Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

TBS,Fuatilia vizuri kesi ya Sheikh Ponda utaona anachokifanya ni utekelezaji kwa vitendo simulizi za mzee wetu Mohamed. Kiwanja alichovamia ndicho mzee Mohamed anachodai palitakiwa kujengwa chuo kikuu cha Waislam. Baada ya uvamizi ule, msikiti wa muda uliojengwa pale ulipewa jina la Sheikh Amir, mmoja wa wazee wa Mohamed. Sheikh Ponda ni mfuasi mzuri sana wa simulizi za Mohamed Said.Kwanini mzee huyu sio shahidi wa Sheikh Ponda? Pengine angemwokoa kwa kuwa kesi hii imemkalia vibaya Ponda. Hatachomoka.

Wild Card,

Kuna mambo kamwe hutayaelewa hadi uwe Muislam.
Unazungumza kuchomoka...

Unadhani Ponda anajuta kuwa pale alipo?

Ponda ameingia katika orodha ya waja wema wa Allah
ambao kawataja katika Qur'an.

Wale wanaosimama kuipigania dini yake kwa mali na nafsi
zao.

Ponda hakuvamia kiwanja kile.
Kiwanja hicho ni mali ya Wakfu ni mali ya Waislam.

Mtu havamii mali yake.

Ama mie kuwa shahidi wa Ponda hilo naliomba kila nikenda sijda.

Nikilipata hilo nami nitakuwa nimeunganishwa na kipenzi changu
marehemu Sheikh Hassan bin Amir.

Nasikitika Allah bado hajanikubalia dua yangu.
 
Ami,

Jana nilikuwa mahakamani kusikiliza kesi ya Sheikh Ponda.

Kilichonifikisha pale ni kumsikiliza Sheikh Bilal Rehani Waikela ambae alipanda kizimbani
kutoa ushahidi wake upande wa washtakiwa.

Sheikh Waikela amekuja kutoka Tabora.

Hakika mahakama jana walisikia ambayo si wengi wamepata kuyasikia katika maisha yao
yote.

Sheikh Waikela ameanza kwa kutaja umri wake wa miaka 87 na akaieleza mahakama kuwa
ameanza kuutumikia Uislam mwaka 1940 akiwa katika Anjuman Muslim na ilipokuja East
African Muslim Society ( EAMWS) akawa kiongozi.

Akaeleza pia yeye ni muasisi wa Mabaraza ya Misikiti Duniani makao makuu yake Makka.

Akasema yeye Tabora ni mtu wa tatu kujiunga na TANU na katika Tanganyika ni mtu wa 264.

Sheikh Waikela akaeleza kuwa yeye alikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kuipigania uhuru
wa Tanganyika na akimchukua Nyerere ndani ya gari yake Tabora na wakila chakula nyumbani
kwake.

Waikela aliichekesha mahakama aliposema wakati ule alikuwa kijana ana fedha na akicheza tennis.

Akaeleza kuwa Gavana Edward Twinning aliingiza fitna nchini kuhusu Waislam kutaka kuwachonganisha
na Wakristo katika suala la elimu ili avunje juhudi za TANU kudai uhuru.

Nyerere alimsihi Waikela kuwa katika hutuba zake ajitahidi sana kuliweka suala hilo vyema ili pasiingie
mtafaruku na nchi ikawa kama India na Pakistani Waislam na Wahindu wakagawana nchi katika misingi
ya dini.

Waikela akasema hilo walilifanyia kazi na hali ikabaki shwari hadi uhuru ukapatikana.

Matatizo yakaja baada ya uhuru kupatikana.

Waikela akaieleza Mahakama jinsi Sheikh Hassan bin Amir alivyomtahadharisha kuhusu njama zilizokuwa
zinapikwa serikali dhidi ya EAMWS na akamweleza kuwa wanafiki ndiyo wanaotumiwa.

Sheikh Waikela aliwataja Mahakamani wanafiki hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.

Akaeleza mkutano wa EAMWS katika Ukumbi wa Aga Khan Girls mwaka 1963 alipomsomea Nyerere risala
ya Waislam kuhusu fitna iliyokuwa ikienezwa nchini dhidi ya Waislam na Uislam.

(Risala hii kwa sasa ni maarufu inajulikana kama ''Moto wa Waislam Ukiwaka.'')

Anasema hotuba hii ndiyo iliyosabaisha yeye kuwekwa kizuizini mwaka uliofuatia 1964 na alipotoka jela alipewa
hati ya kifungo ambayo Sheikh Waikela aliieleza Mahakama kuwa ameitundika nyumbani kwake ukutani kama
pambo.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mmoja wa washitakiwa ni binti yake aitwae Dentation Waikela ambae alizaliwa
baba yake ikiwa jela.

Sheikh Waikela akaeleza jinsi Nyerere alivyowawezesha kundi la Adam Nasib kwa fedha na ushirikiano wa serikali
kupita majimboni kuwashawishi Waislam kujitoa EAMWS lakini hawakufanikiwa.

Katika majimbo 20 ni majimbo 8 tu ndiyo yaliyokubali kujitoa.

Hata hivyo serikali ilikatumia nguvu na kuitisha mkutano wa wanasiasa Waislam Iringa na Bakwata ikaanzishwa na
serikali ikaweka askari wenye silaha katika ofisi zote za EAMWS na kuzifunga na makufuli na minyororo.

