Uchumi unaimarika bei ya mchele yashuka kutoka sh.2600 hadi sh.1300 kwa kilo!

Ndio kazi ya serikali ya awamu ya tano,pesa ipate thamani.
Hongera serikali kwa kudhibiti mfumuko wa bei
Wewe na Joni Mbatizaji nawaweka kapu moja, mnachanganya madesa kwa kuwa kila kitu mnakiangalia kwa macho ya kijani hadi mnaona vitu ambavyo havipo.
 
Hilo ndio tataizo la kuangalia kila kitu kisiasa hadi mtu anasahau kua mazao yana mzunguuko wake wa bei. Hata hakutaka kujiuliza kama huu ni msimu wa mavuno au vipi? Anatulisha matango pori hati uchumi umeimarika-nafikiri huyu ni mchumi kanjanja.
Nashukuru kwa kutambua kuwa bei imeshuka, hiyo misimu ya mavuno iko miaka yote na walanguzi walikuwa wananunua mazao kabla hayajavunwa ili kucontrol price....mwaka huu imekuwaje?!!!
 
nimeamini usiku huu ITV imetangaza kushuka bei kwa mchele tena wachuuzi wenyewe wamehojiwa na wamekiri utashuka mpaka 1,300/ kwa kilo
jamani tuacheni ubishi
huyu Yohana mbatizaji kazipata za kweli
insu sio kushuka bei mchele,insu ni kuwa kushuka bei kwa mchele hakumanishi uchumi umepanda
 
Watanzania daini katiba mpya na tume huru CCM itoke vinginevyo mtapata tabu Sana
 
huo ni ule mchele mjapani sisi tunao kula mchele wa Kahama na mbeya mziki upo pale pale sh 2600 mbona hasemi na sukari.
 
Wewe na Joni Mbatizaji nawaweka kapu moja, mnachanganya madesa kwa kuwa kila kitu mnakiangalia kwa macho ya kijani hadi mnaona vitu ambavyo havipo.
Kudhibitiwa kwa walanguzi na madalali waliokuwa wananunua mazao kabla hsyajavunwa ni sababu mojawapo ya bei za nafaka katika ujumla wake kushuka!
 
jamani ni kweli mchele na baadhi ya vyakula vinashuka bei,hii inatokana na ukweli kuwa uchumi wa Tanzania una promoka kwa kasi kubwa purchasing power ya watu imeshuka watu hawawezi ku affod kununua bidhaa mbalimbali supply ya bidhaa imekuwa kubwa kuzidi mahitaji-mahitaji yamekuwa kidogo kutokana na watu kutoweza kununua.
Exports za bidhaa zetu zimeporomoka mara dufu ukilinganisha na mwaka 2016 na mwaka 2015-someni Monthly Economic Review report ya BOT ya mwezi 4 takwimu zinaonyesha wazi
 
Tatizo Ufipa kila kitu wamekaririshwa kupinga!
Mkuu,
Hebu USILETE siasa kwenye hili

Ktk uhalisia,
Kwa kila mwaka, kipind cha kuanzia KIANGAZI cha mwezi mei mpaka agosti ni miezi ya mavuno.

Hivo suala LA kushuka kwa Bei ya mchele sio LA kushangaza kabisa.

Ktk uchumi wanasema;
"Supply imeizidi Demand"
"Upatikanaji umezidi Mahitaji"

Ni kama vile kipindi cha Masika "january-march" kunapokua na uhaba wa sukari maana viwanda husitisha uzalishaji na kujikita zaid kwenye kulima miwa.

Sasa kipind km hiki, huwez sema moja kwa moja eti uchumi umepanda.
 

YES, MCHELE KITUMBO, HUKU KWETU JERO, UCHUMI WA MCHELE UMEIMARIKA SANA
 
Gharama za kuzalisha huo mpunga nazo zimeshuka au hilo lipo nje ya kibarua chako.
Huyu ndugu yetu ni wa kumuhurumia bure tu.

Ndo maana kuna mdau humu alisema kua

Inawezekana huyu jamaa ni kula kulala kwa shemeji.

Kazi yake ni kutumwa tu supermarket.

WATU KM HAWA HATA HAWAJUI UCHUMI UNAKUAJE.
 
Hata kama sijui uchumi ila kwa hili nehi.. Kuch nehi.. Kwamba hata zile mbaazi ziliyoshuka bei kutoka 3000 kwa kilo mpaka sh 300 kwa kilo ni kukua kwa uchumi? Na zile nyanya debe elfu 2500 ni kukua kwa uchumi?
 
Njoo vijiji vya kata ya Mwamala wilaya ya Nzega mkoani Tabora gunia ni 36,000 mwisho 45,000 na bado wanavuna hapo.

Duru zinadai kilo itafika hata 800 huko lakini hii wala siyo ishara ya uchumi kuimarika,Kuna watu wataumia.
Mkuu unamaanisha kile unachosema?! Kama ni kweli mimi nianze kufunga safari kuja kununua mchele huko Tabora. Maana kwa hesabu za haraka ni kuwa, Ukinunua gunia moja la 100kg kwa sh.45,000, ina maana kila kilo moja utakuwa umenunua kwa sh.450. Na hapo kama bado wanaendelea kuvuna, ina maana itafika mpaka sh.300 kwa kilo. Hii kwangu imekuwa ngumu kuamini, labda kuna tarakimu umezikosea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…