Unajua Barca wametengeneza kautaratibu fulani hivi ka kutaka kuaminisha watu ni timu bora zaidi kuwahi kutokea duniani lakini sijui kama ni makusudi au bahati mbaya ni kama wanafaidika na 'sympathy' fulani ya kitaasisi. Watu wengi na viongozi wengi wa soka duniani wamekuwa na kaupofu fulani hivi in favour ya Barcelona kiasi kwamba ni ngumu kuhukumu against wao. Mimi naamini mpira 'mwingi' wa Barcelona umelevya dunia kiasi cha kuona wao wako sahihi kwa kila kitu.
Mfano, kwa karibu miaka 10 hivi sikumbuki kuwahi kuona Barcelona ikiumizwa na makosa ya kile kinachoitwa bahati mbaya ya waamuzi kama zinavyoumizwa timu nyingine hadi katika mechi kubwa kabisa kama fainali za UEFA.
Pili, pamoja na Barcelona kucheza pasi nyingi lkn ikumbukwe hutumia nguvu kubwa kukaba wanapopoteza mpira, na wakati mwingine hutumia nguvu kubwa kupora mipira kutoka kwa wapinzani wao kiasi cha kuamini ni faulo lkn waamuzi huwa hawatoi faulo nyingi kwa timu pinzani, kinyume na wao Barcelona wakiguswa tu wakati mwingine timu pinzani ni kadi za njano kama njugu.
Mfano, kwa karibu miaka 10 hivi sikumbuki kuwahi kuona Barcelona ikiumizwa na makosa ya kile kinachoitwa bahati mbaya ya waamuzi kama zinavyoumizwa timu nyingine hadi katika mechi kubwa kabisa kama fainali za UEFA.
Pili, pamoja na Barcelona kucheza pasi nyingi lkn ikumbukwe hutumia nguvu kubwa kukaba wanapopoteza mpira, na wakati mwingine hutumia nguvu kubwa kupora mipira kutoka kwa wapinzani wao kiasi cha kuamini ni faulo lkn waamuzi huwa hawatoi faulo nyingi kwa timu pinzani, kinyume na wao Barcelona wakiguswa tu wakati mwingine timu pinzani ni kadi za njano kama njugu.