Binafsi Sheikh Waikela akaeleza Mahakama kuwa alihongwa shs: 40, 000 na Geoffrey Sawaya aliyekuwa Mkurugenzi
wa Makosa ya Jinai, hongo ambayo aliikataa.

Hao waliokubali hongo ile ndiyo walioshirikiana na serikali katika kuiweka BAKWATA madarakani.

Kuhusu kiwanja cha Markaz Chang'ombe anasema kile kiwanja ni mali ya EAMWS na madhumuni yake ilikuwa ni kujenga
Chuo Kikuu.

Kwa hakika alisema mengi na mwisho alimuomba hakimu awape Waislam haki yao.

Naomba kuwajua hao waislamu wanafiki ambao mzee huyo wa Tabora aliwataja wote hapo mahakamani.
 
Ami,

Jana nilikuwa mahakamani kusikiliza kesi ya Sheikh Ponda.

Kilichonifikisha pale ni kumsikiliza Sheikh Bilal Rehani Waikela ambae alipanda kizimbani
kutoa ushahidi wake upande wa washtakiwa.

Sheikh Waikela amekuja kutoka Tabora.

Hakika mahakama jana walisikia ambayo si wengi wamepata kuyasikia katika maisha yao
yote.

Sheikh Waikela ameanza kwa kutaja umri wake wa miaka 87 na akaieleza mahakama kuwa
ameanza kuutumikia Uislam mwaka 1940 akiwa katika Anjuman Muslim na ilipokuja East
African Muslim Society ( EAMWS) akawa kiongozi.

Akaeleza pia yeye ni muasisi wa Mabaraza ya Misikiti Duniani makao makuu yake Makka.

Akasema yeye Tabora ni mtu wa tatu kujiunga na TANU na katika Tanganyika ni mtu wa 264.

Sheikh Waikela akaeleza kuwa yeye alikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kuipigania uhuru
wa Tanganyika na akimchukua Nyerere ndani ya gari yake Tabora na wakila chakula nyumbani
kwake.

Waikela aliichekesha mahakama aliposema wakati ule alikuwa kijana ana fedha na akicheza tennis.

Akaeleza kuwa Gavana Edward Twinning aliingiza fitna nchini kuhusu Waislam kutaka kuwachonganisha
na Wakristo katika suala la elimu ili avunje juhudi za TANU kudai uhuru.

Nyerere alimsihi Waikela kuwa katika hutuba zake ajitahidi sana kuliweka suala hilo vyema ili pasiingie
mtafaruku na nchi ikawa kama India na Pakistani Waislam na Wahindu wakagawana nchi katika misingi
ya dini.

Waikela akasema hilo walilifanyia kazi na hali ikabaki shwari hadi uhuru ukapatikana.

Matatizo yakaja baada ya uhuru kupatikana.

Waikela akaieleza Mahakama jinsi Sheikh Hassan bin Amir alivyomtahadharisha kuhusu njama zilizokuwa
zinapikwa serikali dhidi ya EAMWS na akamweleza kuwa wanafiki ndiyo wanaotumiwa.

Sheikh Waikela aliwataja Mahakamani wanafiki hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.

Akaeleza mkutano wa EAMWS katika Ukumbi wa Aga Khan Girls mwaka 1963 alipomsomea Nyerere risala
ya Waislam kuhusu fitna iliyokuwa ikienezwa nchini dhidi ya Waislam na Uislam.

(Risala hii kwa sasa ni maarufu inajulikana kama ''Moto wa Waislam Ukiwaka.'')

Anasema hotuba hii ndiyo iliyosabaisha yeye kuwekwa kizuizini mwaka uliofuatia 1964 na alipotoka jela alipewa
hati ya kifungo ambayo Sheikh Waikela aliieleza Mahakama kuwa ameitundika nyumbani kwake ukutani kama
pambo.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mmoja wa washitakiwa ni binti yake aitwae Dentation Waikela ambae alizaliwa
baba yake ikiwa jela.

Sheikh Waikela akaeleza jinsi Nyerere alivyowawezesha kundi la Adam Nasib kwa fedha na ushirikiano wa serikali
kupita majimboni kuwashawishi Waislam kujitoa EAMWS lakini hawakufanikiwa.

Katika majimbo 20 ni majimbo 8 tu ndiyo yaliyokubali kujitoa.

Hata hivyo serikali ilikatumia nguvu na kuitisha mkutano wa wanasiasa Waislam Iringa na Bakwata ikaanzishwa na
serikali ikaweka askari wenye silaha katika ofisi zote za EAMWS na kuzifunga na makufuli na minyororo.

Binafsi Sheikh Waikela akaeleza Mahakama kuwa alihongwa shs: 40, 000 na Geoffrey Sawaya aliyekuwa Mkurugenzi
wa Makosa ya Jinai, hongo ambayo aliikataa.

Hao waliokubali hongo ile ndiyo walioshirikiana na serikali katika kuiweka BAKWATA madarakani.

Kuhusu kiwanja cha Markaz Chang'ombe anasema kile kiwanja ni mali ya EAMWS na madhumuni yake ilikuwa ni kujenga
Chuo Kikuu.

Kwa hakika alisema mengi na mwisho alimuomba hakimu awape Waislam haki yao.

