UDSM: Tunaomba msaada wenu JF!

UDSM: Tunaomba msaada wenu JF!

But was all this force really necessary? Maybe hapa ndipo tunapaswa kujadili kidogo; tabia ya polisi ya kutumia mabavu kwa wananchi wanyonge na wasio na silaha zozote. It is unbecoming and a very uncivilised way of handling problems! Halafu tunategemea hawa wanafunzi baadaye wakiwa viongozi waheshimu misingi ya demokrasia ya uhuru wa kujieleza, kukusanyika, kuandamana, etc?

Asante Kitila,

Hili ndilo mimi napigania hapa. Hawa wanafunzi wananyimwa haki yao ya kuchagua viongozi wao kwa mujibu wa katiba zao. Wakigoma au kufanya shinikizo, wanakamatwa, wanapigwa kwa excessive force na mengine mengi.

Tunategemea kujenga taifa la namna gani?

Wanafunzi wa UD, poleni sana kwa mnayopata lakini mnachopigania si bure. Watanzania wote wangekuwa na moyo kama huu basi leo hii tusingekuwa na Buzwagi, Richmonduli, vijisenti, kula nyasi, na mengine mengi.
 
Poleni sana, mgomo mwisho wake huwa haya. I hope hakuna aliyeumia zaidi ya kulia. Ndio kupata haki, mara zote hupiganiwa inapobidi.

Bwana Waga hivi hao viongozi waliosimamishwa masomo walifanya vitendo vya kihalifu kiukweli au wanasingiziwa? Je Serikali ya wanafunzi ili ubariki huu mgomo wa leo? Kama hawakubariki mgomo ndio kusema kuwa hao viongozi ni wasaliti au wanakubali kuwa wanafunzi waliosimamishwa masomo walipaswa kusimamishwa? Bado nina maswali mengi kuliko majibu

Hakuna uhalifu wowote waliofanya zaidi ya kudai haki zao. Msingi wa mgomo huu ni uongozi wa chuo kuingilia demokrasia ya wanafunzi wasomi kuchagua viongozi wao.

Huu ni uzembe na upuuuzi wa hali ya juu sana!
 
Tafadhali mama Na Dada pataneni.

Maanake mkitofautiana sana ndani hapanogi,lakini najua ni tofauti kwenye hoja tu.

Huyo mkandala ni kibaraka.Kwanza unajua CCM wanamtumia mkandala ili kuepuka challenge kutoka kwa wasomi. Hata kama mtawakandamiza walioko hapo UDSM inabidi mjue mna shughuli pevu kukabiliana na pressure kutoka nje.

Jengeni hoja za nguvu kisha anzisheni movement kubwa ya amani. Hizo siku mbili mlizogoma kama madai yenu hayatasikilizwa muongeze ziwe siku tanao huku mkishinikiza kuwa ndani ya siku tano msiposikilizwa mtachukua hatua kali zaidi ya hizo ili liwe ni suala serious la kitaifa mtaungwa mkono na makundi mbali mbali ya jamii na hapo ndipo umma utambue pia mkandala ni mtu anaetishia uhai wa kisima cha fikra Tanzania

Mkuu Ben,

Hakuna ugomvi wowote kati yangu na mama. Mama ni mmoja wa memba wanaoheshimika sana hapa forum. Imekuwa tu yeye yuko upande wa kina Mkandala kwenye hii case na mimi niko upande wa wanafunzi.
 
It is not that simple Mamkwe. Binadamu haishi kwa mkate tu!
Kitila, wewe umeshawahi kujinyima kipande chako cha mkate na kumpa unayedhani kuwa ana njaa kisha akautia mchanga? Kama uliwahi kukutwa na hayo ulijisikiaje?

Nina uchungu sana, mjukuu wangu yupo mwaka wa tatu, mitihani kanambia wataanza wiki mbili zijazo, kisha akifukuzwa inakuwaje? Nihangaike tena?

Mjukuu wangu huyu nimehangaika naye tangu vidudu, nimemsomesha, kesho kutwa naiona digrii hile, halafu alete ujinga?

Kuna rafiki yake Aggy kanipigia simu sasa hivi anasema huko polisi wanarusha mabomu na kuwa watu wameumia. Na huyu aggy hajui alipo. Hapa nilipo tumbo linawaka moto. Aggy mjukuu wangu hana simu.
 
