Udokozi unawaponza Wabongo kupata ajira

Udokozi unawaponza Wabongo kupata ajira

Tatizo la wizi kazini lina mizizi yake: Nitaorodhesha baadhi kama ifuatavyo

1. Mtu ana utaalamu mzuri sana, na yeye anajua hilo halafu unamlipa mshahara wa laki moja wakati foreigner mbumbumbu anachukua dola 4,000.

2. Kutokuwa na job security kwa wafanyakazi wengi, yaani siku boss akilala na pombe kichwani unasikia anakupa pay-off kazi hakuna, je mtu afanyeje?

3. Gap kati matajiri na masikini limekuwa sana kiasi kwamba kila mtu anahitajia afikie matawi ya juu mapema kabla ya jua halijachwa.

4. Vijana wanaona mfano wa wazee wengi waliolitumikia taifa kwa uadilifu mkubwa na uaminifu ambao wengi baada ya kustaafu wanaishia kuwa omba omba ambao watu huwacheka kwa nafasi walizokuwa nazo kutozitumia kwa kuwekeza kwenye maisha ya baadae (Lack of comprehensive social security programs)

5. Viongozi wetu nao ni sehemu ya sisi kutokuwa waaminifu, kwani wao wana-collude na wawekezaji na kuwashawishi wawalipe vijana mshahara wa chini kutokana na maisha kuwa chini tofauti na nchi watokazo wawekezaji. Pia viongozi hao hao hujilimbizia mali mpaka inakuwa siyo siri tena, ambazo ni mali za umma bila kuwajibishwa. Je vijana wafanyeje?

6. Wawekezaji wengi na hasa wahindi ni wanyanyasaji wakubwa wa watanzania wanaofanya kazi kwenye makampuni yao, na kuwafanya watu hao kutokuwa na imani na biashara hizo na kuona ni kama vile haziwahusu kwani hawaaminiki, japo wengine ni waaminifu. Dawa ya mtu asiyekuamini muibie, maana usipofanya hivyo siku akipoteza kwa uzembe wake atasema umemuibia na itakuuma sana, ila kama ni kweli utakuwa na ahueni kuwa kweli nimeiba.

My take: Ni kweli kabisa kuwa uaminifu kazini ni jambo muhimu sana katika kutengeneza mazingira mazuri ya kujipatia mkate wa kila siku. Lakini pia na viongozi wetu kama kina Kapuya wawe mstari wambele katika kujitakasa na wizi wa mali za umma. Viongozi wakiwa waaminifu wataweza misingi mizuri ya social security na kufanya vijana kutokuwa na wasi katika maisha yao baada ya kulitumikia taifa. Vinginevyo "Cat and mouse" game katika sehemu za kazi haitaisha

Mkuu,
Kwa mtazamo wangu we can not compromise maadili kwa maovu. Leo hii kuna untold stories nyingi zikiwemo kupotea kwa sadaka katika makanisa na misikiti yetu, kupotea au kutowafikia misaada watoto yatima. Kwahiyo basi tatizo hili ni la kijamii hasa lipo katika jamii yote ya kitanzania kuanzia katika ngazi ya familia hadi kitaifa. Ni vema tukaangalia ni approach gani itafaa katika kuinusuru jamii ya kitanzania kutoka katika tatizo hili.
Wizi umetanda kila mahali kuanzia majumbani mwetu / katika familia zetu, kwenye mashule na taasisi mbalimbali za elimu, ofisi za serikali na mashirika ya umma, mashirika ya binafsi na yale kigeni, taasisi za kidini, vyama vya siasa, nk. Na wizi huu haufanywi na watu wa tabaka moja bali ni wafanyakazi wa matabaka yote yaani kuanzia juu hadi mtu wa chini kabisa.
Iko haja ya kujadili ukweli na kutoka katika tope hili baya.
 
Mosi; Tuombe tusifike kwenye suala la 'Xenophobia' kama lililotokea mwanzoni mwa mwaka huu huko South Africa maana moto huo ukiwaka kuuzima kwake ni gharama.

Pili; kama wenzangu waliotangulia kusema kwamba samaki anaoza kuanzia kwenye kichwa hiyo ni kweli kabisa mfumo mzima kuanzia juu mpaka chini umelazwa ICU.
 
We acha kabisa. Mimi pia nimegombana sana na vijana wanaouza pale Mlimani City. Wakiona unataka kununua kitu cha thamani kubwa kidogo wanakufuata...oohh boss sasa, tuongee, sisi tunaweza kukupatia kwa bei nzuri na sisi utuangalie. Ukiwauliza kivipi, wanakwambia tutakutolea bila receipt kwa bei chee. Sasa kama mimi nilikuwa nataka kitu cha bei chee si ningeenda Kariakoo, kwani sijui wanapounza bei chee? Ninawaambia nyie vijana ni wajinga hamjui mnalolifanya; huyu mwenye duka akipata hasara kila siku atafunga duka lake na kuliamishia nchi nyingine, na nyie ndiyo mtakaoumia maana mtakosa kazi.

It is really terribly pathetic, yaani roho za watu zimekaa kuibaiba tu. Hili ni tatizo kubwa sana katika nchi yetu, na msingi wake ni watu kupenda vitu vya dezo. Yaani unaweza ukampa mtu kitu cha bure anapokea bila hata kujiuliza kwa nini huyu mtu ananipa hiki kitu. Ile kujua kwamba hiki kitu sio cha kwangu hatuna. Na hili ni tatizo la zaidi ya umaskini. It is something that is increasingly becoming enshrined in our culture. Ndio maana hata maviongozi yetu mengine hayaogopi kutuibia; kumbe yataogopa vipi kama yalianza kuiba tangu yalipokuwa madogo? Jana tulikuwa tunajadili jambo hilihili, kijana moja akasema "kila mtanzania ni mwizi tu, isipokuwa kuna wengine hawajapata nafasi ya kuiba"!!! Nilimkatalia sana, lakini ukitulia kidogo, utaona kwamba kuna ukweli mwingi sana kwenye hii sentensi ya huyu kijana kuliko uongo.