Mohamed Said,

Mara ya mwisho kumuona huyu Mzee wetu mzalendo ilikuwa mwaka 1990.

Hawa ndugu zetu humu ukumbini watasema hizo ni ngano.

Lakini bahati nzuri watu wamemuona na kumsikia Mzee wetu Bilal Waikela.
 
Wild Card,

Kuna mambo kamwe hutayaelewa hadi uwe Muislam.
Unazungumza kuchomoka...

Unadhani Ponda anajuta kuwa pale alipo?

Ponda ameingia katika orodha wa waja wa Allah
ambao kawataja katika Qur'an.

Wale wanaosimama kuipigania dini yake kwa mali
na nafsi zao.

Ponda hakuvamia kiwanja kile.
Kiwanja hicho ni mali ya Wakfu ni mali ya Waislam.

Mtu havamii mali yake.

Ama mie kuwa shahidi wa Ponda hilo naliomba kila nikenda sijda.

Nikilipata hilo nami nitakuwa nimeunganishwa na kipenzi changu
marehemu Sheikh Hassan bin Amir.

Nasikitika Allah bado hajanikubalia dua yangu.

Nasikia Manji ndie hasa alikua anangoja Ponda aingie ktk kumi na nane zake. Bakwata wamepewa viwanja vingi sana hasa mijini na wajane na watu mbalimbali waliotoa wakfu viwanja they are so good at selling them to businessmen hata kariakoo nasikia kuna viwanja vingi wameuza. sasa ponda kama alikichukua kwa nguvu hakuwa sahihi kukitwaa kwa Manji angewafuata Bakwata na wao ndio wana jurisdiction
 
Ami,Jana nilikuwa mahakamani kusikiliza kesi ya Sheikh Ponda.Kilichonifikisha pale ni kumsikiliza Sheikh Bilal Rehani Waikela ambae alipanda kizimbani kutoa ushahidi wake upande wa washtakiwa.Sheikh Waikela amekuja kutoka Tabora.Hakika mahakama jana walisikia ambayo si wengi wamepata kuyasikia katika maisha yao yote.Sheikh Waikela ameanza kwa kutaja umri wake wa miaka 87 na akaieleza mahakama kuwa ameanza kuutumikia Uislam mwaka 1940 akiwa katika Anjuman Muslim na ilipokuja EastAfrican Muslim Society ( EAMWS) akawa kiongozi.Akaeleza pia yeye ni muasisi wa Mabaraza ya Misikiti Duniani makao makuu yake Makka.Akasema yeye Tabora ni mtu wa tatu kujiunga na TANU na katika Tanganyika ni mtu wa 264.Sheikh Waikela akaeleza kuwa yeye alikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kuipigania uhuru wa Tanganyika na akimchukua Nyerere ndani ya gari yake Tabora na wakila chakula nyumbanikwake.Waikela aliichekesha mahakama aliposema wakati ule alikuwa kijana ana fedha na akicheza tennis.Akaeleza kuwa Gavana Edward Twinning aliingiza fitna nchini kuhusu Waislam kutaka kuwachonganisha na Wakristo katika suala la elimu ili avunje juhudi za TANU kudai uhuru.Nyerere alimsihi Waikela kuwa katika hutuba zake ajitahidi sana kuliweka suala hilo vyema ili pasiingie mtafaruku na nchi ikawa kama India na Pakistani Waislam na Wahindu wakagawana nchi katika misingi ya dini.Waikela akasema hilo walilifanyia kazi na hali ikabaki shwari hadi uhuru ukapatikana.Matatizo yakaja baada ya uhuru kupatikana.Waikela akaieleza Mahakama jinsi Sheikh Hassan bin Amir alivyomtahadharisha kuhusu njama zilizokuwazinapikwa serikali dhidi ya EAMWS na akamweleza kuwa wanafiki ndiyo wanaotumiwa.Sheikh Waikela aliwataja Mahakamani wanafiki hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.Akaeleza mkutano wa EAMWS katika Ukumbi wa Aga Khan Girls mwaka 1963 alipomsomea Nyerere risala ya Waislam kuhusu fitna iliyokuwa ikienezwa nchini dhidi ya Waislam na Uislam.(Risala hii kwa sasa ni maarufu inajulikana kama ''Moto wa Waislam Ukiwaka.'')Anasema hotuba hii ndiyo iliyosabaisha yeye kuwekwa kizuizini mwaka uliofuatia 1964 na alipotoka jela alipewa hati ya kifungo ambayo Sheikh Waikela aliieleza Mahakama kuwa ameitundika nyumbani kwake ukutani kama pambo.Mahakama ilifahamishwa kuwa mmoja wa washitakiwa ni binti yake aitwae Dentation Waikela ambae alizaliwa baba yake ikiwa jela.Sheikh Waikela akaeleza jinsi Nyerere alivyowawezesha kundi la Adam Nasib kwa fedha na ushirikiano wa serikali kupita majimboni kuwashawishi Waislam kujitoa EAMWS lakini hawakufanikiwa.Katika majimbo 20 ni majimbo 8 tu ndiyo yaliyokubali kujitoa.Hata hivyo serikali ilikatumia nguvu na kuitisha mkutano wa wanasiasa Waislam Iringa na Bakwata ikaanzishwa na serikali ikaweka askari wenye silaha katika ofisi zote za EAMWS na kuzifunga na makufuli na minyororo.Binafsi Sheikh Waikela akaeleza Mahakama kuwa alihongwa shs: 40, 000 na Geoffrey Sawaya aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, hongo ambayo aliikataa.Hao waliokubali hongo ile ndiyo walioshirikiana na serikali katika kuiweka BAKWATA madarakani.Kuhusu kiwanja cha Markaz Chang'ombe anasema kile kiwanja ni mali ya EAMWS na madhumuni yake ilikuwa ni kujenga Chuo Kikuu.Kwa hakika alisema mengi na mwisho alimuomba hakimu awape Waislam haki yao.
Umeona kesi inakoelekea? Kulekule kwenye simulizi zako. Ushahidi kama huu utamsaidiaje Ponda? Hachomoki!
 
