UDSM: Tunaomba msaada wenu JF!

UDSM: Tunaomba msaada wenu JF!

Unajaribu kuifanya hii ni issue ya siasa lakini huna point. Kwanini Sokoine na vyuo vingine hawagomi?? je hawanamatatizo??. Hii siyo siasa na hutapata watu hapa kwani watu hapa siyo mashabiki bali ni watu wenye uchungu na nchi. Mwafrica huna point na wanachuo wa USDM wana utoto bado na hawajui maisha.

Kwa wale tulioko marekani tumeshuhudia namna vijana wa vyuo vikuu walivyoendesha kampeni ya Obama kwa mafanikio makubwa.

Hili ni swala la kisiasa maana uongozi wa chuo umeingilia haki ya wanafunzi kuchagua viongozi wao kidemokrasia na kisha kutumia vyombo vya dola kama polisi, mahakama na jela kuwanyanyasa.

Kama hukujua kuwa hii ni siasa, just watch this space.

Huyu Muuaji, dikiteta na fisadi (ambaye pia ni mshauri wa serikali ya kifisadi) Mukandala lazima atapata share yake hapa JF
 
Hivi kweli Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na Serikali wameshindwa kabisa:

a. Kutafuta suluhisho la kudumu kuhusu maji?

b. Suluhisho la kudumu kuhusu Mikopo

c. Suluhisho la kudumu kuhusu malazi na miundo mbinu mingine hapo

d. Suluhisho la kudumu la kuwashirikisha wanafunzi katika maamuzi yatakayowaathiri?

e. Kutafuta washauri (councillors) ili kuwasaidia hawa vijana ambao ndio wametoka kwenye balehe na wanaingia kwenye utu uzima ili nguvu (energy) waliyonayo iwe constructive? Kwanini nguvu yao ipotezwe kwenye mambo negative kama haya?

Hivi Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam kina wasomi wenye kutatua matatizo ya jamii inayowazunguka au wanatarajia kwenda kutatua matatizo mikoani?
b.
 
Mwafrica usidanganyike na siasa mimi niko hapa marekani kwa miana 10 sasa. Wanafunzi wa hapa hawagomi na hawana utoto wa wanafunzi wa USDM. Tumia muda mwingi kosoma badala ya kuangalia TV na kusoma hizi forums. Watu wengi hapa wanaelimu yao hivyo msiige. Vilevile nashauri kitu kidogo kama uongozi wa wanafunzi hautoshi kukunyima elimu yako ya chuo. sisi hapa hatuwaombei mabaya lakini tunawaambia ukweli na kama wewe unaona unafanya vizuri then good lucky, lakini utakumbuka mawazo yangu miaka ya baadae.
 
Mwafrica usidanganyike na siasa mimi niko hapa marekani kwa miana 10 sasa. Wanafunzi wa hapa hawagomi na hawana utoto wa wanafunzi wa USDM.

Kamundu, wanafunzi hapa hawagomi kwa sababu serikali ya hapa imejifunza kutokana na makosa na hawafanyi mambo ya kipuuzi kama yale ya miaka ya 60 na 70.

Tumia muda mwingi kosoma badala ya kuangalia TV na kusoma hizi forums. Watu wengi hapa wanaelimu yao hivyo msiige. Vilevile nashauri kitu kidogo kama uongozi wa wanafunzi hautoshi kukunyima elimu yako ya chuo.

Naona sasa wewe unataka kunipelea North Korea na kuniamulia cha kufanya nikiwa shuleni.

sisi hapa hatuwaombei mabaya lakini tunawaambia ukweli na kama wewe unaona unafanya vizuri then good lucky, lakini utakumbuka mawazo yangu miaka ya baadae.

Sidhani kama nina haja ya kusubiri miaka ya baadaye wakati leo hii ninaona serikali ikiachia mafisadi kina Chenge na Mramba wakipeta tu huku ikitumia FFU kupiga wanafunzi wasio na hatia
 
Moderators, hizi thread za mgogoro wa UDSM zote tatu ziunganishwe pamoja tafadhali

PM

PM, nadhani ile ya kufukuzwa wanafunzi ijitegemee maana ina tukio jipya kidogo wakati tukisubiria kujua hatima ya yule mama mjamzito aliyepigwa na FFU bila huruma yoyote.
 
