Uchumi hauwezi kukua bila wawekezaji-JK

Uchumi hauwezi kukua bila wawekezaji-JK

Nne - anatoa trilioni moja ili kufanya stimulation ya kilimo (hata cuba wasingefanya hivi).

...nafikiri hapo tumsifu maana huwezi pata return kama hakuna investment yeyote,kama kweli hizo trillion zimetolewa(sio maneno tuu) na zikapangwa na kusimamiwa vizuri nina uhakika mafanikio yataonekana!
 
JK inabidi awasaidie wawekezaji wa ndani kwa serikali yake kujenga policy nzuri za kuwasaidia kupata mikopo na usalama wa biashara zao,pigana na rushwa na wape unafuu wa kodi kama hao wa nje wanaowapa tax holiday ,na serikali lazima imwage pesa nyingi sana kwenye umeme,barabara na Elimu maana hivyo ndio kama engine ya maendeleo...bila kuwapatia mikopo na kuondoa rushwa/urasimu wawekezaji wa ndani itakuwa ngumu sana kufanikiwa so na Taifa kwa ujumla!
Koba,
Sera za Kikwete hazijazingatia au kulenga wawekezaji wa ndani. Yeye kwake wawekezaji ni watu wa nje. Ni lini alipozunguka Tanzania akihimiza wawekezaji wa ndani?
 
Akili ya maskini jamani?..
Kikwete anaonesha wazi hufikiri akiwa ndani ya sanduku la Umaskini!...Imani yake inamtuma kusema - Wawekezaji binafsi ni watu kutoka nje..kwani ktk agizo lake hakuonyesha kabisa kwamba Wawekezaji binafsi wanaweza kutoka ndani ya nchi.

Mwaka jana nilibahatika kuongea na mwanasiasa mwingine toka TZ nikamwambia kuhusu Ujasiri amali akanambia ati mgeni mwekezaji hawezi kuwa mjasiriamali, hiyo ni nafasi waliyopewa wananchi wazawa...
Taabu kweli kweli kuingilia Ubepari bila kujua yatokanayo!
 
Koba,
Sera za Kikwete hazijazingatia au kulenga wawekezaji wa ndani. Yeye kwake wawekezaji ni watu wa nje. Ni lini alipozunguka Tanzania akihimiza wawekezaji wa ndani?

umesema kweli J
 
Wawekezaji wa nje hawawezi kuja kama JK anavyotamani kwa kuwa wanaona jinsi ambavyo wawekezaji wa ndani wasivyofaidika na uwekezaji huo. Charity begins at home. JK au Rais yeyote mwingine wa nchi hii akitaka kupata wawekezaji wa kweli, ni lazima aamue kuwezesha wawekezaji wa ndani kwa makusudi na kwa kutosha ili wa nje waone mwanya wa maendeleo hayo ya kibiashara. La sivyo, wawekezaji wowote watakaokuja, watakuwa na moja tu..Kufanya biashara haraka kwa mtaji mdogo, na kwa kutoza bei za juu za huduma zao, hatimaye kuondoa rasilimali zao nyingi kadiri watakavyoweza.

Serikali ni lazima kwa makusudi kabisa, iwawezeshe wananchi wake kiutaalam (kuimarisha vyuo vikuu na kuwezesha wengi kuhitimu vizuri) na kutoa vipaumbele muhimu vya kiuchumi kwa wananchi wake kwanza.
 
Nimesikia juzi kuwa Gadafi anataka Afrika ilipwe fidia kutokana na madhara ya ukoloni.Tofauti na Gadafi, hawa wa kwetu wako busy kuwavuta wakoloni huku tukidanganywa kuwa hakuna njia tofauti ya maendeleo isipokuwa kuwagawia wakoloni hao mali zetu!
 
mkuu, unatakiwa ukumbuke kuwa waliosaini hiyo mikataba wananufaika na mikataba yenyewe. Kama ingekuwa hawanufaiki hakunba ambaye angesaini. It is only now that the nation has come to light that catutally this 97 percent inagawiwa kwa hao walioshiriki kusaini mikata hiyo. Ndio maana ukitaka kuvunja mikata hiyo leo, wakawanza watakao kupinga ni watanzania wenyewe na sio wawekezaji wenyewe.

