujenga shule za msingi za bweni kwa watoto wa wafugaji na wavuvi wanaoishi kwa kuhamahama
vi. Kutaifisha shule za binafsi zilizokuwa chini ya mashirika ya dini na watu binafsi. Mpango huu haukuhusisha seminari za Wakristo.
vii. Kupeleka wanafunzi sekondari kwa kigezo cha KUCHAGULIWA badala ya KUFAULU kulikoendana na kuyafanya matokeo ya mtihani wa darasa la saba kuwa ni siri.
viii. Kuanzishwa utaratibu wa "quota system" ambapo kila mkoa ulipangiwa idadi ya wanafunzi watakaochaguliwa kwenda sekondari.
ix. Kuweka utaratibu mgumu wa kuanzisha na kuendesha shule binafsi chini ya sheria ya elimu ya mwaka 1978, hivyo watu wote kulazimika kusoma katika shule chache za sekondari za Serikali
x. Kuanzishwa kwa shule maalum za vipaji katika miaka ya tisini mfano: Kibaha, Kilakala, Ilboru, n.k.
xi. Kutoa upendeleo maalum (Affirmative Action) kwa watoto wa kike kuingia sekondari na vyuo. Aidha kuwepo pia kwa mipango ya kuwasomesha watoto wa kike kutoka familia maskini.
xii. Ujenzi wa Shule za Sekondari za Kata. Sera hizi zote pamoja na nyinginezo hazikusaidia kuondoa uwiano mbaya au ubaguzi wa elimu kwa Waislamu. Tuangalie mfano michache ifuatayo: Ni ukweli usiopingika kwamba UPE awamu ya kwanza iliyosukumwa na UNESCO na awamu ya pili iliyosukumwa na Malengo ya Milenia (MDGs) na Mpango wa Elimu kwa wote (EFA) zimesaidia kuwahakikishia watoto wengi wa Kiislamu elimu hiyo ya msingi. Lakini sera hii ilikuja katika kipindi ambacho elimu ya msingi haikuwezi tena kumpatia mtu ajira katika sekta rasmi na hata ile ya binafsi.
Ikumbukwe kwamba katika kipindi hicho cha miaka ya 60 hadi 2000 nafasi za masomo ya sekondari ziliendelea kuwa haba. Wakati wote huu watoto wa Kikristo ndiyo walioendelea kufaidika na elimu ya sekondari. Masomo hayo ya sekondari hatimaye yaliwapatia fursa za kuingia vyuo vikuu na hivyo kuwa katika nafasi za kuajiriwa serikalini, kuteuliwa katika vyeo na nyadhifa mbalimbali huku Waislamu waliowaacha shule za msingi wakiambulia ajira za usafi na utarishi.
Naam, Mfumokristo umefanikiwa kuwafanya Wakristo kuwa warithi wa wazungu wakoloni na kuwaacha Waislamu katika hadhi lie ile waliokuwa nayo wakati wa ukoloni. Aidha kutaifishwa kwa shule hakujasaidia Waislamu kupata elimu ya sekondari kama inavyodaiwa kuwa Nyerere alitaifisha shule ili Waislamu wasome.
Kama tulivyoona awali kuwa tangu wakati wa Mjerumani serikali ya kikoloni ilikuwa ikitoa pesa kusaidia ujenzi na uendeshaji wa shule za Wakristo ni dhahiri kuwa shule hizi zilikuwa zimeshalemazwa na pesa za serikali kwa kipindi cha miaka 55, tangu mwaka 1914 hadi mwaka 1969 zilipotaifishwa. Tazama maandiko ya Katibu Mkuu wa Baraza la Maskofu Katoliki (TEC) Fr Robinson, D.W 1965:14 kwamba, "The Church is now totally dependent on State aid for the administration of these schools. If this aid were withdrawn the church will be forced to close its schools"
Yaani, Kwa sasa Kanisa limekuwa tegemezi kabisa kwa serikali katika kutoa pesa za kuendesha shule zake na ikiwa serikali itasita kutoa fedha kwa shule hizi basi Kanisa litalazimika kuzifunga. Ni dhahiri basi kwamba hatua aliyochukua Julius Nyerere ilikuwa na malengo makuu ya kuziokoa shule za Kanisa kufungwa kwa sababu ingekuwa jambo la kiroja kwa serikali ya Tanzania kuendelea kutoa pesa za kuendesha shule za Kanisa kwa wakati ule, na pili kuhakikisha kwamba malengo ya shule zile ya kuwasomesha Wakristo yanaendelea kutekelezwa kwa kutumia pesa za umma.