Wakuu heshima mbele, nimeisoma hii thread na kujaribu ku-catch the juice lakini siioni vizuri, haina maana kuwa haipo labda wengine wanaiona vizuri zaidi,

lakini swali langu linalalia zaidi kwenye hoja ya msingi ya mtoa mada, tunawasaidiaje whatever tatizo walilo nalo, ingawa ninajua kuwa kama wamefikia kugoma tayari, uwezo wa kuwasaidia utakuwa mdogo, lakini never toolate,

1. Tatizo ni nini hasa? Maana kwenye siasa tunajua kuwa hapa kuna tatizo kubwa zaidi ya yanayosemwa, wananfunzi au mtoa mada wawe wakweli tatizo hasa ni nini?

2. Halafu kwa mawazo yao, tatizo lilipofikia sasa, tunawasaidiaje?

In the future ni vyema pia wakatufahamisha kabla ya tatizo kufikia kama lilipo sasa, lakini ninaomba tuache kulumbana na tujaribu kuwasaidia kama inawezekana, halafu baadaye tatizo likiiisha ndio tunaanza kuonyana, kama ndugu yako amerundikwa jela, kitu cha kwanza ni kujaribu kila njia kumtoa kwa dhamana, maswali na maonyo yatafanyiak baada ya kutoka jela kwanza,

sasa kama inawezekana tuwaote ndugu zetu jela, tutaonyana baadaye, kama hatuwezi kuwasaidia tuseme wazi! Rafiki wa kweli ni wakati wa shida, wao wasingekuja kuomba msaada hapa kama wanajua kuwa hatuna msaada, kama huwezi kuwasaidia sio lazima useme, kwa sababu sometimes busara ni pamoja na kunyamaza, tusiwakatishe tamaa ndugu zetu ni vijana wadogo wanaohitaji msaada period! Malumbano yalipaswa kuwa namna ya kuwasaidia na sio kuwakatisha tamaa, kwa sababu tukiangalia vizuri historia ya maisha yetu na sisi tumesaidiwa sana na watu hata tusiowajua na ambao hawakuwa na sababu ya kutusaidia!

Ahsante Wakuu
 
Kamundu,
Mkuu nakubaliana na wewe sana tu isipokuwa nadhani itakuwa tunapotosha ukweli wa mada hii kama tutaanza kutoa hukumu kabla hatujaelewa vizuri kulikoni. Hata mtoto mtukutu kuna siku naye huonewa na wapambe waliomzidi nguvu.

Kweli kabisa kwamba Sokoine hawagomi, na vyuo vikuu vingine vilevile hawagomi kama chuo chetu Kikuu cha UDSM. Umevitaja pia vya Marekani lakini hapo hapo sidhani kama hivi vyote vinashikiliwa uongozi na huyu Mukandara. Inawezekana kabisa kuwa tatizo ni Uongozi wa juu wa chuo hiki tofauti na vyuo vingine vyote kiasi kwamba kila mwaka kumekuwa na matatizo kama haya..Mbona haikuwa hivyo zamani?... Je, ni kweli matatizo ni wanafunzi ama ni mabadiliko ya Uongozi ambayo badala ya kuwapatia viongozi imewapatia wanasiasa..tukumbuke tu kwamba kuwa na CV nzito kama Mukandara haina maana imtengeneza mtu huyu kuwa kiongozi bora.
Mkuu kumbuka kwamba Tanzania bado kwa kina fulani tunautumia yale mabaki ya Ubabe ambayo walimu wetu walijiona kuwa wao ni Miungu wa Pili, wakitupiga makofi, bakora na hata kufungiwa masomo bila kumtaarifu mzazi ama kumkanya mwanafunzi kwa kuwashirikisha wazazi..Kisha inawezekana kabisa visa na matukio ya UDSM hayapo ktk vyuo vya huko kama maswala ya kukatiwa Umeme na kadhalika.
Nchi kama Marekani haiwezi kuwafungia wananfunzi masomo bila kuwepo na taratibu.. wala huwezi kumtukana mwanafunzi matusi ya nguoni kwa sababu tu wewe ni mkubwa ama mwalimu...Hivyo kuna tofauti kubwa sana na sidhani kama ni vizuri tukatumia mifano ya Marekani.
Kama alivyosema mkuu FMES, hawa vijana wamewakilisha hoja yao na pengine kabla sisi hatujayavulia maji nguo, muhimu tufahamu joto la maji haya..Yuawezekana zipo haki nyingi sana zimekiukwa..Tunachotaka ni HAKI iwe kwa walimu ama wanafunzi..
 
