Na hata zaidi ya ajira kuna personal creativity and productivity.
Unachosoma kina make sense au unafuata mkumbo tu?
Ndiyo maana mimi nikatoa mfano, kuna mchizi katoka zake Ukraine huko, familia yake iliona rhumba kali imeenda unyamwezini, hata kiingereza cha tabu. Walikuwa wanategemea welfare checks za serikali baada ya mzazi wake mmoja kufa kwa kansa.
Kajibanabana hivyo hivyo kaanza chuo, kaona chuo hakina mpango ka drop out, kajifunza mwenyewe computer programming, kafanya.kazi Yahoo, kapata ujuzi na network, kaacha kazi, kaanzisha Whatsapp na rafiki yake.
Kabadilisha jinsi text messaging system zinavyofanya kazi dunia nzima, katuwezesha kutumiana text kutoka simu yoyote yenye mtandao kwenda simu yoyote, bila kulipa.
Juzi Facebook wametangaza kununua Whatsapp kwa USD bilioni 16, na nyingine USD bilioni 3 wanapewa cha juu. That's some cool 19 billion USD, halafu bado anaendeleza libeneke Whatsapp, with some degree of autonomy.
Sie tunang'ang'ania majina ya vyuo na madegree, mpaka ya kununua, wenzetu ma dropouts hao kina Bill Gates na huyu dogo wa Whatsapp wanabadilisha dunia inavyoenda.