Uchumi wa Kujitegemea bila kunyongana haiwezekani

Uchumi wa Kujitegemea bila kunyongana haiwezekani

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kunyonga wahujumu uchumi ni nyenzo muhimu sana ya uchumi wa kujitegemea. Hakuna mtu wala taasisi inayotakiwa kuwa juu ya sheria, kila mtu lazima aitumikie sheria.

Huko tunakoelekea hakutakuwa na misaada isiyokuwa na madhara kwetu maana kila nchi itakuwa inalalamikiwa na raia wake kuhusu hali za maisha yao. Hivyo, misaafa nafuu na isiyokuwa na mitego itapungua sana, hivyo tunachotakiwa sasa ni kuanza mkakati kabambe wa kuimarisha utawala wa sheria kwa kuanzia na katiba bora na bora na uwezo wa mahakama zetu kwenye kutoa haki.

Tuwe na katiba ambayo kila mtu anashitakika kwa mujibu wa makosa yake aliyoyafanya. Tuanze kukuza na kutumia uwezo wetu katika kujiletea maendelea, na hili halitawekana bila kuwa na serikali za majimbo, maana jimbo lina uwezo mkubwa wa kuzitambua na kuzitumia kikamilifu rasilimali zake zote zilizomo ndani ya jimbo kwa maendeleo ya wanajimbo na taifa kuliko hii ya sasa ya nchi yote kutawaliwa kutoka Dodoma.

Namna ilivyo sasa kuna watu wanatuibia sana lakini hatuna cha kuwafanya, wana kinga madhubuti ya kutoshitakiwa na wengine ni wezi tu lakini sheria iko "mifukoni" mwao.
 
Sasa unategemea kweli hao wezi wapitishe katiba inayokuja kuwabana na kuwanyima fursa? Sidhani.
 
Sasa unategemea kweli hao wezi wapitishe katiba inayokuja kuwabana na kuwanyima fursa? Sidhani.
ndugu yangu tujilaumu sisi wenyewe kwakuwa tumejinyima uwezo wa kusema HAPANA kwa yale tusiyoyataka kwa wanasiasa wetu.
 
Nchi iko mateka kwa majizi na mafisadi, cha ajabu, na walio huru nao wamejifanya mateka!

Nani alaumiwe?

Inafahamika kabisa kwamba, walio huru ndio wengi na wanakili na uchungu wa nchi yao, halafu ndio wengi kuliko wenye kuiteka nchi,

Walio huru, siku watakapojiondoa kwenye umateka wa kujitakia, nchi itanawiri!

Aliyekuwa akimpinga JPM, ndio hao wenye kujifanya mateka na mateka wa nchi, siku wakija kugundua kuwa waliyekuwa wakimpinga ni mtu ambaye hakutaka kujifanya mateka katikati ya mateka wa nchi na ili kuwapa nguvu wenye kujifanya mateka ili fikra zao zuwarudi, wataongeza kelele za kumkumbuka huyu mwamba!
 
Back
Top Bottom