UDSM kuwafukuza wanafunzi wake, Mkandala afafanua

Mwanajamii

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2008
Posts
7,063
Reaction score
70
Makamu mkuu wa chuo kikuu cha dsm sehemu ya mlimani Prof Mkandala anafafanua A to Z ndani ya udsm kuhusu kufukuzwa kwa wanafunzi 60.Anasema waliofukuzwa watapewa haki yao ya msingi kusikilizwa.

Source.USIKU wa habari Tbc saa 4 usiku.
 
anasema uamuzi wa kuwatimua ulifanywa na bodi ya chuo sio na mtu mmoja.makundi yote wadau wa elimu hususan ya chuo kikuu wameshirikishwa ipasavyo ikiwemo serikali ya wanafunzi
 
Nimemsikiliza kwa makini hawa wanafunzi walikurupuka katika maamuzi yao sheria haitawa favour na ndo ushangae mi nimesomea hapo udsm sio siri kuna kasumba ya migomo ya kijinga sometimes na sasa uanaharakati eti kila mwanachuo mlimani ni mwanaharakati uharo mtupu
 

Nawe ni gamba tu huna lolote! Mkandara ni mwanasiasa! Huwezi ku-jump into conclusion kwa kusikiliza maelezo ya huyo dictator wa chuo anayefanyakazi ya kulipa fadhila kwa bosi wake ******!! Hata mimi nimesoma chuo! Migomo yote huwa ina sababu za msingi.
 
Daima kama ni mvivu wa kufikiri daima hata utatachotoa kitakuwa hakina mashiko kama ulisoma UD kwanini unafikia kuhukumu au ndio wale wale wa Madesa tu
 
wasomi hawasikilizi upande mmoja na kutoa hukumu kwahiyo unaweza kuwa kweli umesoma chuo kikuu lakini ukawa kama watanzania wengine waliosoma lakini hawajaelimika.
 
Wewe ndiyo akili yako "Uharo mtupu"
 

Siamini kuwa umesoma chuo kikuu wewe kama hii ndio conclusion yako. Labda utuambie umepitia chuo kikuu na kama una vyeti basi ni vya madesa na mig. Or maybe even vya chupi.
 
Mi nadhani Wa - TZ hasa wanaojiita wasomi wabadilike, ukitazama tangu mwanzo sababu iliyowafanya wagome haikuwa ya msingi, fedha hakuna, serikali imekopa huko duniani mpaka muda huu tunatukanwa hovyo hovyo, rejea matusi ya Ehud Barak wa Israel, David Cameron wa Uingereza na hata ripoti za karibuni zinzoonesha kwamba tunashika nafasi ya tatu kwa kusaidiwa Duniani ukiacha Iraq na Afganistani na bado wasomi hao hao waligoma na kuongezewa posho at their counterparts expenses ya kukosa masomo!! Sasa wasaidiweje hawa, hatuwezi kuwa na taasisi au nchi katika mawanda mapana ambayo viongozi wake hawana mamlaka. My take wale 43 waliofukuzwa mwanzo na ambao kesi zao bado zinaendelea ni sawa, hawa walioongoza ujinga eti mgomo wa amani na kufukuzwa jana ni sawa na wale waliosimamishwa wakibainika kufanya makosa wafukuzwe katika terms zile zile. Mi namshauri Makamu Mkuu wa chuo wa ukweli Prof. Mukandala kama kuna wengine watakaogoma fukuza kabisa baba! bakiza wanafunzi walio tayari kufanye UE tu ambao wanajua wamefata nini hapo chuoni.
 
inasikitisha sana kuona kijana aliefikia level ya chuo kikuu anakatishwa katikati bila kumalizia masomo ili afikie malengo yake ya kujikomboa kimaisha na pia kulisaidia taifa lake.wengi wa wanaosoma katika vyuo vyetu hapa nchini nji watoto wa walalahoi masikini wa kutupwa.nadhani chuo kitumie busara hawa jamaa wamalize masomo.wanafunzi pia watumie busara kufikisha malalamiko yao na kutatua matatizo yao.siku zote fahari wawili hawakai zizi moja.wapiganao.........ziumiazo ni nyasi.tunaoumia ni sisi walipa kodi.
 
k ni . . Na zenu Hayawahusu pigeni kimya Wa nge Nyie Mngejua inavouma kutimuliwa chuo akati mtu ame fanya duty under official Capacity
 

mi sio gamba wala nini..back to the topic hivi hayo maamuzi ya baraza la chuo raisi wa Daruso na makamu wake wamehudhuria na wakayaafiki 2. Ili mgomo utokee sheria mpya yasema lazima ifanyike referandum vote kwa wanachuo wote ili kuupitisha uwe legitimate na vp ilifanyika juhud yeyote juu ya hili? Na kuna watu nawajua wanataka chuo kifungwe ili iweje? Na kugoma sio kila kitu wagoma goma! Mnakoma kama mkifukuzwa sijui utalia na mzaz wako? Fuata taratibu hata mkigoma inakuwa strong? Alafu jiulizeni miaka yote matatizo ya wanafunzi yanazaa migomo muda mfupi kabla ya UE? nadhani siasa iache kuwatumia hawa vijana
 
Siamini kuwa umesoma chuo kikuu wewe kama hii ndio conclusion yako. Labda utuambie umepitia chuo kikuu na kama una vyeti basi ni vya madesa na mig. Or maybe even vya chupi.

we wadhani bila madesa utafaulu? Chupi umevua mwenyewe
 
Daima kama ni mvivu wa kufikiri daima hata utatachotoa kitakuwa hakina mashiko kama ulisoma UD kwanini unafikia kuhukumu au ndio wale wale wa Madesa tu

we wadhani sijui wanachodai ni haki? Tatizo hawajafuata utaratibu na raisi wao kapitisha maamuzi hayo katika baraza la chuo..big mistake iko hapo
 

safi mkuu..unajua ukifika UDSM unajiona mwanaharakati sana na unajiona unajua kuliko mtu mwingine yeyote na mkiwa peer group ni mgomo au kunji tu...sasa kumwagia maji maprof ndo nini? Kuwatimua watu cafeteria ndo nini? Uharo mtupu..
 

mkubwa mi si mshabiki wa wanaogoma, ila sasa chukulia wale waliotoka kanyigu-bukoba kwa mfano (ambao wazazi wao hoi bin taaban kiuwezo) na wapo kwenye list ya kupata boom ya bodi na hawajapewa chao na masomo yanaendelea, wapo chuoni, wamekopa weeee mpaka wamefikia limit ya kukopa na sasa hawana hata sumni ya kula hao unawaambia wafanye nini? mana wakigoma nyumbani...hebu tupe njia mbadala kwa baadae tujue
 
Wewe ndiyo akili yako "Uharo mtupu"

Afu mijitu mingine inatia hasira we kama hujui chanzo na udikteta unaofanywa hapa c ukae kimya? Ndiyo ulisoma hapa huoni wakati wenu na sasa mambo yamebadilika?
COMMON SENSE ARE NOT WORKING NOW DAYS.
 
Matatizo mengi yanayopelekea migomo chuoni yanatokana na serikali kuzembea kwa kiasi fulani au kutanguliza usiri katika haki za wanafunzi hasa unapofika muda wa utekelezaji.

Ni wazi serikali yetu imefulia basi iache usiri iwaambie wanachuo wavute subira kidoga na ingewaafutia kesi hao wanafunzi ambao walikamatwa katika maandamano ya awali.

Mbona nchi za wenzetu hakuna migomo kama hii ya UDSM? Kuna kipindi nafikiri kumpeleka mwanao UD ni kupoteza muda kutokana na ngimbila zisizokwisha.
 
Afu mijitu mingine inatia hasira we kama hujui chanzo na udikteta unaofanywa hapa c ukae kimya? Ndiyo ulisoma hapa huoni wakati wenu na sasa mambo yamebadilika?
COMMON SENSE ARE NOT WORKING NOW DAYS.

njia mliotumia kawa saliti presidaa wenu wa daruso mngedeal nae kwanza huyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…