Unadhani Ponda anajuta kuwa pale alipo?Akili na mawazo ya wafia dini haya. Mzee Mohamed, una tofauti gani na Osama bin Laden?
 
Wild Card,Kuna mambo kamwe hutayaelewa hadi uwe Muislam.Unazungumza kuchomoka...Unadhani Ponda anajuta kuwa pale alipo?Ponda ameingia katika orodha wa waja wa Allah ambao kawataja katika Qur'an.Wale wanaosimama kuipigania dini yake kwa malina nafsi zao.Ponda hakuvamia kiwanja kile.Kiwanja hicho ni mali ya Wakfu ni mali ya Waislam.Mtu havamii mali yake.Ama mie kuwa shahidi wa Ponda hilo naliomba kila nikenda sijda.Nikilipata hilo nami nitakuwa nimeunganishwa na kipenzi changumarehemu Sheikh Hassan bin Amir.Nasikitika Allah bado hajanikubalia dua yangu.
Mwambie Sheikh Ponda akuorodheshe kama shahidi wake. Sijda haitakufanya uwe shahidi! Sijui kwa nini serikali nayo imekuacha katika hili wakati Ponda ni mtekelezaji tu wa maandiko yako!
 
Umeona kesi inakoelekea? Kulekule kwenye simulizi zako. Ushahidi kama huu utamsaidiaje Ponda? Hachomoki!

WildCard,

Uislam umetakaza kufanya dhulma wa kuruhusu dhulma anachofanya Ponda nikupambana na dhulma.

Huko kuchoma au kutokuchoma siyo issue Sheikh Bilal Waikela aliwekwa ndani na Nyerere leo yupo wapi na Nyerere yupo wapi.

Allah ana njia nyingi za kuwasaidia waja wake.
 
WildCard,Uislam umetakaza kufanya dhulma wa kuruhusu dhulma anachofanya Ponda nikupambana na dhulma.Huko kuchoma au kutokuchoma siyo issue Sheikh Bilal Waikela aliwekwa ndani na Nyerere leo yupo wapi na Nyerere yupo wapi.Allah ana njia nyingi za kuwasaidia waja wake.
Dhulma kwenye kiwanja hiki kafanya nani na kafanyiwa nani? Aliyekiuza BAKWATA, taasisi ya Kiislam. Aliyekinunua Muislam safi kabisa ambaye kila kilipo kiwanda chake na msikiti upo!
 
Mwambie Sheikh Ponda akuorodheshe kama shahidi wake. Sijda haitakufanya uwe shahidi! Sijui kwa nini serikali nayo imekuacha katika hili wakati Ponda ni mtekelezaji tu wa maandiko yako!

Unataka kusema Ponda naye ni victim wa mandiko hayo duh!!
 
Unataka kusema Ponda naye ni victim wa mandiko hayo duh!!
Sheikh Ponda haoni wala hasikii kwa maandiko ya mzee Mohamed. Nadhani katika vitabu alivyonavyo huko rumande, hiki cha mzee Mohamed ni cha pili kwa umuhimu baada ya Quran Tukufu
 
Nguruvi,

Abdulwahid Sykes kapewa medali na nchi hii miaka 50 baada ya uhuru mwaka 2011.
Sasa unataka mimi nikuulize wewe ni nani alimnyima medali miaka hiyo yote na kwa nini?

Au kwa nini wameamua kumpa medali?

Mimi nikuulize wewe kwa nini hawakumataja katika kitabu cha Kivukoni.

Maswali hilo nikuulize wewe kwani wewe ndiyo Mwenyekiti wa CCM au una
mamlaka ya kutoa medali?

Niulize swali linalonihusu.
Aliyekasirishwa na makala zangu ie nitamjuaje?

Nimesoma tu vitisho kutoka Idara ya CCM ya Uhamasishaji Umma na barua kaandika
Dk. Kiwanuka.

Akaniita ''mbilikimo.''

Sasa wewe hapo unashindwaje kuona nani alikuwa anapaliwa na povu?
Nguruvi achana na mimi ipo kalamu hapa usifanye mchezo rafiki yangu.

Mie nimeanza alif na aeiou sijenda chuoni wala shule tena ananifundisha
mama yangu binti Sheikh jikoni.

Yeye mwenyewe Kiingereza hajui ananunua vitabu vya Kizungu ananipa
kusoma mie naishia kuangalia picha.

