Udhalilishwaji wa waislam na vyombo vya dola

 
 

Hawa walifosiwa na nani? List of converts to Islam - Wikipedia, the free encyclopedia
 
  1. Waswahili husema palipo ukweli uongo hujitenga. Na wengine husema "Shimo la ulimi, mkono hawezi futika". Mohammed Said ni msomi tena anayeheshimika, ila amechagua kupata umaarufu katika "controversies" za mambo ya kidini. Si jambo la ajabu kwa wasomi kuchagua mwelekeo. Nadhani tatizo kubwa liko kwa wanaosikiliza mihadhara yake, kauli zake na kutafsiri yale anayoyatamka na kuyaamini. Ni kweli jamii yetu imejaa washabiki na watanzania wengi uwezo wao wa kuchambua ni mdogo na kauli na maelezo kama haya kutoka kwa mtu msomi huwasumbua sana na huweza kuleta balaa katika nchi. Wasomi wanaoamua kulalia katika controversies huwa ni watu wasiojali sana madhara ya kauli zao, bali kile wanachokiamini.
  2. Mohammed said anaamini kuwa Nyerere alikuwa hatari sana kwa waislam wa Tanzania, hata kama kuna ushahidi kibao unaothibitisha kinyume chake. Bifu lake na Nyerere liko hai hata kama Nyerere aliondoka Madarakani zaidi ya miaka ishirini iliyopita na kufariki zaidi ya miaka kumi iliyapita, bila shaka moja wapo ya mambo yanayomsumbua sana ni legacy ya Nyerere; amejaribu sana kujenga hoja za kumchafua, lakini anafanikiwa kidogo sana katika lile lile kundi lake, ila ushawishi wake umeshindwa kutoka nje ya mipaka ya kundi hilo.
  3. Hili simulizi la tukio la bwana Mohammed Said kukamatwa, si kitu kipya sana wala kigeni kwa watu wanaosafiri kwenda na kurudi nje ya nchi mara kwa mara. Ni jinsi gani amewianisha tukio hilo na dini yake, ni vigumu sana kuliona hilo katika maandishi yake; ila waweza kuliona kichwani mwake ukifanya mujumuisho wa yale aloyaandika.
  4. Huu mfumo "kristo" unaotawala Tanzania ambao kina Mohammed Said na watu wengine wanaoamini hivyo wanauona, hata kama ushahidi wa kuwepo kwa mfumo huo haupo, ni kivuli tu ambacho wameamua kukitumia ili kuficha udhaifu wa kauli zao. Zamani viongozi wengi walipokuwa wakristo, hilo lilitumika kuwaaminisha watu kuwa ubaguzi upo kwa sababu viongozi wengi ni wakristo. Baada ya waislam kuongezekan katika ngazi mbali mbali za uongozi, sasa inatafutwa sababu nyingine ya kuwepo kwa mfumo ambao ni kristo ambao huwafanya viongozi wote waislam washindwe kufurukuta. Hili si kitu kingine bado ni kiza kile kile cha Chuki dhidi ya Nyerere na wakristo ambayo Mohammed Said ameamua kutumia usomi wake kuitawanya.
  5. Hili la kutafsiri kila unalofanyiwa kuwa ni kubaguliwa kutokana na imani au hali yako wapo wengi wanalo. Afrika ya Kusini (Bondeni) hili limewafanya weusi wajikute wakichukiana wao kwa wao, wenyeji wakiwachukia wageni kuliko hata wanavyowachukia weupe. Sababu yake ni kuwa weusi wa Afrika ya Kusini hutafsiri kila wanachofanyiwa na weupe katika miwani ya ubaguzi. Weusi waliotoka katika nchi za weusi ambao wemeshaumizwa sana na Mabosi weusi, wakifika Afrika Kusini wanashangaa. Wanawaona weusi wa Afrika ya Kusini ni watu wavivu tu! Kwani mabosi wa Kizungu wako fair sana ukilinganisha na mabosi weusi katika nchi za kwao na huvumilia yote wanayofanyiwa wakiona ni mambo ya kawaida kabisa. Matokeo yake weupe wa Afrika ya kusini wakatokea kuwapendelea weusi wanaotokea katika nchi zingine na hivyo kuchochea hicho kinachoitwa "xenophobia." Miwani ya uislam inamfanya Mohammed Said atafsiri kila tukio linalomzunguka kwa minajiri ya kubaguliwa kwa muislam hata kama huo ubaguzi haupo, kama wale wenzetu wa kusini ambavyo kila wanalofanyiwa na mweupe hulitafsiri kwa muktadha wa rangi zao. Na hasa misimamo yake imejikita katika siasa za Kimataifa kuliko hata siasa za hapa Bongo.
  6. Ni kweli utawala wa nchi ulio makini inatakiwa uwe makini na huyu msomi wetu. Hizi "hot buttons" za siasa za kimataifa ukizigusa, popote pale lazima umulikwe. Iran, North Korea na Syria; zilitajwa katika "axis of evil" ya Bush. Ni wazi wamarekani watammulika mtu yeyote anayeonekana kuwa karibu na taasisi za ki-Iran. Kuhusisha hilo na kazi za makanisa au wakristo wa Tanzania, na mifumo ya Nyerere, ni jambo ambalo msomi wa aina ya Mohammed Said hawezi kuepuka, na pengine wasomaji wake inabidi walielewe na walivumilie wakati mwingine, si kwa kukaa kimya ila kwa kuuweka ukweli wazi. Ukweli ukiwekwa wazi mara nyingi Mohammed Said hubadirisha mwelekeo wa mjadala au hubadirisha mada kabisa.
 