Thanks Kitila kukubali kuwa kauli ya "watanzania karibu wote kuwa wezi"; ila tofauti ni kua wengine ni circumstances inawalazimisha hata wale wasiopenda na wengine based on carrier zao kutoa loophole hiyo.

Vijana wetu si wezi hata kidogo they are victims of circumstances na wewe kama moja wa walezi wa vijana I mean part of the training system you share the blame.

Kwanza nianze na wewe na mimi mara ngapi tumeenda field na kuandika leave of abscence kwamba tutakaa siku kadhaa na kumbe si kweli ili tulipwe zaidi? Huo waona si wizi? Mara ngapi tumetumia muda wetu wa kazi kufanya mambo yetu binafsi badala ya ku concentrate na academic issues ili ku train watoto wa taifa hili vizuri sababu tu carrier inaruhusu kuwa na uhuru mpana wa kujiamulia mambo? Hata kama utabisha ila dhamiri yako itakushitaki kwamba somehow hata na wewe/mimi si bora kuliko hao tunao walaumu na kuwaita wajinga; labda kama hatuko objective na tuna self denial.

Tuacheni lawama zisizo na msingi hasa sisi tunaohusika katika ku shape characters za vijana wa taifa hili ni aibu kwetu sisi wazazi na wenye dhamana ya vijana kwani hiyo ni out put yetu. Hakuna binadamu aliyezaliwa jambazi ila malezi na mazingira ndo yanayozalisha majambazi. Kama malezi ni mabovu na haki ya basic needs haizingatiwi na wenye kubeba majukumu hayo then tunalaumu victims au tujilaumu sisi kwakushindwa kutimiza responsibility zetu?


Social capital ni kitu kinacho kuwa built na kwa taifa makini ni sehemu ambayo ni ya muhimu sana kuangaliwa kuliko capital zote tulizo nazo maana yenyewe ina lubricate matumizi na production ya other capitals. Angalia mitaala yetu ya shule ya msingi ni mingapi inazingatia hili? Je kama wengine waliotangulia kusema viongozi wanatoa mifano gani kwa hata watoto wao achilia mbali vijana wa pembeni wako mbali sana na wao. Leo mzazi anathubutu kumpeleka shule mtoto wake na gari la umma huo ni nini si wizi? Na kipi mtoto anajifunza? Leo mtoto anahitaji service for example fax, papers etc ni wangapi wanawaambia watoto wao leo nikirudi kutoka ofisini nitakuletea so and so? Na okay nipe hiyo document nika ku faxie ofisini; je unajenga nini ndani ya brain ya huyo mtoto na wengine wanao mtazama wale wa maskini wanaona lo mzazi wangu angekua nae officer na mimi ningefaidi na nisinge pata hizi shida; mtoto nae anaona kabarikiwa na angependa kuendelea kupata hizo baraka na neema siku zote za maisha yake na asingependa kukosa kama wale anaowaona hawana wazazi walio barikiwa mwisho wa siku ndo output ya vijana wanaoona mtu kua mwizi ni baraka na si dhambi/kosa kwa maendeleo ya taifa. Maana angalia hizo favour zinazotolewa katika budget za wizara they were not budgeted for; so even if ni kitu kidogo lakini ukijumlisha ndo hivyo resources zinatumika isivyotakikana. Angalia matumizi ya watoto yalivyo makubwa yet unakuta hata mtoto hana age/kazi ya kuwa na hiyo income. Hiyo ingekuwa nafuu kama ni resources tu bali na attitude ya kupenda kupata vitu bila kufanyia kazi. Unashangaa mtoto wa waziri nae anataka treatment za uwaziri; mtoto wa mkurugenzi nae ni assistant mkurugenzi hata anavyo behave kwa officers wa serikali na wakati mwingine wanatoa amri then unategemea huyu akiwa mkubwa atakua democratic na je atakuwa tayari ku occupy offices zisizo kuwa na mianya ya kuiba? Never so hili ni janga la taifa na waziri anaehusika anapaswa kuwa analytical na kukubali responsibility yake ili tuweze kutatua haya matatizo.

Mtoto ukimfundisha kulipia kila huduma asiyo stahili akiwa mkubwa hata thubutu kupenda vya bure inakuwa kama ume m-insult yesi nahapo ndo wenzetu walipotuacha kwa mbali. Mtoto/vijana wa developed countries hwapendi vitu vya bure especially akijua hiyo itanyang'anya uhuru wake.

Just few days a go one of my friend was going home for vacation nikaona ni vizuri ninunulie lunch hapo kwenye restaurant ya chuo, surprisingly akaniambia am willing if I can also buy you lunch tomorrow mpaka nikakubali na yeye akakubali. Lakini nikajifunza kuwa tafsiri ya ile lunch kwake si ukarimu bali naweza kuitumia siku za mbeleni ku m-manipulate kwa vitu asivyovipenda. So si tatzo la vijana bali wazazi na viongozi wa leo waziri akiwa mmoja wapo.
 
