hongera Sheikh, Mtaalam, mjuzi, mpembuzi, mbunifu, researcher na sijui nikupe cheo gani. Hao wanapinga tu. kama wanaglikuwa wanajua wanachofanya wangalitoa angalau kimakala kimoja kupitia magazetini. Hongera Mungu akupe umri mrefu
Siyo kukubalika tu. Sheikh Mohamed is on a crusade. He is galvanizing the Moslems in Tanzania so they realize that Christianity is an enemy. Christianity has taken over the government and is the reason the Muslims are lagging behind.
Hujamsikia anasema wameshapeleka malalamiko yao serikalini? Wanasikilizwa? What is to come out of this? An insurrection?
Hilo ni moja ya tatiz kuu alilonalo mzee Mohamed Said,
Haamini katika kweli halisi ya kadamnasi bali kile alicholishwa na awaitao wazee wake!
Kichekesho ni kuwa kila mzee wakiislamu anaemtaja hapa anadai ni babu, baba, bibi, nk,
Sasa sijui yupi ni ndugu yake wa damu na ni yupi ndugu tu?
usichokijua kuhusu mimi ndicho wewe kinakushangaza na unatumia neno ''nafunguka.''
ngoja nikufahamishe kukuweka sawa.
Mimi si ccm sijapata kuwa.
Sina anijuaye ccm kwa bahati mbaya sana.
Achana na lugha ''kumtimua.''
unapoteza ladha na ''seriousness'' ya huu mnakasha.
Hiyo hotuba ya ''moto wa kiislam ukiwaka'' ni milestone katika
historia ya waislam.
Hotuba hiyo ilisomwa na bilal rehani waikela na taarifa ya habari ya
tanganyika broadcasting corporation (tbc) waliirusha.
Kutokana na hotuba ile bilal waikela alipokelewa kwa zafa na waislam tabora
akasindikizwa hadi nyumbani kwake.
(hebu nifafanulie kuhusu kujiuzulu kwa tewa na fundikira sijaelewa mantiki).
Sheikh hassan bin amir harakati zake ilikuwa elimu kwa vijana wa kiislam na ndiyo
kisa cha chuo kikuu.
Mimi ukiniuliza habari za nchi nyingine unanikwamisha sizijui.
Hizo za kilwa na nyingine za akina farid tuzitafutie wakati wake.
Hapa tuwe na mpaka wa majadiliano ''keep your eye on the ball.''
uthibitisho wa kuuliwa kwa eamws kama mahakama inavyotaka ni tabu kupata katika
''social research.''
hili nishalisema humu ndani mara nyingi tu.
Na Karume je? Unamweka kundi gani? Naye alitumiwa kuhujumu Waislamu?
naam shekhe...!
Wanipa raha sana,mnakasha ukipotea wewe waurudisha kwenye track,,
yan wakisima nchale wakikaa nchalee..!
Yani hoja kwa hoja,bali wengi wao si wenye kuutaka ukweli,ila wewe wape tuh kwa manufaa ya wengi.
Mohamed,
'keep your eye on the ball'' fair enough!
Ulipotaja kuwa EAMWS iliuawa na kanisa na Nyerere tayari ulikuwa na ushahidi.
Kama hukuwa nao hilo tunaweza kusamehe, kwa lugha nyingine ni kuwa 'umehisi''.
Hata hivyo uliposema hivyo ni lazima utakuwa na mzingira ya kiushahidi kuwa kanisa lilihusika.
Hicho ndicho wasomaji walitaka kuelewa, je, logic ya ushiriki wa kanisa ipo vipi.
Endapo hakuna ushahidi au ushahidi wa kimazingira basi tungekushauri uondoe kauli hiyo.
Vinginevyo hiyo tu inaondoa thamani nzima ya ''social research''.
Katika ''reserach'' yako uliweza kutumia maneno ''inasemekana'' dhidi ya Nyerere.
Hata kama hakuna mahali aliponukuliwa au kuhojiwa bado uliweza kufanya link kati ya mlezi wake padre wa kikatoliki, nafasi zake za masomo na kikazi na hata kuunganisha ajira yake na utata katika kupigania uhuru.
Vipi unashindwa kutumia mwenendo huo kutueleza ushiriki wa kanisa katika kuua EAMWS?
Mohamed! Mohamed Said Abdallah Salum Mwekapopo Samtungo!Alhamdulilah,
Sisi hatusemi uongo Allah kakataza.