Wana JF,

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatamka hivi (ninanukuu):

20.-(1) Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria
za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au ashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.

Tukiangalia mtazamo (au reaction) ya dola, kwa kuwatumia askari polisi 'kuwatuliza' na au kuwanyamazisha wanafunzi pale ambapo walikuwa wamekusanyika (mara nyingi kwa amani), fujo na vurugu huanzia pale ambapo polisi wanapowalazimisha wanafunzi hao kutawanyika, wanapokataa kutii amri hiyo, humwagiwa tindikali, maji yanayowasha, mabomu ya machoni, n.k., mambo ambayo yanawafanya wa-react kutokana na sababu za kisaikolojia (self defence).

You will always defend yourself when attacked!

Kama serikali ingekuwa inakubali majadiliano na kuwapa wananchi uhuru wa kupinga (right of peaceful assembly, vis-a-vis public procession), basi, hakungekuwapo na matukio ya vurungu, uvunjwaji wa sheria, n.k.

Nani alaumiwe? Aliyedai haki yake kwa kuandamana au aliyekwenda kumnyamazisha asiidai haki yake, kwa kumpiga virungu, kumwagia maji ya upupu na mabomu ya machozi?

Jambo hili linanikumbusha mwaka 1995, wakati Serikali, Mkoani Kilimanjaro, iliposema kwamba isingewamwagia watu mabomu ya machozi wakati walipokwenda kumpokea aliyekuwa mgombea urais wakati huo, kupitia chama cha kisiasa cha NCCR-Mageuzi, Augustine Lyatonga Mrema.

Watu hao walikusanyika pembezoni mwa barabara (nilikuwa mmoja wa waandishi wa habari waandamizi tuliokuwa na Mrema wakati wa ziara yake, tukiripoti matukio mbali mbali...), wakisubiri kumlaki Mrema, kwa amani. Magari ya FFU na askari wakapita barabarani wakitupa mabomu ya machozi, watu walikimbia nyumbani kunawa nyuso zao, na kurudi tena barabarani! Ilikuwa aibu na kichekesho cha mwaka!

Lakini ya UDSM ni mengine... wako wanaotoa lawama, na wako wanaowaunga mkono. Zote hizo ni hoja, ni maoni, kila mtu anao uhuru wa kutoa maoni yake... Ibara ya 18 (1) na (2) ya Katiba!

Someni katiba muielewe waungwana!

./Mwana wa Haki
 
Jamani, kama wanafunzi wa UDSM hata kama wangekuwa wamekosea, wamefikishwa mahakamani siku moja tu baada ya kukamatwa, mbona mafisadi wamejulikana hadi wakajiuzuru, na wamekaa nyumbani kwao wakila kuku kwa mrija na wake zao wanene bila hata kukamatwa na polisi? hii inasikitishwa, kwasababu mafisadi ndo wamekula hela nyingi ambazo zingetumika kuhudumia hawa wanafunzi chuo, hata izo fujo zisingetokea kabisa. hebu tuangalie chanzo. ni bilion ngapi ilikuwa inahitajika university pale ili kusettle zile claims za wanafunzi kipindi kile?chenge amekula ngapi?Lowasa kajilimbikizia ngapi?mkapa je huko kiwila? kama kuna matumizi mazuri ya pesa za selikali, hao wanafunzi wangegoma nini? na je, kuwafukuza ndo solution?si ndo umepunguza wasomi wa tz?jamani hivi huyu Jumanne magimbi waziri ana nini?

