Udanganyifu wa free WiFi na full AC kwenye mabasi

Udanganyifu wa free WiFi na full AC kwenye mabasi

Protector

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2019
Posts
422
Reaction score
893
Mara nyingi mabasi mengi kama sio yote yana stika pembeni zikionesha huduma wanazotoa ni FREE WI-FI na FULL AC lakini ukiingia hakuna hata kimoja.

Inawezekana wakati likiwa jipya lilikuwa na huduma hizo (kwa Wi-Fi) sina uhakika sana maana sijawahi kutumia hata siku moja hata kwenye basi jipya, angalau AC huwa wanajaribu basi linapokuwa jipya.

Kwa mfano nikakata tiketi kwa sababu nimeona kuna Wi-Fi na AC halafu nisivikute ndani yake, swali ni je naweza kuishitaki kampuni husika kwa kunisababishia usumbufu.

Na kama hivyo vitu havipo kwa nini wasibandue hizo stika. Au kumdanganya abiria ni njia inayokubalika kisheria? Maana mabasi mengi yana stika hizo na LATRA sijui SUMTRA hawachukui hatua yoyote kuzuia udanganyifu huo.
 
Inabidi wawe wakweli. Hizo mambo zinaongeza nauli kupanda wakati ni uongo. Abiria analipia gharama ya free Wi-Fi kwenye nauli ambayo ni uongo. SUMATRA waliangalie hilo pia.
 
Hiyo ni pesa.
Ukienda kufungua shauri la madai unalipwa pesa ya kuinulia mhengo kabisa . Sema tu bongo tunapuuzia vitu vingi.
US. hata ukiliungurumisha sabufa ndani kwako sauti ikimkera jirani tu anakupiga pesa , hakuna kujuana kipuuzi huko mbele
 
Huwa nawauliza kabisa, tena nakuwarecord kabisa..ole wao wazingue.... nawawashia moto
 
Mara nyingi mabasi mengi kama sio yote yana stika pembeni zikionesha huduma wanazotoa ni FREE WI-FI na FULL AC lakini ukiingia hakuna hata kimoja.

Inawezekana wakati likiwa jipya lilikuwa na huduma hizo (kwa Wi-Fi) sina uhakika sana maana sijawahi kutumia hata siku moja hata kwenye basi jipya, angalau AC huwa wanajaribu basi linapokuwa jipya.

Kwa mfano nikakata tiketi kwa sababu nimeona kuna Wi-Fi na AC halafu nisivikute ndani yake, swali ni je naweza kuishitaki kampuni husika kwa kunisababishia usumbufu.

Na kama hivyo vitu havipo kwa nini wasibandue hizo stika. Au kumdanganya abiria ni njia inayokubalika kisheria? Maana mabasi mengi yana stika hizo na LATRA sijui SUMTRA hawachukui hatua yoyote kuzuia udanganyifu huo.
Wakiwasha AC wengine hawataki na hawajui jinsi ya kuzima alipokaa, Wifi ukihitaji omba pasiwedi kwa kondakita, atakupa.
 
Unakuta matangazo yameandikwa kwenye basi kwa rangi za kudumu. Unakuta huduma ilikuwepo kwa muda mfupi ika stop ila matangazo hawa change!
 
Inabidi wawe wakweli. Hizo mambo zinaongeza nauli kupanda wakati ni uongo. Abiria analipia gharama ya free Wi-Fi kwenye nauli ambayo ni uongo. SUMATRA waliangalie hilo pia.

LATRA wanatakiwa wawaamuru wamiliki wa Mabasi kuondoa mara moja stika zenye viashiria vya udanganyifu
 
Back
Top Bottom