Kimsingi kilichobadilika ni jina la mmiliki tu uongozi na malengo ya shule yalibaki vile vile. Ndiyo maana hakuna mtu yoyote aliyethubutu au atakayethubutu kudai eti kwamba ukienda katika shule zilizotaifishwa mfano, Pugu, Minaki, Tambaza, Zanaki, Jangwani, Kibasila, Ilboru, Weruweru, Tosamaganga, Msalato, Umbwe, Ndanda n.k, utakuta idadi ya kuridhisha ya wanafunzi Waislamu wanaosoma huko. Lakini hata katika shule za sekondari chache mpya ambazo serikali ilijenga au kujengewa mwishoni mwa miaka ya 70, kama vile: Kibiti, Ruvu, Karatu, Bagamoyo n.k , kote walimu, wafanyakazi na wanafunzi ni Wakristo kwa zaidi ya asilimia 80.
Watoto wachache wa Kiislamu wanaosoma huko huonekana kama wakimbizi wanaosaidiwa katika nchi ya ughaibuni. Kuhusu kuingia sekondari kwa kigezo cha kuchaguliwa na mpango wa quota system, watendaji Wakristo waliojazana katika mfumo wa elimu nchini wamekuwa wakihakikisha kwamba Waislamu hawasomi kutokana mbinu zifuatazo:-
i. Kufanya matokeo ya darasa la saba kuwa ni siri hivyo kuweza kuibadili nafasi walizoshinda Waislamu na kuwapa wengine. Tazama ushahidi mzito uliotolewa na Njozi mwaka 2000; katika kitabu cha Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania uk. wa 62 -70. Hapa vijana wa Kiislamu waliofaulu darasa la saba walinyimwa nafasi kuingia sekondari na wale waliofaulu kidato cha nne walinyimwa kuingia kidato cha tano. Kazi hii ya kuwakwamisha vijana wa Kiislamu ilifanywa vyema na mawakala wa Mfumokristo waliojazana katika mfumo wote wa elimu nchini.
ii. Kuhamisha wanafunzi Wakristo kutoka maeneo yenye ushindani mkubwa kwenda Mikoa iliyokuwa na alama ndogo za kuchaguliwa kama Pwani, Dar, Lindi, Mtwara na Tanga ambayo pia ni maeneo ya Waislamu . Tazama Malekela 1983 in "Access to secondary education in Sub- Sahara Africa"
iii. Huko nyuma kabla ya wanafunzi kupangiwa shule za sekondari namba zao za mtihani ziliambatanishwa na majina ili kujua nani Mkristo apendelewe na nani siyo awachwe iv. Kuhakikisha kwamba viongozi na watendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) wote ni Wakristo. Aidha kwa asilimia kubwa kabisa watungaji wa mitihani na wasahihishaji pia ni dini hiyo hiyo. Tazama kitabu cha Miaka Thelathini ya NECTA, 2004 au www.necta.ca.tz
Vema sana mkuu, sasa tunaweza kusonga mbele hoja kwa hoja!
Ikiwa umeaminisha kuwa Mapinduzi yale yaliyoungwa mkono na Nyerere yalikuwa Kharama, kwamaana ya yalikuwa ya kuua uislamu,
Naomba ujibu swali hili,
Kwanini Mapinduzi hayo ya (Okello) leo hii yaadhimishwe tena kwa heshima tere huku ikiaminika kuwa Zanzibar ni 99% ni waislamu?
Kadogoo,
..naomba nianze na suala la Biafra kwanza.
..kwa mtizamo wangu Nigeria kulikuwa na vita ya kikabila, siyo vita ya kidini. sidhani kama ilikuwa vita baina ya Wakristo vs Waislamu, kwasababu huo upande unaodaiwa kuwa na Waislamu ulikuwa na wanajeshi Wakristo. Olusegun Obasanjo, Mkristo, alikuwa upande wa federal gov of Nigeria.
..kwa hiyo Nyerere alikwenda kusaidia Waibo, waliokuwa wakichinjwa na Wanigeria wenzao.
