Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nitakujibu moja tu.
La Nyerere maana hilo ndilo ulipendalo.

Hakuna awezae kushusha hadhi ya Nyerere katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Hapo hakuna ubishi.

Wewe kama kawaida yako mzee unajaribu kushusha hadhi ya Nyerere kwa kutumia mbinu mbalimbali za maneno. Unazungusha maneno na kumdharaulisha mbele ya jamii; unamfanya duni ili uwainue wazee 'wako' na uko tayari kusema lolote dhidi yake kama unavyosema hapa.

Lakini historia ya uhuru haikuanza na yeye.
Historia ya TANU haiwezi kuanza na Nyerere 1954 kama ilivyogongomewa.

Tatizo ni kuwa hakuna mahali hata pamoja hadi leo miaka yote hii ambapo umewahi kuonesha kuwa Nyerere alidai kuwa historia ya uhuru ilianza na yeye au kuwa TANU ilianza na Nyerere mwaka 1954. Hakuna andiko lolote la historia ambapo linasema historia ya Uhuru ilianza na Nyerere. NONE na hujawazeza kuonesha popote. Na hakuna Mtanzania yeyote aliyesoma historia kidogo ya Tanganyika ambaye anaweza kudhania hata kidogo kuwa historia ya Kupigania uhuru ilianza na Nyerere. Hakuna kitabu hata kimoja makini kinachosema hivyo. Wewe mwenyewe hadi LEO HII hujaweza kuonesha wapi Nyerere aliwahi kudai kuwa historia ya uhuru imeanza na yeye au ya TANU kuanza na yeye.

Lakini tumeshakuonesha mara kadhaa kuwa Nyerere mwenyewe amekiri nafasi ya pekee ya wazee wa Dar na amekiri mchango wao kabla ya yeye kufika Dar na siyo wao tu bali pia mchango wa wengine wengi nchi nzima. Historia ya kupigania uhuru haikuanza na Dar na wala historia ya TANU haikuanza na wazee wako wa Dar.


Hata kama Nyerere atakasirika.

Hata angekuwa hai hawezi kukasirika. Kwa sababu unachosema hakina msingi wa ukweli hivyo hakikasirishi.

Hapa ndipo paliponifanya ninyanyue kalamu.
Ndiyo maana leo nimo humu jamvini natoa darsa na kipande ninachodarsisha ni 1929 - 1961.

Lakini unachofanya hata kidogo hakikaribiani na hiyo historia. Wenyewe wanakiita 'historical revisionism"...

You are a true historical revisionist per excellence...
 
Lakini historia ya uhuru haikuanza na yeye.
Historia ya TANU haiwezi kuanza na Nyerere 1954 kama ilivyogongomewa...
Ndiyo maana leo nimo humu jamvini natoa darsa na kipande ninachodarsisha ni 1929 - 1961.
Hapa ndipo maneno yako yanakusuta na yataendelea kukusuta...unachanganya mambo. Kama unavyochanganya Udaresalama na Uislaam, ndivyo hivyo hivyo unaanza sasa kuchanganya...historia ya uhuru inaanzia lini na kuishia lini? Ni uhuru gani unauongelea hapa...ni kutoka mikononi mwa Waarabu, Wajerumani au Waingereza. Ni uhuru wa mtu mweusi, mwafrika au mtanganyika? Unadai unatoa darasa(sic), 1929-1961...kwa nini isiwe kabla ya 1929 au baada ya 1961. Historia ya TANU iliyozaliwa mwaka 1954 inaanzia na kuishia lini? Mimi naamini kama ni historia ya Chama cha Kwanza cha siasa kudai uhuru kutoka mikononi mwa Uingereza?, jibu ni simple, TANU. Tanu haikuwapo kabla na ni Julius Nyerere, Raisi wake wa Kwanza, aliyeongoza kuanzishwa kwake mwaka 1954 na kumiliki kadi namba moja, wengine wote wale walikuwa wasaidizi wake tu...that's the naked truth and you can take that to the bank!
 
Mhh! Mpaka sasa hakuna hata mmoja anayethubutu kusema kuwa nyerere ndiye mwanzilishi wa TAA (labda kama aliianzisha akiwa na miaka 7)
-Hakuna awezaye kusema Sheikh Hassan Ameir,Abdu Sykes,Mshume Kiyate,Sheikh Suleiman Takadir hawakuwahi ku exist.