Mbona mzee wenu huyo mzushi na mchochezi hawaambii kuwa masheh wa1964 waliwekwa kizuizini kwa kuwa walikuwa wanapanga njama za kuiangusha serikali halali na kutaka kuiweka serikali ya kiislam? Alitaka Nyerere akae anawachekea wahaini eti kwakuwa na masheh?
 
Ndio maana makundi kwa makundi ya watu wanaingia na kufata mfumo wa Maisha wa Mwenyeezi Mungu nao ni Uislaam.

Na unaelezeaje maovu yanayofanyika kwenye nchi ambazo raia zake ni 100% waislamu? Au hao raia wa nchi kama Pakistan, Indonesia, Nigeria Kaskazini, Syria, Mali na Somalia si waislamu?
 
Hadithi nzuri sana!

Kweli!? Mlongolongo wa hisia za kunyanyaswa tena na mtu msomi!
Sikatai hio hadithi ya kushikiliwa pale uwanja wa ndege kwani ni jambo la kawaida, nimewahi mimi kushikiliwa Paris! Ninakataa maelezo yake- sio lazima iwe ni ukristo na uislamu! Prejudices- kila kukicha jamani tumefanyiziwa tena! Hatuwezi kuendelea kwa namna hii, adui wa maendeleo yuko pembeni sisi tunaanza kugombana, atatufaidi!
 

Dizaini nyinyi ndugu zetu mnaoitwa waislam HAMJIAMINI hata kidogo kwanini mnalalamika nyie kila siku?..sisi hatutaki habri za kukua na kusambaa kwa dini..tunachoamini ni kwa MUNGU wetu mmoja aliye juu kinachofuata ni kumuabudu na kufanya maendeleo hayo mengine mnayoyatafuta sijui ya nini...jamaniiii mnataka tanzania igeuke iran au pakistan nchi za kislaam..kule ndo dini zilipozaliwa ziachen huko sisi tumezipokea tu basiiii..
 

Dini maana yake nini? ni dini pi iliyozaliwa Iran na Pakistan?
 
Na unaelezeaje maovu yanayofanyika kwenye nchi ambazo raia zake ni 100% waislamu? Au hao raia wa nchi kama Pakistan, Indonesia, Nigeria Kaskazini, Syria, Mali na Somalia si waislamu?

Wewe unaelezeaje majeshi ya NATO yanapozipiga nchi kama Iraq, Afghanistan, Libya, Albania, kwingine kama Chechnya wanatandikwa na Mrusi.