Hii ndiyo siri ya sisi kung'ara humu ndani juu ya
kuwa tu wachache.
Nilikianza kitabu changu na Bismillah Rahman Rahim.
Publisher kanikatalia kitabu kisianze hivyo.
Oh,Mohamed yaani ungejua tunavyowathamini Watanganyika waliojitolea kuikomboa nchi hii usingesema hayo.Nyerere, Nyerere, Nyerere...
Nyie hamtaki kujua mchango wa Ali Migeyo, Idd watatu wale niliokutajieni?
Idd Faiz aliyempeleka Nyerere UNO, Idd Tosiri aliyempeleka Nyerere Bagamoyo
kwa Sheikh Mohamed Ramia Khalifa wa Quadiriyya.
Ukimpata Sheikh Ramia una maelfu wa wanachama katika TANU.
Hawa ni murid na Sheikh Ramiya ndiye Khalifa.
Hutaki kujua habari za Idd Tulio wasukaji wa mambo ndani ya Baraza la Wazee wa TANU?
Basi mmekalia Nyerere, Nyerere, Nyerere tu?
Ukitaka kujua habari za kanisa msome Sivalon.
Sivalon hakuandika kuhusu kifo cha EAMWS! Uliyeandika ni wewe na ni wewe mwenye dhima ya kutetea hoja yako.Ukitaka kujua habari za kanisa msome Sivalon.
Teh teh tehImam Shafi akiwaogopa wajinga.
Akisema yeye kwa hoja anaweza kusimama hata
na watu mia moja.
Lakini mjinga mmoja tu anamshinda.
Hotuba hiyo ilisomwa na Bilal Rehani Waikela na taarifa ya habari ya
Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC) waliirusha.
Kaka kuna tofauti kubwa kati ya malezi na ustaarabu wa Musoma na Dar es Salaam. Pwani mtu yeyote mwenye umri wa baba yake ni mzee wako.
Tuendelee kusemezana.
Really? Nani alikuwa Mkurugenzi wa TBC wakati huo? na TBC ilikuwa chini ya serikali ya Nyerere huyo huyo mwenye chuki dhidi ya Waislamu?
N
Basi mmekalia Nyerere, Nyerere, Nyerere tu?
Ukitaka kujua habari za kanisa msome Sivalon.
Labda hujui historia ya nchi hii.
Soma Sivalon ndiye aliyetuambia kuwa Kanisa Kaltoliki linaona Uislam kama adui.
Inaelekea Bwana Jasusi wewe ni mgeni katika mambo haya.
Sisi tumebobea tuna rejea lukuki.
Usidhani tumo humu kutania.
Angalia hapa chini:
The second book is by Dr John C. Sivalon, who in his expose, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985, [1] unmasks a conspiracy in the government to subvert Islam. Sivalon revealed that the Catholic Church as far back as 1961 was worried by two prospects. First, was the unity between the Muslim madhheb (sect) of Sunni, Bohora, Ismailia and Ithnasheri in Tanganyika; and the second, was the transfer of the headquarters of the East African Muslim Welfare Society (EAMWS) from Mombasa to Dar es Salaam. The Church was worried that the resources in the hands of rich Asian Muslim community in East Africa, coupled with the political power of African Muslims, particularly in Tanganyika, would endanger Christian interests in East Africa. The Church therefore declared Islam as its enemy in the country and plotted to thwart its progress.[2]
[1] John C. Sivalon, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985, (Ndanda, 1992).
[2]Ibid. p 37.
Ndipo ninaposema nyie mambo haya hamyawezi.
Basi manashindwa hata kusoma kidogo.
Utafiti kidogo.
Hiyo ilikuwa Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC) 1963.
Nyie ni mafundi wa ubishi.
Sivalon hakuandika kuhusu kifo cha EAMWS! Uliyeandika ni wewe na ni wewe mwenye dhima ya kutetea hoja yako.
Mohamed Said, waambie wanajamvi Kanisa liliua vipi EAMWS! hiyo ndiyo hoja.
Kama itakosa majibu basi, izike kauli hiyo kama ulivyzika tuhuma za namba za mitihani.
Hatumezi kama makinda ya chole au mbayu wayu tunduni, tunatumia akili zetu! Hapa ni Jamvini kila kitu hadharani, haonewi au hasamehewi mtu!