Col FEN
JF-Expert Member
- Jun 16, 2017
- 327
- 460
Ndugu zangu Watanzania,
Kwa kweli inasikitisha kuona taasisi zetu mbali mbali, kama vile Uhamiaji, SUMATRA, TRA n.k zikiwa zimekaa kimya wakati Tanzania tunaibiwa mchana kweupe. Naomba nitoe mfano mmoja ili kuonyesha ni jinsi gani tulivyo lala na wakoloni wakiendelea kuneemeka.
Mola ametujaalia kuwa na Bandari ambayo imekaa eneo zuri sana na hivyo kuwa ni rahisi kwa nchi majirani kuitumia. Hivyo mizigo mingi ya Majirani zetu inapitia hapa Bandari ya DAR! JE MOLA ALIFANYA MAKOSA KUTUPA BANDARI HII?
Hivi sasa kumezuka wimbi la wageni wengi kuja hapa Dar Wahindi, Wachina, na Wazungu ambao wanafungua vikampuni vidogo vidogo kwa ajili ya kudaka mizigo yote unayopitia hapa Dar (Clearing & Forwarding na Cargo Consolidation) ieleweke kuwa hii mizigo inayo kuja na kupitia hapa inaanzia huko kwao hivyo kufanya raisi kwa wao kupata habari mapema ya ujio ya mizigo husika hivyo basi kupelekea kazi nyingi za mizigo inayo kuja hapa TZ hufanywa na wao wageni huku sisi Watanzania tukibakia kuwa vibarua tu. Kwa njia hii Pesa nyingi ambazo zingebakia hapa Tanzania kwa biashara ya Bandari yetu 80% ya kipato hiki kinarejeshwa kwa wakoloni wakati sisi tumelala.
Hivyo basi naziomba sana taasisi zetu ziamke kutoka usingizini na kuanza mara moja kufanya uchunguzi wa kampuni zote Wakala wa Mizigo ili kuhakikisha zinamilikiwa kwa 100% na Watanzania wenyewe tena ikibidi tuwe Watanzania weusi. Haiwezekani Wazungu watoke kwao huko kuja hapa kufanya kazi ya ukarani tu wa mizigo na kuondoka na Dola zetu, tusione haya kutetea uchumi wetu ili kuhakikisha unanufaisha Taifa letu kwa 100%.
Mola ametupa Bandari ili itunufaishe sisi Watanzania wazawa. Vita ya Uchumi ni vita ngumu sana kwani vibaraka wa Wakoloni wapo wengi. LAZIMA TULINDE RASILIMALI ZETU KWA NGUVU ZOTE NA BANDARI NI RASILIMALI KUBWA AMBAYO TUMEIZARAU. TUAMKE NA TUPAMBANE KULINDA UCHUMI WETU.
Je tujiulize Wakala wa Mizigo na Meli kunaulazima gani ya kuwa na Mtaalam wa kigeni? Jamani hadi kazi ya Ukarani tunahitaji Mzungu aje kutusimamia? Tumelala Jamani tunaibiwaa kweupe!
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa kweli inasikitisha kuona taasisi zetu mbali mbali, kama vile Uhamiaji, SUMATRA, TRA n.k zikiwa zimekaa kimya wakati Tanzania tunaibiwa mchana kweupe. Naomba nitoe mfano mmoja ili kuonyesha ni jinsi gani tulivyo lala na wakoloni wakiendelea kuneemeka.
Mola ametujaalia kuwa na Bandari ambayo imekaa eneo zuri sana na hivyo kuwa ni rahisi kwa nchi majirani kuitumia. Hivyo mizigo mingi ya Majirani zetu inapitia hapa Bandari ya DAR! JE MOLA ALIFANYA MAKOSA KUTUPA BANDARI HII?
Hivi sasa kumezuka wimbi la wageni wengi kuja hapa Dar Wahindi, Wachina, na Wazungu ambao wanafungua vikampuni vidogo vidogo kwa ajili ya kudaka mizigo yote unayopitia hapa Dar (Clearing & Forwarding na Cargo Consolidation) ieleweke kuwa hii mizigo inayo kuja na kupitia hapa inaanzia huko kwao hivyo kufanya raisi kwa wao kupata habari mapema ya ujio ya mizigo husika hivyo basi kupelekea kazi nyingi za mizigo inayo kuja hapa TZ hufanywa na wao wageni huku sisi Watanzania tukibakia kuwa vibarua tu. Kwa njia hii Pesa nyingi ambazo zingebakia hapa Tanzania kwa biashara ya Bandari yetu 80% ya kipato hiki kinarejeshwa kwa wakoloni wakati sisi tumelala.
Hivyo basi naziomba sana taasisi zetu ziamke kutoka usingizini na kuanza mara moja kufanya uchunguzi wa kampuni zote Wakala wa Mizigo ili kuhakikisha zinamilikiwa kwa 100% na Watanzania wenyewe tena ikibidi tuwe Watanzania weusi. Haiwezekani Wazungu watoke kwao huko kuja hapa kufanya kazi ya ukarani tu wa mizigo na kuondoka na Dola zetu, tusione haya kutetea uchumi wetu ili kuhakikisha unanufaisha Taifa letu kwa 100%.
Mola ametupa Bandari ili itunufaishe sisi Watanzania wazawa. Vita ya Uchumi ni vita ngumu sana kwani vibaraka wa Wakoloni wapo wengi. LAZIMA TULINDE RASILIMALI ZETU KWA NGUVU ZOTE NA BANDARI NI RASILIMALI KUBWA AMBAYO TUMEIZARAU. TUAMKE NA TUPAMBANE KULINDA UCHUMI WETU.
Je tujiulize Wakala wa Mizigo na Meli kunaulazima gani ya kuwa na Mtaalam wa kigeni? Jamani hadi kazi ya Ukarani tunahitaji Mzungu aje kutusimamia? Tumelala Jamani tunaibiwaa kweupe!
Sent using Jamii Forums mobile app