Oppomall
JF-Expert Member
- Feb 8, 2017
- 3,683
- 3,966
Nikienda kwenye Mada moja kwa moja.
Serikali iliamua kuja na mpango mzuri wa usafiri wa umma wa haraka kama ilivyo kwenye Majiji mengine huko duniani ingawaje wenzetu wamepiga hatua zaidi wakaenda mpaka kwenye matumizi ya treni za umeme.
Changamoto kubwa iliyopo kwetu kwa huu usafiri ni uharaka wa utoaji wa huduma.
Karibia kila mtumiji wa usafiri huu anapokwenda ama kurudi katika majukumu yake lazima apoteze muda wa takribani saa 3 ama 4 kwa siku akisubiria usafiri wa kumtoa point moja kwenda nyingine.
Huu ni ufujaji wa rasilimali muda na kupoteza nguvu kazi.
Walau mteja afike kituoni mchakato wa kutoka usichukue zaidi ya dakika 20 lakini si hali ilivyo sasa.
Kinachoshangaza wakati watu wakiwa katika foleni ndefu hasa Vituo vya Gerezani, Mbezi louis na Kimara mwisho utaona gari inaingia na kupita tu shwaaaa eti sababu yenyewe siyo ya route hiyo,seriously tumejipanga?
Tunategemea ufanisi ikiwa watu wetu tunawaibia muda wa kuanza kazi na muda wa kurudi kuona familia zao kweli?
Tuna uhakika gani na usalama wa watu tunaowajaza vituoni bila sababu kwa saa kadhaa,siku akitokea kichaa mmoja akalipua hapo mahali tutapoteza nguvu kazi ngapi kwa kutokuwa makini?
Maana mkusanyiko umetengenezwa pasi kuwakagua wanaoingia kituoni wamebeba silaha gani.
Ili kuondoa upotevu wa muda nashauri haya yafanyike;
1. Mwekezaji apate mshindani ambae watatumia njia moja kwa wakati mmoja.
2. Daladala ziruhusiwe kuingia mjini kwa kutumia barabara ya Morogoro.
3. Mfumo wa tiketi za makaratasi uachwe badala yake kadi zinazotumika kulipia pale Kivukoni,stendi ya Magufuli nk zitumike pia kwenye Mwendokasi.
4. Magari yasiwe na route Maalum bali yapatiwe route yanapofika kituo husika kulingana na uhitaji mkubwa ulipo,hivyo Kiongozi wa Kituo atamwelekeza dereva pakia kuelekea eneo fulani.
Nawasilisha!
Soma Uteuzi na Utenguzi: Dkt. Kihamia ateuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa DART, Kuji awa Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA
Serikali iliamua kuja na mpango mzuri wa usafiri wa umma wa haraka kama ilivyo kwenye Majiji mengine huko duniani ingawaje wenzetu wamepiga hatua zaidi wakaenda mpaka kwenye matumizi ya treni za umeme.
Changamoto kubwa iliyopo kwetu kwa huu usafiri ni uharaka wa utoaji wa huduma.
Karibia kila mtumiji wa usafiri huu anapokwenda ama kurudi katika majukumu yake lazima apoteze muda wa takribani saa 3 ama 4 kwa siku akisubiria usafiri wa kumtoa point moja kwenda nyingine.
Huu ni ufujaji wa rasilimali muda na kupoteza nguvu kazi.
Walau mteja afike kituoni mchakato wa kutoka usichukue zaidi ya dakika 20 lakini si hali ilivyo sasa.
Kinachoshangaza wakati watu wakiwa katika foleni ndefu hasa Vituo vya Gerezani, Mbezi louis na Kimara mwisho utaona gari inaingia na kupita tu shwaaaa eti sababu yenyewe siyo ya route hiyo,seriously tumejipanga?
Tunategemea ufanisi ikiwa watu wetu tunawaibia muda wa kuanza kazi na muda wa kurudi kuona familia zao kweli?
Tuna uhakika gani na usalama wa watu tunaowajaza vituoni bila sababu kwa saa kadhaa,siku akitokea kichaa mmoja akalipua hapo mahali tutapoteza nguvu kazi ngapi kwa kutokuwa makini?
Maana mkusanyiko umetengenezwa pasi kuwakagua wanaoingia kituoni wamebeba silaha gani.
Ili kuondoa upotevu wa muda nashauri haya yafanyike;
1. Mwekezaji apate mshindani ambae watatumia njia moja kwa wakati mmoja.
2. Daladala ziruhusiwe kuingia mjini kwa kutumia barabara ya Morogoro.
3. Mfumo wa tiketi za makaratasi uachwe badala yake kadi zinazotumika kulipia pale Kivukoni,stendi ya Magufuli nk zitumike pia kwenye Mwendokasi.
4. Magari yasiwe na route Maalum bali yapatiwe route yanapofika kituo husika kulingana na uhitaji mkubwa ulipo,hivyo Kiongozi wa Kituo atamwelekeza dereva pakia kuelekea eneo fulani.
Nawasilisha!
Soma Uteuzi na Utenguzi: Dkt. Kihamia ateuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa DART, Kuji awa Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA