Udom udom udom


Ndugu UDOM bado wachanga aisee, usiwalinganishe na UDSM,SUA, MUHAS au MZUMBE, wao bado mambo hayaja settle vizuri, utawafurahia baada ya miaka kadhaa ijayo.
 
Ndugu UDOM bado wachanga aisee, usiwalinganishe na UDSM,SUA, MUHAS au MZUMBE, wao bado mambo hayaja settle vizuri, utawafurahia baada ya miaka kadhaa ijayo.

!
!
nimeanza kuelewa angalau, ila kwa sasa kwa hali ilivyo na hizi intake zetu za kutaka kujaza majengo na hawa wanafunzi wa kizazi hichi? lets see, time will tell
 

!
!
kilo moja ya sukari haibadilishi ladha ya maji ya bahari.
 

am sorry mkuu but u have no idea about udom is all about siasa na udini
 
Am sorry mkuu unaijua udom kweli?
 
MLETA maada unawazo zuri lakini wazo lako limekosa ushahidi/research ya kisomi. Chuo kikuu cha Dodoma ni kweli kimekusanya watu wenye elimu ya kiwango cha juu sana na wenye upeo wa hali ya juu katika kutizama mambo kwa upana wake na urefu. Wapo ma Professer, madoctor, maphd holders,n.k na hawa wote wanashiriki kwa nafasi zao katika kuzungumzia mambo mbalimbali inayohusu taifa letu kwa ujumla. Wanatoa maoni yao sehemu mbalimbali ikiwemo Makongamano, warsha,seminars, vyombo vya habari vingi tu vyakutosha Tanzania. Sasa wewe kama huwasikii ni bora ungejisemea nafsi yako kuliko kufanya inference without any scientific research for your argument. Unaporukia kwenye conclusion bila research ni dalili pia za kuonyesha wewe ni msomi/uelewana wako ni wa aina gani. Dhana ya Dodoma University kuwa chuo cha kata ni dhana ambayo wengi mnaimba kila siku bila kujua what are you saying. Kwakuwa hata nikikuhoji ni nini kinaifanya Udom kuwa chuo cha kata na ili chuo kiwe cha kata kina sifa gani wengi hamna majibu zaidi ya kurukaruka kama mmekanyaga siafu. DHANA ya kuwa Udom ni chuo cha kata imejengwa na watu wenye akili zao hasa kwa malengo ya kupotosha wasiochukua muda wao kufikiria yasemwayo hasa vijana wanaohitimu A level na collegus mbalimbali na wanaoitaji kujiunga na elimu ya juu. Lengo ni kutengeneza soko la vyuo vyao ambavyo kimsingi kusoma katika vyuo hivyo hata ukiwa 100% ya mkopo still maisha yako kama mwanafunzi yatakuwa tofauti na mwanafunzi wa udom. Hii ni kwasababu hasa ya miundombinu mizuri iliyopo chuo kikuu cha Dodoma. Pia intake ya chuo kile kwa taarifa tu kikikamilika uzuri per year kinaweza kupokea wanafunzi elfu kumi natano 15000 na chuo kizima kuwa na jumla ya wanafunzi elfu arubaini (40000) wote wakiwa wanapata kila mmoja malazi palepale. Takwimu hii ni hatari sana kwa ustawi wa vyuo vingine hasa vya private kwani kuna uwezekana wanao apply wasiombe kabisa vyuo hivyo. Mimi hii kwangu ni hoja dhaifu kwani Tcu kwa sasa andio taasisi inayowajibika kupangia vyuo wanafunzi na sio matakwa pekee ya wanafunzi. Kifupi chuo kile kama hujuma hazitoendelea kufanyika ili kisifanikiwe malengo yake few years ahead kitakuwa si kuwa ni bora tu Tanzania bali na Afrika kwa ujumla. Kuna hujuma nyingi sana nazijua kinafanyiwa UDOM lakini leo nadhani itatosha. Nawakumbusha tu kwamba Udom before 2015 Hospitali bora zaidi ya muhimbili itakuwa imefunguliwa ndani ya chuo hicho. Magonjwa yanayotibiwa India km Moyo yatatolewa huduma zako chuo kikuu cha dodoma. Nalo hili lina maelezo yake yanayopelekea kupakwa matope yasiostahili.
 
!
!
samahani lakini,ila wawakilishi wenu huku mtaani ni majanga. Nilikuwa na demu wangu huko,na yeye duh kumkichwa ni sifuri ila nae kahitimu eti. Dah......hivi wanafundishaje pale!au mitihani hakuna imefutwa?mh

wewe kichaa wewe acha kubeza vyuo vya watu! Enhe nyie mliosoma kwenye vyuo unavyojua ni vvya maana mmetufanyia nn ktk taifa hili zaidi ya ufisadi?huu uzandiki,upuuzi,uchafu,makapi na aina zoote za usaha peleka kwa demu wako siyo hapa!vijana acheni madharau ya kiji..nga
 

Hujui hata kudanganya kaka
Udom intake ya kwanza tumeingia 2007 kabla hata haijajengwa
 

Kaka ulisoma udom? Au umetumwa kukitetea hata kinapo onekana kutoenda sawa? Mimi nimesoma pale udom tena education Ninacho kisema ni kitu cha kujionea sio wewe unae ambiwa!! Udom pia ina udini, u chama na ukabila kama ulikuwa hujui fanya utafiti. Kwa sasa udini umepanda pale kama bei ya luku. Pia ukabila uko juu kama mfumuko wa bei. Nyumba usio lala hujui yaliyomo, uliza wanao soma pale utapata majibu. Sio kutetea upuuzi. Ungejua pesa za watanzania nyingi zimepotea kujenga udom! Hadi sasa bajeti ya udom haijawahi kusomwa bungeni kuwa ni trion ngapi, watu wanakiharibu wewe unakuja kuweka siasa hapa! Acha utoto ndugu kuwa mzarendo!
 
Inasikitisha vijana wadogo mnajadili vitu vikubwa msivyovijua, kazi za university..Academics-Teaching, Research and Consultance, hamfikilii kuhusu academic institutional credibility hufikiwa kwa vigezo gani, staffing credentials, years and quality of academic, research conducted and consultancy. Msiwe wepesi kuhukumu UDOM kwa muda huu, mnafanya reference ya UDSM wakati hiyo credibility imepatikana in years of operation.
 


Unajifhalilisha we kanjanja maana huyo kaka yako kasoma form 1-6 hajui kuandika barua?? Ina maana alitegemea barua akajifunzie kuandika chuoni?? Hilo Ni janga
 

Nyerere kitu gani bhana inchi imepata uhuru miaka zaidi ya 50 iliyopita na yeye katawala nusu yake nchi bado masikini ptuuuu
 

Wewe uliye fanya research na credibility zako fanya research ya kukua kwa udini udom au kwa kuwa kiko karibu na pwani? Why not Udsm neither Sua? Fanya credibility zako sasa! Tambua kwamba wasomi wetu hujifanya kila kitu wanajua wao kwa kuwa wana vyeti vingi. Ukiuliza mbona umeme unapaa kila siku utaletewa maneno mengi ya kisayansi mara running costs, mara maintainance costs, mara water supply in power dams na mengine mengi ili mradi utapeli tu. Ndio maana Idi amini dada hakujali usomi wa mtu yeye alijali accountability.
 
Nashangaa watu badala ya kuwajadili wahadhiri kama mada ilivyo, wanajadili wahitimu! Jamani graduate anaweza akafanya mambo ya hovyo au mazuri, hiyo inategem,eana na yeye pia, sio lazima iwe imesababishwa na chuo chake. Mbona Mwigulu hakuna kitu?
 
Unajifhalilisha we kanjanja maana huyo kaka yako kasoma form 1-6 hajui kuandika barua?? Ina maana alitegemea barua akajifunzie kuandika chuoni?? Hilo Ni janga

!
!
utakuwa ama umemaliza udom, au bado unasoma katika hiyo sekondari
 
Chuo kikuu hakifundishi kuandika barua. Mm nimesoma udom niko vizuri tu and am proud of it.
Kama ulipita huko chini kimagumashi usitegemee udom ikafundishe namna ya kuandika barua. Wao watakuelekeza namna na ya kupambana na kuyakabili mazingira. Kuamua na kufikiri kitunduizi.
Ukilaza wa mtu hautokani na chuo alichosoma wapo waliosoma udsm, Makerere lakini kichwani hakuna kitu. Kuna waliosoma IFM wako vizuri mno lakini wengine hawajui hata tanzania ina mikoa mingapi.
Udom ina matatizo kama ilivyo kwa vyuo vingine vya serikali lakini si kama wahuni wachache ambao wanajiona wako vizuri kichwani ili hali maisha yao yako sifuri. Umesoma chuo bora sawa, je elimu yake imekusaidiaje au ndio walewale wa kutembea na bahasha posta na kuilaumu serikali?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…