Felister:

Nakubaliana kabisa na wewe; tatizo hapa sio them and not us. Ni sisi sote, jamii nzima kwa ujumla. Ndio maana yule kijana akasema kila mtanzania ni mwizi kwa nafasi yake. Tena umetoa mifano mizuri sana, ikwemo hiyo ya kutumia vifaa vya ofisi kwa matumizi binafsi. Ni vizuri kwamba tunaanza kuliona na kulisema hili tatizo. One step ahead already....how far are we prepared to go, is everybody's guess. At the end of the day we need tough laws and tough people to implement them and this is where the leadership comes in. Sote tunawajibika, lakini kuna watu wanawajibika zaidi, na hawa ni wale tuliowakabidhi mamlaka ya kiuongozi. But again tough laws and their enforcement is only one step or only a part of the solution. Hulka, tabia na pengine utamaduni wetu pia una sehemu ya kubadili hili. Sasa chukulia mfano, serikali inatengeneza uwanja mzuri na kuweka vitu vizuri kabisa, watu wanaenda kunya juu ya hivyo vitu, utaacha kuwalaumu na kubaki kulaumu mfumo wa elimu pekee? Surely, it is must be more than mfumo wa elimu!!
 
Felister:

Nakubaliana kabisa na wewe; tatizo hapa sio them and not us. Ni sisi sote, jamii nzima kwa ujumla. Ndio maana yule kijana akasema kila mtanzania ni mwizi kwa nafasi yake. Tena umetoa mifano mizuri sana, ikwemo hiyo ya kutumia vifaa vya ofisi kwa matumizi binafsi. Ni vizuri kwamba tunaanza kuliona na kulisema hili tatizo. One step ahead already....how far are we prepared to go, is everybody's guess. At the end of the day we need tough laws and tough people to implement them and this is where the leadership comes in. Sote tunawajibika, lakini kuna watu wanawajibika zaidi, na hawa ni wale tuliowakabidhi mamlaka ya kiuongozi. But again tough laws and their enforcement is only one step or only a part of the solution. Hulka, tabia na pengine utamaduni wetu pia una sehemu ya kubadili hili. Sasa chukulia mfano, serikali inatengeneza uwanja mzuri na kuweka vitu vizuri kabisa, watu wanaenda kunya juu ya hivyo vitu, utaacha kuwalaumu na kubaki kulaumu mfumo wa elimu pekee? Surely, it is must be more than mfumo wa elimu!!
Kwa kitila na Felister na wengineo, kama nilivyo sema hapo mwanzo tatizo ni la samaki kuoza toka kichwani, na sehemu zingine za maungo kushindwa kukikosoa hiki kichwa, nao ni Wasomi au viongozi iwe wa Serikali au wadini, ndipo utaweza kutatua tatizo la mitaala, na kuwafundisha watoto majumbani mwetu katika level ya familia. Kwa sababu wazazi wengi wanawaeleza watoto wao faida ya kuwa waaminifu, kusoma etc, lakini hizi kauli za wazazi haziwi reinforce mazingira ya nje ya nyumba eg leo hii yanotokea Polisi, mahakamani, makazini na hususana kutoka kwa viongozi, hivyo kunakuwa na tundu moja kubwa ambalo mtu anafikiria huyu mzazi anaweza kiliziba, na Double standard inaanzia kwa viongozi kuwapendelea watu wao katika shughuli nyingi iwe tender, uteuzi wa kazi etc etc, na hata hao polisi wanaishi under pressure ya hao viongozi. sasa ukishashindwa kupingana na mfumo kama huu, ndipo linakuja suala "kama huwezi kupingana nao basi jumuika nao" ndio hapo mtu anaanza tumia faksi ya kazini, etc kutimiza ndoto au kiu yake ya maendeleo. Mfano ni raisi mstaafu Mkapa alipoanza kupindisha mambo kwa faida yake aliwapa nafasi na wengine wafanye hivyo ili kukosekane wakumsema mwingine kwamba mzee hapa mbona umefanya tofauti. hapa ndipo controls zinaanza kuvunjwa na kufanywa, zisiwe na maana. sasa mtu kama huyo anaeweza kumkemea Polisi mla rushwa au hakimu, au Daktari etc etc. Tukitaka kutatua hili tatizo tunatakiwa tutumie Top Down approach , ili awepo atakaye weza kukemea na kusimamia taratibu tulizojiwekea , ambazo zipo, wala hazihitaji miitaala wala nini, hii mambo ya mitaala itakuwa ni kama mbuni kuficha kichwa chake mchangani wakati mwili wote upo exposed.
 
Ni aibu ilioje kumsikia waziri mzima wa serikali ya watu wa Tanzania akijustify kuwanyima Watanzania nafasi za kazi kwa kuwaruhusu wageni kuja na wafanyikazi wao nchini Tanzania kinyume na sheria za kazi nchini. Kama ameamua kuwa waziri wa wawekezaji aseme tujue moja.
 
Felister na Kitila Mkumbo, kuna haja ya kufanya mdahalo wa wazi, tuanzie kwenye vyuo vyetu vikuu ambapo ndo majiko ya viongozi wetu, nadhani haya makampuni hayaongelei vibarua na wahitimu wa veta. yanaongelea viongozi na mameneja ambao kwa namna moja wanatokana na vyuo vyetu. Social Capital na Human capital ni resources muhimu katika kujenga taifa lenye nidhamu ya kazi, kapuya bado hajatoa constractive argument.
 
Felister na Kitila Mkumbo, kuna haja ya kufanya mdahalo wa wazi, tuanzie kwenye vyuo vyetu vikuu ambapo ndo majiko ya viongozi wetu, nadhani haya makampuni hayaongelei vibarua na wahitimu wa veta. yanaongelea viongozi na mameneja ambao kwa namna moja wanatokana na vyuo vyetu. Social Capital na Human capital ni resources muhimu katika kujenga taifa lenye nidhamu ya kazi, kapuya bado hajatoa constractive argument.