Una uhakika hizo nchi ulizotaja ni 100% Waislaam? kama hauna uhakika bora ukafuta kauli yako.
 
Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu. Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa. Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisafi sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa.''Strength of a woman''
 
Wewe unaelezeaje majeshi ya NATO yanapozipiga nchi kama Iraq, Afghanistan, Libya, Albania, kwingine kama Chechnya wanatandikwa na Mrusi.

Una uhakika hizo nchi ulizotaja ni 100% Waislaam? kama hauna uhakika bora ukafuta kauli yako.

Nina uhakika - wewe google halafu uniambie populations ya nchi hizo zikoje. Na unajichanganya, jibu hoja. Kauli yako ya mwanzo ilidai kuwa kwa kuwa maovu yanaongezeka ndio maana "makundi na makundi" ya watu wanajiunga na uislamu (which implies mara tu wanapojiunga maovu yanapungua na/au penye uislamu hakuna maovu). Sasa ya NATO yanahusiana vipi na uislamu au kuongezeka/kupungua maovu duniani? Au huko "kupigwa' kwa Russia kunahusiana vipi na uislamu? I wish you would make up your mind na ujikite katika kujibu hoja ULIYOILETA MWENYEWE!!!
 
Ha, ha, haaa! mbavu zangu...hadithi njoo, uwongo njoo, utamu kolea!
Hapo zamani za kale karibu sana na siku hizi, palitokea mzee mmoja aliyeitwa Mohamed Said, mzee huyu alijitambulisha kuwa msomi aliye bobea katika fani isiyojulikana zaidi ya uchochezi, chuki, uzandiki na kuwajaza chuki za kidini watanzania. Mzee huyo hatari kwa mstakabari wa watanzania, kila kukicha alikuja na tuhuma nzito kuwa waislam watanzania walikuwa wanaonewa na jini lisilo julikana, lakini wajukuu wakimnyapalia awaeleze dharimu ni nani alikuwa anakuja na kauri tata eti wakristo ndio wabaya..............................Ah! mzee huyu ni hatari sana............, anataka vijana watanzania waache kuwa wamoja katika kuukabiri umaskini, anataka vijana wachukiane kwa imani zao zakidini,. Vijana wa kitanzania mkataeni mzee huyu, mwacheni afe na chuki zake!
 

Wewe google halafu uone nchi zinazoongoza kwa maovu ni zipi, zenye Waislaam wengi au wakristo wengi, Mie nikikuletea utajiaibisha.

Njoo katika njia ya haki, njoo katika kujisalimisha kwa mmoja tu, hajazaa wala hajazaliwa!
 
Wewe google halafu uone nchi zinazoongoza kwa maovu ni zipi, zenye Waislaam wengi au wakristo wengi, Mie nikikuletea utajiaibisha.

Njoo katika njia ya haki, njoo katika kujisalimisha kwa mmoja tu, hajazaa wala hajazaliwa!

You are missing the point here dude!! Anaefanya uovu na kuhukumiwa ni MTU BINAFSI, si dini yake, ukoo wake au taifa lake. Kuna watu wanaojiita waislamu/wakristo/wahindu/Budha/wapagani na bado wakawa ni waovu. Imani yangu ni YANGU BINAFSI, hata kama ninaabudu ng'ombe bado ni imani yangu. Uhusiano wa mtu na MUNGU wake ni wa HIARI NA BINAFSI. Katika nchi zilizostaraabika, mtu ana hiari ya kufuata dini yake bila kubughudhiwa - ndio maana kuna misikiti USA, UK, Norway, Netherlands, France na kwingineko ambako traditionally hakukuwa na uislamu.
 

Kama unayajuwa hayo usinge/asingesema nchi za Kiislaam ndio zenye uhalifu mkubwa.
 
Wakati unakamatwa 2006 mtawala wa nchi alikuwa muislam,wakati wa kuvunja mabanda ya nguruwe,na damu ya waislam ikamwagika mtawala alikuwa muislam.....wakitawala wakristo mnalalamika, wakitawala waislam mnaonewa sasa nani anawatenga waislam?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…