Uchumi wa China wakua kwa asilimia 5.5 katika nusu ya kwanza ya mwaka huu

Uchumi wa China wakua kwa asilimia 5.5 katika nusu ya kwanza ya mwaka huu

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111445896189.jpg
Idara Kuu ya Takwimu ya China hivi karibuni ilitoa takwimu ambazo zinaonesha kuwa, pato la taifa la China katika nusu ya kwanza ya mwaka huu lilikuwa dola trilioni 8.27 za Kimarekani, ambalo ni ongezeko la asilimia 5.5 ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hicho.

Kwa kulinganishwa na asilimia 4.5 ambacho ni wastani wa kiwango cha ukuaji wa uchumi wa China katika miaka mitatu iliyopita, kiwango hicho ni cha kasi, hali ambayo inaonesha kuwa uchumi wa China unafufuka kwa utulivu.

Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita wakati China ilipokuwa ikikabiliana na janga la COVID-19, ilichukua hatua kali mbalimbali za kuzuia virusi, ili kulinda afya na usalama wa maisha ya watu.

Hatua hizo zilifanikisha China kukabiliana na janga hilo, lakini wakati huo huo zilileta athari mbaya kwa uchumi. Tangu kumalizika kwa hatua hizo mwishoni mwa mwaka jana, uchumi wa China umeonyesha maendeleo ya kufufuka, hasa katika sekta ya huduma.

Ikilinganishwa na nchi nyingine, ukuaji wa uchumi wa China katika nusu ya kwanza ya mwaka huu ulikuwa wa kasi zaidi kuliko wa nchi kubwa kiuchumi. Katika robo ya kwanza ya mwaka huu, pato la taifa la Marekani, Umoja wa Ulaya na Japan lilikua kwa asilimia 1.8, 1 na 1.9.

Nchi zilizoendelea zinahangaika kukabiliana na changamoto za mseto za mfumuko wa bei na kudidimia kwa uchumi. Utulivu wa maendeleo ya uchumi wa China umeendelea kuwa injini muhimu ya uchumi wa dunia.

Biashara kati ya China na nchi za nje pia imeendelea kustawi katika nusu ya kwanza ya mwaka huu. Takwimu zilizotolewa na Idara Kuu ya Forodha ya China zinaonesha kuwa, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, thamani ya jumla ya biashara ya bidhaa kati ya China na nchi za nje ilikuwa yuan trilioni 20.1 sawa na dola trilioni 2.8 za Kimarekani, ambalo ni ongezeko la asilimia 2.1 ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hicho.

Mauzo ya magari ya nishati mpya, betri za lithiamu-ioni, na paneli za umeme wa jua za China kwa nchi za nje yameongezeka kwa haraka sana. Wakati huo huo, nchi za ASEAN na nchi husika za Pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja” zimekuwa sehemu mpya zenye ukuaji wa haraka wa biashara na China.

Hata hivyo, hivi sasa maendeleo ya uchumi wa China yanakabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo kupungua kwa mahitaji ya kimataifa, na tishio la vikwazo vya kibiashara vya Marekani na nchi nyingine za Magharibi.

Kuhusu ajira, kwa kuwa uchumi wa China uko katika mchakato wa kubadilika kutoka kutegemea zaidi nguvu kazi hadi kutegemea zaidi teknolojia na elimu ya juu, kiwango cha ukosefu wa ajira kimepanda kwa kiasi fulani. Lakini kwa upande mwingine, hatimaye uboreshaji wa muundo wa uchumi husaidia kutatua suala la ajira.

Kwa ujumla, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, uchumi wa China umeendelea kwa utulivu na kasi inayofaa, ambayo imeweka msingi mzuri wa maendeleo ya baadaye, na pia kuleta imani kwa maendeleo ya uchumi wa dunia.
 