Mh!, nimesoma vibaya maelezo ya Kapuya nini?. Ila ukweli ni kwamba whether una elimu au hauna mtanzania wa leo amekuwa na mawazo ya kuiba zaidi ya kufanya kazi kwa bidii ili afanikiwe. Sababu kubwa hasa ni kuwa hard working in Tanzania doesn't reward grip fruits, na hii inatokana na uongozi mbovu wa kutojali hard working for rewards ni ubinafsi tu basi. ni wachache sana wanaoweza fanikiwa kwa kufanya kazi kwa bidii tena wawe na self employment siyo kuajiriwa, majority ya waajiriwa ni wakwapuzi, iwe , Rais wa nchi, Waziri, Manager au hata mmwaga zege.
 
Last edited:
Wote mmekosa jibu sahihi.

1.Tatizo la watanzania sisi hatuna kasumba ya kuumiza akili hili ndilo tatizo kuu,tunapenda kusonteana vidole tatizo linapotokea ,hatuna kasumba ya kulifukuwa tatizo na kulitambuwa mizizi yake iko vipi yatoka wapi hadi wapi na badala yake tunamajibu rahisi sana yasiyo na tija ya kwamba tatizo hili lazima chanzo chake ni fulani.

Ni tabia mbovu tuliojijengea ni sugu iliyonamizizi yake kama mmea wa daikotiledoni ni tabia mbovu na sharti tuiache, Hii tabia ukiangalia ndiyo inapelekea huku kanda ya ziwa kuawa vibibi ya kwamba mtu akifariki lazima kosa lake aangushiwe bibi hata kama mhusika kafa kwa ukimwi.

Tabia hii sasa wasomi wameimodeni kwa kujaribu kukwepa lawama na mzigo wote na makosa yetu binafsi lazima tuyahamishie mahala fulani ama yamesababishwa na mtu fulani .

Kwanza lazima tukili tatizo mama ni wasomi ndilo tatizo na kikwazo kwa maendeleo ya nchi hii,wasomi ndio tatizo wala sio wale wadokozi wanaojaribu kupata angalau mlo kwa kudokoa.
 
Wakuu zangu, Tukubali yaishe kwamba tumevamia Ubepari bila kujipanga kwanza. Kwa mnaosema Kenya hakuna wizi labda hamuijui Kenya..hizi habari za wizi zilianza toka miaka ya 70, tena wao waliuvalia suti na kufika hatua nyingine kabisa ambayo hadi leo hii Wabongo hatujafikia wala hatutafikia kwani sisi bado ni petty theives..Wakenya, na Ogah (WaNigeria) wao wizi upo ktk mifupa yao - Ubepari.

Kwa nini nimefikia kusema ni Ubapari, jamani kumbukeni wakati wa mwalimu wizi haukuwa kiasi hiki. Wizi ulikuwepo kama madhambi mengine.. yaani huweziu kuzuia wizi kabisa lakini sii mfumko huu ulotokea baada ya RUKSA..Kisha basi iweje nchi za Kijamaa hazikuwa na maswala haya hadi siku waliopongia Ubepari..Maanake tukubali kwanza kuwa Ubepari unakuja na mengi matamanio ambayo yahnahitaji fedha..Leo hii unashindwa hata kum trust Ur own father au ndugu yako na kama utafanya hivyo atakumaliza.

Ukisema mishahara mbona kina Lowassa na hao kina Rostam wana mabillionim lakini bado hawtosheki..Wakuu wote wa benki zetu, mashirika yetu wote wanatafuta njia za mkato kujitajirisha na mara zote wizi wao huufanya na Wageni hasa Wahindi kwa sababu tunaamini wahindi wana keep siri.. yaani kuliibia taifa ni sifa moja inayotaka Usiri unaokubalika ktk sheria za mtaani.

Tatizo kubwa la Ubepari ni kujitahadhalisha na GAP inayoweza kuwepo kati ya maskini na Tajiri..Mfumo mzima wa Kibepari hutegemea misingi na nguzo ambazo zinamtazama mtu wa chini kumwezesha kupanda juu afikie kati (middle class) ili mtu huyo kesho awe na uwezo wa kununua mali zinazozalishwa.

Hivyo ndio maana wenzetu walipotaka kuingia Ubepari au walivyoanza walihakikisha wanajenga misingi ya uzalishaji ili kuzalisha AJIRA kwa wananchi wake. na hao wananchi wenye ajira (kazi) ndio customer watakaonunua mali zilizozalishwa ama kuingizwa toka nje.. Tanzania na nchi nyingi tulizovamia Ubepari tulifikiria tu kuwepo kwa vitu madukani...Tukautazama ujamaa kama ni kiwkazo cha kutopata mali safi toka nje hivyo mageuzi yetu yalikuwa kujaza mali madukani. trust me ukimuuliza mdanganyika Ubepari una sifa gani atakwambia vitu vinapatikana madukani..free market na kadhalika bila kuelewa kwamba vitu hivi vimesimama ktk nguzo zinazolenga kutengeneza uwezo wa kununua mali hizo -middle class..Huna middle class mali itanunuliwa na kitu gani hata kama demand na supply zipo..