Mzee Saidi kuna wakati nikisoma maandishi yako najikuta nacheka peke yangu, ngoja nikukumbushe kidogo hapo nyuma nilikuuliza swali, ukazuga kama hujasikia kama kawaida yako. Baadae Son of Alaska akasisitiza.

Nyambala tafadhali tufungue macho naona Mohamed Said hili swali anajifanya hakuliona

"
The last one kwa faida ya Mkanasha, wanajamvi na vijana wako "Unaweza kututajia wazee waliokuwa na Nyerere kwenye negotiating team na waingereza kuhusu upatikanaji uhuru wa Tanganyika??" Please. Maana hiyo ndiyo hasa ilikuwa nguzo ya kupatikana uhuru Dec 09, 1961. If not basi usipepese sema sijui utapewa darasa. Inshalah tutaonana panapo majaliwa

Ukadai nimeuliza kwa kukupima uwezo au? Swali bado hujajibu!!!!!
Nikakujibu
By Nyambala
Hapana Mzee Saidi sijauliza kwa kupima uwezo wako bali ni kwa nia nzuri tu ya kutaka kuweka mambo sawa. Na ni muhimu vijana wetu wafahamu historia nzima mpaka uhuru wenyewe ulipopatikana.

Ukajibu majibu yangu lakini si swali la msingi

Nyambala,
Siwezi kusema sana.

Lakini ungelitanguliza heshima na ustaarabu ukaja na picha
tuko kwenye barza tunazungumza ungekuja na lugha nzuri.

Huwa nasisitiza kuwa haya ni majadiliano hapana uhasama.
Najua kwenu nyie hakika maneno ninayoandika yanataabisha.

Hampendi kusikia kuwa kulikuwa na watu walifanya makubwa
na wala Nyerere walikuwa hawajasikia jina lake.

Lakini huu ndiyo ukweli.

Nikakukumbusha
Kama kawaida Mzee Saidi, swali bado limesimama lakini unakuja na hii habari ya "nyie", sisi na nani? Mimi niko mwenyewe lakini ghafla unanitengenezea ushirika!!!!!!!!! Kama jibu hakuna si isemwe basi?? Na kwa taarifa tu mimi sitaabishwi na maneno hata siku moja ila huwa naatabishwa pale tu "urongo" unapofinyangwa na kuitwa ukweli.

Ukajibu majibu lakini swali la msingi holaaaaaa!!!!!!!!!!

Nyambala,

Niwie radhi kwa kukujumuisha kwa neno nyie.

Ikiwa ushaitikadi pana uongo katika maelezo yangu hiyo ni sababu
tosha ya mtu yoyote kunipuuza kwa sababu muongo hana muamana.

Katika Uislam ikishathibiti kuwa mtu ni muongo huo ndiyo mwisho wake
neno lake haliaminiki tena.

Mimi ni Muislam na kwa kuwa umeniita muongo hapa ndiyo mwisho wetu.

Sasa naomba nikujibie maana najua jibu unalijua ila linakuumiza. Unajisikiaje unapokuta kwenye negotiations hakukuwa na wazee wala akina Skyes It was again the same man, himself alone and solo. How does that feel???? Nyerere again and was there by himself. Waambie tu vijana Mzee Saidi ndiyo maana ya historia. But what a coincidence? Nyerere huyu huyu anakuwa mwenyekiti wa kwanza wa TANU ambayo unadai iliasisiwa na kina Sykes, Nyerere tena huyu huyu anakwenda kutuwakilisha watanganyika milioni tisa UNO na kama unavyodai kwa nauli zilizotolewa na kina Sykes. Sasa inakuwaje tena mtu huyo huyo ndiyo negotiator by himself akiwakilisha watanganyika wote dhidi ya wakoloni?, Do you wanna know how old was he by then? Why, why, why? Kuna mlinganisho wowote wa mtu huyu na mtanganyika yeyote achilia mbali akina Sykes.

Mzee Saidi una haki kabisa ya kuwa obsessed na Abdu kwa sababu zako binafsi lakini huna haki hata kidogo kutaka kulazimisha ukuu wa Abdu dhidi ya Nyerere, au kudunisha ushujaa wa Nyerere ili kuelevate umahiri wa Abdu. Watu hawa wawili hawalinganishiki, na hawafanani ni sawa na Bahari na maji ya kikombe. Hata zije historia milioni na baada ya miaka alf, Nyerere bado around this time hakuna aliyekuwa mfano wake. Endelea kuchapa ngano mkuu lakini eneo hili umekwama.
 
Mzee wangu Mohamed Said utetezi wa Sheikh Bilal Rehani Waikela hauna mashiko wala hauwezi kuwasaidia watuhumiwa.Ikiwa watuhumiwa walikuwa wakisubiri utetezi wa aina hii hakika bado wana safari ndefu,hata hiyo mipango ya ujenzi wa Chuo kikuu itabidi mtafute vichwaa vingine akina Sheikh Ponda na kundi lake watazidi kuwaangamiza katika lindi la ujinga na mtabaki na ngonjera za mfumo kristo milele.




Ami,

Jana nilikuwa mahakamani kusikiliza kesi ya Sheikh Ponda.

Kilichonifikisha pale ni kumsikiliza Sheikh Bilal Rehani Waikela ambae alipanda kizimbani
kutoa ushahidi wake upande wa washtakiwa.