Na kitu kingine, tangu huyo profesa mukandara toka aingie kuwa makamu mkuu wa chuo cha DSM(aliopewa na kikwete baada ya kumfagilia na kumtabiria kuwa atashinda uchaguzi kipindi kile cha uchaguzi), toka aingie pale, ana kiburi sana. hapendi negotiations na wanafunzi, anajua yeye amewekwa pale na mkubwa. sijawai kuona mkuu wa chuo mwenye kiburi kama huyo.Mtu mzima ana maindi kushindana na wanafunzi, yeye ashakuwa professa, wenzie hata degree hawana, nani huwa ana shindana na mtoto wake?ni na wewe utaonekana mtoto?uprofesa wake huyu jamaa uko wapi. mbona kiwa wakati wanafunzi wakidai vitu yeye hufurahia kuwakomoa kwa kuwafukuza?hakuna hata siku moja ambayo aliwahikuonyesha kuwa hana kisirani na wanafunzi.

na huyu jamaa alikuwa profesa wa pale zamani ujue. hatujamuweka pale ili atupunguzie wasomi tz, tunataka awe ana wa encourage ili tz tuwe na wasomi, ndo kazi iliyompeleka pale. hajaajiriwa na kikwete pale, ameajiliwa na watz wote. ananikeraga sana uyu jamaa.Jamani, mnasemaje kuhusu hili? au nakosea kufikiri hivi?
 
Jamani, kama wanafunzi wa UDSM hata kama wangekuwa wamekosea, wamefikishwa mahakamani siku moja tu baada ya kukamatwa, mbona mafisadi wamejulikana hadi wakajiuzuru, na wamekaa nyumbani kwao wakila kuku kwa mrija na wake zao wanene bila hata kukamatwa na polisi? hii inasikitishwa, kwasababu mafisadi ndo wamekula hela nyingi ambazo zingetumika kuhudumia hawa wanafunzi chuo, hata izo fujo zisingetokea kabisa. hebu tuangalie chanzo. ni bilion ngapi ilikuwa inahitajika university pale ili kusettle zile claims za wanafunzi kipindi kile?chenge amekula ngapi?Lowasa kajilimbikizia ngapi?mkapa je huko kiwila? kama kuna matumizi mazuri ya pesa za selikali, hao wanafunzi wangegoma nini? na je, kuwafukuza ndo solution?si ndo umepunguza wasomi wa tz?jamani hivi huyu Jumanne magimbi waziri ana nini?

Na kitu kingine, tangu huyo profesa mukandara toka aingie kuwa makamu mkuu wa chuo cha DSM(aliopewa na kikwete baada ya kumfagilia na kumtabiria kuwa atashinda uchaguzi kipindi kile cha uchaguzi), toka aingie pale, ana kiburi sana. hapendi negotiations na wanafunzi, anajua yeye amewekwa pale na mkubwa. sijawai kuona mkuu wa chuo mwenye kiburi kama huyo.Mtu mzima ana maindi kushindana na wanafunzi, yeye ashakuwa professa, wenzie hata degree hawana, nani huwa ana shindana na mtoto wake?ni na wewe utaonekana mtoto?uprofesa wake huyu jamaa uko wapi. mbona kiwa wakati wanafunzi wakidai vitu yeye hufurahia kuwakomoa kwa kuwafukuza?hakuna hata siku moja ambayo aliwahikuonyesha kuwa hana kisirani na wanafunzi.

na huyu jamaa alikuwa profesa wa pale zamani ujue. hatujamuweka pale ili atupunguzie wasomi tz, tunataka awe ana wa encourage ili tz tuwe na wasomi, ndo kazi iliyompeleka pale. hajaajiriwa na kikwete pale, ameajiliwa na watz wote. ananikeraga sana uyu jamaa.Jamani, mnasemaje kuhusu hili? au nakosea kufikiri hivi?
 
Jamani, kama wanafunzi wa UDSM hata kama wangekuwa wamekosea, wamefikishwa mahakamani siku moja tu baada ya kukamatwa, mbona mafisadi wamejulikana hadi wakajiuzuru, na wamekaa nyumbani kwao wakila kuku kwa mrija na wake zao wanene bila hata kukamatwa na polisi? hii inasikitishwa, kwasababu mafisadi ndo wamekula hela nyingi ambazo zingetumika kuhudumia hawa wanafunzi chuo, hata izo fujo zisingetokea kabisa. hebu tuangalie chanzo. ni bilion ngapi ilikuwa inahitajika university pale ili kusettle zile claims za wanafunzi kipindi kile?chenge amekula ngapi?Lowasa kajilimbikizia ngapi?mkapa je huko kiwila? kama kuna matumizi mazuri ya pesa za selikali, hao wanafunzi wangegoma nini? na je, kuwafukuza ndo solution?si ndo umepunguza wasomi wa tz?jamani hivi huyu Jumanne magimbi waziri ana nini?