Below projection
 

Attachments

  • 4517D9C0-ABDE-46A5-AB36-2471ACC55B61.png
    4517D9C0-ABDE-46A5-AB36-2471ACC55B61.png
    127 KB · Views: 8
Robo ya kwanza (Jan-March) ulikua kwa 4.5

Robo ya pili (Apr-June) ulikuwa kwa 6.5

Unapata wastani wa 5.5 kwa miezi sita ya kwanza 2023
 
Hiyo siyo kweli ni propaganda tu hizo, haiwezekani uchumi wa mataifa mengine makubwa yakuwe kwa wastani mdogo lkn eti ule wa China ukue kwa wastani mkubwa hivyo wakati zinategemeana kwa kiasi kikubwa sana.

Hizo ni porojo tu za Chinese state controlled media. Uchumi wa dunia umeathirika kwa kiasi kikubwa sana bila kujali nchi na Tanzania ikiwemo.
 
Hiyo siyo kweli ni propaganda tu hizo, haiwezekani uchumi wa mataifa mengine makubwa yakuwe kwa wastani mdogo lkn eti ule wa China ukue kwa wastani mkubwa hivyo wakati zinategemeana kwa kiasi kikubwa sana.

Hizo ni porojo tu za Chinese state controlled media. Uchumi wa dunia umeathirika kwa kiasi kikubwa sana bila kujali nchi na Tanzania ikiwemo.
Hujui kitu kuhusu China. Aliyekwambia China inaendeshwa sawasawa na nchi nyingine nani.
Kama ingekuwa hivyo kwanini zaidi ya 28% ya manufacturing ya dunia ifanyike China, kwanini wasiwe % sawasawa.
Yani Rwanda na Burundi ambazo ni poor countries hazifanani kimwenendo sembuse superpowers zenye ideologies tofauti ndio zifanane.

Na kama hizi taarifa ni propaganda tuletee source yako isiyo propaganda
 
Says who?
Chombo gani huru cha kimataifa kilichoupima huo uchumi mnaoutangaza hivyo kwa nguvu?

Sheria ye untiespionage ilikuwa updated imekataza katakata kwa mtu au taasisi yyte kukusanya data zozote za aina yyte.., aya mtuambie nani aliethibitisha ukuaji huu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ingekuwa ni Marekani usingehoji hivi ila kwa kuwa wewe ni anti-Sino lazima uje ni hoja dhaifu kama hizi. Tunakujua
 
Acheni kudanganya watu,
Ni mamlaka gani iliyo huru ya kimataifa iliyothibitisha ukuaji huoo mnaoutangaza...?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hilo swali muulize mleta mada, tazama nilichoquote ndio uulize. Na mamlaka za kimataifa zinaweza zisitoe taarifa ya nusu mwaka zikatoa ya mwaka. Na isitoshe China haijiendeshi kwa taarifa na takwimu za mamlaka za kimataifa, ina maana sensa nayo huwa unasubiri mamlaka za kimataifa zikwambie China ina watu wangapi?
Hizo mamlaka taarifa wanazitoa wapi kama baadhi sio rejea ya data za China wenyewe?

Hata hivyo siwezi shupaza shingo kukataa kwamba China haiwezi kua kiuchumi 5.5% kwa nusu mwaka. Hiyo ni nchi ambayo ilishawahi kukua 11% kwa mwaka sasa ajabu iko wapi.
Miaka kadhaa kwenye hii karne ya 21 China imekua kwa 6% kiuchumi. Sioni ajabu kwa 5.5% nusu mwaka
 
View attachment 2693878Idara Kuu ya Takwimu ya China hivi karibuni ilitoa takwimu ambazo zinaonesha kuwa, pato la taifa la China katika nusu ya kwanza ya mwaka huu lilikuwa dola trilioni 8.27 za Kimarekani, ambalo ni ongezeko la asilimia 5.5 ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hicho.

Kwa kulinganishwa na asilimia 4.5 ambacho ni wastani wa kiwango cha ukuaji wa uchumi wa China katika miaka mitatu iliyopita, kiwango hicho ni cha kasi, hali ambayo inaonesha kuwa uchumi wa China unafufuka kwa utulivu.

Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita wakati China ilipokuwa ikikabiliana na janga la COVID-19, ilichukua hatua kali mbalimbali za kuzuia virusi, ili kulinda afya na usalama wa maisha ya watu.

Hatua hizo zilifanikisha China kukabiliana na janga hilo, lakini wakati huo huo zilileta athari mbaya kwa uchumi. Tangu kumalizika kwa hatua hizo mwishoni mwa mwaka jana, uchumi wa China umeonyesha maendeleo ya kufufuka, hasa katika sekta ya huduma.

Ikilinganishwa na nchi nyingine, ukuaji wa uchumi wa China katika nusu ya kwanza ya mwaka huu ulikuwa wa kasi zaidi kuliko wa nchi kubwa kiuchumi. Katika robo ya kwanza ya mwaka huu, pato la taifa la Marekani, Umoja wa Ulaya na Japan lilikua kwa asilimia 1.8, 1 na 1.9.

Nchi zilizoendelea zinahangaika kukabiliana na changamoto za mseto za mfumuko wa bei na kudidimia kwa uchumi. Utulivu wa maendeleo ya uchumi wa China umeendelea kuwa injini muhimu ya uchumi wa dunia.

Biashara kati ya China na nchi za nje pia imeendelea kustawi katika nusu ya kwanza ya mwaka huu. Takwimu zilizotolewa na Idara Kuu ya Forodha ya China zinaonesha kuwa, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, thamani ya jumla ya biashara ya bidhaa kati ya China na nchi za nje ilikuwa yuan trilioni 20.1 sawa na dola trilioni 2.8 za Kimarekani, ambalo ni ongezeko la asilimia 2.1 ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hicho.

Mauzo ya magari ya nishati mpya, betri za lithiamu-ioni, na paneli za umeme wa jua za China kwa nchi za nje yameongezeka kwa haraka sana. Wakati huo huo, nchi za ASEAN na nchi husika za Pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja” zimekuwa sehemu mpya zenye ukuaji wa haraka wa biashara na China.

Hata hivyo, hivi sasa maendeleo ya uchumi wa China yanakabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo kupungua kwa mahitaji ya kimataifa, na tishio la vikwazo vya kibiashara vya Marekani na nchi nyingine za Magharibi.

Kuhusu ajira, kwa kuwa uchumi wa China uko katika mchakato wa kubadilika kutoka kutegemea zaidi nguvu kazi hadi kutegemea zaidi teknolojia na elimu ya juu, kiwango cha ukosefu wa ajira kimepanda kwa kiasi fulani. Lakini kwa upande mwingine, hatimaye uboreshaji wa muundo wa uchumi husaidia kutatua suala la ajira.

Kwa ujumla, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, uchumi wa China umeendelea kwa utulivu na kasi inayofaa, ambayo imeweka msingi mzuri wa maendeleo ya baadaye, na pia kuleta imani kwa maendeleo ya uchumi wa dunia.
Uchumi wa Tanzania ungekua kwa kasi, ila tatizo ni hili

1689886148544.jpeg
 
Unanipa vigezo gani kuamini data hizi? unemployment rate inazid kukua China, 21.3% ya vijana kati ya 16 ba 24 year old hawana ajira hapo haujagusa makundi mengine,

Decoupling, derisking and diversifying of economy itawaumiza sana China.


Sent using Jamii Forums mobile app
Tuanze na manufacturing, China inazalisha 28% ya uzalishaji wote duniani. Hilo tu linatosha kuipa ukuaji mzuri kiuchumi. Kutokana na COVID-19 zile restrictions zilifanya uchumi udorore na sasa ugonjwa huo ni kama unaisha na vizuizi vya kusafiri vimeondolewa ilikuwa ni matter of time ukuaji utokee sababu ya demand kubwa ya consumers.

China inazalisha magari almost mara tatu ya Marekani ambayo ndio ya pili kwa uzalishaji magari duniani.