Msome vizuri Mwanakijiji, kashushiwa nondo mpaka kabakia kutaka hawa wazee wetu waandikwe na Mohamed Said kama wazalendo na si kwa dini yao!
Kwa maana Mwanakijiji kaikubali historia inayoandikwa na Mohamed Said! tatizo lake ni kuwa dini yao isitumike!l
 
Hell yes! katika orodha yako ongezea Sheikh Chaurembo, Rupia, Boman, Fundikira, Phombeah, Mwapachu, Tatu binti Said, Dr Lugazia, Dr Vedastus Kyaruzi, Clement Mtamilwa,Migeyo,Kirlo, Cecil Matola, Stephen Mhando, Dunstan Omar, Seikh Amir, Amir Kweyamba, Asha binti Mohamed, Mzee Abdallah Mwekapopo Samtungo, Babu Isevya n.k. n.k.

Nikuulize swali, ni kweli kuwa Abdul Sykes alimuingiza Nyerere kwa mara ya kwanza katika siasa mwaka 1953.
Swali hilo tu!
 
Sidhani kama MS anazungumzia namba. Fulani wa kwanza na yule wa ... Anazungumzia dhulma hadi ya kiuandishi. Anaandikwa mesi tu utadhani alicheza peke yake. Na hili mnalijua, lipo wazi, ila mnalipotezea tu.

sawa; lakini tumeuliza imeandikwa wapi kuwa Nyerere alikuwa peke yake? Au wewe umewahi kusoma wapi kuwa Nyerere alikuwa peke yake katikaharakati za uhuru au katika kuanzisha TANU?
 

aah hata kidogo; hutasikia wengine tunataka Kyaruzi, Rupia na wengine waandikwe kwa sababu ni Wakristu. Lakini kubwa ambalo labda hujalisoma vizuri hakuna mahali popote katika maandishi ya Bw. Said ambapo amedai kuwa wazee wake walipokuwa wanapigania uhuru walikuwa wanapigania Uislamu au ili wao Waislamu wapate nafasi ya pekee. Na huwezi kukuta mahali popote pa maandishi ya Mzee Said akionesha kuwa harakati za Uhuru zilikuwa ni harakati dhidi ya Ukristu na kwa ajili ya Uislamu na hivyo wazee 'wake' walifanya hivyo kwa ajili ya Uislamu. Dini haikuwa issue imekuwa issue kwenye maandishi ya ndugu yetu huyu.
 
Tanu haikuwapo kabla na ni Julius Nyerere, Raisi wake wa Kwanza, aliyeongoza kuanzishwa kwake mwaka 1954 na kumiliki kadi namba moja, wengine wote wale walikuwa wasaidizi wake tu...that's the naked truth and you can take that to the bank!

Atakuambia kadi ile namba moja alipewa tu kama hisani ya wazee wa Dar; lakini kwa haki ilikuwa ni kadi ya Abdulwahid Sykes akaamua kumpisha Nyerere tu.
 
Nikuulize swali, ni kweli kuwa Abdul Sykes alimuingiza Nyerere kwa mara ya kwanza katika siasa mwaka 1953.

Swali hilo tu!
Neno pana hilo! unamaanisha siasa za wapi? za kimataifa? za kitaifa? au unakusudia wapi?

Mathalan unawezi kuwa mwanasiasa chuoni kwenu lakini kitaifa mimi ndiye niliyekuingiza kwenye duru la siasa za kitaifa, je siwezi kusema kuwa mimi ndiye niliyekuingiza katika siasa?