..mimi ningekushauri utafute hotuba iliyotolewa na C.Y.Mgonja[waziri wa nchi ofisi ya Raisi ] kuelezea kwanini Tanzania iliamua kuitambua Biafra. naamini kabisa kama uko open minded utakubaliana na hoja zilizotolewa na serikali ya Tanzania.
..Hata mimi nashangazwa sana na hii process ya kumfanya Mwalimu Nyerere mwenye heri na baadaye Mtakatifu. Mimi namuelewa zaidi Mwalimu kama mwanasiasa, yes he was a devout Catholic, lakini sidhani kama alifanya mambo yoyote yale ya "kiroho" au "kitume" kustahili ngazi ya wenyeheri and eventually utakatifu.
..Lakini Mwalimu amepewa sifa nyingi sana, na wakati mwingine hata yeye mwenyewe alikuwa anashangaa. Kuna kipindi India walimpa nishani ya amani na unaharakati wa kuzuia silaha za nuklia[naomba kusahihishwa kama kuna makosa]. Mwalimu katika hotuba ya kushukuru alisema bayana kwamba ameshangaa yeye kupewa nishani hiyo ukizingatia kwamba siyo mara moja ambapo aliunga mkono mapambano ya silaha.
..Umeuliza kuhusu mauaji ya Zanzibar na Mwembechai kama yangeweza kutokea wakati wa Mwalimu. Kwa mtizamo wangu naweza kusema yasingeweza kutokea. Nasema hivyo kwasababu Mwalimu na vyombo vyake vya usalama walikuwa na tabia ya "kunyakua" vinara wa machafuko kabla hawajaleta madhara kwa jamii nzima.
..Mwalimu pia alikuwa haogopi kujibu shutuma zozote zile dhidi ya serikali yake. Kwa mfano, hawa jamaa wanaohubiri mfumo Kristo wasingeachiwa wakatamba nchi nzima kwa miaka kadhaa bila kujibiwa na Mwalimu mwenyewe, au kutiwa kizuizini.
..Mwisho, nadhani Mwalimu alichukia dhuluma kwa namna ya kipekee kabisa. Kutokana na msimamo huo ndiyo maana unaona alikuwa radhi kwenda kinyume na OAU charter kuwatetea Waibo wa Biafra. Ndiyo maana akakubali Tanzania ikose misaada ya kiuchumi toka Uingereza kwa msimamo wetu wa kuwatetea wananchi wa Zimbabwe. Kwa kuchukia dhuluma hakuogopa kutoa msaada wa kijeshi kwa Frelimo waliokuwa wakipambana na Wareno, wanachama wa NATO.
cc: Jasusi, Kudi Shauri, gombesugu, Ritz, Wickama
Yericko,
Kuna mengi sana ya kusimulia katika haya kwani siku ya mapinduzi mimi nilikuwepo kabisa na niliona kila kitu namna tulivyozuiliwa watu wa shanghani tusitoke mjini.
Sikubaliani na wewe hata kidogo unapoita mapinduzi ya OKELLO. Tujiulize Okello mmoja aliweza fanya mapinduzi hayo pekee kuanzia mjini mpaka ng'ambu? au alitumika kama Muwa tu baada ya kuisha utamu unatupwa.
Kadogoo,
Hili suala tulishalijadilia kwa kirefu sana hapa JF. Kwanza si kweli kwamba Nyerere alipeleka majeshi yetu Biafra kuwasaidia Waibo. Hilo la kwanza, pili, ni dhana potofu kuwa uamuzi wa Tanzania kuitambua Biafra ulikuwa na misingi ya kidini. Kilichotokea, kwa kifupi tu ni kwamba baada ya mapinduzi ya Tafawa Balewa, yaliyofanywa na vijana wa kijeshi akiwemo Gowon, ambaye si Muibo, na Ojukwu, Muibo, ndugu zetu wa kaskazini, Wahausa ambao majority ni waislamu, wakadhani kuwa ni Waibo ambao wamempindua Mhausa mwenzao. Walianzisha machinjo ya kulipiza kisasi kwa kila Muibo aliyekuwa katika jimbo lao. Si mwenye duka, mwenye teksi, mwalimu wa darasani, mauaji kama yale yaliyotokea Rwanda 1994 yalifanyika Nigeria. Waibo waliosalimika wakakimbilia kwao, na kwa kuwa hawakuliamini jeshi linaloongozwa na Wahausa, wauaji wao, wakaamua kujitenga. Mwezi Februari 1967, Mwalimu Nyerere alifanya ziara Afrika magharibi ambako alikutana na rais wa Ivory Coast, na pia alikutana na Gowon. Akamwambia Gowon kuwa lazima ajadiliane na Ojukwu wapate muafaka katika mauaji yanayoendelea Nigeria. Gowon alikataa akasema kuwa hawezi kujadiliana na "junior" wake. Arrogance. Tanzania, Zambia,Ivory Coast na nchi nyingine nimeisahau zikaamua kuitambua Biafra. Lengo lilikuwa ni kusimamisha mauaji yaliyokuwa yanaendelea dhidi ya Waibo. Lakini kwa sababu ya international politics, Uingereza iliunga mkono serikali ya Gowon na hatimaye walishinda vita. Lakini the genocide was real na kama wewe ni mtu unayependa kupekua mabuku nakushauri usome kitabu "The International Politics of the NIgerian Civil War, 1967-1970." Kimeandikwa na John J. Stremlau. Nakumbuka siku tulipotangaza kuitambua Biafra ilikuwa ni easter na jumapili Mwalimu Nyerere alikuja nyumbani kwa easter dinner. Alifuatana na Mnanka na Philemon Mgaya. Wakati Mnanka anampongeza kwa uamuzi huo Mwalimu alikuwa akijiuliza loudly, "will Africa understand?" Kwa sababu aliiona hiyo contradiction ya kuunga mkono kujitenga kwa Biafra wakati huo huo unahubiri umoja wa Afrika. Will Africa understand?
Unaweza kunitajia marais wangapi duniani ambao ni Wakatoliki ambao wamekidhi vigezo ivyo na kutangazwa wenye heri kisha watakatifu.
Mimi na maswali mawili kwako kwa faida ya wanaukumbi ungetupa majibu kutokana na bandiko lako.
1) Waislam wa wapi wanawaita maswahaba watakatifu, hii umeipata wapi tupe dalili, katika Uislam ni makosa makubwa kumuita binanadamu mwenzako mtakatifu hiyo sifa ni ya Allah peke yake.
2) Unataka kutuambia Kanisa Katoliki limemuita Nyerere mwenye heri na mtakatifu sababu aliandika vitabu vya sala za Kikatoliki kwa Kizanaki. Ni watu wangapi ambao wameitwa watakatifu na wenye heri kutokana na kuandika vitabu vya sala kutokana na lugha zao.
Cc.. gombesugu, Kadogoo,
Jasusi,
Mbona unaleta mambo ya dinner table ya Nyerere's Clan hapa jamvini!?
Yaani mazungumzo ya Nyerere na Wakristo wenzie wana-discuss na kupongezana religious war/conflict at the dinner table ambayo yeye Nyerere amehusika kwa kina...halafu unaleta hayo mazungumzo hapa jamvini ili iwe ndio kianzio cha discussion!?
Kama ni hivyo,haina neno maana nasisi wengine pia tunazo saana hizo stori za "vinyozi wa Kipata na Mkunguni" kama mnavyoziita!
Hivi vitu si ndo siku zote nyinyi mnamkebehi Sheikh Mohammed hapa jamvini!? Mimi binafsi hicho kitabu chako nilipitia kiducu kitambo,lakini nikakitupa sababu yule mwandishi wako tayari alikua na agenda zake!
Zipo sources credible na vitabu vingine vingi kwa mwenye kutaka kujua mtafaruku ule wa Biafra.
Huo ni mtazamo wako binafsi na wenzio. Nyerere aliingia kule kwa mtizamo wa kidini.
Nipa fursa kukuuliza suali kiduchu.
Nahisi wewe ni mmojawapo kati ya wanaodai yakuwa Nyerere hakuhusika wala haku-influence yale maafa ya Zanzibar 1964!? Kwanini unafikiri Nyerere hakufanza hivyo kusikitisha yale mapinduzi haramu dhidi ya ile Serikali ya mseto ilochaguliwa kihalali!?
Ahsanta.
Mkuu naomba nijue mambo machache toka kwako ili twende sawa na mnakasha huu,
Kwanza naomba kujua, Je unatambua Okello ndie aliyeongoza mapinduzi yale?
Pili nikuwa, je utawala mkono wa chuma wa Field Marshal au Mungu wa Afrika kama alivyopenda kuitwa wa miezi sita ndani ya ardhi ya Zanzibar ulikuwa na mkono wa Nyerere?