Hakuna uhalifu wowote waliofanya zaidi ya kudai haki zao. Msingi wa mgomo huu ni uongozi wa chuo kuingilia demokrasia ya wanafunzi wasomi kuchagua viongozi wao.

Huu ni uzembe na upuuuzi wa hali ya juu sana!

Na kibaya zaidi wasomi wazima ma (prof) kujifanya mdebwedo
 
Mlimani pamechafuka sana na huo ni ukweli ila kitendo hiki kitakiweka chuo kwenye mazingira ya kufungwa.

Vijana wa uhandisi wameamua kujiunga rasmi kwenye maandamano ya leo na hapo ndio polisi waliitwa kuja chuoni ila bado wanajipanga kama nilivyosema jana .
 
Migomo mingi sana ya mlimani inafanikiwa
Kama kuna migomo mingi iliyokwisha fanikiwa ni vema wakarudia kwenye makablasha ya migomo hiyo ili kuweza kupata mbinu zilizo tumia. Kwani hadi sasa JF imeshindwa kutoa njia ya kuweza kufanikisha mgomo wao.

Wanafunzi wa UD, poleni sana kwa mnayopata lakini mnachopigania si bure. Watanzania wote wangekuwa na moyo kama huu basi leo hii tusingekuwa na Buzwagi, Richmonduli, vijisenti, kula nyasi, na mengine mengi.

Wanamlimani kwa kauli yako ya pale juu wamekuwa wakishinda migomo mingi, na huu sio wa kwanza, hivyo kuna idadi kubwa kabisa ya waliopitia mlimani ambao wapo mitaani na bado kuna skandari nyingi tu...!
 
Hakuna uhalifu wowote waliofanya zaidi ya kudai haki zao. Msingi wa mgomo huu ni uongozi wa chuo kuingilia demokrasia ya wanafunzi wasomi kuchagua viongozi wao.

Huu ni uzembe na upuuuzi wa hali ya juu sana!

Hilo la uongozi wa chuo nalielewa, au kwa vile ni Mtatiro yumo basi nisihoji chochote. Sitaki malumbano period!
 
Mimi kwa upande wangu hawa wanafunzi wa Chuo kikuu wa karne hii ni mabishoo waliojaa ubinafsi. Kuna ishu chungu nzima zinazogusa mustakabali wa nchi hii lakini hukuti hata siku moja wakizichambua na kuzitolea matatamko.

Wao kama wasomi wanaotegemewa na Taifa kuwa viongozi na watendaji, wanawajibu wa kuyachambua mambo muhimu kwa taifa hili kwa niaba ya watanzania wao ambao hawakupata nafasi hiyo. Hivi hawafahamu kuwa wakulima masikini wanawategemea wao kuwasaidia katika kuikosoa serikali kwa mambo mengi ya kijinga inayofanya??

Inanitia kinyaa kuona muda wote wapo kimya na wanapoona masuala yao yameguswa ndio wanaomba msaada kwa watanzania.

Mkuu nyangumi,

Hawa vijana wamekuwa wanatoa matamko mengi tu hapa kuhusu hali ya ufisadi inayoendelea Tanzania. Huyu kijana Mtatiro ni very active kwenye masuala ya nchi na serikali ya ccm haimpendi na hata waziri wa elimu ya juu ameonyesha hilo.

Ni very wrong kusema kuwa hawa ni mabishoo na kuwa hawajali hali ya nchi wakati ukweli umeonyesha kuwa ni vijana wanajali hali ya nchi yao hata pamoja na mazingira magumu wanayosomea.
 
Mlimani pamechafuka sana na huo ni ukweli ila kitendo hiki kitakiweka chuo kwenye mazingira ya kufungwa.

Vijana wa uhandisi wameamua kujiunga rasmi kwenye maandamano ya leo na hapo ndio polisi waliitwa kuja chuoni ila bado wanajipanga kama nilivyosema jana .


Utawala unawaogopa sana maengineer, unajua wakiingia hao jamaa moto wao si wa kipole pole.
 
Hakuna uhalifu wowote waliofanya zaidi ya kudai haki zao. Msingi wa mgomo huu ni uongozi wa chuo kuingilia demokrasia ya wanafunzi wasomi kuchagua viongozi wao.

Huu ni uzembe na upuuuzi wa hali ya juu sana!