China inatengeneza zaidi ya 40% ya meli za mizigo duniani.

Hiyo ni nchi ya pili kiuchumi, cha ajabu ni nini kukua kwa 5.5% kwa nusu mwaka?

Mwaka 2007 ilikua kwa 14.2%. Najua utauliza nani kadhinitisha, ni IMF usiulize. Sasa waweze 14.2% washindwe 5.5?
Mwaka 2018 mwaka kabla ya COVID-19 uchumi wao ulikua kwa 6.6% report by IMF.

Mwaka 2024 IMF ilifanya projection kwamba China itakua kiuchumi kwa 5.5% hii ambayo unataka kulia unaona haiwezekani.
Cha ajabu au kipya ni nini au hizo decoulping na unemployment IMF hawazijui.
"The fastest sustained expansion by a major economy in history" hao ni IMF wanauzungumzia trend ya ukuaji wa uchumi wa China
 
Lazima waboreke,kama Kuna mnaowapa mamlaka wanaiba mali ya umma halafu wanaenda kununua mayutong,mnategemea nn?
 
Ni taasisi gani huru ya kuaminika iliyofanya tafiti na kutoa majibu haya?

Jibu swali?

Kama jibu lako ni CCP ama selikari ya uchina then utuelezee ni kwann unemployment imezidi kukua China? Kwann antiespinage law imekataza watu wasikusanye data zozote za kiuchumi?


Sent using Jamii Forums mobile app
Ngoja nikujibu, aliyetoa taarifa ni China wenyewe. Hapo tumemaliza.
Unakomaa na unemployment sijui anti espionage law.

Kama anti espionage ndio inashusha uchumi wa nchi duniani. Kwa kutumia hizo data za world's acknowledged instituons tunakutana na nchi zenye uhuru wa vyombo vya habari za juu zaidi zikiwa ni Norway, Denmark na Sweden. Hizo kwenye top 10 ya chumi bora duniani zipo?
Ukitafuta nchi 20 zenye Free mass media utazikuta zote kwenye 20 bora za kiuchumi? Hata nusu utazikuta?

Na kukua kwa uchumi haimaanishi ni kukua kwa GDP per capita. Kama ingekuwa ndio hivyo basi Luxembourg, Qatar, Switzerland na wenzake wenye higher GDP per capita ndio zingekuwa nchi kubwa kiuchumi duniani. Nchi zinazoongoza kuwa na employment rate kubwa sio zinazoongoza kuwa na uchumi mkubwa wala ukuaji.

Na jambo la msingi China inaondoka kwenye uchumi wa manpower inakuja kwenye uchumi wa machinery, automation na robotics lazima ajira zipungue ukizingatia ina watu bilioni 1.3.

Hata Burundi ikiamua inaweza kua hata 10% kiuchumi kwa mwaka. Sio uchawi ni mipango hiyo. Wenzake wako kufundishana kuchagua jinsia, yeye yuko busy kwenye production. Kila mmoja ashinde mechi zake
 
We jamaa usinipe porojo, hizi ulizotoa hapa ni porojo..

China unemployment rate imezidi kukua mwaka hadi mwaka, derisking, decoupling and diversification of world's economy imezidi kukua kwa makampuni kuzidi kuhama china.

Leo hii Mexico na India ndio largest importer wa consumer goods kwa USA na Europe unalijua hili kwanza?

China real estate inayochangia more than 30% ya GDP imeingia hasara kubwa sana madeni chungu nzima unasemaje uchumi unakuwa?

Nimekuuliza ni taasisi gani huru iliyofanya utafiti na kuleta ripoti hiyo ya ukuaji wa uchumi mnaoutangaza?
Ni vigezo vipi vitumike kuamini data zenu na wakati hali halisi inaonesha tofauti kabisa na uhalisia?

Kama hauwezi kunijibu ni afadhali useme hauna majibu sahihi kuliko kuleta porojo..., sijui magari nani ambae hatengenezi magari? India, Europe, south Africa, Mexico, kote huko Kuna viwanda vya kila aina

Watafute wa kuwadanganya.