Leo hii mali zipo kweli lakini wananchi hawana uwezo, gap baina ya masikini na matajiri inazidi kuwa kubwa.. matajiri wetu sii wanunuzi wa mali wala sii wawekezaji ila wezi pia kama sisi..Kila mmoja wetu wala asikudanganye mtu tunataka maisha bora (matanuzi)..Na ndipo jina la Bongoland linapoingia akilini..Nchi ya wezi maanake mwizi siku zote hutumia akili jinsi ya kuiba bila kujulikana na kama itakuja julikana basi iwe too late..
Wakati wa mwalimu na Ujamaa mtu uliogopa kuiba na hata ukiiba unaogopa utazitumia vipi maanake ukijenga watu watashtuka, ukitumia sana utashtukia na zaidi ya hapo hapakuwa na anasa za kusema unaweza hitaji mamillioni..Kwa hiyo watu waliridhika na kidogo walichopata maadam kina cover mahitaji yao madogo madogo..
wakuu zangu sii leo, nachelea kusema karibu kila mtu mwizi na tapeli.. Utake usitake,utaingizwa mjini tu sema wengine kina sisi kuna wakati unakubali kuingizwa mmjini sii kwa sababu wewe mjinga ila unataka kumwondoa mtu huyo kabisa ktk picha ya maisha yako..Mtu akisha kuibia (tapeli) ndio harudi tena na ndipo wewe unapata kupumua..
Kinachosikitisha ni kwamba wizi umekuwa hadi ktk sehemu za kazi, watu wanya wanapopatia riziki..ndio maana mimi husema Watanzania ni maskini wa HALI (elimu, akili) na MALI (utajiri)..vitu hivi viwili haviwezi kabisa kuondolewa na mikakati ya serikali sijui MKUKUTA n.k...tunazidi kujaza maji ktk ndoo ilotoboka..na amini maneno yangu fedha zote zinazoibiwa ni waste kama maji yanayomwagika kwa sababu wezi hawana cha kuinvest - sii wabunifu. Elimu ndogo sana tunaimba kila siku kwamba - Fedha sio msingi wa maendeleo, lakini Wadanganyika watakwambia fedha ni sabuni ya roho!
Hadi wananchi wajue tofauti.. Ajira hazitaweza kuthaminiwa ngazi zote toka serikali hadi wananchi wenyewe...
 
Last edited:
Wawekezaji wanatunyima ajira kutokana na udokozi wetu, tumewapa viongozi wetu dhamana ya kuongoza nchi wakaishia kupora rasirimali zetu kwa kuwa ni wadokozi. Tumrejeshe mkoloni kwa kuwa sisi wote ni wadokozi?
Hayo maneno mzito mkuu, mwenye masikio ya kusikiana asikie. Kama kisingizio cha Kapuya ni hicho wadokozi wakubwa a mali za Watanzania ni kina Kapuya na genge lao.

Teh teh teh teh

Kwa hiyo mnakili kuwa tatizo la ufisadi si tatizo la chama fulani bali ni kwa sisi watanzania wote.

Hapa wamekupa cha kusema mpwa w fisadi GM. Mimi ni Mtanzania lakini siyo fisadi hivyo usiniweke kwenye kundi lenu.
 
Wakuu,
Chondechonde nawaomba tujadili hili tatizo kwa kuzingatia kuwa ni tatizo la kijamii zaidi yakisiasa.

Hebu tuangalie hapo chini, ni malalamiko toka kwa mtanzania wa kawaida ambayo yamepostiwa katika moja ya blogs za kitanzania ndani ya masaa 24 yaliyopita wakati huohuo sisi tuko katikati ya mjadala. Hili tatizo ni kubwa na inawezekana kila baada ya muda mfupi, mtanzania mmoja au mgeni wetu mmoja anakuwa tayari ameshaathirika.


msaada tutani: yale yaleeeeee.....

Anko nanihii ambaye ni mkuu wa
wilaya ya nanihiino na balozi wa nanihii,

Bila kukupoteza muda, naomba unisaidie kupata maoni ya wadau kuhusu swala hili ambalo kwa muda sasa linanisumbua saaaaaaaaana kichwa. Ni kuhusu wizi wa mizigo eapoti ya uwanja wa ndege Dar.

Sijui mimi nina gundu, sijui ndo utaratibu? ila nimechoka.

Mwaka jana June nilienda home kutoka Japan nilikuwa na digital Camera nne,laptop moja, simu za mkononi tatu na vifaa vingine vidogo vya electronics. Hizi zilikuwa ni zawadi kwa ajili ya ndugu zangu kwani ilikuwa ni siku
nyingi sijaenda nyumbani..


Tulivyotua eapoti ya uwanja wa ndege wa Dar, nilishangaa kuona masanduku yangu hayajafungwa. Na ile kufungua nikakuta vitu vyangu vyote havimo! Nikalalamika sana mpaka kwa mkuu wa kitengo cha mizigo nikaambiwa wala hawajaona kitu.

Nikabwaga manyanga...vekesheni yangu yote sikuwa na raha.

Sasa la kusikitisha zaidi, juzi nilikutana na mzungu mmoja raia wa Norway, yeye ni mhadhiri wa wa Chuo. Katika maongezi yetu nikamwambia natokea Tanzania, akasema alikuwa Tanzania mwezi wa tano ila akasema hatasahau safari hiyo, kisa? Akasema aliibiwa vifaa vyake vyote vya electronics alivyofika Eapoti.

Anasema aliumia sana kwani aliibiwa laptop iliyokuwa na information muhimu sana alizotakiwa kupresent kwenye mkutano Tanzania, kidogo achanganyikiwe.

Sasa hapa ndo mambo yananichanganya zaidi, kabla ya kwenda nyumbani nilituma laptop mbili kupitia Express mail, nilitrack mzigo mpaka Dar. Ila zilivyofika Dar. Posta wakasema kwamba hawajapata mzigo wowote na wala hawana information zozote, niliongea na Postal manager Dar. akasema wala wao hawausiki kabisa na kupotea kwa mizigo kwani hawaiwafikii.

Naomba wadau mnipe mawazo, tukisafiri na vitu vyetu wenyewe vinaibiwa na tukisema tuvitume bado vinaibiwa! Besides insurance, nini cha kufanya kuhakikisha unapata mizigo yako kamili?