Nakubaliana na wewe, dada! Tatizo ni kwamba UDSM kwa miaka mingi imekuwa politicized na itaendelea kuwa hivyo kutokana na kuwa:
1. Wanafunzi na vijana wasomi kwa kawaida hupenda sana masuala ya siasa na wanajaribu ku-apply wanayoyafunza darasani including democracy
2. CCMi litambua mapema kuwa chanzo cha dissent duniani ni kwa vijana hususan wanavyuo, kwa hiyo imekuwa ikifanya jitihada makusudi kuhakikisha kuwa wanaingilia uongozi wa wanafunzi. Ndiyo maana kila baada ya miaka kadhaa wanafunzi hutimuliwa (hata akina Sitta walitimuliwa!)

Lakini hii ya leo kuleta FFU naona ni TOO MUCH! Hao wanafunzi walikuwa wanatishia vipi amani? Labda tuendelee kupata habari.
 
Kitila, wewe umeshawahi kujinyima kipande chako cha mkate na kumpa unayedhani kuwa ana njaa kisha akautia mchanga? Kama uliwahi kukutwa na hayo ulijisikiaje?

Nina uchungu sana, mjukuu wangu yupo mwaka wa tatu, mitihani kanambia wataanza wiki mbili zijazo, kisha akifukuzwa inakuwaje? Nihangaike tena?

Mjukuu wangu huyu nimehangaika naye tangu vidudu, nimemsomesha, kesho kutwa naiona digrii hile, halafu alete ujinga?

Kuna rafiki yake Aggy kanipigia simu sasa hivi anasema huko polisi wanarusha mabomu na kuwa watu wameumia. Na huyu aggy hajui alipo. Hapa nilipo tumbo linawaka moto. Aggy mjukuu wangu hana simu.

Mjukuu wako akijiangalia peke yake atakuwa mbinafsi wa hali ya juu. Kumbuka aliyevujisha siri za serikali hapa JF naye alikuwa anafikiria kuwa anaweza kukamatwa na akawekwa ndani na familia yake ikapata shida.

But you know what, alivujisha mikataba na siri za serikali anyway kwa sababu kwake huyo, maisha ya watanzania wote ni muhimu zaidi kuliko yeye binaafsi.

Angekuwa mbinafsi, angekaa kimya ili kulinda kibarua chake. Unajua kuwa kuna watu wanafuatiliwa benki ya posta kwa vile wamevujisha siri za ufisadi huko? Hawa wangekuwa na mawazo kama yako wangekaa kimyaaaaaaaa
 
Kuna mtu kanitumia email akini-update na hali ilivyo chuo; inaonekana hali sio shwari. Ni kama vita. I am surprised and shocked maana sijasikia cha kutisha walichofanya hawa wanafunzi hadi waletewe polisi wenye masilaha yote haya. It looks lile the leadership failure in our country is right across the board! Herebelow I share with you some few phrases from the email I received.

242 said:
"Kitila, chuo leo tumeingiliwa na FFU na mabomu ya machozi na bunduki. Nakuambia watu wengine wamezimia na kukimbizwa hospitali na ninasikia wengine wamevunjika miguu kwenye harakati za kukimbizwa. Mpaka sasa wako campus ni fujo tupu. Wengi wetu tumejifungia maofisini. Ilikuwa tishio kama vile tuko Irag. Chuo kilitetemeshwa na mabomu, wewe acha tu. Nasubiri kidogo nione kama nitaweza kukimbilia nyumbani. Kitila, sijui tunakoenda lakini ni aibu kwetu kabisa. Lazima tujirekebishe na kuthamini mawazo ya watu wengine hata kama ni maskini au watoto. We cannot develp critical thinking if we want to feed our children with what we want. Tuombeeni."
 
Mlimani pamechafuka sana na huo ni ukweli ila kitendo hiki kitakiweka chuo kwenye mazingira ya kufungwa.

Vijana wa uhandisi wameamua kujiunga rasmi kwenye maandamano ya leo na hapo ndio polisi waliitwa kuja chuoni ila bado wanajipanga kama nilivyosema jana .

Kwa hiyo ile kitu inaitwa Kunji au FoE spirit bado kipo??
 
Hilo la uongozi wa chuo nalielewa, au kwa vile ni Mtatiro yumo basi nisihoji chochote. Sitaki malumbano period!

Hakuna malumbano mama, unaweza kuhoji chochote unachopenda na ukapata majibu kama kawa ya JF. Ukipata majibu yako basi usiyachukulie kama malumbano. Okay?
 
Back
Top Bottom