Hii mikatabaka ya 3% ilisainiwa wakati wa Nkapa.

Tumeona JMK akiunda tume ya kuirudia hii mikataba na kujaribu kuirekebisha ili Tanzania ifaidike na nnadhani wengine katika hii tume walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani (Zitto kama sikosei alikuwemo). Swali, kwa nini alaumiwe JMK aliyekuja kuitazama upya hii mikataba? Mimi nadhani JMK ni wakusifiwa kwa japao kuitazama na upya na kuwaweka mpaka wa vyama vya upinzani kufuatilia hili suala.

Katika hili kwa nini alaumiwe JMK na asilaumiwe Nkapa, alietutosa?
 
Nimesikia juzi kuwa Gadafi anataka Afrika ilipwe fidia kutokana na madhara ya ukoloni.Tofauti na Gadafi, hawa wa kwetu wako busy kuwavuta wakoloni huku tukidanganywa kuwa hakuna njia tofauti ya maendeleo isipokuwa kuwagawia wakoloni hao mali zetu!

Wengine huwa wanaponda ''wakoloni'' wakati wao wanaishi huko huko kwa ''wakoloni'', mijitu mingine bwana, haieleweki!
 
Hii mikatabaka ya 3% ilisainiwa wakati wa Nkapa.

Tumeona JMK akiunda tume ya kuirudia hii mikataba na kujaribu kuirekebisha ili Tanzania ifaidike na nnadhani wengine katika hii tume walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani (Zitto kama sikosei alikuwemo). Swali, kwa nini alaumiwe JMK aliyekuja kuitazama upya hii mikataba? Mimi nadhani JMK ni wakusifiwa kwa japao kuitazama na upya na kuwaweka mpaka wa vyama vya upinzani kufuatilia hili suala.

Katika hili kwa nini alaumiwe JMK na asilaumiwe Nkapa, alietutosa?

wote walaumiwe, kupitia mikataba pekee hakutusaidii kitu, alisema ataipitia na ataifanyia marekebisho lakini kaipitia tu halafu kimyaa, tunataka marekebisho kama alivyoahidi kama hairekebishiki aseme tuende Bulyanhulu tukamngoe bepari kivyetu vyetu..alaa!!!
 
Hii mikatabaka ya 3% ilisainiwa wakati wa Nkapa.

Tumeona JMK akiunda tume ya kuirudia hii mikataba na kujaribu kuirekebisha ili Tanzania ifaidike na nnadhani wengine katika hii tume walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani (Zitto kama sikosei alikuwemo). Swali, kwa nini alaumiwe JMK aliyekuja kuitazama upya hii mikataba? Mimi nadhani JMK ni wakusifiwa kwa japao kuitazama na upya na kuwaweka mpaka wa vyama vya upinzani kufuatilia hili suala.

Katika hili kwa nini alaumiwe JMK na asilaumiwe Nkapa, alietutosa?

Wakati wa kampeni za 2005 Kikwete aliahidi kuiangalia upya hii mikataba ili kuifanya marekebisho kwa manufaa ya Watanzania. Leo ni mwaka wa nne tangu aingie madarakani na hajafanya lolote, hivyo naye pia anastahili lawama za hili la Tanzania kutofaidika na rasilimali zetu.
 
Wakati wa kampeni za 2005 Kikwete aliahidi kuiangalia upya hii mikataba ili kuifanya marekebisho kwa manufaa ya Watanzania. Leo ni mwaka wa nne tangu aingie madarakani na hajafanya lolote, hivyo naye pia anastahili lawama za hili la Tanzania kutofaidika na rasilimali zetu.

Tumuulize Zitto Kabwe, aliteuliwa kwenye hii kamati, kama JMK hakufanya lolote kuiteua hii kamati kushughulikia hili jambo na kama kaiteuwa kamati ambayo inahusisha mpaka wapinzani basi JMK kafanya kitu na sasa tunauliza, Jee, kamati mmefanya nini? kwani nnauhakika mnapitia humu JF, kama si wote basi japo Zitto huwa yumo humu mara kwa mara.