Sheikh Waikela amekuja kutoka Tabora.

Hakika mahakama jana walisikia ambayo si wengi wamepata kuyasikia katika maisha yao
yote.

Sheikh Waikela ameanza kwa kutaja umri wake wa miaka 87 na akaieleza mahakama kuwa
ameanza kuutumikia Uislam mwaka 1940 akiwa katika Anjuman Muslim na ilipokuja East
African Muslim Society ( EAMWS) akawa kiongozi.

Akaeleza pia yeye ni muasisi wa Mabaraza ya Misikiti Duniani makao makuu yake Makka.

Akasema yeye Tabora ni mtu wa tatu kujiunga na TANU na katika Tanganyika ni mtu wa 264.

Sheikh Waikela akaeleza kuwa yeye alikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kuipigania uhuru
wa Tanganyika na akimchukua Nyerere ndani ya gari yake Tabora na wakila chakula nyumbani
kwake.

Waikela aliichekesha mahakama aliposema wakati ule alikuwa kijana ana fedha na akicheza tennis.

Akaeleza kuwa Gavana Edward Twinning aliingiza fitna nchini kuhusu Waislam kutaka kuwachonganisha
na Wakristo katika suala la elimu ili avunje juhudi za TANU kudai uhuru.

Nyerere alimsihi Waikela kuwa katika hutuba zake ajitahidi sana kuliweka suala hilo vyema ili pasiingie
mtafaruku na nchi ikawa kama India na Pakistani Waislam na Wahindu wakagawana nchi katika misingi
ya dini.

Waikela akasema hilo walilifanyia kazi na hali ikabaki shwari hadi uhuru ukapatikana.

Matatizo yakaja baada ya uhuru kupatikana.

Waikela akaieleza Mahakama jinsi Sheikh Hassan bin Amir alivyomtahadharisha kuhusu njama zilizokuwa
zinapikwa serikali dhidi ya EAMWS na akamweleza kuwa wanafiki ndiyo wanaotumiwa.

Sheikh Waikela aliwataja Mahakamani wanafiki hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.

Akaeleza mkutano wa EAMWS katika Ukumbi wa Aga Khan Girls mwaka 1963 alipomsomea Nyerere risala
ya Waislam kuhusu fitna iliyokuwa ikienezwa nchini dhidi ya Waislam na Uislam.

(Risala hii kwa sasa ni maarufu inajulikana kama ''Moto wa Waislam Ukiwaka.'')

Anasema hotuba hii ndiyo iliyosabaisha yeye kuwekwa kizuizini mwaka uliofuatia 1964 na alipotoka jela alipewa
hati ya kifungo ambayo Sheikh Waikela aliieleza Mahakama kuwa ameitundika nyumbani kwake ukutani kama
pambo.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mmoja wa washitakiwa ni binti yake aitwae Dentation Waikela ambae alizaliwa
baba yake ikiwa jela.

Sheikh Waikela akaeleza jinsi Nyerere alivyowawezesha kundi la Adam Nasib kwa fedha na ushirikiano wa serikali
kupita majimboni kuwashawishi Waislam kujitoa EAMWS lakini hawakufanikiwa.

Katika majimbo 20 ni majimbo 8 tu ndiyo yaliyokubali kujitoa.

Hata hivyo serikali ilikatumia nguvu na kuitisha mkutano wa wanasiasa Waislam Iringa na Bakwata ikaanzishwa na
serikali ikaweka askari wenye silaha katika ofisi zote za EAMWS na kuzifunga na makufuli na minyororo.

Binafsi Sheikh Waikela akaeleza Mahakama kuwa alihongwa shs: 40, 000 na Geoffrey Sawaya aliyekuwa Mkurugenzi
wa Makosa ya Jinai, hongo ambayo aliikataa.

Hao waliokubali hongo ile ndiyo walioshirikiana na serikali katika kuiweka BAKWATA madarakani.

Kuhusu kiwanja cha Markaz Chang'ombe anasema kile kiwanja ni mali ya EAMWS na madhumuni yake ilikuwa ni kujenga
Chuo Kikuu.

Kwa hakika alisema mengi na mwisho alimuomba hakimu awape Waislam haki yao.
 
Last edited by a moderator:
Ahahahahahah..Naamini mpaka mtanange huu ukifika mwisho watu watakuwa wamejifunza mengi sana.Wakuu mwanakijiji,nguruvi3,mag3 na yericko nyerere na wote wenye mlengo wa aina yenu nawaombeni sana muweze kuandika kitabu chenye title ya hii thread.Na Mzee Mohamedi Saidi nakupongeza sana kwa kuendelea kuwepo hapa jukwaani,nimependa umekuwa muwazi.Safi sana.
 
Ahahahahahah..Naamini mpaka mtanange huu ukifika mwisho watu watakuwa wamejifunza mengi sana.Wakuu mwanakijiji,nguruvi3,mag3 na yericko nyerere na wote wenye mlengo wa aina yenu nawaombeni sana muweze kuandika kitabu chenye title ya hii thread.Na Mzee Mohamedi Saidi nakupongeza sana kwa kuendelea kuwepo hapa jukwaani,nimependa umekuwa muwazi.Safi sana.

Twende Kazi,

Ahsante kwa maneno yako mazuri.
Sifa ya Uislam ni ukweli.

