THE BIG SHOW
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 16,950
- 13,527
Ami,
Alhamdulilah.
Shukurani zote zinamstahiki Allah.
Alhamdulillah kwa Ilmu unayotupatia katika historia hii,,
Mnamo tarehe 9 september 2000,gazeti la majira lilitoa taarifa kuwa halmashauri kuu ya maaskofu ya baraza la kanisa la pentekoste la tanzania(PCT),Walitoa kitabu chao walichokiita "AMANI KATIKA TANZANIA ITALINDWA KWA KUTENGANISHA DINI NA MAMLAKA YA NCHI",
Walitoa tamko rasmi kuwa kwa tanzania kujiunga na shirika la OIC sharti kuwepo na kura za maoni,tamko hili la maaskofu wa kipentekoste lilitanguliwa na lile la maaskofu wa kanisa la KKKT,lililotolewa kitambo kidogo,lenyewe lilikataa kabisa wazo la tanzania kuijunga na OIC,
lile la maaskofu wa KKKT.LILIFUATIWA NA tamko la KADINALI PENGO wa kanisa katoliki,yeye alipendekeza kuwa wazo hili lazima lipelekwe bungeni,kwenye barua yake aliyomuandikia katibu mkuu wa halmashauri ya waislam tarehe 17.12.1999 mh RAIS MKAPA,KUHUSU suala hilo alisema ya kwamba ni serikali ni lazima iwasikilize wasiokuwa waislam wana maoni gani kuhusu hilo..
Sasa tukirud kwenye MEMORANDUM OF UNDERSTANDING YA 1992 BAINA YA SERIKALI NA MAKANISA ya TEC NA CCT NA MASHIRIKA YA DINI ZA NJE PAMOJA NA SERIKALI ZAO,
Kwanini serikali haikuona umuhimu wa kuwauliza wasiokua wakristo kuhus mambo nyeti kama hayo?na badala yale wakachukua tuh jukum lakufanya maamuz ambayo wanayajua wao tena bila hata bunge kuhusishwa??
Pia kama hizo kura za maoni kuhusu OIC zilikuwa na umuhimu,lini serikali iliitisha kura za maoni kuwahoji wasiokuwa wakristo kuhusu uwepo wa UBALOZI WA VATIKAN AMBAYO NI KAMA TAASISI TUH YA KIDINI NA SI NCHI YENYE MAMLAKA NA RAIA WAKE?
Yaliyofichikana na yanayoleta ukakasi ni mengi sana..