Na nimefuatilia na watu wa ndege wanasema mizigo haifunguliwa tena mpaka final destination. Tafadhali nimechooka na hii kitu.

Mungu azidi kutubariki
Libeneke lidumu

Mdau Mwenye Usongo
 
yaani uibe usiibe yote sawa tu hakuna atakaye kusifia kwamba jamaa haibi ila utachekwa na machungu ya maisha utayaona wakati wenzio wanapiga dili wanachekelea,ni kuiba tu mwanzo mwisho mpaka kieleweke ukipigwa chini kazi poa unatumia ulizoiba mpaka upate kazi ingine,

Babukijana,
Umekuwa mkweli, japo sikubaliani na fikra kama hizi.
Ni fikra kama hizi zinazofanya waajiri makini kufikiria mara mbili kabla ya kumkabidhi Mtz DAWATI/OFISI nyeti.Nimewahi kukaa kwenye interview panels kadhaa na nimeweza kupata undani unaofanya watz na hasa waliosoma TZ kukosa kazi - Wrong attitudes and Not Necessarily kujua ama kutokujua kiingereza!From the word GO, fikra ni za kuiba.... mtu anauliza ..hii kazi inalipa?Akimaanisha kuna namna na maarifa ya kujikwapulia chochote nje ya utaratibu? Je kuna uwezekano wa ama rushwa au magendo flani?
Najua kuna watakaonishambulia kwa ukweli huu--- ukweli utabaki ukweli hata kama unauma namna gani.Bahati mbaya sana hakuna namna ya ku sugar coat ili kupooza ukweli huo.
Migogoro mingi ya kazi hasa kwenye private sector inatokana na mambo ya kukosa uaminifu na maadili ya kazi.Bahati mbaya kwa mwajiri na nzuri kwa mwajiriwa - sheria za kazi kwa kiasi zililea sana wazembe kwa maana mlolongo mzima ulitoa mianya ya rushwa na hata kumlinda mfanyakazi mbovu. Ni mambo mengi lakini mwisho wa siku Watz jamani tubadilike.
 
Wizi! watanzania hatuna budi tujisahihishe na tubadilike. Sababu yeyote inayotetea wizi haiwezi kuwa na uzito wowote kwa namna yeyote ile. Huu si wakati wa kulalamika na kutafuta visingizio visinvyokuwa na maana, wizi ni mbaya!
Haiwezekani kila mtu anayeajiriwa anafikiria kwanza ni jinsi gani atamfisadi mwajiri wake.
Hawa jamaa wa maofisi ya nje wanataarifa kamili juu ya tabia zetu hizi mbaya na kamwe hawatatoa ajira hata zile ambazo kwa kawaida zinatakiwa ziwe ni kwa ajili ya watanzania.
Tukioneshwa kukerwa na jambo hili na kuweka mijadala ya wazi basi nina imani kuwa imani inaweza kuanza kujengeka baina ya watanzania na hao waajiri wanaotuogopa.

Sema hapana kwa Wezi na tuache Wizi!
 
Wakuu,
Chondechonde nawaomba tujadili hili tatizo kwa kuzingatia kuwa ni tatizo la kijamii zaidi yakisiasa.

Hebu tuangalie hapo chini, ni malalamiko toka kwa mtanzania wa kawaida ambayo yamepostiwa katika moja ya blogs za kitanzania ndani ya masaa 24 yaliyopita wakati huohuo sisi tuko katikati ya mjadala. Hili tatizo ni kubwa na inawezekana kila baada ya muda mfupi, mtanzania mmoja au mgeni wetu mmoja anakuwa tayari ameshaathirika.


msaada tutani: yale yaleeeeee.....

Anko nanihii ambaye ni mkuu wa
wilaya ya nanihiino na balozi wa nanihii,

Bila kukupoteza muda, naomba unisaidie kupata maoni ya wadau kuhusu swala hili ambalo kwa muda sasa linanisumbua saaaaaaaaana kichwa. Ni kuhusu wizi wa mizigo eapoti ya uwanja wa ndege Dar.

Sijui mimi nina gundu, sijui ndo utaratibu? ila nimechoka.

Mwaka jana June nilienda home kutoka Japan nilikuwa na digital Camera nne,laptop moja, simu za mkononi tatu na vifaa vingine vidogo vya electronics. Hizi zilikuwa ni zawadi kwa ajili ya ndugu zangu kwani ilikuwa ni siku
nyingi sijaenda nyumbani..

Tulivyotua eapoti ya uwanja wa ndege wa Dar, nilishangaa kuona masanduku yangu hayajafungwa. Na ile kufungua nikakuta vitu vyangu vyote havimo! Nikalalamika sana mpaka kwa mkuu wa kitengo cha mizigo nikaambiwa wala hawajaona kitu.

Nikabwaga manyanga...vekesheni yangu yote sikuwa na raha.

Sasa la kusikitisha zaidi, juzi nilikutana na mzungu mmoja raia wa Norway, yeye ni mhadhiri wa wa Chuo. Katika maongezi yetu nikamwambia natokea Tanzania, akasema alikuwa Tanzania mwezi wa tano ila akasema hatasahau safari hiyo, kisa? Akasema aliibiwa vifaa vyake vyote vya electronics alivyofika Eapoti.

Anasema aliumia sana kwani aliibiwa laptop iliyokuwa na information muhimu sana alizotakiwa kupresent kwenye mkutano Tanzania, kidogo achanganyikiwe.