Haki daima itakuwa juu.
Haki si kitu cha kuwa chini ya kitu kingine.

Ndiyo maana unaona nimeweza kuwa hapa
na kueleza yale yote niliyokuwa nayajua kuhusu
wazee wangu bila hofu.
 
Huo ni uongo wa wazi kabisa (RED)! Nyerere alistaafu uenyekiti wa CCM mwaka 1990! chama kilikuwa kimeshika hatamu hivyo Mwenyekiti wa CCM ndie aliekuwa na kauli ya mwisho ktk maamuzi yote nchini! na hata Mwinyi alikiri hilo wakati anaapishwa kuwa Rais mwaka 1985 kuwa ana deko sababu Nyerere bado ni Mwenyekiti wa CCM na zawadi toka Mbinguni!

Sahihisha uongo wako na wacha kukanusha historia kwani wewe unaonekana bado mtoto sana!

Waache waendelee kutapa tapa wafa maji..
Ati wanajigamba wamemweka moh said kwenye kona..!
Sasa hiyo kona iko wapi?
Yan wanachosubiri ni kutafuta point of weakness na wao kuanza kuishambulia kama wanacheza chandimu.,
ni kazi kubwa sana kuupinga ukweli,
bure wataumiza mikono ukuta wakijipigia,
maji ya shingo yamewafika..
 
Mzee wangu Mohamed Said utetezi wa Sheikh Bilal Rehani Waikela hauna mashiko wala hauwezi kuwasaidia watuhumiwa.Ikiwa watuhumiwa walikuwa wakisubiri utetezi wa aina hii hakika bado wana safari ndefu,hata hiyo mipango ya ujenzi wa Chuo kikuu itabidi mtafute vichwaa vingine akina Sheikh Ponda na kundi lake watazidi kuwaangamiza katika lindi la ujinga na mtabaki na ngonjera za mfumo kristo milele.

Ngongo,

Mimi siwezi kukuuliza hukumu yako imesimama kwenye sheria ipi.

Lakini ambalo wewe hulijui na limekupita ni kuwa Waikela kaeleza
ukweli wa mambo yalivyokuwa.

Nini Waislam wamefanya katika kupigania uhuru wa Tanganyika na
aliyesimama kueleza hayo mahakamani ni Sheikh Bilali Rehani Waikela
mmoja wa waasisi wa TANU.

Unaweza kufanya kebehi na kejeli.
You can as a Christian afford to do that.

Sijashangazwa na wewe.
 
Twende Kazi,

Ahsante kwa maneno yako mazuri.
Sifa ya Uislam ni ukweli.

Haki daima itakuwa juu.
Haki si kitu cha kuwa chini ya kitu kingine.

Ndiyo maana unaona nimeweza kuwa hapa
na kueleza yale yote niliyokuwa nayajua kuhusu
wazee wangu bila hofu.

wameishiwa nguvu kabisa..
Yani kama ni kwenye ulingoni basi benchi lao la ufundi limerusha taulo kati kati ya ulingo ili kumnusuru mpiganaji wao..
 
Mzee Saidi kuna wakati nikisoma maandishi yako najikuta nacheka peke yangu, ngoja nikukumbushe kidogo hapo nyuma nilikuuliza swali, ukazuga kama hujasikia kama kawaida yako. Baadae Son of Alaska akasisitiza.



Ukadai nimeuliza kwa kukupima uwezo au? Swali bado hujajibu!!!!!
Nikakujibu


Ukajibu majibu yangu lakini si swali la msingi



Nikakukumbusha


Ukajibu majibu lakini swali la msingi holaaaaaa!!!!!!!!!!



Sasa naomba nikujibie maana najua jibu unalijua ila linakuumiza. Unajisikiaje unapokuta kwenye negotiations hakukuwa na wazee wala akina Skyes It was again the same man, himself alone and solo. How does that feel???? Nyerere again and was there by himself. Waambie tu vijana Mzee Saidi ndiyo maana ya historia. But what a coincidence? Nyerere huyu huyu anakuwa mwenyekiti wa kwanza wa TANU ambayo unadai iliasisiwa na kina Sykes, Nyerere tena huyu huyu anakwenda kutuwakilisha watanganyika milioni tisa UNO na kama unavyodai kwa nauli zilizotolewa na kina Sykes. Sasa inakuwaje tena mtu huyo huyo ndiyo negotiator by himself akiwakilisha watanganyika wote dhidi ya wakoloni?, Do you wanna know how old was he by then? Why, why, why? Kuna mlinganisho wowote wa mtu huyu na mtanganyika yeyote achilia mbali akina Sykes.

Mzee Saidi una haki kabisa ya kuwa obsessed na Abdu kwa sababu zako binafsi lakini huna haki hata kidogo kutaka kulazimisha ukuu wa Abdu dhidi ya Nyerere, au kudunisha ushujaa wa Nyerere ili kuelevate umahiri wa Abdu. Watu hawa wawili hawalinganishiki, na hawafanani ni sawa na Bahari na maji ya kikombe. Hata zije historia milioni na baada ya miaka alf, Nyerere bado around this time hakuna aliyekuwa mfano wake. Endelea kuchapa ngano mkuu lakini eneo hili umekwama.