Na kitu kingine, tangu huyo profesa mukandara toka aingie kuwa makamu mkuu wa chuo cha DSM(aliopewa na kikwete baada ya kumfagilia na kumtabiria kuwa atashinda uchaguzi kipindi kile cha uchaguzi), toka aingie pale, ana kiburi sana. hapendi negotiations na wanafunzi, anajua yeye amewekwa pale na mkubwa. sijawai kuona mkuu wa chuo mwenye kiburi kama huyo.Mtu mzima ana maindi kushindana na wanafunzi, yeye ashakuwa professa, wenzie hata degree hawana, nani huwa ana shindana na mtoto wake?ni na wewe utaonekana mtoto?uprofesa wake huyu jamaa uko wapi. mbona kiwa wakati wanafunzi wakidai vitu yeye hufurahia kuwakomoa kwa kuwafukuza?hakuna hata siku moja ambayo aliwahikuonyesha kuwa hana kisirani na wanafunzi.

na huyu jamaa alikuwa profesa wa pale zamani ujue. hatujamuweka pale ili atupunguzie wasomi tz, tunataka awe ana wa encourage ili tz tuwe na wasomi, ndo kazi iliyompeleka pale. hajaajiriwa na kikwete pale, ameajiliwa na watz wote. ananikeraga sana uyu jamaa.Jamani, mnasemaje kuhusu hili? au nakosea kufikiri hivi?
 
Jamani, mbona Mukandara siku zote huwa ana negative attitude na wanafunzi anaowasimamia pale udsm?hivi mbona huwa hataki diplomasia au kunegotiate, siku zote yeye huwa anamaindi kuwakomoa, utafikiri yeye hana watoto vile. lini toka aingie aliwahi kuonyesha walau kuwa na upendo kwa wanafunzi?, kwa upande wa Jumanne magimbi, mimi huyo simwongelei, kwasababu ni sifuri. profesa mzima badala ya kwenda kufundisha waibue vipaji huko vyuo vikuu, yeye anakimbila kuwa waziri. vyuo vikuu atafundisha nani sasa? well, hata kama hivyo, angekuwa basi anaonyesha uprofesa wake akiwa waziri kwa kutatua matatizo vizuri bile kukomoana kama sisi so wote watz vile. aonyeshe kama yeye profesa by solving these kinds of conflicts. kwa hapo, kufukuza wanafunzi, hata mtu wa darasa la saba hawezi fanya hivyo. nafikiri uprofesa wake ameshasahau vitabu, umeliwa na kile kiburi cha sauti yake na raha za uwaziri. sio profesa tena.
 
Wakuu heshima mbele, nimeisoma hii thread na kujaribu ku-catch the juice lakini siioni vizuri, haina maana kuwa haipo labda wengine wanaiona vizuri zaidi,

lakini swali langu linalalia zaidi kwenye hoja ya msingi ya mtoa mada, tunawasaidiaje whatever tatizo walilo nalo, ingawa ninajua kuwa kama wamefikia kugoma tayari, uwezo wa kuwasaidia utakuwa mdogo, lakini never toolate,

1. Tatizo ni nini hasa? Maana kwenye siasa tunajua kuwa hapa kuna tatizo kubwa zaidi ya yanayosemwa, wananfunzi au mtoa mada wawe wakweli tatizo hasa ni nini?

2. Halafu kwa mawazo yao, tatizo lilipofikia sasa, tunawasaidiaje?

In the future ni vyema pia wakatufahamisha kabla ya tatizo kufikia kama lilipo sasa, lakini ninaomba tuache kulumbana na tujaribu kuwasaidia kama inawezekana, halafu baadaye tatizo likiiisha ndio tunaanza kuonyana, kama ndugu yako amerundikwa jela, kitu cha kwanza ni kujaribu kila njia kumtoa kwa dhamana, maswali na maonyo yatafanyiak baada ya kutoka jela kwanza,

sasa kama inawezekana tuwaote ndugu zetu jela, tutaonyana baadaye, kama hatuwezi kuwasaidia tuseme wazi! Rafiki wa kweli ni wakati wa shida, wao wasingekuja kuomba msaada hapa kama wanajua kuwa hatuna msaada, kama huwezi kuwasaidia sio lazima useme, kwa sababu sometimes busara ni pamoja na kunyamaza, tusiwakatishe tamaa ndugu zetu ni vijana wadogo wanaohitaji msaada period! Malumbano yalipaswa kuwa namna ya kuwasaidia na sio kuwakatisha tamaa, kwa sababu tukiangalia vizuri historia ya maisha yetu na sisi tumesaidiwa sana na watu hata tusiowajua na ambao hawakuwa na sababu ya kutusaidia!