Sasa hapa ndo mambo yananichanganya zaidi, kabla ya kwenda nyumbani nilituma laptop mbili kupitia Express mail, nilitrack mzigo mpaka Dar. Ila zilivyofika Dar. Posta wakasema kwamba hawajapata mzigo wowote na wala hawana information zozote, niliongea na Postal manager Dar. akasema wala wao hawausiki kabisa na kupotea kwa mizigo kwani hawaiwafikii.

Naomba wadau mnipe mawazo, tukisafiri na vitu vyetu wenyewe vinaibiwa na tukisema tuvitume bado vinaibiwa! Besides insurance, nini cha kufanya kuhakikisha unapata mizigo yako kamili?

Na nimefuatilia na watu wa ndege wanasema mizigo haifunguliwa tena mpaka final destination. Tafadhali nimechooka na hii kitu.

Mungu azidi kutubariki
Libeneke lidumu

Mdau Mwenye Usongo

Huo mfano hapo juu wala hauna uhalisia wowote. Kuna uthibitisho gani hivyo vitu vilipotelea Tanzania? Mwisho wake mtasema mtu akianzia safari yake TZ akifika mwisho wa safari asione vitu atasema Watanzania wezi.
Bottom line ni kuwa kauli ya kapuya ni ovyo ovyo na ya kipuuzi hataa kama kuna wadokozi.
 
Hayo maneno mzito mkuu, mwenye masikio ya kusikiana asikie. Kama kisingizio cha Kapuya ni hicho wadokozi wakubwa a mali za Watanzania ni kina Kapuya na genge lao.



Hapa wamekupa cha kusema mpwa w fisadi GM. Mimi ni Mtanzania lakini siyo fisadi hivyo usiniweke kwenye kundi lenu.

Huyo fisadi GM ni nani tena si umtaje watu waelewe nani.? teh teh wewe ni fisadi tu ila kama hujafisadi basi hujapata upenyo wa kufisadi.

Kuingilia kwenye europe kama upo yawezekana umefisadi bank statement ya mtu na kuiwakilisha pale ubalozini.Kama umewaza kuuhadaa ubalozi kwa forging unadhani ukipewa nafasi kwenye pesa hutoforge?? teh teh teh

Watu mmepewa mkopo na serikali kwenda kusoma europe lakini wapi bwana mmejificha huko mliko hamtaki kurudisha ama kulipa huo mkopo ,lipeni basi huo mkopo hamtaki unafikiri huo si ufisadi? ukipewa nafasi kwa roho ngumu kama hiyo utazifanyia nini fedha.
 
Last edited:
Huo mfano hapo juu wala hauna uhalisia wowote. Kuna uthibitisho gani hivyo vitu vilipotelea Tanzania? Mwisho wake mtasema mtu akianzia safari yake TZ akifika mwisho wa safari asione vitu atasema Watanzania wezi.
Bottom line ni kuwa kauli ya kapuya ni ovyo ovyo na ya kipuuzi hataa kama kuna wadokozi.

Mkuu,
Si mimi wala wewe ambaye anaweza kukanusha kwamba hakuna wizi katika taasisi zetu kama ambavyo amelalamika huyu ndugu.
Huwezi kuja hapa jamvini na MAJIBU MEPESI yasiyofanyiwa utafiti na ku-make conclusion zako za kisiasa. Sababu ya kuweka bango hilo hapo juu ni kuendelea kuwahabarisha wachangiaji wengine waone jinsi watanzania wa kawaida wanavyopata shida kwa tabia hii mbaya ya wizi.
In the first place huonekani kama tabia ya wizi inakukera hata kidogo, kulikoni mwenzetu?

Hivi kweli wewe unataka mabadiliko ndani ya nchi hii?
 
Babukijana,
Umekuwa mkweli, japo sikubaliani na fikra kama hizi.
Ni fikra kama hizi zinazofanya waajiri makini kufikiria mara mbili kabla ya kumkabidhi Mtz DAWATI/OFISI nyeti.Nimewahi kukaa kwenye interview panels kadhaa na nimeweza kupata undani unaofanya watz na hasa waliosoma TZ kukosa kazi - Wrong attitudes and Not Necessarily kujua ama kutokujua kiingereza!From the word GO, fikra ni za kuiba.... mtu anauliza ..hii kazi inalipa?Akimaanisha kuna namna na maarifa ya kujikwapulia chochote nje ya utaratibu? Je kuna uwezekano wa ama rushwa au magendo flani?
Najua kuna watakaonishambulia kwa ukweli huu--- ukweli utabaki ukweli hata kama unauma namna gani.Bahati mbaya sana hakuna namna ya ku sugar coat ili kupooza ukweli huo.
Migogoro mingi ya kazi hasa kwenye private sector inatokana na mambo ya kukosa uaminifu na maadili ya kazi.Bahati mbaya kwa mwajiri na nzuri kwa mwajiriwa - sheria za kazi kwa kiasi zililea sana wazembe kwa maana mlolongo mzima ulitoa mianya ya rushwa na hata kumlinda mfanyakazi mbovu. Ni mambo mengi lakini mwisho wa siku Watz jamani tubadilike.
kuhusu hili swala ni ngumu sana kwani katika muda huu sidhani kama kuna mtu atakubali kubadilika,nakumbuka kuna kipindi nilipokua tz kuna mahali ilikua baada ya interview lazima ukubaliane na staff wengine kama utakubali kuwa kwenye line yao au utawasaliti?na hii huulizwi kazini wala wapi unaandaliwa paty ya kufa mtu kisha mwisho unapewa ukweli utakataa?na hata pesa ya ulinzi wiki nzima utapewa nawewe umetoka ubaoni utafanyaje?dada mimi nimeona yote hayo kwa miaka 15 niliyofanya kazi na nikaona itafika final nikaamua nikimbie kabla sijazeeka na mungu amenisaidia nimejikomboa,ingawa hata mimi sasa naona machungu ya kuibiwa na kudanganywa na ndugu bongo.
 