Hili hata moyo wa Mo'h unamsuta, anajiona kavuliwa nguo hadharani
 
Mzee Saidi kuna wakati nikisoma maandishi yako najikuta nacheka peke yangu, ngoja nikukumbushe kidogo hapo nyuma nilikuuliza swali, ukazuga kama hujasikia kama kawaida yako. Baadae Son of Alaska akasisitiza.



Ukadai nimeuliza kwa kukupima uwezo au? Swali bado hujajibu!!!!!
Nikakujibu


Ukajibu majibu yangu lakini si swali la msingi



Nikakukumbusha


Ukajibu majibu lakini swali la msingi holaaaaaa!!!!!!!!!!



Sasa naomba nikujibie maana najua jibu unalijua ila linakuumiza. Unajisikiaje unapokuta kwenye negotiations hakukuwa na wazee wala akina Skyes It was again the same man, himself alone and solo. How does that feel???? Nyerere again and was there by himself. Waambie tu vijana Mzee Saidi ndiyo maana ya historia. But what a coincidence? Nyerere huyu huyu anakuwa mwenyekiti wa kwanza wa TANU ambayo unadai iliasisiwa na kina Sykes, Nyerere tena huyu huyu anakwenda kutuwakilisha watanganyika milioni tisa UNO na kama unavyodai kwa nauli zilizotolewa na kina Sykes. Sasa inakuwaje tena mtu huyo huyo ndiyo negotiator by himself akiwakilisha watanganyika wote dhidi ya wakoloni?, Do you wanna know how old was he by then? Why, why, why? Kuna mlinganisho wowote wa mtu huyu na mtanganyika yeyote achilia mbali akina Sykes.

Mzee Saidi una haki kabisa ya kuwa obsessed na Abdu kwa sababu zako binafsi lakini huna haki hata kidogo kutaka kulazimisha ukuu wa Abdu dhidi ya Nyerere, au kudunisha ushujaa wa Nyerere ili kuelevate umahiri wa Abdu. Watu hawa wawili hawalinganishiki, na hawafanani ni sawa na Bahari na maji ya kikombe. Hata zije historia milioni na baada ya miaka alf, Nyerere bado around this time hakuna aliyekuwa mfano wake. Endelea kuchapa ngano mkuu lakini eneo hili umekwama.

Nyambala,

Mimi sioni sababu ya kuniuliza maswali ndiyo mimi nikataka kujua iweje uniulize swali
kama hilo lina tija gani?

Kwani mimi si kawaida yangu kuwa najibu kila kitu niulizwacho tungefahamiana kitambo
hili ungelijua.

Kwa hakika mimi nimekuwa na obsession na Abdu Sykes toka udogo wangu.

Baba yangu akimpenda sana Bwana Abdu na mara nyingi akihadithia habari za kupigania
uhuru akimtaja Abdu Sykes.

Ikitokea kuwa katika marafiki wa baba yangu hapa Dar es Salaam nikatokea kumuusudu
sana Bwana Abdu.

Tuje kwa Nyerere.

Hapana popote pale mimi nilipojaribu kumdunisha Nyerere na kumweka Abdu juu yake.
Siwezi kuwa na ujinga huo.

Na hilo isingewezekana kwa kwa uongozi wao ulipishana.
Nayajua alofanya Nyerere katika ulimwengu kama sote tunavyojua.

Hili halijapata kuwa na shaka kwangu hata kidogo.

Isipokuwa katika historia ya kuunda TANU siku zote na hata ninapohadhiri ndani na nje
ya nchi nikisema na shingo naitoa kuwa Nyerere hangeweza kumwangalia Abdu Sykes
machoni na akasema, ''Mimi Nyerere ndiye niliyounda TANU.''

Nyerere asingeweza.
TANU haikuanza mwaka 1954.

Historia ya TANU inaanza na baba yake Abdu Sykes mwaka 1929 katika kuunda African
Association.

Hapa ndipo ilipo tofauti yangu na yako na wengi sana pamoja na Nyerere mwenyewe.

Na sikusema haya kwa kificho.
Nimesema haya Nyerere yu hai na magazeti yakachapa na watu wakasoma.

Nishaweka hapa rejea za magazeti hayo sina haja ya kurudia tena.

Sasa tuje safari ya UNO ya 1955.

Ikiwa umekisoma kitabu changu utaona kuwa safari ile iliratibiwa na Baraza la Wazee
wa TANU chini ya uenyekiti wa Sheikh Suleiman Takadir na mweka hazina wa Al Jamiatul
Islamiyya na TANU Idd Faiz Mafongo ndiye aliyekuwa akikusanya fedha na katika fedha
zilizotiwa katika mfuko ule ni kutoka hazina ya Al Jamiatul Islamiyya.

Sasa hapo wala mimi sitotaka kukuuliza swali lolote isipokuwa hili dogo sana.
Swali lenyewe ni hili hapa: Kabla mimi sijasema haya ulikuwa ukiijua historia hii?

Nyambala,

Wewe na mfano wa wewe si wa kunikwamisha mimi na ukipenda nakupa changamoto njoo
na historia uijuayo wewe mimi nitakupa majibu yake.

Hivi haikushangazi hata chembe kuwa hata Idara ya Historia ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam
hadi leo hawajaweza kuandika chochote kuhusu historia ya kudai uhuru?

Wewe hushangazwi na hilo?
 
Back
Top Bottom