Hebu naomba ujibu hayo ili tujenge hoja hapo na zijibiwe hoja kwa hoja!
Yericko Nyerere,
Nashukuru umeamua kwenda na mimi taratibu,maana unajua akili za Madrassa majambo mengi sisi hutupa taabu kuyajua kwa wepesi kulinganisha na nyinyi wenzetu...
Lile suali nimemuuliza huyo nduguyo kwa maana yangu makhusus...lakina haina neno mindhal umeamua kuja wewe maana natambua yakuwa damu ni nzito kuliko maji.
Hayo masuali yoote mimi binafsi sina majibu yake na wala siyajui,ndo maana nikaanza kwa kumdodosa huyo nduguyo.
Lakini kama dasturi ya hili jamvi letu,naona na wewe badala ya kunisaidia majibu unaniletea furushi la masuali mengine!?
Tumuombe Shariff Ritz,labda aeza kuwa na jibu japo kiduchu...au watoa ushauri gani ndugu yangu Yericko!?
Shukran.
Cc;Ritz
Haina neno mkuu,
Sio kwamba nimeuliza kwakuwa sijui, laa hasha!
Nimeuliza ili kama unayafahamu vema basi nipate fursa yakujenga hoja kulingana na majibu yako mkuu!
Kama Ritz atajibu kulingana na maswali yalivyo ni jambo jema!
Nasubiri
Gombesugu,Jasusi,
Mbona unaleta mambo ya dinner table ya Nyerere's Clan hapa jamvini!?
Yaani mazungumzo ya Nyerere na Wakristo wenzie wana-discuss na kupongezana religious war/conflict at the dinner table ambayo yeye Nyerere amehusika kwa kina...halafu unaleta hayo mazungumzo hapa jamvini ili iwe ndio kianzio cha discussion!?
Kama ni hivyo,haina neno maana nasisi wengine pia tunazo saana hizo stori za "vinyozi wa Kipata na Mkunguni" kama mnavyoziita!
Hivi vitu si ndo siku zote nyinyi mnamkebehi Sheikh Mohammed hapa jamvini!? Mimi binafsi hicho kitabu chako nilipitia kiducu kitambo,lakini nikakitupa sababu yule mwandishi wako tayari alikua na agenda zake!
Zipo sources credible na vitabu vingine vingi kwa mwenye kutaka kujua mtafaruku ule wa Biafra.
Huo ni mtazamo wako binafsi na wenzio. Nyerere aliingia kule kwa mtizamo wa kidini.
Nipa fursa kukuuliza suali kiduchu.
Nahisi wewe ni mmojawapo kati ya wanaodai yakuwa Nyerere hakuhusika wala haku-influence yale maafa ya Zanzibar 1964!? Kwanini unafikiri Nyerere hakufanza hivyo kusikitisha yale mapinduzi haramu dhidi ya ile Serikali ya mseto ilochaguliwa kihalali!?
Ahsanta.
Kaka Jasusi,Gombesugu,
Kama kuna vitabu ambavyo wewe unaviona ndivyo credible katika suala la Nigerian civil war vitaje ili na sisi tuvidadavue.
Usibanie ilm. Hiki nilichokitaja nilikuta kinakubaliana na yale niliyoyajua kuhusu vita ya Biafra. Kama wewe una sources nyingine unazizipachika jina credible, zimwage hapa sote tuchote ilm. Kama dinner ya Nyerere clan imekuchefua ungechefuliwa siku nyingi na stori za Nyerere kununuliwa chakula Kariakoo. Kuhusu mapinduzi ya Zanzibar sina hakika kuwa Shamte alichaguliwa kihalali. Hayo nawaachia akina Nassor Moyo. My hands are full with our problems kule Mara.
Yericko Nyerere,
Mimi pia nilishahisi yakuwa jibu unalo kibindoni...maana wewe ni mjuzi mzuri, MwanaHistoria mahiri na mwandishi stadi.
Kwanini tu usitoe ulonalo,mpaka ufanze kwa kutegeshea!? Yakhusu nini kusubiria ilhali jawaba ulinkalia!? Mbona watufanzia inda...watutamanisha khabari halafu wafanza kuringishia!?
Tafadhali fanza kila njia ututoe hii kiu ulotuletea hapa jamvini.
Shukran.
Cc;Ritz