Je, unakubali kuwa nyerere si mwanzilishi wa TAA?
 

jamani sasa maswali mengine basi yaoneshe hata dalili ya upeo wa kufikiri; TAA ilianzishwa mwaka gani?
 
unaijua medula oblangata? au unaandika tu. nirudi kwenye mada. nimesoma hii makala yako uchwara yote. si kwamba nakutukana ila najaribu kukuweka wazi kuwa ni uchwara na fabricated. tunajua mnafanya kila liwezekanalo kusawazisha mambo ili ionekane kuwa na wakristo walishiriki. yes wapo walishiriki, lakini niwachache tena wakiwa karibu sana na waislam, eg john rupia. lakini. yapo mengi ila na kazi za kufanya, ila kwa kifupi tu, angalia mikoa iliyopigania uhuru,je ni ya waislam (muslim dominated) au wakristo? Tanga, tabora, Dar and so on. what do you learn from this? hivi unajua mikoa kama kilimanjaro, mbeya na bukoba waliandamana kupinga uhuru kwa kisingizio kuwa hatujawa tayari kujitawala? hivi unajua nyerere walivyomtoa pale pugu alikwa mwl? nani alikuwa akimlipa baada ya kuacha ualimu? kwa taarifa yako alichokifanya slaa ndo alichokifanya nyerere, kuwa siachi kazi/ubunge mpaka nifidiwe kipato sawa na cha kazi/ubunge w/yangu. I have many, but sorry. mtajidanganya sana tu mkuu. ila ukweli hujitenga.
na mwisho kabisa, hivi ni nina kati ya waislam na wakristo wanaomezeshwa na kumeza kirahisi? hivi hujasikiaga bakora misikitini kwa kiongozi kutaka kuwamezesha uongo waumini?
 

ukweli na haki ikidhihiri,shari na upotofu hukimbilia gizani,nani tena wa kunitoa kwenye haki na kunirejesha gizani baada ya ukweli kuniingia??
Daima nitauthamini na kuutunza ukweli huu,wala sio kiushabiki,la hasha.
 
Hizi data zitasaidia kuiua CDM.
Waislam wengi wanaiogopa CDM
Kama kweli uko mfumokristo itaacha waislam kutoichagua CDM wakimhofia Slaa.
 
Hizi data zitasaidia kuiua CDM.
Waislam wengi wanaiogopa CDM
Kama kweli uko mfumokristo itaacha waislam kutoichagua CDM wakimhofia Slaa.

Darwin,

Soma haya machache kutoka paper yangu ''Christian Hegemony and the Rise of Muslim Militancy in Tanzania'' (Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin. Paper hii niliiwasilisha Ujerumani 2011:


''It took a decade to bring the Muslim movement back on track and the irony for that was, it was not CCM the old enemy which was responsible for that but an opposition party, Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) seemingly under the tutelage of Catholic Church out to oust a Muslim president, Mrisho Jakaya Kikwete, which broke the camel’s back. The Catholic Church prior to election issued an Election Manifesto and a document of guidance on how Christians should vote. The presidential candidate for CHADEMA was a former Roman Catholic priest. That said it all. Muslims mobilised for the general election in a manner never seen before to oppose CHADEMA and the Church. Muslims irrespective of their political affiliations campaigned for the return to office of a Muslim president Jakaya Mrisho Kikwete.''

Siasa zetu ndipo zilipotufikisha hapa. Wakati umefika wa kujiuliza vipi tumefikia hali hii ilhali wakati wa kupigani uhuru wa nchi hii tulikuwa wamoja?
 

Ngwendu,

Kwa uchache angalia yalliyotokea Moshi wakati wa kuunda TANU 1954:

Historia ya harakati za kudai uhuru wa Tanganyika kama walivyoshiriki wananchi wa Kilimanjaro, haiwezi kamwe kukamilika bila ya kutaja jina la Yusuf Ngozi.

Uchagga ilikuwa chini ya utawala wa machifu waliokuwa wakijulikana kama Mangi.

Baadhi ya machifu hawa walikuwa katika Baraza la Kutunga Sheria na kwa ujumla wao walikuwa karibu na serikali ya kikoloni kuliko walivyokuwa na wananchi wanaowaongoza. Hali ya siasa Jimbo la Kaskazini ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

Wakati TANU inakabiliwa na Kura Tatu mgogoro wa ardhi ya Wameru ulikuwa umekwisha kwa wananchi kudhulumiwa haki yao.

Japhet Kirilo alikuwa amerudi kutoka Umoja wa Mataifa alikopeleka madai ya Wameru mikono mitupu.

Kirilo hakuwa na chochote cha kuwaonyesha Watanganyika. Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye aliyeweza kuifanya TANU iingie kwanza Moshi mjini kwa vishindo na kutoka hapo mjini akaieneza vijijini.