Haya Zitto tujuze!
 
wote walaumiwe, kupitia mikataba pekee hakutusaidii kitu, alisema ataipitia na ataifanyia marekebisho lakini kaipitia tu halafu kimyaa, tunataka marekebisho kama alivyoahidi kama hairekebishiki aseme tuende Bulyanhulu tukamngoe bepari kivyetu vyetu..alaa!!!

Muulize Zitto, kamati yao imefanya nini, ime recommend nini na hatua gani zimechukuliwa baada ya hapo?
 
wote walaumiwe, kupitia mikataba pekee hakutusaidii kitu, alisema ataipitia na ataifanyia marekebisho lakini kaipitia tu halafu kimyaa, tunataka marekebisho kama alivyoahidi kama hairekebishiki aseme tuende Bulyanhulu tukamngoe bepari kivyetu vyetu..alaa!!!
Jamani, msilie na hii mikataba kwani kanuni yake ilikuwa ni ndogo sana. Na michezo yenyewe ilikuwa kama ifuatavyo.

Kimsingi Bepari hakufutii deni hata siku moja. Mliposikia kuwa Mkapa kafanikisha kufuta madeni kulikuwa na gharama ya kulipa vile vile. Gharama yake ndio ilikuwa kulilipa deni hilo kupitia madini, indirectly. Tukajisifu sana kwa kufutiwa madeni, kumbe tuliliwa. Sasa mchezo umeanza, mnalilia nini. India walipotaka kufutiwa walikataa, mnajua kwanini? Kwasababu walijua gharama yake ilikuwa kubwa zaidi. Hivi kweli nyie watanzania mliamini kuwa tumefutiwa deni hilo kabisa, hata kifutia jasho wao wasipate? Hiyo sahau kabisa, nafikiri mmesahau Nyerere aliwaitaje hawa "mabepari, wanyonyji, kupe" na kila aina ya jina ilimradi tu ionyeshe jitu fulani lisilokwenda kwa hasara.

Mkapa aliambiwa na alifahamu na akatuacha majuha kama Nyerere alivyotuacha na kipindi cha miezi 18 ya shida baada ya Vita vya Uganda. Kumbe alielewa ni milele, na imetoka. Hata hivyo hii ni fundisho kwa Watanzania. Watanzania amkeni, msipende vya bure!!!!!!!!!
 
Wakati wa kampeni za 2005 Kikwete aliahidi kuiangalia upya hii mikataba ili kuifanya marekebisho kwa manufaa ya Watanzania. Leo ni mwaka wa nne tangu aingie madarakani na hajafanya lolote, hivyo naye pia anastahili lawama za hili la Tanzania kutofaidika na rasilimali zetu.
Hastahili lawama hata kdogo. Hebu som maelezo hapa chini ndio utafahamu kwanini hastahili lawama.
Jamani, msilie na hii mikataba kwani kanuni yake ilikuwa ni ndogo sana. Na michezo yenyewe ilikuwa kama ifuatavyo.

Kimsingi Bepari hakufutii deni hata siku moja. Mliposikia kuwa Mkapa kafanikisha kufuta madeni kulikuwa na gharama ya kulipa vile vile. Gharama yake ndio ilikuwa kulilipa deni hilo kupitia madini, indirectly. Tukajisifu sana kwa kufutiwa madeni, kumbe tuliliwa. Sasa mchezo umeanza, mnalilia nini. India walipotaka kufutiwa walikataa, mnajua kwanini? Kwasababu walijua gharama yake ilikuwa kubwa zaidi. Hivi kweli nyie watanzania mliamini kuwa tumefutiwa deni hilo kabisa, hata kifutia jasho wao wasipate? Hiyo sahau kabisa, nafikiri mmesahau Nyerere aliwaitaje hawa "mabepari, wanyonyji, kupe" na kila aina ya jina ilimradi tu ionyeshe jitu fulani lisilokwenda kwa hasara.

Mkapa aliambiwa na alifahamu na akatuacha majuha kama Nyerere alivyotuacha na kipindi cha miezi 18 ya shida baada ya Vita vya Uganda. Kumbe alielewa ni milele, na imetoka. Hata hivyo hii ni fundisho kwa Watanzania. Watanzania amkeni, msipende vya bure!!!!!!!!!
 
Jamani, msilie na hii mikataba kwani kanuni yake ilikuwa ni ndogo sana. Na michezo yenyewe ilikuwa kama ifuatavyo.

