MM na Darwin,
Wale wanajopo wa Chuo Cha Kivukoni walitatizwa sana inaelekea na historia
ya ukoo mzima wa Sykes katika historia ya siasa katika Tanganyika kama vile
Nyerere mwenyewe alipotatizwa na ule mradi wa kuandika historia ya TANU pale
walipojaribu kuiandika mwaka 1962.
Na tatizo linakuja pale unapomtia Abdu.
Ukimtia Abdu katika historia ya uhuru wa Tanganyika inakubidi umtaje na baba
yake kwa sababu baba yake alikuwa muasisi wa African Association kama katibu
mwaka 1929.
Sasa ikiwa nia ni kumkweza Nyerere kama wewe ni mtu jasiri itakubidi na uandike
habari za Chief Burito Nyerere baba yake Nyerere kuonyesha kuwa wazee wa wakati
ule wote walikuwa hadhir katika kuwakusanya wananchi kuleta umoja.
Hii kwa mtafiti wa historia ya Tanganyika itakuwa kazi ngumu sana.
Mtafiti ambae atapenda kuandika historia ya uhuru kwa kuanza na Nyerere kwa ajili
hii ni lazima amtoe Abdu na asimtaje kabisa.
Kwa mimi kule kumleta Abdu katika maisha ya siasa ya Nyerere hii ikawa imewaleta
wazalendo wengi vijana waliokuwa katika harakati toka siku ile 1950 vijana walipokichukua
chama kutoka uongozi wa wazee akina Thomas Plantan.
Matokeo yake ndiyo leo tuko hapa JF.