Huyo fisadi GM ni nani tena si umtaje watu waelewe nani.? teh teh wewe ni fisadi tu ila kama hujafisadi basi hujapata upenyo wa kufisadi.

Kuingilia kwenye europe kama upo yawezekana umefisadi bank statement ya mtu na kuiwakilisha pale ubalozini.Kama umewaza kuuhadaa ubalozi kwa forging unadhani ukipewa nafasi kwenye pesa hutoforge?? teh teh teh

Watu mmepewa mkopo na serikali kwenda kusoma europe lakini wapi bwana mmejificha huko mliko hamtaki kurudisha ama kulipa huo mkopo ,lipeni basi huo mkopo hamtaki unafikiri huo si ufisadi? ukipewa nafasi kwa roho ngumu kama hiyo utazifanyia nini fedha.

Kuhusu GM gonga hapa; https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...alizotafuna-mama-mongela-bunge-la-afrika.html
Hayo mengine ni kutapatapa tu. Ka kwambia nani kuwa kila anaye changia humu yuko nje? Besides hata kama nimeenda kwa bank statement ya kufoji sijamwibia mtu pesa yeyote. Kuzidi kujichanganya unasema nimepewa mkopo kwenda kusoma nje kitu kinaonyesha ndio njia ulizotumia. Kwa taarifa yako mimi elimu yangu ya mkoloni darasa la nne pale Ikizu na ndio inayonifanya niendeshe maisha.

Mkuu,
Si mimi wala wewe ambaye anaweza kukanusha kwamba hakuna wizi katika taasisi zetu kama ambavyo amelalamika huyu ndugu.
Huwezi kuja hapa jamvini na MAJIBU MEPESI yasiyofanyiwa utafiti na ku-make conclusion zako za kisiasa. Sababu ya kuweka bango hilo hapo juu ni kuendelea kuwahabarisha wachangiaji wengine waone jinsi watanzania wa kawaida wanavyopata shida kwa tabia hii mbaya ya wizi.
In the first place huonekani kama tabia ya wizi inakukera hata kidogo, kulikoni mwenzetu?

Hivi kweli wewe unataka mabadiliko ndani ya nchi hii?

Wewe kweli Punda(milia). Rudia soma tena nilichoandika "hakuna ushahidi kuwa mizigo ile ilipotelea Tanzania." Uvivu wa kufikiri ndo unakufanya ufikie conclusion zako imeibiwa na WTZ. Hakuna mahali nilipokataa kuwa wizi kutokuwepo Tanzania. Huwezi kuniambia ni kerwe na kitu cha kufikirika. Nikubali watu wameiba then what? Huwezi ku-accuse watu kuwa wameiba bila ushahidi hizo zitakuwa sheria za porini. Naelewa uanafuata hizo kwa sababu that is where you belong.
 
Kuhusu GM gonga hapa; https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...alizotafuna-mama-mongela-bunge-la-afrika.html
Hayo mengine ni kutapatapa tu. Ka kwambia nani kuwa kila anaye changia humu yuko nje? Besides hata kama nimeenda kwa bank statement ya kufoji sijamwibia mtu pesa yeyote. Kuzidi kujichanganya unasema nimepewa mkopo kwenda kusoma nje kitu kinaonyesha ndio njia ulizotumia. Kwa taarifa yako mimi elimu yangu ya mkoloni darasa la nne pale Ikizu na ndio inayonifanya niendeshe maisha.



Wewe kweli Punda(milia). Rudia soma tena nilichoandika "hakuna ushahidi kuwa mizigo ile ilipotelea Tanzania." Uvivu wa kufikiri ndo unakufanya ufikie conclusion zako imeibiwa na WTZ. Hakuna mahali nilipokataa kuwa wizi kutokuwepo Tanzania. Huwezi kuniambia ni kerwe na kitu cha kufikirika. Nikubali watu wameiba then what? Huwezi ku-accuse watu kuwa wameiba bila ushahidi hizo zitakuwa sheria za porini. Naelewa uanafuata hizo kwa sababu that is where you belong.

Mkuu,
Angalia mambo kwa undani zaidi na usiendelee kufanya hizo conclusions zako kwa kuendelea kutoa MAJIBU MEPESI-MEPESI yasiyokuwa na tija.
Kama nilivyosema hapo awali malalamiko juu ya wizi katika viwanja vya ndege na Posta hapa Tanzania yapo mengi sana. Leo hii mzigo unasafirishwa baina ya miji yetu hapahapa Tanzania bado vitu vinapotea. Nenda Lost and Found offices za Swissport pale uwanja wa ndege wa JKN, malalamiko ni ya kila siku na wafanyakazi kadhaa wamekwisha kamatwa kuhusiana na matukio ya wizi pale. Nenda Posta, hali si nzuri kabisa vifurushi na vitu vingine vinaibwa. Nataka tujadili hali hii na kuona athari zake katika level ya chini kabisa inayomhusisha mwananchi wa kawaida. hakuna haja ya kutafuta mchawi ilhali haya matatizo yana ushuhuda mbalimbali kama ule nilioubandika hapo juu. Hatuwezi kuchanganya mambo kwa nia ya kutaka kukwepa ukweli, katika tatizo hili viongozi wana nafasi yao kamawao na sisi wananchi wa kawaida ambao ndiyo walengwa wa mwisho wa mfumo wowote ule tuna sehemu yetu ya kuweka haya mambo sawa.
Ninakerwa sana na hii tabia ya udokozi-dokozi mahali popote hasa sehemu za kazi.
 
Back
Top Bottom