Mohamed Said
Ilikuwaje Abdul akamwomba Kidaha Makwaia (another up country guy) ili washindanie urais kwenye uchaguzi? Au alitaka apate weak opponent ambaye angemshinda kirahisi? Je inawezekana ndio sababu akamwomba na Nyerere badala yake na wakaishia kwenye stiff election ambapo yeye akashindwa? Was he (Abdul) a hypocrite with lust for power au alikuwa na nia nzuri ya kukamilisha democratic excercise? Funguka zaidi mzee wetu Moh.
N,
Kinyume cha hivyo.
Abdu hakuwa mtu wa kupenda cheo.
Chief Kidaha aliporudi kutoka Uingereza masomoni
akachaguliwa kuwa mjumbe Baraza la Kutunga
Sheria.
Chief Kidaha alikuwa kati ya machifu wakubwa wa
kutajika kama Abdiel Shangali, Marealle, Fundikira
na wengineo.
Waingereza wakisikizananae sana.
TAA 1950 ilikuwa inataka kujigeuza iwe fully fledged
political party.
Abdu alikuwa anajua kuwa kwa ule uongozi wa New
Street peke yake bila ya kupata mtu kutoka bara na
Mkristo TAA itabakia ya "Waswahili."
Abdu alimtaka Chief Kidaha kwa sababu nyingine kuwa
alikuwa chifu wa Wasukuma na kama angechukua uongozi
wa TANU Kidaha angekuja na watu wake wote.
Ile stiff election na Nyerere Abdu hakuitegemea kabisa na
ndiyo maana Nyerere alipochukua uongozi wa TAA chama
kikafa.
Katika uongozi wakati ule hapakuwa na ushindani wa uadui.
Kwanza ilikuwa kazi ya hatari na kiongozi ndiye alitegemewa
kukiendesha chama kwa fedha zake.
Hili lilikuwa jambo gumu na mzigo mzito sana kuubeba.
Ndiyo maana ukaona TAA ikawa mikononi mwa akina Sykes
kwa robo karne na uongozi wa juu ukawa ni Rupia na Dossa.
Moja ya sababu kuu ni ule uwezo wao na kujitolea kutoa mali
zao katika kupigania nchi.
Halafu ngoja nikupe kitu.
Kidaha hakuwa push over.
He was the best of the best and flamboyant kama
Abdu.
Pangechimbika.