Ahsante Wakuu

Asante sana Mkulu FMES,

Unajua inawezekana kweli vijana hawa wameshindwa kujipanga vizuri na kujieleza kwa uwazi zaidi kile kinachowasibu. Ndio maana mimi nawapa support hapa ili wajifunze namna zaidi ya kufikisha hoja kwa audience kubwa kama ya JF.

Katika hili mkuu, msaada mkubwa sasa hivi kwa hawa vijana ni kuwasaidia kwenye hii case, case ambayo ni ya uonevu na isiyo na msingi wowote. Msaada wa pili ni kuweka pressure kwa Mukandala na wenzake kuwarudisha hawa vijana.

Cha tatu na ni kikubwa zaidi ni kumtaka Mukandala aache kuingilia uhuru wa wanafunzi wa chuo kikuu wa kuchagua viongozi wao. Najua sio wengi watasaidia (maana hata wana JF waliposhikwa ni wachache sana walijitokeza kusaidia) lakini ni vyema baadhi yetu tukawapa support kwa kile kilichowasibu.

Asante sana FMES kwa support yako.
 
Hivi ni kwanini Uongozi wa Chuo Kikuu uliamua kuingilia uchaguzi wa serikali ya Chuo?
 
Jamani, kama wanafunzi wa UDSM hata kama wangekuwa wamekosea, wamefikishwa mahakamani siku moja tu baada ya kukamatwa, mbona mafisadi wamejulikana hadi wakajiuzuru, na wamekaa nyumbani kwao wakila kuku kwa mrija na wake zao wanene bila hata kukamatwa na polisi? hii inasikitishwa, kwasababu mafisadi ndo wamekula hela nyingi ambazo zingetumika kuhudumia hawa wanafunzi chuo, hata izo fujo zisingetokea kabisa. hebu tuangalie chanzo. ni bilion ngapi ilikuwa inahitajika university pale ili kusettle zile claims za wanafunzi kipindi kile?chenge amekula ngapi?Lowasa kajilimbikizia ngapi?mkapa je huko kiwila? kama kuna matumizi mazuri ya pesa za selikali, hao wanafunzi wangegoma nini? na je, kuwafukuza ndo solution?si ndo umepunguza wasomi wa tz?jamani hivi huyu Jumanne magimbi waziri ana nini?

Mwenzangu,

wao hawafikiri haya. Ni ubabe mbele kwa mbele

na kitu kingine, tangu huyo profesa mukandara toka aingie kuwa makamu mkuu wa chuo cha DSM(aliopewa na kikwete baada ya kumfagilia na kumtabiria kuwa atashinda uchaguzi kipindi kile cha uchaguzi), toka aingie pale, ana kiburi sana. hapendi negotiations na wanafunzi, anajua yeye amewekwa pale na mkubwa. sijawai kuona mkuu wa chuo mwenye kiburi kama huyo.Mtu mzima ana maindi kushindana na wanafunzi, yeye ashakuwa professa, wenzie hata degree hawana, nani huwa ana shindana na mtoto wake?ni na wewe utaonekana mtoto?uprofesa wake huyu jamaa uko wapi. mbona kiwa wakati wanafunzi wakidai vitu yeye hufurahia kuwakomoa kwa kuwafukuza?hakuna hata siku moja ambayo aliwahikuonyesha kuwa hana kisirani na wanafunzi.

Hii ni sababu ambayo Rwekaza Mukandala atapata titles kama za mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata Rostam Azizi hapa JF. Toka aoneshe kiburi na dharau kubwa kiasi hiki kwenye demokrasia ya wanafunzi wasomi, Mukandala anajulikana kama fisadi (mshauri wa mafisadi serikali), dikiteta (kuingilia chaguzi huru za wanafunzi), na muuaji (kwa kusababisha kifo cha mwanafunzi) Mukandala.

na huyu jamaa alikuwa profesa wa pale zamani ujue. hatujamuweka pale ili atupunguzie wasomi tz, tunataka awe ana wa encourage ili tz tuwe na wasomi, ndo kazi iliyompeleka pale. hajaajiriwa na kikwete pale, ameajiliwa na watz wote. ananikeraga sana uyu jamaa.Jamani, mnasemaje kuhusu hili? au nakosea kufikiri hivi?

