Udukuzi juu ya udukuzi: Mwendelezo wa vita baridi kati ya Marekani na Urusi

Udukuzi juu ya udukuzi: Mwendelezo wa vita baridi kati ya Marekani na Urusi

Sehemu ya 3
Inaendelea:
Hivyo basi anatakiwa kurudi Urusi lakini baadaye baada ya kuingia uongozi wa Bill Clinton bwana Lyskenko alisamehewa kwa makubaliano mataifa hayo mawili kuendeleza urafiki wa kidiplomasia.

Mwaka 1986 Rais wa Marekani Ronald Reagan aliwafukuza wanadiplomasia 55 wa Urusi baada ya kuwahisi Warusi wanaiba siri za Marekani, vivyo hivyo Urusi ikawazuia wafanyakazi wa muungano wa Kisoviet sosholist republic zaidi ya 260 waliokuwa wanafanya kazi katika ubalozi wa marekani kuacha kufanya kazi mara moja. Hii ndio idadi kubwa zaidi ya Wanadiplomasia wa Urusi kuwahi kufukuzwa nchini Marekani.
Mgogoro ulianza baada ya Gennadi F. Zakharov aliyekuwa mfanyakazi wa kisoviet katika makao makuu ya Umoja wa mataifa (United Nation) kukamatwa kwa madai ya Udukuzi wa Siri muhimu za Jeshi la Marekani. Urusi walijibu mapigo kwa kumkamata Nicholas S. Daniloff ambaye walimtuhumu juu ya ukusanyaji wa taarifa muhimu za Urusi na kuzituma nchini marekani. Kwa historia hii inaonyesha wazi ya Kwamba vita baridi katika mataifa haya inaendelea na haijawahi kusimama.

Uhasimu wa mataifa haya utamalizika pale ambapo taifa moja litakubali kuwa Mfuasi wa Taifa lingine au kama ikitokea Vita ya tatu ya Dunia na Taifa moja likapoteza nguvu kiuchumi, kiteknolojia na kisiasa kwa kupigwa katika vita hiyo.
Urusi na Marekani ndio mataifa yenye ushindani mkubwa katika teknolojia ya silaha na shughuli za kijasusi.
Mwisho,
Asanteni na shukrani
 
Mkuu ni kweli kwamba marekani ndo walikuwa washindi kwa sababu wao ndo walihakikisha Gabashev na Boris wanakuwa marais wa USSR kwa kipindi hicho. ikumbukwe kuwa hawa walisoma marekani na wakapewa mafunzo nini cha kufanya wakiwa urusi
 
Back
Top Bottom