Kupitia kumbukumbu za Mzee Yusuf ngozi ndipo unapokutana na historia za awali kabisa za wanasiasa maarufu waliopata majina na vyeo; na wengine kuwa mawaziri katika Tanganyika huru, kama Lucy Lameck, Enesmo Eliufoo na wengineo.

Ilikuwa Yusuf Ngozi ndiye pamoja na wazalendo wengine waliifanya TANU ishinde uchaguzi wa Kura Tatu mwaka 1958.

Kupitia kumbukumbu zake halikadhalika ndipo kwa huzuni kubwa utakapokutana na mashujaa waliosahaulika kama yeye mwenyewe, mashujaa wa kike na wa kiume, wazalendo kama marehemu Mama Bint Maalim, Amina Kinabo, Halima Selengia, Juma Ngoma, Melkezedek Simon, Gabrieli Malaika na wengineo. Hawa ndiyo mashujaa ambao kwa muda waliamua wasahau nguvu na utawala wa machifu wao na kujiweka chini ya TANU.

Kutoka ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...''

 

Jambo hilo Mohamed Said hapendi kabisa, achilia mbali kumfedhehesha anakofanya, lakini anafikiria hata kumtoa kabisa Mwalimu Nyerere kwenye kundi la wapigania Uhuru.
 

MM,

Unasema hayo kwa kuwa hujui historia ya TANU. Suala la Ukristo ndani ya TAA na baadae ndani ya TANU lilikuwa likiwahangaisha viongozi wa wakati ule hata ikapelekea mwaka 1955 Sheikh Hassan bin Amir kuitisha mkutano wa siri Mtaa wa Pemba kujadili tatizo hili.

Haya hapo chini ndiyo niliyoandika katika ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes..."

The transition from TAA to TANU at the headquarters was smooth.

There were no problems of personality clashes at the headquarters apart from a small faction of radical Muslims who were plotting to oust Nyerere from Party leadership for being a Christian.

This was the second time the issue of religion had cropped up since Nyerere assumed leadership of the movement for the first time in 1953.

A meeting was called to clarify the status of Christianity in TANU and to establish a nationalist-secularist ideology as a way of preserving national unity. This meeting was held in a house in Pemba Street and its resolution was supported by Sheikh Hassan Bin Amir, Sheikh Nurdin Hussein from Lindi and Sheikh Abdallah Chaurembo of Dar es Salaam.

This meeting coined the name ‘Yuda’ which was to be the label of any member of TANU who discriminated his fellow African because of his faith. [1]

The name Yuda coined by TANU had direct relationship with Judas Iscariot of the Bible, the traitor who betrayed Jesus for thirty pieces of silver.

The problems which TANU encountered were mainly from colonial government or those inspired by it using fellow Africans as puppets to try to derail the movement.




[1] See article by Rajab Diwani, 'TANU Ilipambana na Misukosuko Mingi' UHURU 3rd July, 1974.



Tatizo kubwa linalokupateni ni kuwa hamuhifahamu historia hii wala hamkupata kuwasikia watu kama Sheikh Hassan bin Amir.

Nyie mmefunguka macho na Nyerere, Nyerere, Nyerere.

Kuja kusikia kuwa historia si hiyo imekuumizeni sana. Na khasa kusikia kuwa Waislam ndiyo walioongoza vita dhidi ya Waingereza.
 
Hizi data zitasaidia kuiua CDM.
Waislam wengi wanaiogopa CDM
Kama kweli uko mfumokristo itaacha waislam kutoichagua CDM wakimhofia Slaa.

Kwanini unapenda kuishi kwa hisia bila kuutafuta ukweli halisi na kuishi nao?

Hao watu watakao ikimbia Chadema kwamadai ya mfumo kristu, watakuwa na matatizo ya akili tu, ikiwa haohao watu wanamtusi na kumdhalilisha Mwalimu Nyerere ambae ni mwasisi wa CCM iliyopo madarakani sasa yenye mfumo kristu kama wanavyo dai, itakuweje tena waikimbie Chadema na kurudi ccm kwa madai hayo hayo ya Mwalimu kuweka mfumo kristu CCM na Tz?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…