Kiburi chake kinakutana na kipimo cha mwafrika wa kike na wana JF. Yeye atajiona kwa sasa kuwa yuko matawi ya juu kwa vile ni rafiki ya Kikwete na ni mshauri wake wa kisiasa. Lakini ajue kuwa yeye ni adui namba moja wa demokrasia chuoni na kwa sasa amewekwa kwenye notice... ni bango mpaka kieleweke.

Just visit Jamboforums daily......
 
Hivi ni kwanini Uongozi wa Chuo Kikuu uliamua kuingilia uchaguzi wa serikali ya Chuo?

Tell me about it!

Bado hawajatoa sababu zozote za kueleweka. Huyu Mukandala ni mtu mwenye dharau sana na hata maelezo yake kwa vyombo vya habari jana yanaonesha kibri ya hali ya juu sana!
 
Wandugu,

Mi nadhani kuna weakness kwa upande wa hawa vijana kama kweli kuna wenzao baadhi wanashutumiwa kufanya fujo na uharibifu sababu tu kukosa maji nina mashaka na uwezo wao wa kufikiri na kuamua mambo. Sioni mantiki ya kufikia kufanya vitendo vya kihuni kwa kisingizio cha kukosa maji nina imani kulikuwa na njia sahihi za ku-address suala lao....UDSM ndio jiko la kupika manpower za nchi katika nyanja mbali mbali lakini kama vijana ndio wanakuwa hivi bendera kufata upepo i can imagine product za chuo hicho in 10- 15 years to come...

Mnatakiwa kujifuza kutumia busara na hekima katika kufanya decisions kinyume cha hivyo kila siku mtakuwa mnalia mnaonewa kumbe mnachemka wenyewe...

Acha tu hivi vitoto vinavyoonekana vilikiuka taratibu vitimuliwe wanaburuzwa kufanya maamuzi na "Mvuto wa makundi"..

Jiangalieni upya vijana mnategemewa kuja kuliokoa taifa la Tz...

Kapumzikeni nyumbani tu may be mtakapokuwa mnatafakari lililotokea kila mtu kivyake mtajua mlipotoka wapi...
 
Wandugu,

Mi nadhani kuna weakness kwa upande wa hawa vijana kama kweli kuna wenzao baadhi wanashutumiwa kufanya fujo na uharibifu sababu tu kukosa maji nina mashaka na uwezo wao wa kufikiri na kuamua mambo. Sioni mantiki ya kufikia kufanya vitendo vya kihuni kwa kisingizio cha kukosa maji nina imani kulikuwa na njia sahihi za ku-address suala lao....UDSM ndio jiko la kupika manpower za nchi katika nyanja mbali mbali lakini kama vijana ndio wanakuwa hivi bendera kufata upepo i can imagine product za chuo hicho in 10- 15 years to come...

Kapinga,

Nadhani unaongelea vitu viwili tofauti hapa. Huu mgomo umetokana na uamuzi wa chuo kuingilia uchaguzi huru wa wanafunzi.

Mnatakiwa kujifuza kutumia busara na hekima katika kufanya decisions kinyume cha hivyo kila siku mtakuwa mnalia mnaonewa kumbe mnachemka wenyewe...

Acha tu hivi vitoto vinavyoonekana vilikiuka taratibu vitimuliwe wanaburuzwa kufanya maamuzi na "Mvuto wa makundi"..

Jiangalieni upya vijana mnategemewa kuja kuliokoa taifa la Tz...

Kapumzikeni nyumbani tu may be mtakapokuwa mnatafakari lililotokea kila mtu kivyake mtajua mlipotoka wapi...

Usidhani kuwa unawakomoa hawa watoto kwa kuwatuma nyumbani na kutisha kuwa hawatapata udhamini wa serikali. Hapa unacreate radicals ambao wanaweza kufanya chochote in the future kama life itaharibika kwa sababu ya udikiteta ulioonyesha kwenye hili.
 
Back
Top Bottom