Sent using Jamii Forums mobile app
Usiongee kama umekatwa kichwa. Inabidi useme kitu fulani nilichodai sio kweli, kilicho kweli ni hiki. Sio unajificha kwenye neno "porojo". Unakuwa kama mpumbavu.

Mfano, unatakiwa upinge pale niliposema China imekua kwa 6.6% kiuchumi mwaka 2018 data za IMF sio kweli bali data za mwaka huo zinasema China imeshuka kwa -5%. Hapo ndipo upate uhalali wa kusema ni porojo.

Mexico na India zikiwa largest importer wa consumer goods inahusiana vipi na 5.5% semi-annual economic growth ya China?
Kwani China ikikua kiuchumi nchi zingine zinatakiwa zisimame?

Hilo swali la taasisi huru ni la kitoto. Nimekupa za IMF zikionyesha projection ya 2024 na zikionyesha hali ya 2018. Nazo unazikataa. Kwamba una akili sana na tools kuliko wao? Kuandika terminologies tu hujui, sembuse kujua data za kiuchumi.
 
Toa porojo zako hapa!!

China ni mfano sahihi wa ubovu wa Autocratic government.

Wachina wenyewe wanalalamika kila mahali, nakutana nao masaki huku hawaishi kulalamikia kushuka ama kudumaa kwa uchumi wao kutokana na Sera mbovu na mahusiano mabaya ya kimataifa halafu ww unaleta porojo zako hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hio inazuia 5.5% semi-annual economic growth?
Mbona unaongea vitu vingine kabisa, au hujui kinachozungumzwa ni nini hapa? Au mambo ya kiuchumi yamekushinda?

China iko na CCP hiihii, iko na mfumo huu huu wa utawala na uchumi. Mwaka 2007 wakiwa na mfumo huu huu wakakua kiuchumi kwa 14.2% data za IMF. Na zenyewe unapinga kisa "ubovu wa autocratic government"?

Mtu akiwa na roho mbaya kisha akawa na hela, roho mbaya inafuta hela anazokuwa nazo?
Au mtu akiwa mrefu alafu mchoyo, uchoyo unafuta urefu wake na kumfanya awe mfupi?

Baadae tutazungumzia ukuaji wa uchumi utabisha uzungumzie uhuru wa kuwa shoga as if matako yana mchango wowote kiuchumi.
 
Moja ya kiashiria cha ukuaji wa kiuchumi popote pale Duniania ni kupungua kwa tatizo la ajira.

GDP ni ukuaji wa pato la mtu mmoja mmoja na kuunganishwa kwa pamoja kwa nchi kwa ujumla

Unasemaje pato la mtu mmoja mmoja limekuwa na wakati janga la ajira limezidi kuongezeka.

We jamaa ni utakuwa na akili za hovyo kama hata jambo simple kama hili huwezi kulitambua

Usinielezee kitu sitaki tena kusikia porojo zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu kama matajiri wanaongezeka utajiri wao si wanaweza kuongeza GDP alafu wale unemployed wakaongezeka pia?
 
Matajiri gani wanao ongezeka?
Hivi unayajua yanayoendelea China?
Unajua hali ya utajiri wa Boss na mwanzilishi wa Alibaba ulivyoshuka?
Unajua ni matajiri wangapi wameondoka na mitaji Yao China tangia Xi Jinping aanze harakati za kutaka kuivamia Taiwan?
Mwaka huu tu peke yake watafiti wa maswala ya kiuchumi wanakadiria watu zaidi ya milioni 90 wenye vipato vya juu na vya kati watahama na kuhamisha mitaji yao kutoka China. Unalijua hili?

Hakuna mtu anaependa vita, hata wachina wenye akili wanapenda AMANI.

Sent using Jamii Forums mobile app
sawa mkuu ila kwa hoja yako hii china haijawahi uchumi wake kukua kwa kua wanapika data zao
 
Back
Top Bottom