Kimsingi Bepari hakufutii deni hata siku moja. Mliposikia kuwa Mkapa kafanikisha kufuta madeni kulikuwa na gharama ya kulipa vile vile. Gharama yake ndio ilikuwa kulilipa deni hilo kupitia madini, indirectly. Tukajisifu sana kwa kufutiwa madeni, kumbe tuliliwa. Sasa mchezo umeanza, mnalilia nini. India walipotaka kufutiwa walikataa, mnajua kwanini? Kwasababu walijua gharama yake ilikuwa kubwa zaidi. Hivi kweli nyie watanzania mliamini kuwa tumefutiwa deni hilo kabisa, hata kifutia jasho wao wasipate? Hiyo sahau kabisa, nafikiri mmesahau Nyerere aliwaitaje hawa "mabepari, wanyonyji, kupe" na kila aina ya jina ilimradi tu ionyeshe jitu fulani lisilokwenda kwa hasara.

Mkapa aliambiwa na alifahamu na akatuacha majuha kama Nyerere alivyotuacha na kipindi cha miezi 18 ya shida baada ya Vita vya Uganda. Kumbe alielewa ni milele, na imetoka. Hata hivyo hii ni fundisho kwa Watanzania. Watanzania amkeni, msipende vya bure!!!!!!!!!

Unaona mabaya ya Nyerere na Mkapa tu kwa vile si Waislamu, siyo?

Nani alifungua nchi kwa mabepari kupitia kigezo cha soko huria, pamoja na kuingia mikataba na IMF, World Bank nk kama si Mwinyi? Hata Kikwete anahusika moja kwa moja na mikataba mibovu ya madini akiwa Waziri wa Madini wakati huo.
 
Muulize Zitto, kamati yao imefanya nini, ime recommend nini na hatua gani zimechukuliwa baada ya hapo?

..huyo alikunja zake za vikao na hana idea nini kiliandikwa kwenye ile report,sasa hivi yuko busy kutafuta ukubwa ndani ya Chadema wakati ubunge umeshamshinda,mtu wa ukweli Dr Slaa tuu na yule mama Kilango hawa wengine ni wababaishaji tuu
 
Mkapa aliambiwa na alifahamu na akatuacha majuha kama Nyerere alivyotuacha na kipindi cha miezi 18 ya shida baada ya Vita vya Uganda. Kumbe alielewa ni milele, na imetoka. Hata hivyo hii ni fundisho kwa Watanzania. Watanzania amkeni, msipende vya bure!!!!!!!!!

kwa hiyo wewe Zawadi Ngoda unajua hili halafu sisi watanzania na JK akiwemo ndani tumeachwa majuha, ndio maana JK out of ignorance anasema atapitia mikataba na kuirekebisha kwa sababu asilimia 3 ni ndogo sana. au na yeye anatudanganya kama Mkapa?

na kwa nini yeye kama waziri aliyepita wa nishati madini na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa hakupitia kitu muhimu na nyeti kama mikataba ya kugawa madini anasubiri mpaka awe rais?

kwa nini hawawajibishi waliohusika na huu upuuzi?

Hebu angalia wanakomba mpaka wanakuwa the biggest gold company in the world, halafu tunaleta longolongo nyiingi huku tukiwa masikini wa kutupwa

In 1999, following Placer Dome's lead, Barrick went to Africa and soon acquired Sutton Resources. Sutton had been exploring the Bulyanhulu property, situated in northwestern Tanzania, extolled as East Africa's largest gold deposit with reserves of 8.8 million ounces of exceptionally high-grade gold. For every Bulsang, there was a Bulyanhulu--and Barrick had far more of the latter than the former. The company finished the year with gold sales of $1.42 billion, net income of $331 million (up 10 percent from the previous year), and production up another 500,000 ounces for a total of 3.7 million ounces of gold.
http://www.fundinguniverse.com/company-histories/Barrick-Gold-Corporation-Company-History.html
 
Swali bado linabakia vile vile kuwa bila wawekezaji kutoka nje(kama JK anavyoamini) tunaweza kweli kuendelea? Tutaweza vipi? isije kuwa tunajaribu kukataa kitu ambacho kina ushahidi waukweli wake.
 
Back
Top Bottom